Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp22 Na. 1 kur. 12-13
  • 4 | Shinda Chuki kwa Msaada wa Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 4 | Shinda Chuki kwa Msaada wa Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inasema:
  • Inamaanisha Nini?
  • Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:
  • Biblia Inabadili Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Jinsi ya Kushinda Chuki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
  • Tunaweza Kushinda Chuki!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
  • Kwa Nini Kuna Chuki Sana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2022
wp22 Na. 1 kur. 12-13
Watu wakitembea kuelekea Biblia kubwa iliyofunguliwa ambayo inatoa mwangaza. Vivuli vyao vinawakilisha mtazamo wa chuki waliokuwa nao zamani.

JINSI YA KUSHINDA CHUKI

4 | Shinda Chuki kwa Msaada wa Mungu

Biblia Inasema:

“Tunda la roho ni upendo, shangwe, amani, subira, fadhili, wema, imani, upole, kujizuia.”​—WAGALATIA 5:22, 23.

Inamaanisha Nini?

Inawezekana kushinda chuki kwa msaada wa Mungu. Roho yake takatifu inaweza kutusaidia kusitawisha sifa ambazo hatungeweza kuzisitawisha kwa uwezo wetu wenyewe. Hivyo, badala ya kujaribu kushinda chuki kwa nguvu zetu wenyewe, itakuwa vizuri ikiwa tutategemea msaada wa Mungu. Tukifanya hivyo, tutakuwa kama mtume Paulo, aliyeandika hivi: “Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yule anayenipa nguvu.” (Wafilipi 4:13) Kwa kweli, tutaweza kusema hivi: “Msaada wangu hutoka kwa Yehova.”​—Zaburi 121:2.

Jinsi ya Kutumia Kanuni Hii:

“Kwa msaada wa Yehova, nimefaulu kushinda hasira yangu kali na sasa naishi kwa amani.”​—WALDO

Sali kwa Yehova, ukimwomba kwa unyoofu akupe roho takatifu. (Luka 11:13) Mwombe akusaidie uonyeshe sifa nzuri maishani mwako. Jifunze mambo ambayo Biblia inasema kuhusu sifa zitakazokusaidia kushinda chuki, kama vile upendo, amani, subira, na kujizuia. Tafuta fursa za kusitawisha sifa hizo maishani mwako. Na shirikiana na wale wanaojitahidi kusitawisha sifa hizo. Watu hao wanaweza ‘kuchochea ndani yako upendo na matendo mazuri.’​—Waebrania 10:24.

Simulizi la Maisha​—WALDO

Alishinda Chuki na Jeuri

Waldo.

Waldo alilelewa katika mazingira yaliyomfanya awe na chuki. Anasema hivi: “Nilihusika katika mapigano na wauzaji wa dawa za kulevya . . . Pindi moja, niliponea chupuchupu baada ya kudungwa kisu na mtu aliyekodiwa na genge la wahalifu ili aniue.”

Waldo hakufurahia mke wake alipoanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Anasema: “Niliwachukia Mashahidi, na mara nyingi niliwatukana kwa sauti. Lakini sikuzote walikuwa wapole.”

Hatimaye, Waldo alianza kujifunza Biblia. Anasema hivi: “Ilikuwa vigumu kufuata mambo niliyokuwa nikijifunza. Niliamini kwamba singeweza kamwe kuidhibiti hasira yangu kali.” Hata hivyo, jambo moja alilojifunza katika Biblia lilimsaidia sana.

Waldo anasema: “Siku moja, Alejandro, ambaye alikuwa akinifundisha Biblia, aliniambia nisome Wagalatia 5:22, 23. . . . Alejandro aliniambia ili nisitawishe sifa hizo, sikupaswa kutegemea uwezo wangu, bali roho takatifu ya Mungu. Hilo lilibadili kabisa maoni yangu!”

Kwa msaada wa Mungu, Waldo amefaulu kushinda chuki maishani mwake. Anasema: “Watu wa ukoo na rafiki zangu wa zamani hawaamini kwamba nimebadilika. Kwa msaada wa Yehova, nimefaulu kushinda hasira yangu kali na sasa naishi kwa amani.”

Ili ujue mengi zaidi kuhusu simulizi la Waldo, soma gazeti la Mnara wa Mlinzi Oktoba 1, 2013, ukurasa wa 12-13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki