Ndoa
Mpango wa ndoa ulianzaje?
Mkristo anapaswa kumchagua nani awe mwenzi wake wa ndoa?
Kwa nini Mkristo wa kweli hapaswi kukubali mwana au binti yake aliyebatizwa afunge ndoa na mtu ambaye si mtumishi wa Yehova aliyejiweka wakfu na kubatizwa?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 24:1-4, 7—Abrahamu aliyezeeka anaazimia kumtafutia mke, Isaka, mwana wake, kutoka kwa watu wanaomtumikia Yehova, si kutoka kwa Wakanaani, wanaoabudu miungu mingine
Mwa 28:1-4—Isaka anamwongoza Yakobo, mwana wake, akatafute mke kwa waabudu wenzake, wala si kutoka kwa Wakanaani
Yehova anahisije kuhusu wale wanaofunga ndoa na watu wasiomwabudu?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Fa 11:1-6, 9-11—Yehova anamkasirikia Mfalme Sulemani kwa kupuuza onyo kutoka kwake, kwa kuoa wanawake wa kigeni, na kuwaruhusu waupotoshe moyo wake
Ne 13:23-27—Kama Yehova, Gavana Nehemia anakasirika sana Waisraeli wanapooa wanawake wa kigeni ambao hawamtumikii Yehova, hivyo Nehemia anawatia nidhamu na kuwarekebisha
Kwa nini ni jambo la hekima kuchagua mwenzi wa ndoa mwenye sifa nzuri na anayemtumikia Yehova kwa uaminifu?
Tazama pia Efe 5:28-31, 33
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Sa 25:2, 3, 14-17—Nabali ni mwanamume tajiri, lakini ni mkali na mkatili, na hilo linafanya awe mume mbaya kwa Abigaili
Met 21:9—Kuchagua mwenzi wa ndoa asiyefaa kunaweza kutufanya tusiwe na furaha na kutunyang’anya amani yetu
Ro 7:2—Mtume Paulo anaeleza kwamba mwanamke anapoolewa anakuwa chini ya mamlaka ya kadiri ya mume wake asiye mkamilifu; kwa hiyo mwanamke mwenye hekima anakuwa mwangalifu anapochagua mwenzi wa ndoa
Kujitayarisha kwa ajili ya ndoa
Kwa nini mwanamume anapaswa kujitayarisha kwa ajili ya jukumu la kutegemeza familia kabla ya kufunga ndoa?
Simulizi la Biblia linalohusika:
Met 24:27—Kabla mwanamume hajaoa au kupata watoto, anapaswa kufanya kazi kwa bidii ili awe tayari kutegemeza familia
Kwa nini watu wawili wanaochumbiana wanapaswa kukazia fikira kutafuta ushauri wenye hekima na kufahamiana vizuri, badala ya kuangalia tu mwonekano wa nje?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ru 2:4-7, 10-12—Boazi anamfahamu zaidi Ruthu kwa kuchunguza mazoea yake ya kufanya kazi, na kwa kuzingatia ripoti zinazotegemeka kuhusu sifa zake, jinsi anavyoshughulika na familia yake, na hali yake ya kiroho
Ru 2:8, 9, 20—Ruthu anamfahamu vizuri Boazi kwa kuchunguza jinsi alivyo mwenye fadhili, mkarimu, na upendo wake kwa Yehova
Kwa nini Yehova anataka tudumishe usafi wa kiadili wakati wa urafiki wa kimapenzi na uchumba?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Met 5:18, 19—Baadhi ya matendo ya kimahaba yanapaswa kufanywa na wenzi wa ndoa tu
Wim 1:2; 2:6—Wakati wa uchumba, kijana mchungaji na msichana Mshulami wanaelezana upendo wao kwa njia safi, si kwa maneno machafu ya kimahaba
Wim 4:12; 8:8-10—Msichana Mshulami anadumisha usafi wa kiadili na anaonyesha sifa ya kujizuia; yeye ni kama bustani iliyofungwa
Kwa nini wanaopanga kufunga ndoa wanapaswa kufunga ndoa kisheria?
Majukumu ya waume
Ni majukumu gani mazito aliyopewa mume?
Waume wanapaswa kuiga mfano wa nani wanapotimiza jukumu lao la ukichwa?
Kwa nini ni muhimu kwa mume kumwonyesha upendo mke wake na kuelewa mahitaji na hisia zake?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 21:8-12—Yehova anamwagiza Abrahamu amsikilize Sara, mke wake, hata ingawa mapendekezo ya Sara hayakumpendeza
Met 31:10, 11, 16, 28—Mume mwenye hekima wa mke mwema anayetajwa kwenye mistari hii, hamtawali mke wake au kutafuta makosa yake; bali anamwamini mke wake na kumsifu
Efe 5:33—Maneno ya mtume Paulo yaliyoongozwa na roho yanadokeza kwamba mke ana uhitaji wa pekee wa kuhisi kwamba anapendwa na mume wake
Jukumu la mke
Ni jukumu gani la pekee kutoka kwa Yehova ambalo mke Mkristo anatimiza?
Je, jukumu la mke linamshushia heshima?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Met 1:8; 1Ko 7:4—Katika ndoa na maisha ya familia, mke na mama wamepewa mamlaka ya kadiri na Mungu
1Ko 11:3—Mtume Paulo anaeleza kwamba kulingana na mpango wa Yehova, sisi sote tupo chini ya ukichwa isipokuwa Mungu Mweza-Yote
Ebr 13:7, 17—Katika kutaniko, wanaume na wanawake wanapaswa kujitiisha na kuwatii wale wanaoongoza
Mke Mkristo ambaye ana mume asiyeamini anawezaje kumfurahisha Yehova?
Kwa nini mke Mkristo anapaswa kudumisha mtazamo wa heshima kuelekea mume wake?
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mwa 18:12; 1Pe 3:5, 6—Sara anamheshimu sana mume wake hata katika mawazo yake, akimwona kama “bwana” wake au kichwa cha kiroho
Ni mke wa aina gani anayesifiwa katika Biblia?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 24:62-67—Rebeka anamsaidia Isaka, mume wake, kupata faraja baada ya kifo cha mama yake
1Sa 25:14-24, 32-38—Abigaili anamlinda mume wake mpumbavu na kuokoa nyumba yake kwa kumwomba kwa unyenyekevu Daudi aonyeshe rehema
Est 4:6-17; 5:1-8; 7:1-6; 8:3-6—Malkia Esta anahatarisha uhai wake mara mbili kwa kwenda kwa mume wake, mfalme, bila kuitwa, ili amwombe awalinde watu wa Mungu
Kutatua hali ya kutoelewana
Ni kanuni gani zinazoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kutatua matatizo yanayotokea katika ndoa?
Ni kanuni gani zinazoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kuwa na maoni yenye usawaziko kuhusu pesa?
Lu 12:15; Flp 4:5; 1Ti 6:9, 10; Ebr 13:5
Tazama pia “Pesa”