Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 27, 2010. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 20 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Novemba 1 hadi Desemba 27, 2010.
1. Tunajifunza nini kutokana na maneno ya sifa ya waimbaji Walawi yaliyo kwenye 1 Mambo ya Nyakati 16:34? [w02 1/15 uku. 11 fu. 6-7]
2. Je, 1 Mambo ya Nyakati 22:8 inaonyesha kwamba Daudi alikosea kwa kupigana vita, kwa kuwa Yehova hakutaka amjengee nyumba? Eleza. [it-2-E uku. 987 fu. 1]
3. Mfalme Daudi alitaka mwana wake Sulemani awe na maoni gani kumhusu Mungu? (1 Nya. 28:9) [w08 10/15 uku. 7 fu. 18]
4. Kwa nini kiwakilishi cha ng’ombe-dume kilitumiwa katika ujenzi wa sehemu ya chini ya bahari ya kuyeyushwa? (2 Nya. 4:2-4) [w05 12/1 uku. 19 fu. 3; w98 6/15 uku. 16 fu. 17]
5. Je, sanduku la agano lilikuwa tu na yale mabamba mawili ya mawe, au lilikuwa pia na vitu vingine? (2 Nya. 5:10) [w06 1/15 uku. 31]
6. Sulemani alimaanisha nini alipomwomba Yehova asikilize sala za wote ‘waliosali kuelekea nyumba hii’? (2 Nya. 6:21, 32, 33) [it-1-E uku. 137 fu. 1]
7. Maneno “agano la chumvi” yanayopatikana katika 2 Mambo ya Nyakati 13:5 yanamaanisha nini? [w05 12/1 uku. 20 fu. 2; it-2-E uku. 842 fu. 7]
8. Tunaweza kutumia kanuni ya 2 Mambo ya Nyakati 17:9, 10 katika huduma yetu kwa njia gani? [w09 6/15 uku. 12 fu. 7]
9. Watu wa Mungu leo watatendaje kupatana na 2 Mambo ya Nyakati 20:17? [w03 6/1 uku. 21-22 fu. 14-17]
10. Tunaweza kujifunza nini kutokana na simulizi la Mfalme Uzia aliyetenda kwa majivuno? (2 Nya. 26:15-21) [w99 12/1 uku. 26 fu. 1-2]