Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Februari 27, 2012. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa, ili ndugu na dada waweze kufanya utafiti wakati wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.
1. Je, ni sawa kusema kwamba rehema ya Yehova hupunguza uzito wa haki yake? (Isa. 30:18) [Jan. 9, w07 9/15 uku. 24 fu. 13, 14]
2. Kisa cha Shebna kuachishwa kazi kama msimamizi-nyumba wa Hezekia kinatufunza nini? (Isa. 36:2, 3, 22) [Jan. 16, w07 1/15 uku. 8 fu. 6]
3. Andiko la Isaya 37:1, 14-20 linatufunza nini kuhusu mambo ya kufanya tunapopatwa na taabu? [Jan. 16, w07 1/15 uku. 9 fu. 1-2]
4. Mfano katika Isaya 40:31 unawatiaje moyo watumishi wa Yehova? [Jan. 23, w96 6/15 uku. 10-11]
5. Maneno ya Yehova katika Isaya 41:14 yanatutia moyo kuhusiana na shambulio gani linalokuja? [Jan. 23, ip-2 uku. 24 fu. 16]
6. Tunaweza kumwonyeshaje Yehova kwamba ‘tunafuatilia uadilifu’? (Isa. 51:1) [Feb. 6, ip-2 uku. 165 fu. 2]
7. Watu “wengi” wanaotajwa katika Isaya 53:12 ni akina nani, na mambo ambayo Yehova anawafanyia yanatufunza somo gani lenye kugusa moyo? [Feb. 13, ip-2 uku. 213 fu. 34]
8. Watumishi wa Yehova wamejionea jambo gani katika siku za mwisho ambalo linaelezwa kwa njia ya mfano katika Isaya 60:17? [Feb. 20, ip-2 uku. 316 fu. 22]
9. Ni nini maana ya “mwaka wa nia njema” ambao Yesu na wafuasi wake waliagizwa kutangaza? (Isa. 61:2) [Feb. 20, ip-2 uku. 324-325 fu. 7-8]
10. Ni sifa gani nzuri ya Yehova inayokaziwa katika andiko la Isaya 63:9? [Feb. 27, w03 7/1 uku. 19 fu. 22-23]