Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 11/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Watakaoenda Mbinguni​—Je, Ni Watu Wote Wazuri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kutakuwa na Ufufuo!
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ufufuo Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 11/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Je, wafu wataishi tena?

Watu wakiwakaribisha wapendwa wao waliofufuliwa katika Paradiso

Tuna uhakika kwamba Muumba anaweza kuwafufua wafu

Yehova Mungu ndiye Chanzo cha uhai. (Zaburi 36:9) Hivyo, ni jambo linalopata na akili kukubali kwamba Mungu atawafufua wafu. Biblia inatuhakikishia kwamba atafanya hivyo wakati ujao. (Soma Matendo 24:15) Kwa nini atafanya hivyo?

Muumba wetu alikusudia wanadamu waishi milele duniani. (Mwanzo 1:31; 2:15-17) Kusudi lake kwa wanadamu halijabadilika. Anaumia sana anapoona tunateseka na kufa.—Soma Ayubu 14:1, 14, 15.

Watakaofufuliwa wataishi wapi?

Je, Mungu aliumba wanadamu waishi mbinguni? Hapana. Mungu aliumba malaika waishi mbinguni. Aliumba wanadamu waishi duniani. (Mwanzo 1:28; Ayubu 38:4, 7) Ukiwa na hilo akilini, fikiria miujiza ya ufufuo aliyofanya Yesu. Watu aliowafufua waliendelea kuishi duniani. Vivyo hivyo, wengi watakaofufuliwa wakati ujao wataishi duniani.—Soma Yohana 5:28, 29; 11:44.

Hata hivyo, Mungu amechagua watu wachache wanaofufuliwa na kuishi mbinguni wakiwa na miili ya roho. (Luka 12:32; 1 Wakorintho 15:49, 50) Wale wanaofufuliwa na kuishi mbinguni watatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo juu ya dunia.—Soma Ufunuo 5:9, 10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki