MAISHA YA MKRISTO
Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Watie Moyo Wanaopendezwa Wahudhurie Mikutano
KWA NINI NI MUHIMU: Kuhudhuria mikutano kunatupatia nafasi ya ‘kumwimbia Yehova’ na ‘kumsifu.’ (Zb 149:1) Tunapokuwa mikutanoni, tunafundishwa kufanya mapenzi ya Mungu. (Zb 143:10) Kwa kawaida, wanafunzi wa Biblia na watu wanaopendezwa hufanya maendeleo zaidi wanapohudhuria mikutano.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Waalike mapema iwezekanavyo. Huhitaji kungoja hadi funzo la Biblia lianzishwe.—Ufu 22:17
Mweleze mtu anayependezwa mambo atakayoona na yatakayozungumziwa kwenye mkutano unaofuata. Vifaa vifuatavyo vinaweza kukusaidia kufanya hivyo: mwaliko wa kuhudhuria mikutano, video Ni Nini Hutendeka Katika Jumba la Ufalme?, na somo la 5 na la 7 kwenye broshua Mapenzi ya Yehova
Uwe tayari kumsaidia. Je, anayependezwa anahitaji usafiri au msaada wa kuchagua mavazi yanayofaa? Keti naye mkutanoni, na ushiriki naye machapisho yako. Mtambulishe kwa wengine