Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 28, 2014.
Ni nini kilichomsaidia Yosefu akatae kufanya uasherati na mke wa Potifa? (Mwa. 39:7-12) [Mac. 3, w13 2/15 uku. 4 fu. 6; w07 10/15 uku. 23 fu. 16]
Yosefu ni mfano mzuri jinsi gani kwa wale wanaokabiliana na maafa na ukosefu wa haki? (Mwa. 41:14, 39, 40) [Mac. 10, w04 1/15 uku. 29 fu. 6; w04 6/1 uku. 20 fu. 4]
Ni nini kilichomsukuma Yosefu kuwaonyesha rehema ndugu zake? [Mac. 17, w99 1/1 uku. 30 fu. 6-7]
Kabila la Benyamini hatimaye lilitimiza jinsi gani unabii wa andiko la Mwanzo 49:27? [Mac. 24, w12 1/1 uku. 29, sanduku]
Andiko la Kutoka 3:7-10 linatufundisha nini kumhusu Yehova? [Mac. 31, w09 3/1 uku. 15 fu. 3-6]
Yehova alitendaje kulingana na maana moja ya jina lake katika siku za Musa? (Kut . 3:14, 15) [Mac. 31, w13 3/15 uku. 25-26 fu. 5-6]
Kulingana na andiko la Kutoka 7:1, Musa alifanywaje kuwa “kama Mungu kwa Farao”? [Apr. 7, w04 3/15 uku. 25 fu. 8]
Licha ya kushuhudia nguvu za Yehova za kuokoa alipowakomboa kutoka Misri, Waisraeli walionyesha mtazamo gani muda mfupi baadaye, nasi tunaweza kujifunza somo gani? (Kut. 14:30, 31) [Apr. 14, w12 3/15 uku. 26-27 fu. 8-10]
Kwa nini maneno ‘niliwachukua ninyi juu ya mabawa ya tai’ yanaonyesha jinsi Yehova alivyolitendea taifa changa la Israeli kwa upendo? (Kut. 19:4) [Apr. 28, w96 6/15 uku. 10 fu. 5–uku. 11 fu. 2]
Yehova huletaje ‘adhabu kwa sababu ya kosa la akina baba’ juu ya vizazi vijavyo? (Kut. 20:5) [Apr. 28, w04 3/15 uku. 27 fu. 1]