-
Hesabu 4:15Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
15 “Haruni na wana wake wanapaswa kumaliza kufunika mahali patakatifu+ na vifaa vyote vya mahali patakatifu wakati kambi itaondoka. Kisha wana wa Kohati wataingia ili kuvibeba,+ lakini hawapaswe kugusa mahali patakatifu ili wasikufe.+ Vitu hivyo ni daraka la* wana wa Kohati kuhusiana na hema ya mukutano.
-
-
Hesabu 4:20Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
20 Hawapaswe kuingia na kuona vitu vitakatifu hata kwa wakati kidogo, ili wasikufe.”+
-
-
Hesabu 16:39, 40Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
39 Kwa hiyo Eleazari kuhani akakamata vyetezo vya shaba vyenye vililetwa na wale wenye walikuwa wameteketezwa kwa moto, na akavipiga-piga ili vifunike mazabahu, 40 kama vile Yehova alikuwa amemuambia kupitia Musa. Hilo lilikumbusha Waisraeli kwamba mutu yeyote mwenye haruhusiwe* mwenye haiko muzao wa Haruni hapaswe kukaribia ili kuchoma uvumba mbele ya Yehova+ na kwamba mutu yeyote hapaswe kuwa kama Kora na wale wenye walimuunga mukono.+
-