Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 2/1 uku. 3
  • Musa Alikuwa Nani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Musa Alikuwa Nani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Musa—Jinsi Maisha Yake Yanavyokuhusu
    Amkeni!—2004
  • Yesu Kristo Alikuwaje Nabii Kama Musa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kichaka Kinachowaka Moto
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 2/1 uku. 3

KICHWA KIKUU: TUNAJIFUNZA NINI KUTOKA KWA MUSA?

Musa Alikuwa Nani?

[Picha katika ukurasa wa 3]

Wewe hukumbuka nini unaposikia jina Musa? Je, unafikiria . . .

  • mtoto ambaye mama yake alimficha ndani ya kikapu kwenye Mto Nile?

  • mvulana aliyelelewa na binti ya Farao katika maisha ya kifahari nchini Misri—ambaye hakusahau kwamba alikuwa Mwisraeli?

  • mwanamume aliyekuwa mchungaji huko Midiani kwa miaka 40?

  • mwanamume aliyeongea na Yehovaa mbele ya kichaka kilichokuwa kikiwaka moto?

  • mwanamume aliyemwambia kwa ujasiri mfalme wa Misri awaachilie Waisraeli kutoka utumwani?

  • mwanamume ambaye kwa mwongozo wa Mungu, alitangaza Mapigo Kumi dhidi ya Misri baada ya mfalme wa nchi hiyo kumdharau Mungu wa kweli?

  • mwanamume aliyewaongoza Waisraeli kutoka Misri?

  • mwanamume aliyetumiwa kutenganisha Bahari Nyekundu?

  • mwanamume aliyewapa Waisraeli Amri Kumi kutoka kwa Mungu?

MUSA alitimiza mambo hayo yote na mengine mengi. Si ajabu kwamba mwanamume huyo mwaminifu anaheshimiwa sana na Wakristo, Wayahudi, na Waislamu vilevile!

Bila shaka, Musa alikuwa nabii ambaye alionyesha “hofu kuu.” (Kumbukumbu la Torati 34:10-12) Aliruhusu Mungu amtumie katika njia kubwa. Ingawa hivyo, Musa alikuwa mwanadamu wa kawaida. Kama nabii Eliya, ambaye alionekana kando ya Musa kwenye maono wakati wa huduma ya Yesu duniani, Musa alikuwa mtu “mwenye hisia kama zetu.” (Yakobo 5:17; Mathayo 17:1-9) Musa alikabili matatizo kama tunayokabili, na alifanikiwa kuyashinda.

Je, ungependa kujua jinsi alivyofanikiwa? Acheni tuchunguze sifa tatu nzuri ambazo Musa alionyesha na yale tunayoweza kujifunza kutokana na mfano wake.

a Yehova ni jina la Mungu kama linavyofunuliwa kwenye Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki