Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Februari 24, 2014.
1. Shetani alifanikiwa kumfanya Hawa akazie fikira nini, na Hawa alionyesha nini kwa kula tunda alilokatazwa? (Mwa. 3:6) [Jan. 6, w11 5/15 uku. 16-17 fu. 5]
2. Huenda Abeli alisitawishaje imani yenye nguvu, na matokeo yalikuwa nini? (Mwa. 4:4, 5; Ebr. 11:4) [Jan. 6, w13 1/1 uku. 12 fu. 3; uku. 14 fu. 4-5]
3. Wazazi wanaweza kuwalindaje watoto wao wasivutiwe na “watu wenye nguvu” na “wanaume wenye sifa” walio katika ulimwengu huu? (Mwa. 6:4) [Jan. 13, w13 4/1 uku. 13 fu. 2]
4. Tunajifunza mambo gani kutokana na simulizi la Loti na mke wake kama tunavyosoma kwenye Mwanzo 19:14-17, na 26? [Jan. 27, w03 1/1 uku. 16-17 fu. 20]
5. Abrahamu alionyeshaje imani katika ufufuo na ahadi ya Yehova kwamba uzao ungetokea kupitia Isaka? (Mwa. 22:1-18) [Feb. 3, w09 2/1 uku. 18 fu. 4]
6. Ni kweli gani muhimu tunazoweza kujifunza kutokana na unabii unaopatikana kwenye Mwanzo 25:23, ambao unasema kwamba “mkubwa atamtumikia mdogo”? [Feb. 10, w03 10/15 uku. 29 fu. 1]
7. Ndoto ya Yakobo iliyohusisha kile ambacho tafsiri nyingine huita ngazi ilimaanisha nini? (Mwa. 28:12, 13) [Feb. 10, w04 1/15 uku. 28 fu. 6]
8. Kwa nini Labani alihangaikia sana kupata terafimu iliyokuwa imeibiwa? (Mwa. 31:30-35) [Feb. 17, it-2 uku. 186 fu. 2]
9. Tunajifunza nini kutokana na jinsi malaika alivyomjibu Yakobo kwenye andiko la Mwanzo 32:29? [Feb. 24, w13 8/1 uku. 10]
10. Ni njia gani moja ya kuepuka matokeo mabaya kama yale yaliyompata Dina? (Mwa. 34:1, 2) [Feb. 24, w01 8/1 uku. 20-21]