Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • T-30 kur. 1-4
  • Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?
  • Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?
  • Habari Zinazolingana
  • Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
    Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
  • Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?
    Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Je, Kuteseka Kutaisha?
    Je, Kuteseka Kutaisha?
Pata Habari Zaidi
Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?
T-30 kur. 1-4

Una Maoni Gani Kuhusu Biblia?

Je, ungesema ni . . .

  • kitabu cha hekima ya wanadamu?

  • kitabu cha hadithi na hekaya?

  • Neno la Mungu?

BIBLIA HUSEMA HIVI

“Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu.”—2 Timotheo 3:16, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

FAIDA ZA KUAMINI JAMBO HILO

Majibu yenye kuridhisha ya maswali muhimu zaidi maishani.—Methali 2:1-5.

Mwongozo wenye kutegemeka kwa ajili ya maisha ya kila siku.—Zaburi 119:105.

Tumaini hakika la wakati ujao.—Waroma 15:4.

Mwanamke na mwanamume wakisoma Biblia; familia yenye shangwe ikifurahia wakati pamoja
Mwanamke na mwanamume wakisoma Biblia; familia yenye shangwe ikifurahia wakati pamoja

JE, KWELI TUNAWEZA KUAMINI KILE AMBACHO BIBLIA HUSEMA?

Ndiyo, kwa angalau sababu tatu:

  • Upatano wenye kustaajabisha. Biblia iliandikwa kwa kipindi cha miaka 1,600 na watu tofauti-tofauti wapatao 40 hivi. Wengi wao hawakuwahi kuonana. Hata hivyo, kitabu chote kizima kina upatano, na kinazungumzia kichwa kimoja kikuu!

  • Waandikaji wanyoofu. Mara nyingi wanahistoria hawaelezi kuhusu kushindwa kwa mataifa yao. Kinyume na hilo, waandikaji wa Biblia waliandika kwa unyoofu kuhusu makosa yao wenyewe na ya taifa lao.—2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16; Zaburi 51:1-4.

  • Unabii unaotegemeka. Miaka 200 hivi mapema Biblia ilitabiri kuhusu kuharibiwa kwa jiji la kale la Babiloni. (Isaya 13:17-22) Biblia haikutaja tu jinsi ambavyo uharibifu huo wa Babiloni ungetokea bali pia jina la yule ambaye angeshinda jiji hilo!—Isaya 45:1-3.

    Pia, unabii mwingine mwingi wa Biblia ulitimizwa kwa ukamili kabisa. Bila shaka, tungetazamia kitabu kutoka kwa Mungu kiwe hivyo, sivyo?—2 Petro 1:21.

JAMBO LA KUFIKIRIA

Baba, mama, mwana, na binti
Baba, mama, mwana, na binti

Neno la Mungu linaweza kuboreshaje maisha yako?

Biblia inajibu swali hilo kwenye ISAYA 48:17, 18 na 2 TIMOTHEO 3:16, 17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki