Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 2/1 uku. 16
  • Je, Kweli Biblia Ni Neno la Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Kweli Biblia Ni Neno la Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Kweli Habari Njema Imetoka kwa Mungu?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Biblia​—Kitabu Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Je! Kweli Biblia Ilitoka kwa Mungu?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?
    Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 2/1 uku. 16
Maandishi ya Biblia kwenye kitabu cha kale cha kukunjwa

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Je, kweli Biblia ni Neno la Mungu?

Mtu angetazamia Neno la Mungu liwe la pekee, na ndivyo Biblia ilivyo. Nakala nyingi sana za Biblia zimechapishwa katika lugha nyingi. Hekima inayopatikana katika Biblia inaweza kubadili watu wawe na mwenendo mzuri.​—Soma 1 Wathesalonike 2:13; 2 Timotheo 3:16.

Tunajua kwamba Biblia ni Neno la Mungu kwa sababu inatabiri kwa usahihi wakati ujao. Hakuna mwanadamu anayeweza kufanya hivyo kwa uwezo wake mwenyewe. Kwa mfano, hebu fikiria unabii wa kitabu cha Isaya. Nakala ya kitabu hicho iliyoandikwa zaidi ya miaka mia moja kabla ya Yesu kuzaliwa ilipatikana kwenye pango lililo karibu na Bahari ya Chumvi. Unabii huo ulitabiri kwamba jiji la Babiloni lingeachwa ukiwa. Hilo lilitimia kwa mara ya kwanza miaka mingi baada ya Yesu kurudi mbinguni.​—Soma Isaya 13:19, 20; 2 Petro 1:20, 21.

Biblia iliandikwaje?

Biblia iliandikwa kwa kipindi cha karibu miaka 1,600. Iliandikwa na watu 40 hivi, na walifuata kichwa kimoja kikuu bila kupingana. Hilo liliwezekanaje? Mungu aliwaongoza.​—Soma 2 Samweli 23:2.

Nyakati nyingine Mungu alizungumza na waandikaji wa Biblia kupitia malaika, maono, au ndoto. Kwa kawaida, Mungu aliweka mawazo yake katika fikira za mwandikaji na kumruhusu achague maneno ambayo angetumia kutangaza ujumbe wa Mungu.​—Soma Ufunuo 1:1; 21:3-5.

Ili upate habari zaidi, soma sura ya 2 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kukipakua kwenyewww.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki