Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 1 uku. 10
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoka Kitabu Cha Kukunjwa hadi Kodeksi—Jinsi Ambavyo Biblia Ilifanywa Kuwa Kitabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Kitabu cha Kukunjwa cha Zamani “Chakunjuliwa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Kuhani Mkuu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 1 uku. 10

JE, WAJUA?

Katika nyakati za Biblia, vitabu vya kukunjwa vilitengenezwaje, na vilitumiwa jinsi gani?

Kitabu cha kukunjwa cha Biblia cha Esta kilichotengenezwa kwa ngozi, kilichopatikana katika karne ya 18 W.K.

Kitabu cha kukunjwa cha Biblia cha Esta kilichotengenezwa kwa ngozi, kilichopatikana katika karne ya 18 W.K.

Injili ya Luka inasema kwamba Yesu alifungua kitabu cha kukunjwa cha Isaya, akakisoma na kisha akakikunja. Mwishoni mwa Injili yake, Yohana alizungumzia pia kitabu cha kukunjwa aliposema kwamba hakuweza kuandika katika kitabu chake cha kukunjwa ishara zote alizofanya Yesu.—Luka 4:16-20; Yohana 20:30; 21:25.

Vitabu hivyo vya kukunjwa vilitengenezwa jinsi gani? Ili kuvitengeneza, ngozi au mafunjo yaliunganishwa pamoja. Kisha yalisokotwa kwenye fimbo na upande wenye maandishi unaviringishwa ndani. Maandishi yaliandikwa katika safu fupi zilizo wima kulingana na upana wa kitabu cha kukunjwa. Ikiwa kitabu cha kukunjwa kilikuwa kirefu, kingekuwa na fimbo ndogo au mbao mbili mwishoni mwa kitabu hicho ambazo msomaji angeshika upande mmoja ili kufungua na upande mwingine kufunga kitabu mpaka atakapopata maandishi anayotaka kusoma.

Kitabu The Anchor Bible Dictionary kinasema, “Kitabu cha kukunjwa kilikuwa na urefu [meta 10 hivi] wa kutoshea maandishi ya kitabu kizima na kuchukua nafasi ndogo kinapokunjwa.” Kwa mfano, inakadiriwa kwamba Injili ya Luka ilitoshea katika kitabu cha kukunjwa chenye urefu wa meta tisa na nusu. Katika baadhi ya vitabu vya kukunjwa, kingo za fimbo zilizokuwa mwishoni zilikatwa na kuchongwa vizuri kwa kutumia jiwe la kukwaruzia na kisha kutiwa rangi.

“Wakuu wa makuhani” wanaotajwa katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo walikuwa nani?

Wakuu wa makuhani wa Kiyahudi

Tangu kuanzishwa kwa ukuhani katika taifa la Israeli, cheo cha kuhani mkuu kilikuwa kwa ajili ya mtu mmoja, na angedumu katika cheo hicho mpaka atakapokufa. (Hesabu 35:25) Haruni alikuwa wa kwanza kutumikia katika cheo hicho. Mtoto wa kwanza wa kiume angerithi cheo cha kuhani mkuu kutoka kwa baba yake. (Kutoka 29:9) Wazao wengi wa Haruni walitumikia wakiwa makuhani, lakini ni wachache waliotumikia wakiwa makuhani wakuu.

Waisraeli walipotawaliwa na mataifa mengine, watawala wa mataifa hayo waliwaweka na kuwatoa makuhani wakuu Wayahudi kadiri walivyopenda. Hata hivyo, inaonekana kwamba sikuzote waliowekwa rasmi kutumikia katika cheo hicho walichaguliwa katika familia maalumu hasa kutoka katika ukoo wa Haruni. Maneno “wakuu wa makuhani” yalirejelea washiriki wakuu wa ukuhani. Huenda wakuu wa makuhani walitia ndani vichwa vya migawanyo 24 ya ukuhani; washiriki wa kudumu wa familia za kuhani mkuu; na makuhani wakuu wa zamani kama vile Anasi, ambaye aliondolewa katika cheo chake.​—1 Mambo ya Nyakati 24:1-19; Mathayo 2:4; Marko 8:31; Matendo 4:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki