Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w11 10/1 uku. 3
  • Je, Wewe Umedanganywa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Umedanganywa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Matokeo Mabaya ya Uwongo wa Kwanza
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Petro na Anania Walidanganya—Tunajifunza Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kwa Nini Ni Rahisi Sana Kusema Uwongo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Kwa Nini Uwe Mnyoofu?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 10/1 uku. 3

Je, Wewe Umedanganywa?

NI MAMBO machache yanayoumiza zaidi kuliko kujua kwamba mtu fulani unayemwamini amekudanganya. Unaweza kukasirika, kuhisi umedharauliwa au hata kusalitiwa. Udanganyifu unavunja urafiki na ndoa; na unafanya watu wapoteze mamilioni ya pesa.

Basi, wazia jinsi ambavyo ungehisi kama ungejua kwamba umedanganywa kumhusu Mungu. Ikiwa unamwogopa Mungu, matokeo yanaweza kuwa mabaya kama ilivyokuwa kwa watu wafuatao ambao walikuwa wafuasi wa dini:

● “Nilihisi kwamba nimesalitiwa na kanisa.”—DEANNE.

● “Nilikasirika. Nilihisi kuwa nimedanganywa, yaani, nilihisi kuwa matumaini na malengo yangu hayana maana yoyote.”—LUIS.

Huenda hata usiwazie kwamba inawezekana kuwa umedanganywa kumhusu Mungu. Yaelekea mambo unayojua kumhusu uliyasikia kutoka kwa mtu unayemwamini na ambaye hawezi kamwe kukuumiza kimakusudi, kama vile mzazi wako, kasisi, pasta, au rafiki wa karibu. Huenda umeamini fundisho fulani katika maisha yako yote. Lakini je, hukubali kwamba fundisho fulani linaweza kuwa la uwongo ingawa watu wengi wanaliamini? Aliyekuwa rais wa Marekani, Franklin D. Roosevelt alitambua jambo hilo, kwa kuwa alisema: “Kurudia-rudia uwongo hakuufanyi kuwa ukweli.”

Unaweza kujua jinsi gani kwamba umedanganywa? Wakati mmoja Yesu alisali hivi kwa Mungu: “Neno lako ni kweli.” (Yohana 17:17) Ndiyo, Neno la Mungu, Biblia, linatusaidia kutofautisha ukweli na uwongo.

Acha tuone mafundisho matano ya uwongo kumhusu Mungu ambayo Biblia inafunua. Utaona jinsi ukweli unavyoweza kubadili maisha yako yawe bora.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki