Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp23 Na. 1 kur. 10-11
  • 3 | Jinsi Mifano ya Biblia Inavyoweza Kutusaidia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 3 | Jinsi Mifano ya Biblia Inavyoweza Kutusaidia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2023
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Inamaanisha nini?
  • Hilo Linaweza Kutusaidiaje?
  • Kuishi na Ugonjwa wa Kihisia
    Amkeni!—2004
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2004
  • Wengine Wanaweza Kusaidiaje?
    Amkeni!—2004
  • Tumaini kwa Wanaougua
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2023
wp23 Na. 1 kur. 10-11
Nabii Musa akiwa na mahangaiko, akiangalia mbinguni na kusali kwa Mungu.

3 | Jinsi Mifano ya Biblia Inavyoweza Kutusaidia

BIBLIA INATAJA . . . Wanaume na wanawake waaminifu waliokuwa na “hisia kama zetu.”​—YAKOBO 5:17.

Inamaanisha nini?

Biblia ina masimulizi halisi ya wanaume na wanawake waliokabili hisia mbalimbali. Tunaposoma Biblia tunaweza kujifunza kuhusu mtu ambaye alikuwa na hisia kama zetu.

Hilo Linaweza Kutusaidiaje?

Sote tungependa wengine watuelewe. Lakini tunahisi hivyo hasa ikiwa tunakabili matatizo ya akili. Tunaposoma Biblia tunajifunza kuhusu watu ambao waliwaza na kuhisi kama sisi. Mwishowe tunatambua kwamba wengine waliteseka kama sisi na hivyo hatutahisi upweke.

  • Biblia ina masimulizi mengi ya watu waliokuwa na wasiwasi na mahangaiko. Je, umewahi kuwaza, ‘Nimechoshwa kabisa na hii hali’? Musa, Eliya na Daudi walihisi hivyo pia.​—Hesabu 11:14; 1 Wafalme 19:4; Zaburi 55:4.

  • Biblia inasimulia kuhusu mwanamke anayeitwa Hana aliyekuwa na “uchungu mwingi sana” kwa sababu hakuweza kupata watoto na alidhihakiwa sana na mke mwenzake.​—1 Samweli 1:6, 10.

  • Biblia inasimulia kuhusu mwanamume anayeitwa Ayubu ambaye alikuwa na hisia kama zetu. Ingawa alikuwa na imani yenye nguvu, aliteseka sana kihisia na wakati fulani alisema: “Ninachukia maisha yangu; sitaki kuendelea kuishi.”​—Ayubu 7:16.

Sisi pia tunaweza kupata nguvu ya kukabiliana na mahangaiko yetu, kwa kujifunza jinsi watu hawa wanaotajwa katika Biblia walivyofanikiwa kushughulikia njia yao mbaya ya kufikiri.

Jinsi Biblia Inavyomsaidia Kevin

Jinsi Ugonjwa wa Kubadilika Hisia Unavyoniathiri

Kevin akinywa kahawa na marafiki zake.

“Niligundulika nina ugonjwa wa kubadilika hisia (bipolar disorder) nilipokaribia miaka 50. Kuna pindi ambazo ninahisi ninaweza kushughulikia tatizo lolote maishani mwangu. Lakini wakati mwingine ninahisi hakuna sababu ya kuishi.”

Jinsi Biblia Inavyonisaidia

“Mtu mmoja anayetajwa katika Biblia ambaye alihisi kama mimi ni mtume Petro. Alifanya makosa yaliyomfanya ahisi hana thamani. Petro alitafuta msaada wa marafiki waliomjali badala ya kuendelea kufikiria mambo hayo. Hali yangu ya kubadilika hisia inapokuwa mbaya, ninalemewa na makosa yangu na kuhisi sina thamani. Kama Petro, nimejifunza kuwa karibu na marafiki ambao wananisaidia nisikate tamaa maishani.

“Mfalme Daudi ni mtu mwingine anayetajwa katika Biblia ambaye ananifariji sana. Mara nyingi alihangaishwa na hali yake na alijutia makosa aliyofanya zamani. Ninaelewa hisia zake kwa sababu wakati mwingine mimi hutenda au kusema mambo ambayo ninajutia baadaye. Mimi hufarijiwa sana na mambo aliyosema Daudi katika Zaburi 51. Daudi alisema hivi kwenye mstari wa 3: ‘Ninajua vizuri makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yangu daima.’ Hivyo ndivyo ninavyohisi wakati ninaposhuka moyo sana, siwezi kufikiria mawazo mazuri kujihusu. Lakini pia ninaelewa maneno ya Daudi katika mstari wa 10 aliposema: ‘Umba moyo safi ndani yangu, Ee Mungu, na uweke roho mpya ndani yangu, iliyo imara.’ Mimi pia husali kwa Mungu ili anisaidie niwe na hisia nzuri kujihusu. Mwishowe mstari wa 17 unanifariji. Unasema: ‘Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaukataa.’ Mstari huu unanihakikishia kwamba Mungu ananipenda.

“Tumaini langu la wakati ujao linaimarika kwa kukazia fikira mifano ya Biblia na mambo ambayo Mungu ananifanyia sasa. Ahadi zinazotajwa katika Biblia zimekuwa halisi kwangu na zinanisaidia kuvumilia.”

Kwa Msaada Zaidi:

Soma makala yenye kichwa “Kuishi na Ugonjwa wa Kihisia,” kwenye gazeti la Amkeni! la Januari 8, 2004, linalopatikana kwenye jw.org/sw.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki