Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Juni 29, 2015. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.
Kwa nini njia ya Mikali ya kuzungumza na Daudi haikuwa sawa, na wenzi wa ndoa wanajifunza nini kutokana na kisa hicho? (2 Sam. 6:20-23) [Mei 11, w11 8/1 uku. 12 fu. 1]
Nabii Nathani alifanya nini aliporekebishwa na Yehova kwa kumwambia Daudi atimize tamaa yake ya kumjengea Yehova hekalu? (2 Sam. 7:2, 3) [Mei 11, w12 2/15 uku. 24 fu. 6-7]
Kwa nini Nathani alimsimulia Daudi mfano ulio katika 2 Samweli 12:1-7 badala ya kumweleza moja kwa moja kwamba alikuwa amefanya dhambi nzito? Na kisa hicho kinaweza kutusaidiaje kuwa walimu wazuri zaidi? [Mei 18, w12 2/15 uku. 24 fu. 2-3]
Kwa nini Absalomu aliweza kuwapumbaza Waisraeli, na tunawezaje kujilinda dhidi ya watu walio kama Absalomu leo? (2 Sam. 15:6) [Mei 25, w12 7/15 uku. 13 fu. 7]
Daudi alipokuwa na uhitaji mkubwa, Yehova alimwandaliaje mahitaji yake, na tunajifunza nini kutokana na hilo? (2 Sam. 17:27-29) [Juni 1, w08 9/15 uku. 6 fu. 15-16]
Tunaweza kunufaikaje na mfano wa Daudi wa jinsi alivyoshughulika na mwanamume fulani asiye Mwisraeli aliyeitwa Itai? (2 Sam. 18:2) [Juni 1, w09 5/15 uku. 27 fu. 7]
Watu wenye umri mkubwa kutanikoni wanawezaje kuiga mfano wa Barzilai? (2 Sam. 19:33-35) [Juni 8, w07 7/15 uku. 15 fu. 1-2]
Maneno ya Daudi kuhusu ushikamanifu yanawapa watumishi wa Yehova leo uhakikisho gani? (2 Sam. 22:26) [Juni 15, w10 6/1 uku. 26 fu. 6-7]
Nathani alionyeshaje ushikamanifu kwa Mungu, nasi tunawezaje kuiga sifa hiyo leo? (1 Fal. 1:11-14) [Juni 22, w12 2/15 uku. 25 fu. 1, 4-5]
Ni katika sehemu gani za maisha ambazo huenda mtumishi wa Mungu akatoa visingizio vya kutotii sheria za Mungu kama alivyofanya Sulemani? (1 Fal. 3:1) [Juni 29, w11 12/15 uku. 10-11 fu. 12-14]