Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w10 5/1 uku. 31
  • Jumba la Ufalme ni nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jumba la Ufalme ni nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Hapa Ni Mahali Petu pa Ibada
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mipango ya Mahali pa Ibada
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Upanuzi wa Haraka Wahitajiwa kwa Sababu ya Ongezeko Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kudhihirisha Imani kwa Matendo Mema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
w10 5/1 uku. 31

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Jumba la Ufalme ni nini?

▪ Jumba la Ufalme ni nyumba ya ibada inayotumiwa na Mashahidi wa Yehova kwa ajili ya mikutano yao ya ibada. Kuna makumi ya maelfu ya Majumba ya Ufalme yanayotumiwa ulimwenguni pote. Kila juma, makutaniko zaidi ya 105,000 ya Mashahidi wa Yehova yanakutana katika majumba hayo.

Kila Jumba la Ufalme lina ukumbi ambamo hotuba na programu za kujifunza Biblia zinafanyiwa. Katika majumba mengi, wale wanaofundisha na kuongoza mikutano wanasimama kwenye jukwaa. Kwa kawaida, kuna viti kwa ajili ya watu kati ya 100 na 300. Jumba la Ufalme linaweza pia kuwa na madarasa ya ziada, ofisi, na maktaba ndogo ya vitabu vya Biblia na vya utafiti ambavyo vinaweza kutumiwa na mshiriki yeyote wa kutaniko kufanya utafiti.

Hata hivyo, katika Jumba la Ufalme, hutapata mifano au sanamu zozote za kidini ambazo zinapatikana katika makanisa ya dini zinazodai kuwa za Kikristo. Hakuna madhabahu, sanamu, au misalaba. Kwa nini? Kwa sababu Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba kutumia vitu kama hivyo kunapingana na amri ya Biblia ya ‘kukimbia ibada ya sanamu.’ (1 Wakorintho 10:14; Yohana 4:24) Makanisa mengi na mahekalu yana madoido na yamepambwa kupita kiasi. Kinyume na hilo, Majumba ya Ufalme yamejengwa kwa njia ya kiasi, nzuri na inayofaa. Mafundisho ya Biblia yanayotolewa katika jengo hilo ndiyo yanayokaziwa badala ya jengo lenyewe.

Kwa nini linaitwa Jumba la Ufalme? Kwa sababu mikutano ya watu wote inayofanywa katika Jumba la Ufalme inakazia hasa mafundisho ya Biblia na ujumbe wake wa msingi kuhusu “ufalme wa Mungu,” ambao ulikuwa ujumbe mkuu katika huduma ya Yesu. (Luka 4:43) Kwa hiyo, jina Jumba la Ufalme, ambalo lilitungwa katika miaka ya 1930, linaeleza kwa kufaa kusudi la majengo hayo, yaani, kuendeleza ibada ya kweli na kutumika kama kitovu cha kuhubiri “habari njema ya ufalme.” (Mathayo 24:14) Kwa hiyo, Majumba ya Ufalme hayatumiwi kwa ajili ya shughuli za kijamii au za kibiashara. Gharama za kujenga, kuendesha, na kutegemeza majumba hayo zinatokana tu na michango ya hiari. Hakuna sahani ya sadaka inayozungushwa katika mikutano. Badala yake, kuna sanduku ambalo limewekwa mahali fulani ili yeyote anayetaka atoe mchango.

Majumba ya Ufalme yanatumiwa kwa kusudi hilohilo ulimwenguni pote, lakini yanajengwa yakiwa na ukubwa na mitindo mbalimbali. Mtindo wa ujenzi unategemea vifaa vya ujenzi ambavyo vinapatikana katika eneo fulani, hali ya hewa, na hali ya kifedha ya Mashahidi wa Yehova wa eneo hilo. Majengo fulani yanajengwa kwa matofali, mbao, na mawe. Mengine hayana kuta au yana kuta za mianzi na yamefunikwa kwa paa la nyasi.

Sikuzote wageni wanakaribishwa kuhudhuria mikutano katika Jumba lolote la Ufalme. (Waebrania 10:25) Kuna mkutano wa watu wote unaofanywa kila juma, ambao unakazia habari fulani inayotegemea Biblia ambayo inawahusu washiriki wa kawaida wa kutaniko na wageni pia. Unakaribishwa kwenye Jumba la Ufalme la eneo lenu.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Malawi, Afrika

[Picha katika ukurasa wa 31]

Uingereza

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki