Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp17 Na. 1 kur. 5-6
  • Ni Nini Kitakachofanya Nifurahie Kusoma Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Kitakachofanya Nifurahie Kusoma Biblia?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Sura na Mistari​—Ni Nani Aliiweka katika Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Kunufaika kwa Usomaji wa Biblia Kila Siku
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Dokezo la Kujifunza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Jinsi Unavyoweza Kunufaika Zaidi Unaposoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
wp17 Na. 1 kur. 5-6
Mwanamke akitumia vifaa vya kujifunzia anaposoma Biblia

HABARI KUU | JINSI YA KUFAIDIKA ZAIDI UNAPOSOMA BIBLIA

Ni Nini Kitakachofanya Nifurahie Kusoma Biblia?

Je, kusoma Biblia kunakuchosha au kunakufurahisha? Yote hayo yanategemea njia unayotumia katika usomaji wako. Acheni tuchunguze mambo unayoweza kufanya ili uongeze hamu ya kusoma na ufurahie zaidi.

Chagua tafsiri sahihi na yenye lugha inayoeleweka. Ikiwa unasoma habari fulani yenye maneno magumu au yasiyoeleweka, ni wazi kwamba hutafurahia usomaji huo. Kwa hiyo, chagua Biblia yenye lugha rahisi kueleweka ambayo itagusa moyo wako. Wakati huohuo, Biblia hiyo inapaswa kuwa tafsiri sahihi na inayotegemeka.a

Tumia teknolojia ya kisasa. Leo, Biblia inapatikana katika nakala zilizochapishwa, na pia katika mfumo wa vifaa vya elektroniki. Baadhi ya Biblia zinaweza kusomwa mtandaoni au kupakuliwa na kusomwa kupitia kompyuta, tablet, au simu. Baadhi ya programu za elektroniki zina mfumo unaoweza kukusaidia kulinganisha mistari ya Biblia inayohusu jambo unalosoma au hata kulinganisha tafsiri kadhaa. Ikiwa unapenda kusikiliza badala ya kusoma, Biblia pia inapatikana katika rekodi za kusikiliza kwa baadhi ya lugha. Wengi hupenda kusikiliza wanapotumia usafiri wa umma, wanapofua nguo, au wanapofanya kazi nyingine yoyote inayowaruhusu kusikiliza. Kwa nini usijaribu njia inayokufaa?

Tumia vifaa vya kujifunzia Biblia. Vifaa vya kujifunzia Biblia vinaweza kukusaidia ufaidike zaidi na usomaji wako. Kuna ramani za nchi zinazotajwa katika Biblia, ambazo zitakusaidia kujua mahali ambapo jambo unalosoma lilitukia na hivyo kukuwezesha kuwazia matukio. Makala mbalimbali, kama zile zinazopatikana kwenye gazeti hili au sehemu yenye kichwa “Mafundisho ya Biblia” iliyo kwenye tovuti ya jw.org/sw, zinaweza kukusaidia kuelewa maana ya mistari mbalimbali ya Biblia.

Tumia njia mbalimbali kusoma Biblia. Ikiwa kusoma Biblia kuanzia mwanzo hadi mwisho kunaoneka kuwa kunachosha, jaribu kusoma sehemu fulani za Biblia ambazo zinakuvutia. Pia, unaweza kutumia njia ya kusoma habari zinazohusu mtu mmoja-mmoja kati ya wale wanaotajwa katika Biblia. Mfano mmoja wa jinsi ya kufanya hivyo umeonyeshwa katika sanduku lenye kichwa, “Chimba Katika Biblia kwa Kuwajua Watu Wanaotajwa Humo.” Njia nyingine ni kusoma habari fulani hususa, moja baada ya nyingine, au kusoma kulingana na mfuatano wa matukio. Unaonaje ukitumia njia moja kati ya hizo?

a Wengi wameona kwamba Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ni sahihi, inategemeka, na ni rahisi kusoma. Biblia hiyo inachapishwa na Mashahidi wa Yehova, na inapatikana katika lugha zaidi ya 130. Unaweza kupakua nakala yako katika tovuti ya jw.org/sw au kupakua programu ya JW Library. Au wasiliana na Mashahidi wa Yehova wakuletee nakala ya Biblia.

CHIMBA KATIKA BIBLIA KWA KUWAJUA WATU WANAOTAJWA HUMO

Baadhi ya wanawake waaminifu

Abigaili

1 Samweli sura ya 25

Esta

Esta sura ya 2-5, 7-9

Hana

1 Samweli sura ya 1-2

Maria

(Mama ya Yesu) Mathayo sura ya 1-2; Luka sura ya 1-2; pia soma Yohana 2:1-12; Matendo 1:12-14; 2:1-4

Rahabu

Yoshua sura ya 2, 6; pia soma Waebrania 11:30, 31; Yakobo 2:24-26

Rebeka

Mwanzo sura ya 24-27

Sara

Mwanzo sura ya 17-18, 20-21, 23; pia soma Waebrania 11:11; 1 Petro 3:1-6

Baadhi ya wanaume washikamanifu

Abrahamu

Mwanzo sura ya 11-24; pia soma 25:1-11

Daudi

1 Samweli sura ya 16-30; 2 Samweli sura ya 1-24; 1 Wafalme sura ya 1-2

Yesu

Vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana

Musa

Kutoka sura ya 2-20, 24, 32-34; Hesabu sura ya 11-17, 20, 21, 27, 31; Kumbukumbu la Torati sura ya 34

Noa

Mwanzo sura ya 5-9

Paulo

Matendo sura ya 7-9, 13-28

Petro

Mathayo sura ya 4, 10, 14, 16-17, 26; Matendo sura ya 1-5, 8-12

VIFAA VYA KUJIFUNZIA BIBLIA VILIVYOANDALIWA NA MASHAHIDI WA YEHOVA

  • JW.ORG​—Tovuti hii ina vipengele vingi vya kujifunzia, kutia ndani sehemu ya “Majibu ya Maswali ya Biblia.” Pia, inaeleza jinsi ya kupakua programu ya JW Library

  • “Ona Nchi Nzuri”​—Broshua hii ina ramani na picha za maeneo yanayotajwa katika Biblia

  • Insight on the Scriptures​—Ni mabuku mawili ya ensaiklopidia ya Biblia yenye ufafanuzi wa kina kuhusu watu, maeneo, na lugha iliyotumiwa katika Biblia

  • “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”​—Kitabu hiki cha kujifunzia kinaeleza ni lini, wapi, na sababu ya kuandikwa kwa kila kitabu cha Biblia, pia, kinaeleza kwa ufupi ujumbe ulio katika kila kitabu

  • Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?​—Ni kitabu kidogo chenye utafiti wa kina unaothibitisha kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho

  • Biblia​—Ina Ujumbe Gani?​—Ni broshua yenye kurasa 32 inayoeleza kifupi habari kuu zilizo katika Biblia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki