Ni nini njo inaletaka furaa mu famiye?
Unawaza ni . . .
mapendo?
makuta?
ao kintu kingine?
SHIKIA VILE BIBLE INASEMA
“Bale beko na furaa ni bale beko nashikia Sauti ya Mungu na kuitumikisha!”—Luka 11:28, Tradiksion ya dunia ya sasa.
KUYUWA VILE KUTAKUSAIDIA JE?
Utapata mapendo ya bya kweri.—Waefeso 5:28, 29.
Batakueshimia sana.—Waefeso 5:33.
Utekala na salama.—Marko 10:6-9.
ILE MAMBO BIBLE INASEMA NI YA BYA KWERI TU?
Ni ya bya kweri, nju:
Mungu njo arianzisha famiye. Bible inasema kama Jeova Mungu njo “arifanya ma famiye yote . . . ikuyeko.” (Waefeso 3:14, 15) Mu maneno ingine ni kusema, kama famiye ikwako, ni nju Mungu aripenda ikuyeko. Njo kusema nini?
Waza kiloko: Kama uko nakurya byakurya bya butamu, na unapenda kuyuwa vile baribipika, utauliza nani? Kusema tu bya kweri, utauliza ule aribipika.
Ni pamoya na famiye ile iko na furaa. Kama unapenda kuyuwa kile kinaletaka furaa mu famiye, itakuwa muzuri umulize Jeova, nju yeye njo arianzishaka ma famiye.—Mwanzo 2:18-24.
Mungu anakuangaikiaka. Itakuwa muzuri kama ma famiye inatafuta mashauri ya Jeova ile iko mu Sauti yake. Nju ya nini? ‘Nju anatuangaikiaka.’ (1 Petro 5:6, 7) Jeova anapenda tukuwe na maisha ya muzuri sana, na mashauri yake inaletaka tu baraka kama tunaifwata!—Mezali 3:5, 6; Isaya 48:17, 18.
WAZA MBELE
Unezi kufanya nini nju ukuwe bwana muzuri, bibi muzuri, ao muzazi muzuri?
Bible inajibu ile ulizo mu WAEFESO 5:1, 2 na mu WAKOLOSAI 3:18-21.