Mateso
Kwa nini Wakristo wanapaswa kutarajia mateso?
Kwa nini tunapaswa kumtegemea Yehova tunapoteswa?
Zb 55:22; 2Ko 12:9, 10; 2Ti 4:16-18; Ebr 13:6
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Fa 19:1-18—Alipoteswa, nabii Eliya alimimina moyo wake kwa Yehova na akapata kitia moyo na faraja
Mdo 7:9-15—Yosefu anateswa na ndugu zake, lakini Yehova anaendelea kuwa mshikamanifu kwake, anamwokoa, na kumtumia Yosefu kuiokoa familia yake
Kuna aina gani za mateso?
Matukano
2Nya 36:16; Mt 5:11; Mdo 19:9; 1Pe 4:4
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Fa 18:17-35—Msemaji wa mfalme wa Ashuru, Rabshake, anamtukana Yehova na kuwadhihaki watu wa Yerusalemu
Lu 22:63-65; 23:35-37—Watu wanaomtesa Yesu wanamtukana na kumdhihaki anapokuwa amekamatwa na anapokuwa kwenye mti wa mateso
Upinzani kutoka kwa watu wa ukoo
Kukamatwa na kupelekwa mbele ya maofisa wa serikali
Kuteswa kimwili
Kushambuliwa na vikundi vyenye ghasia
Kuuawa
Wakristo wanapaswa kujiendeshaje wanapoteswa?
Mt 5:44; Mdo 16:25; 1Ko 4:12, 13; 1Pe 2:23
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mdo 7:57–8:1—Ingawa anakaribia kufa kwa sababu ya kushambuliwa na umati wa watu wenye hasira, mwanafunzi Stefano anamwomba Mungu awaonyeshe rehema watesaji wake, ambao wanatia ndani Sauli wa Tarso
Mdo 16:22-34—Ingawa mtume Paulo amepigwa na kuwekwa kwenye mikatale, anamwonyesha fadhili mlinzi wa jela, jambo linalofanya mwanamume huyo na familia yake yote wawe waamini
Ni nini kilichowapata baadhi ya Wakristo wa karne ya kwanza?
Tunapaswa kuhisije tunapoteswa?
Tumaini letu la wakati ujao linatuimarishaje wakati wa mateso?
Kwa nini hatupaswi kuruhusu mateso yafanye tuhisi aibu, woga, au kuvunjika moyo, na kwa nini hatupaswi kuacha kumtumikia Yehova kwa sababu ya mateso?
Zb 56:1-4; Mdo 4:18-20; 2Ti 1:8, 12
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Nya 32:1-22—Anapokabili tishio la kushambuliwa na jeshi lenye nguvu la Mfalme Senakeribu, mfalme mwaminifu Hezekia anamtegemea Yehova na kuwaimarisha watu; naye anathawabishwa sana
Ebr 12:1-3—Watesaji wanajaribu kumwaibisha Yesu, lakini anaidharau aibu, na kutoruhusu imvunje moyo kwa njia yoyote
Mateso yanaweza kuwa na matokeo gani mazuri?
Tunapovumilia majaribu tunamfurahisha Yehova na kuliletea heshima jina lake
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ayu 1:6-22; 2:1-10—Ingawa hakujua kwamba Shetani ndiye anayesababisha majaribu yake makali, Ayubu anakataa kumwacha Yehova, hivyo anamtukuza Mungu na kuthibitisha kwamba Shetani ni mwongo
Da 1:6, 7; 3:8-30—Vijana waaminifu Hanania, Mishaeli, na Azaria (Shadraki, Meshaki, na Abednego) wapo tayari kukabili kifo cha kikatili badala ya kutomtii Yehova; matokeo ni kwamba mfalme mpagani Nebukadneza anamtukuza Yehova hadharani
Mateso yanaweza kutoa fursa ya kutoa ushahidi zaidi
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mdo 11:19-21—Wakristo waliotawanyika kwa sababu ya mateso wanaendelea kuhubiri habari njema kotekote
Flp 1:12, 13—Mtume Paulo anafurahi kwamba kifungo chake kimeendeleza habari njema
Tunapovumilia chini ya mateso tunaweza kuwaimarisha waabudu wenzetu
Viongozi wa kidini na wanasiasa wanahusikaje katika kuwatesa watumishi waaminifu wa Yehova?
Yer 26:11; Mk 3:6; Yoh 11:47, 48, 53; Mdo 25:1-3
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mdo 19:24-29—Watengenezaji wa vihekalu vya Artemi jijini Efeso, wanauona ujumbe wa Wakristo unaopinga kuabudu sanamu kuwa tishio kwa biashara yao inayowapatia faida, hivyo wanawatesa Wakristo
Gal 1:13, 14—Kabla ya kuwa Mkristo, Paulo (Sauli) akiwa amechochewa na bidii kwa ajili ya dini yake ya Kiyahudi, analitesa kutaniko