Kunywa
Je, Biblia inakataza kunywa kileo kwa kiasi?
Zb 104:14, 15; Mhu 9:7; 10:19; 1Ti 5:23
Simulizi la Biblia linalohusika:
Yoh 2:1-11—Katika karamu ya ndoa, Yesu anafanya muujiza wake wa kwanza, kwa ukarimu anabadili maji kuwa divai nzuri, na hivyo anawasaidia bwana na bibi harusi wasiaibike
Tunaweza kupata madhara gani tukinywa kupita kiasi au tukiwa walevi?
Watumishi wa Mungu wana maoni gani kuhusu ulevi?
1Ko 5:11; 6:9, 10; Efe 5:18; 1Ti 3:2, 3
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 9:20-25—Kwa sababu Noa amelewa, mjukuu wake anapata fursa ya kutenda dhambi nzito
1Sa 25:2, 3, 36—Nabali, mwanamume mkali na mpumbavu, anafanya mambo mengi mabaya kutia ndani ulevi
Da 5:1-6, 22, 23, 30, 31—Mfalme Belshaza anakunywa divai kupita kiasi na kumtukana Yehova Mungu; hivyo anauawa usiku huohuo
Kwa nini tunahitaji kuwa waangalifu kuhusu kiasi tunachokunywa hata ingawa hatulewi?
Met 23:20; Isa 5:11; Lu 21:34; 1Ti 3:8
Tazama pia 1Pe 4:3
Tunawezaje kumsaidia Mkristo mwenzetu anayepambana na tatizo la kunywa kupita kiasi?
Ro 14:13, 21; 1Ko 13:4, 5; 1Th 4:4
Tazama pia “Kujizuia”