Ufalme wa Mungu njo nini?
Unawaza ni . . .
mapendo ya Mungu mu roo ya bantu?
ni ndoto tu?
ao ni guvernema ile iko ku mbingu?
SHIKIA VILE BIBLE INASEMA
“Mungu wa ku mbingu ataleta ufalme ile abatalabishaka ata shiku moya.”—Danieli 2:44, Tradiksion ya dunia ya sasa.
“Banatupachia mutoto na guvernema itakuwa pa mabeka yake.”—Isaya 9:6; mafasirio ya chini.
KUYUWA VILE KUTAKUSAIDIA JE?
Kutakusaidia uyuwe kama kuko guvernema ile itakuletea mambo ya muzuri.—Isaya 48:17, 18.
Kutakusaidia uyuwe kama mu dunia ya sasa ile iko nakuya, utakuwa na maisha ya muzuri sana na ya furaa.—Ufunuo 21:3, 4.
ILE MAMBO BIBLE INASEMA NI YA BYA KWERI TU?
Ni ya bya kweri, nju:
Yesu arioneshaka mambo ile ufalme wa Mungu itafanya. Yesu arifundishaka banafunzi yake baombe ufalme wa Mungu ikuye na mapenzi yake ifanshike apa pa dunia. (Matayo 6:9, 10) Yesu arioneshaka vile Mungu atajibu ile sala.
Pale arikuwa pa dunia, Yesu aripachiaka byakurya bale barikuwaka na njala, ariponeshaka ba malari, na arifufulaka bafu! (Matayo 15:29-38; Yohana 11:38-44) Vile Yesu njo atakuwa mufalme wa ufalme wa Mungu, mambo ile arifanyaka pale arikuwa pa dunia, inatonesha mambo ya mingi sana ile atafanya pale ufalme wa Mungu itanza kutawala pa dunia.—Ufunuo 11:15.
Mambo ile tuko naona mu dunia leo inaonesha asema ufalme wa Mungu iko karibu. Yesu aritabiri kama mbele ufalme wa Mungu ikuye kuleta amani, mu iyi dunia muripashwa mbele kuyala mvita, njala, na ma tramblema de tere.—Matayo 24:3, 7.
Ile njo mambo tuko naona leo. Njo maana tunapashwa kuwa sire kama ufalme wa Mungu iko karibu kuya kwisha mateso yote.
WAZA MBELE
Maisha itakuwa je pale ufalme wa Mungu itanza kutawala?
Bible inajibu ile ulizo mu ZABURI 37:29 na mu ISAYA 65:21-23.