Wimbo wa Sulemani
3 “Kama muti wa tofaa kati ya miti ya pori,
Ni vile mupenzi wangu iko* kati ya wana.
Ninatamani sana kukaa katika kivuli chake,
Na tunda lake ni tamu katika kinywa changu.
4 Aliniingiza katika nyumba ya karamu,*
Na bendera yake juu yangu ilikuwa upendo.
5 Uniburudishe kwa keki za zabibu;+
Unitegemeze kwa matunda ya matofaa,
Kwa maana ninagonjwa ugonjwa wa mapenzi.
Musijaribu kuamusha ao kuchochea upendo ndani yangu mupaka wakati huo wenyewe utataka.+
8 Sauti ya mupendwa wangu!
Angalia! Anakuja,
Akipanda milima, na kuruka vilima.
9 Mupenzi wangu ni kama swala, kama paa mudogo.+
Yeye ule, amesimama nyuma ya ukuta wetu,
Anachungulia katika madirisha,
Anaangalia kupitia kayungio za madirisha.
10 Mupenzi wangu anasema, ananiambia:
‘Simama, mupenzi wangu,
Muzuri wangu, kuja tuende zetu.
11 Angalia! Kipindi cha baridi* kimepita.
Mvua imeisha na imeenda zake.
12 Maua yametokea katika inchi,+
Wakati wa kukata matawi umefika,+
Na wimbo wa njiwa-tetere umesikiwa katika inchi yetu.+
13 Muti wa tini unakomalisha tini za kwanza-kwanza;+
Mizabibu imetoa maua na inatoa harufu ya muzuri.
Simama, mupenzi wangu, na ukuje.
Muzuri wangu, kuja tuende zetu.
14 Ee njiwa wangu, katika mapango ya miamba,+
Sehemu za ndani kabisa za muteremuko mukali,
Acha nikuone na kusikia sauti yako,+
Kwa maana sauti yako ni yenye kupendeza na sura yako ni yenye kuvutia.’”+
15 “Mutukamatie mbweha,
Mbweha wadogo wenye wanaharibu mashamba ya mizabibu,
Kwa maana mashamba yetu ya mizabibu yametoa maua.”
16 “Mupenzi wangu ni wangu na mimi ni wake.+