Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • nwt Mwanzo 1:1-50:26
  • Mwanzo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwanzo
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Mwanzo

MWANZO

1 Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.+

2 Sasa dunia haikukuwa na umbo na ilikuwa bila kitu, na giza lilikuwa juu ya uso wa maji yenye kuenda chini sana;*+ na nguvu ya utendaji ya Mungu*+ ilikuwa inaenda huku na huku juu ya uso wa maji.+

3 Na Mungu akasema: “Kukuwe mwangaza.” Kisha kukakuwa mwangaza.+ 4 Kisha Mungu akaona kama mwangaza ulikuwa muzuri, na Mungu akaanza kutenganisha mwangaza na giza. 5 Mungu akaita mwangaza Muchana, lakini giza akaliita Usiku.+ Na ikakuwa mangaribi na ikakuwa asubui, siku ya kwanza.

6 Kisha Mungu akasema: “Anga+ likuwe katikati ya maji, na kukuwe mugawanyiko kati ya maji na maji.”+ 7 Kisha Mungu akafanya anga na kutenganisha maji yenye kuwa chini ya anga na maji yenye kuwa juu ya anga.+ Na ikakuwa vile. 8 Mungu akaita anga hilo Mbingu. Ikakuwa mangaribi na ikakuwa asubui, siku ya pili.

9 Kisha Mungu akasema: “Maji yenye kuwa chini ya mbingu yakusanywe nafasi moja, na inchi kavu itokee.”+ Na ikakuwa vile. 10 Mungu akaita hiyo inchi kavu Dunia,+ lakini mukusanyo wa maji akauita Bahari.+ Na Mungu akaona kwamba ilikuwa muzuri.+ 11 Kisha Mungu akasema: “Dunia ioteshe majani, mimea yenye kuzaa mbegu na miti ya matunda kulingana na aina zake, yenye kuzaa matunda yenye mbegu juu ya dunia.” Na ikakuwa vile. 12 Na dunia ikaanza kutokeza majani, mimea yenye kuzaa mbegu+ na miti yenye kuzaa matunda yenye mbegu, kulingana na aina zake. Kisha Mungu akaona kwamba ilikuwa muzuri. 13 Na ikakuwa mangaribi na ikakuwa asubui, siku ya tatu (3).

14 Kisha Mungu akasema: “Kukuwe vitu vya kutoa mwangaza+ katika anga la mbingu ili vitenganishe muchana na usiku,+ na vitakuwa alama ya vipindi na siku na miaka.+ 15 Na vitakuwa vitu vya kutoa mwangaza katika anga la mbingu ili kuangazia dunia.” Na ikakuwa vile. 16 Na Mungu akafanya vitu mbili vikubwa vya kutoa mwangaza, kitu kikubwa cha kutoa mwangaza ili kutawala muchana+ na kitu kidogo cha kutoa mwangaza ili kutawala usiku, na pia nyota.+ 17 Basi Mungu akaviweka katika anga la mbingu ili viangazie dunia 18 na kutawala muchana na usiku na kutenganisha mwangaza na giza.+ Kisha Mungu akaona kwamba ilikuwa muzuri. 19 Na ikakuwa mangaribi na ikakuwa asubui, siku ya ine (4).

20 Kisha Mungu akasema: “Maji yajae viumbe vyenye* uzima, na viumbe vyenye kuruka viruke juu ya dunia kwenye anga la mbingu.”+ 21 Na Mungu akaumba viumbe vikubwa vya bahari na viumbe vyote vyenye uzima vyenye kutembea na kujaa katika maji kulingana na aina yavyo* na kila kiumbe chenye kuruka na chenye mabawa kulingana na aina yacho. Na Mungu akaona kwamba ilikuwa muzuri. 22 Basi Mungu akabariki viumbe hivyo, na kusema: “Muzae na mukuwe wengi na mujaze maji ya bahari,+ na viumbe vyenye kuruka vikuwe vingi katika dunia.” 23 Na ikakuwa mangaribi na ikakuwa asubui, siku ya tano (5).

24 Kisha Mungu akasema: “Dunia itokeze viumbe vyenye uzima kulingana na aina yavyo,* wanyama wa kufugwa na wanyama wenye kutambaa* na wanyama wa pori kulingana na aina yao.”+ Na ikakuwa vile. 25 Na Mungu akafanya wanyama wa pori kulingana na aina yao na wanyama wa kufugwa kulingana na aina yao na wanyama wote wenye kutambaa kulingana na aina yao. Na Mungu akaona kwamba ilikuwa muzuri.

26 Kisha Mungu akasema: “Tufanye+ mutu kwa mufano wetu,+ kwa sura yetu,+ na watawale samaki wa bahari na viumbe vyenye kuruka vya mbinguni na wanyama wa kufugwa na dunia yote na kila munyama mwenye kutambaa juu ya dunia.”+ 27 Na Mungu akaumba mutu kwa mufano wake, kwa mufano wa Mungu alimuumba; mwanaume na mwanamuke aliwaumba.+ 28 Zaidi ya hiyo, Mungu akawabariki, na Mungu akawaambia: “Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia+ na kuitawala,+ na mutawale+ samaki wa bahari na viumbe vyenye kuruka vya mbinguni na kila kiumbe chenye uzima chenye kutembea juu ya dunia.”

29 Kisha Mungu akasema: “Angalia, nimewapatia kila mumea wenye kuzaa mbegu wenye kuwa juu ya dunia yote na kila muti wenye kuzaa matunda yenye mbegu. Vikuwe chakula kwa ajili yenu.+ 30 Na nimetoa majani yote ya mubichi kuwa chakula+ kwa kila munyama wa pori na kwa kila kiumbe chenye kuruka cha mbinguni na kwa kila kiumbe chenye kutembea juu ya dunia chenye kuwa na uzima* ndani yake.” Na ikakuwa vile.

31 Kisha mambo hayo Mungu akaona kila kitu chenye alikuwa amefanya, na angalia! kilikuwa kizuri sana.+ Na ikakuwa mangaribi na ikakuwa asubui, siku ya sita (6).

2 Basi mbingu na dunia pamoja na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake* vikamalizika kufanywa.+ 2 Na kufikia siku ya saba (7), Mungu alikuwa amemaliza kazi yenye alikuwa amefanya, na akaanza kupumuzika siku ya saba kisha kazi yake yote yenye alikuwa amefanya.+ 3 Na Mungu akabariki siku ya saba (7) na kuitangaza kuwa takatifu, kwa kuwa katika siku hiyo Mungu amekuwa akipumuzika kutokana na kazi yote yenye aliumba, yote yenye alikusudia kufanya.

4 Hii ndiyo historia ya mbingu na dunia wakati ziliumbwa, katika siku yenye Yehova* Mungu alifanya dunia na mbingu.+

5 Dunia ilikuwa haijakuwa na muti mudogo wa shamba na hapakukuwa majani yenye ilikuwa imeanza kuota, kwa sababu Yehova Mungu hakukuwa amefanya mvua inyeshe juu ya dunia na hapakukuwa mutu wa kulima udongo. 6 Lakini kunguku ilikuwa inapanda kutoka juu ya dunia, na kumwanga maji juu ya uso wa inchi.*

7 Na Yehova Mungu akaumba mwanadamu kutoka katika mavumbi+ ya udongo na akapuliza katika matundu ya pua yake pumuzi ya uzima,+ na mwanadamu akakuwa mutu mwenye uzima.*+ 8 Zaidi ya hiyo, Yehova Mungu akapanda bustani katika Edeni,+ kuelekea upande wa mashariki; na akatia katika bustani hiyo ule mutu mwenye alikuwa amefanya.+ 9 Kwa hiyo Yehova Mungu akaotesha juu ya udongo kila muti wenye kupendeza macho na wenye kufaa kwa chakula na pia muti wa uzima+ katikati ya bustani na muti wa ujuzi wa mema na mabaya.+

10 Sasa kulikuwa muto wenye ulikuwa unateremuka kutoka katika Edeni ili kumwanga maji ndani ya bustani, na kutoka pale uligawanyika na kuwa mito ine (4).* 11 Jina la muto wa kwanza ni Pishoni; muto huo ndio unazunguka inchi yote ya Havila, kwenye kuko zahabu. 12 Zahabu ya inchi hiyo ni ya muzuri. Pia kuko ulimbo* wa bedola na jiwe la shohamu. 13 Jina la muto wa pili ni Gihoni; muto huo ndio unazunguka inchi yote ya Kushi. 14 Jina la muto wa tatu (3) ni Hidekeli;*+ muto huo ndio unaenda upande wa mashariki wa Ashuru.+ Na muto wa ine (4) ni Efrati.+

15 Yehova Mungu akachukua ule mutu na kumutia katika bustani ya Edeni ili ailime na kuitunza.+ 16 Pia, Yehova Mungu akamupatia ule mutu amri hii: “Unaweza kula matunda ya kila muti wa bustani mupaka ushibe.+ 17 Lakini kuhusu matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya, usikule, kwa maana siku yenye utakula matunda yake, hakika utakufa.”+

18 Kisha Yehova Mungu akasema: “Haiko muzuri mwanaume huyu aendelee kuwa peke yake. Nitamufanyia musaidizi, akuwe kikamilisho chake.”+ 19 Sasa Yehova Mungu alikuwa amefanya kutoka katika udongo kila munyama wa pori na kila kiumbe chenye kuruka cha mbinguni, na akaanza kuwaleta kwa huyo mutu kusudi aone ni jina gani atapatia kila kiumbe; na jina lenye huyo mutu alikuwa anapatia kila kiumbe chenye uzima,* ni hilo lilikuwa jina lake.+ 20 Kwa hiyo, ule mutu akapatia majina wanyama wote wa kufugwa na viumbe vyote vyenye kuruka vya mbinguni na kila munyama wa pori, lakini kwa ajili ya huyo mwanaume hapakukuwa musaidizi wa kuwa kikamilisho chake. 21 Kwa hiyo Yehova Mungu akamufanya huyo mwanaume alale usingizi muzito, na wakati alikuwa amelala, Mungu akakamata ubavu wake mumoja na akafunika nyama mahali pake. 22 Na Yehova Mungu akamufanya mwanamuke kwa kutumia ubavu wenye alikuwa ametosha katika mwanaume, na akamuleta kwa ule mwanaume.+

23 Basi ule mwanaume akasema:

“Mwishowe huyu ni mufupa wa mifupa yangu

Na nyama ya nyama yangu.

Huyu ataitwa Mwanamuke,

Kwa sababu alitoshwa katika mwanaume.”+

24 Kwa sababu hiyo mwanaume atamuacha baba yake na mama yake na atashikamana* na bibi yake, nao watakuwa mwili mumoja.+ 25 Na wote wawili walikuwa uchi,+ huyo mwanaume na bibi yake; lakini hawakukuwa wanasikia haya.

3 Basi nyoka+ alikuwa muangalifu* kuliko wanyama wote wa pori wenye Yehova Mungu alikuwa amefanya. Kwa hiyo, akamuuliza mwanamuke: “Je, ni kweli kwamba Mungu alisema hamupaswe kula matunda ya kila muti wa bustani?”+ 2 Kwa hiyo mwanamuke akamuambia nyoka: “Tunaweza kula matunda ya miti ya bustani.+ 3 Lakini kuhusu matunda ya muti wenye kuwa katikati ya bustani+ Mungu amesema: ‘Hamupaswe kuyakula, hapana, hamupaswe kuyagusa; mukifanya vile mutakufa.’” 4 Kwa hiyo nyoka akamuambia mwanamuke: “Hakika hamutakufa.+ 5 Kwa sababu Mungu anajua kwamba siku ileile yenye mutakula matunda ya muti huo, macho yenu yatafunguliwa na mutakuwa kama Mungu; mukijua mema na mabaya.”+

6 Basi mwanamuke akaona kwamba muti huo ulikuwa wenye kufaa kwa chakula na ulikuwa kitu chenye kupendeza macho, ndiyo, muti huo ulikuwa wenye kupendeza macho. Kwa hiyo mwanamuke akaanza kukamata matunda ya muti huo na kuyakula.+ Kisha, wakati alikuwa pamoja na bwana yake, akamupatia pia, naye akaanza kuyakula.+ 7 Kisha macho ya wote wawili yakafunguliwa, na wakatambua kwamba walikuwa uchi. Kwa hiyo wakashona majani ya muti wa tini na kujifanyia nguo za kufunika kiuno.+

8 Kisha wakati fulani wakasikia sauti ya Yehova Mungu wakati alikuwa anatembea katika bustani karibu na wakati wa upepo mutulivu wa siku, na ule mwanaume na bibi yake wakajificha kutoka mbele ya uso wa Yehova Mungu katikati ya miti ya bustani. 9 Na Yehova Mungu akaendelea kumuita ule mwanaume na kumuambia: “Uko wapi?” 10 Mwishowe akasema: “Nilisikia sauti yako katika bustani, lakini niliogopa kwa sababu nilikuwa uchi, kwa hiyo nilijificha.” 11 Basi Mungu akasema: “Ni nani mwenye alikuambia kwamba uko uchi?+ Je, umekula matunda ya muti wenye nilikuamuru usikule matunda yake?”+ 12 Mwanaume huyo akasema: “Mwanamuke mwenye ulinipatia ili akuwe pamoja na mimi, alinipatia tunda la ule muti, kwa hiyo nikakula.” 13 Kisha Yehova Mungu akamuuliza mwanamuke: “Ni jambo gani hili lenye umefanya?” Mwanamuke akajibu: “Nyoka alinidanganya, kwa hiyo nikakula.”+

14 Kisha, Yehova Mungu akamuambia nyoka:+ “Kwa sababu umefanya jambo hili, umelaaniwa kati ya wanyama wote wa kufugwa na kati ya wanyama wote wa pori. Utaenda kwa tumbo lako, na utakula mavumbi siku zote za maisha yako. 15 Na nitatia uadui*+ kati yako+ na ule mwanamuke+ na kati ya uzao wako*+ na uzao wake.*+ Ataponda* kichwa chako,+ na wewe utamupiga* kwenye kisigino.”+

16 Akamuambia mwanamuke: “Nitaongeza sana maumivu ya mimba yako; utazaa watoto kwa maumivu, na utatamani sana bwana yako, naye atakutawala.”

17 Na akamuambia Adamu:* “Kwa sababu ulisikiliza sauti ya bibi yako na ukakula matunda ya muti wenye nilikupatia amri hii,+ ‘Haupaswe kula matunda yake,’ udongo umelaaniwa kwa sababu yako.+ Kwa maumivu utakula mazao yake siku zote za maisha yako.+ 18 Udongo utakuzalia miiba na michongoma, na utakula mimea ya shamba. 19 Kwa jasho la uso wako utakula mukate* mupaka wakati utarudia katika udongo, kwa maana ulitoshwa katika udongo.+ Kwa maana wewe ni mavumbi na utarudia katika mavumbi.”+

20 Kisha mambo hayo Adamu akamupatia bibi yake jina Eva,* kwa sababu ni yeye angekuwa mama ya kila mutu mwenye uzima.+ 21 Na Yehova Mungu akamutengenezea Adamu na bibi yake nguo za murefu za ngozi, ili kuwavalisha.+ 22 Kisha Yehova Mungu akasema: “Angalia, mutu huyu amekuwa kama mumoja wetu kwa kujua mema na mabaya.+ Sasa ili asinyooshe mukono wake na kukamata pia matunda ya muti wa uzima+ na kula na kuishi milele,*⁠—” 23 Kwa hiyo Yehova Mungu akamufukuza atoke katika bustani ya Edeni+ ili alime udongo wenye alikuwa ametoshwa ndani yake.+ 24 Kwa hiyo akamufukuza huyo mutu, na akaweka upande wa mashariki wa bustani ya Edeni makerubi+ na upanga wenye kuwaka wenye ulikuwa unaendelea kuzunguka-zunguka ili kulinda njia ya kuenda kwenye muti wa uzima.

4 Sasa Adamu akafanya ngono na Eva bibi yake, naye akapata mimba.+ Wakati alimuzaa Kaini,+ akasema: “Nimemuzaa* mutoto mwanaume kwa musaada wa Yehova.” 2 Kisha wakati fulani akazaa tena, Abeli+ ndugu yake.

Abeli akakuwa muchungaji wa kundi, lakini Kaini akakuwa mulimaji wa udongo. 3 Kisha wakati fulani, Kaini akaleta mazao ya shamba ili ayatolee Yehova. 4 Lakini Abeli alileta wazaliwa wa kwanza wa kundi lake,+ pamoja na mafuta ya wanyama hao. Hata kama Yehova alimukubali Abeli na toleo lake,+ 5 hakumukubali Kaini na toleo lake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana na kuhuzunika.* 6 Kisha Yehova akamuambia Kaini: “Sababu gani unakasirika sana na kuhuzunika? 7 Ukibadilika na kutenda mambo ya muzuri, je, hautakubaliwa?* Lakini kama haubadilike na kutenda mambo ya muzuri, zambi inashutama kwenye mulango, na inatamani sana kukutawala; lakini je, utaishinda?”

8 Kisha mambo hayo Kaini akamuambia Abeli ndugu yake: “Tuende kwenye eneo la mashamba.” Basi wakati walikuwa kwenye eneo la mashamba, Kaini akamushambulia Abeli ndugu yake na akamuua.+ 9 Kisha wakati fulani, Yehova akamuuliza Kaini: “Ndugu yako Abeli iko* wapi?” naye akajibu: “Sijue. Je, niko mulinzi wa ndugu yangu?” 10 Kwa hiyo Mungu akasema: “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako iko inanililia kutoka katika udongo.+ 11 Na sasa umelaaniwa kwa kufukuzwa kutoka kwenye udongo wenye umefungua kinywa chake ili kupokea damu ya ndugu yako kutoka katika mukono wako.+ 12 Wakati utalima udongo, hautakurudishia mazao yake.* Utakuwa mutu wa kutanga-tanga na mukimbizi katika dunia.” 13 Kwa hiyo Kaini akamuambia Yehova: “Azabu ya kosa langu ni kubwa sana, siwezi kuivumilia. 14 Leo unanifukuza kutoka katika inchi,* na mimi nitafichwa mbali na uso wako; na nitakuwa mutu wa kutanga-tanga na mukimbizi juu ya dunia, na kila mutu mwenye ataniona hakika ataniua.” 15 Kwa hiyo Yehova akamuambia: “Kwa sababu hiyo, mutu yeyote mwenye atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba (7).”

Basi Yehova akaweka alama kwa ajili ya Kaini ili kila mutu mwenye atamuona asimupige. 16 Kisha Kaini akatoka mbele ya Yehova na akaanza kuishi katika inchi ya Uhamisho,* upande wa mashariki wa Edeni.+

17 Kisha Kaini akafanya ngono na bibi yake,+ naye akapata mimba na kumuzaa Enoko. Kisha akajenga muji, akaita muji huo Enoko, jina la mwana wake. 18 Kisha wakati fulani Enoko akamuzaa Iradi. Na Iradi akamuzaa Mehuyaeli, na Mehuyaeli akamuzaa Metushaeli, na Metushaeli akamuzaa Lameki.

19 Lameki akachukua wanamuke wawili. Jina la mwanamuke wa kwanza lilikuwa Ada, na jina la wa pili lilikuwa Zila. 20 Ada akamuzaa Yabali. Alikuwa mwanzilishi wa wale wenye kuishi katika mahema na wenye kuwa na mifugo. 21 Jina la ndugu yake lilikuwa Yubali. Alikuwa mwanzilishi wa wale wote wenye kupiga kinubi na zumari.* 22 Pia, Zila alimuzaa Tubal-kaini, mwenye alitengeneza vyombo vya kila namna vya shaba na chuma. Na dada ya Tubal-kaini alikuwa Naama. 23 Kisha Lameki akatunga maneno haya kwa ajili ya bibi zake Ada na Zila:

“Musikie sauti yangu, ninyi bibi za Lameki;

Musikilize maneno yangu:

Nimemuua mutu mumoja kwa sababu aliniumiza,

Ndiyo, kijana mwanaume kwa sababu alinipiga.

24 Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba (7),+

Basi Lameki ni mara makumi saba na saba (77).”

25 Adamu akafanya ngono tena na bibi yake, naye akamuzaa mwana. Akamuita jina Seti,*+ kwa sababu, alisema: “Mungu amenichagulia uzao mwingine* pa nafasi ya Abeli, kwa sababu Kaini alimuua.”+ 26 Na Seti pia akamuzaa mwana, na akamuita jina Enoshi.+ Wakati huo watu wakaanza kuitia jina la Yehova.

5 Hiki ni kitabu cha historia ya Adamu. Katika siku yenye Mungu alimuumba Adamu, alimufanya kwa mufano wa Mungu.+ 2 Mwanaume na mwanamuke aliwaumba.+ Siku yenye aliwaumba,+ aliwabariki na kuwaita Mwanadamu.*

3 Adamu akaishi miaka mia moja makumi tatu (130), kisha akamuzaa mwana kwa sura yake, kwa mufano wake, na akamupatia jina Seti.+ 4 Kisha kumuzaa Seti, Adamu akaishi miaka mia munane (800). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 5 Basi siku zote za maisha ya Adamu zikakuwa miaka mia kenda makumi tatu (930), kisha akakufa.+

6 Seti akaishi miaka mia moja na tano (105), kisha akamuzaa Enoshi.+ 7 Kisha kumuzaa Enoshi, Seti akaishi miaka mia munane na saba (807). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 8 Basi siku zote za maisha ya Seti zikakuwa miaka mia kenda kumi na mbili (912), kisha akakufa.

9 Enoshi akaishi miaka makumi kenda (90), kisha akamuzaa Kenani. 10 Kisha kumuzaa Kenani, Enoshi akaishi miaka mia munane kumi na tano (815). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 11 Basi siku zote za maisha ya Enoshi zikakuwa miaka mia kenda na tano (905), kisha akakufa.

12 Kenani akaishi miaka makumi saba (70), kisha akamuzaa Mahalaleli.+ 13 Kisha kumuzaa Mahalaleli, Kenani akaishi miaka mia munane makumi ine (840). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 14 Basi siku zote za maisha ya Kenani zikakuwa miaka mia kenda na kumi (910), kisha akakufa.

15 Mahalaleli akaishi miaka makumi sita na tano (65), kisha akamuzaa Yaredi.+ 16 Kisha kumuzaa Yaredi, Mahalaleli akaishi miaka mia munane makumi tatu (830). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 17 Basi siku zote za maisha ya Mahalaleli zikakuwa miaka mia munane makumi kenda na tano (895), kisha akakufa.

18 Yaredi akaishi miaka mia moja makumi sita na mbili (162), kisha akamuzaa Enoko.+ 19 Kisha kumuzaa Enoko, Yaredi akaishi miaka mia munane (800). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 20 Basi siku zote za maisha ya Yaredi zikakuwa miaka mia kenda makumi sita na mbili (962), kisha akakufa.

21 Enoko akaishi miaka makumi sita na tano (65), kisha akamuzaa Metusela.+ 22 Kisha kumuzaa Metusela, Enoko akaendelea kutembea pamoja na Mungu wa kweli* kwa miaka mia tatu (300). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 23 Basi siku zote za maisha ya Enoko zikakuwa miaka mia tatu makumi sita na tano (365). 24 Enoko akaendelea kutembea pamoja na Mungu wa kweli.+ Kisha hakukuwa tena, kwa sababu Mungu alimuchukua.+

25 Metusela akaishi miaka mia moja makumi munane na saba (187), kisha akamuzaa Lameki.+ 26 Kisha kumuzaa Lameki, Metusela akaishi miaka mia saba makumi munane na mbili (782). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 27 Basi siku zote za maisha ya Metusela zikakuwa miaka mia kenda makumi sita na kenda (969), kisha akakufa.

28 Lameki akaishi miaka mia moja makumi munane na mbili (182), kisha akamuzaa mwana. 29 Akamupatia jina Noa,*+ na kusema: “Huyu atatufariji katika kazi yetu ya jasho na katika kazi ya nguvu yenye kuumiza ya mikono yetu kwa sababu ya udongo wenye Yehova amelaani.”+ 30 Kisha kumuzaa Noa, Lameki akaishi miaka mia tano makumi kenda na tano (595). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. 31 Basi siku zote za maisha ya Lameki zikakuwa miaka mia saba makumi saba na saba (777), kisha akakufa.

32 Wakati Noa alieneza miaka mia tano (500), akamuzaa Shemu,+ Hamu,+ na Yafeti.+

6 Sasa wakati wanadamu walianza kuongezeka juu ya uso wa inchi na kuzaa watoto wanamuke, 2 wana wa Mungu wa kweli*+ wakaanza kutambua kwamba mabinti wa wanadamu walikuwa wenye sura na umbo ya muzuri. Basi wakaanza kuchukua wale wote wenye walichagua ili wakuwe bibi zao. 3 Kisha Yehova akasema: “Roho yangu haitaendelea kuvumilia mwanadamu milele,+ kwa sababu yeye ni mwili tu.* Kwa hiyo siku zake zitakuwa miaka mia moja makumi mbili (120).”+

4 Katika siku hizo na kuendelea kulikuwa Wanefili* juu ya dunia. Wakati huo wana wa Mungu wa kweli waliendelea kulala na mabinti wa wanadamu na kuzaa wana. Wao ndio walikuwa watu wenye nguvu wa nyakati za zamani, watu wenye sifa.

5 Basi Yehova akaona kwamba uovu wa mwanadamu ulikuwa mwingi juu ya dunia na kila muelekeo wa mawazo ya moyo wake ulikuwa tu mubaya wakati wote.+ 6 Yehova akasikitika* kwamba alikuwa ameumba wanadamu kwenye dunia, na moyo wake ukahuzunika.*+ 7 Kwa hiyo Yehova akasema: “Nitafuta juu ya uso wa inchi wanadamu wenye nimeumba, mwanadamu pamoja na wanyama wa kufugwa, wanyama wenye kutambaa, na viumbe vyenye kuruka vya mbinguni, kwa sababu ninasikitika kwamba nimewafanya.” 8 Lakini Noa akakubaliwa mbele ya macho ya Yehova.

9 Hii ndiyo historia ya Noa.

Noa alikuwa mwenye haki.+ Alijiendesha bila kosa* kati ya watu wa siku zake.* Noa alitembea pamoja na Mungu wa kweli.+ 10 Kisha wakati fulani Noa alizaa wana watatu (3), Shemu, Hamu, na Yafeti.+ 11 Lakini dunia ilikuwa imeharibika mbele ya macho ya Mungu wa kweli, na dunia ilikuwa inajaa jeuri. 12 Ndiyo, Mungu akaangalia dunia, na ilikuwa imeharibika;+ kwa sababu miili yote ilikuwa imeharibu* njia yake juu ya dunia.+

13 Basi Mungu akamuambia Noa: “Nimeamua kuharibu miili yote, kwa kuwa dunia imejaa jeuri kwa sababu yao, kwa hiyo nitawaharibu pamoja na dunia.+ 14 Ujijengee safina kwa mbao za muti wenye utomvu.+ Utatengeneza vyumba ndani ya safina na uifunike na lami*+ ndani na inje. 15 Utaitengeneza hivi: Urefu wa safina utakuwa mikono mia tatu (300),* upana wake mikono makumi tano (50), na urefu wake kuenda juu mikono makumi tatu (30). 16 Utatengeneza dirisha la kuingiza mwangaza* ndani ya safina, mukono mumoja kutoka juu. Unapaswa kuweka muingilio wa safina katika ubavu wake+ na utaifanyia gorofa ya chini, gorofa ya pili, na gorofa ya tatu (3).

17 “Mimi, nitaleta maji ya garika+ juu ya dunia ili kuharibu miili yote yenye iko na pumuzi ya uzima* yenye iko chini ya mbingu. Kila kiumbe chenye kuwa katika dunia kitakufa.+ 18 Na ninafanya agano pamoja na wewe, na unapaswa kuingia ndani ya safina, wewe, wana wako, bibi yako, na bibi za wana wako.+ 19 Na utaingiza ndani ya safina viumbe vyenye uzima+ viwili-viwili vya kila aina ili kulinda uzima wa viumbe hivyo pamoja na wewe, dume na dike;+ 20 viumbe vyenye kuruka kulingana na aina yavyo, wanyama wa kufugwa kulingana na aina zake, na wanyama wote wenye kutambaa juu ya inchi kulingana na aina yao, wataingia wawili-wawili kwako ili kulinda uzima wao.+ 21 Kwa upande wako, unapaswa kukusanya na kukamata kila namna ya chakula,+ kwa ajili yako na kwa ajili ya wanyama.”

22 Basi Noa akafanya kulingana na mambo yote yenye Mungu alimuamuru. Ni vile alifanya kabisa.+

7 Kisha mambo hayo Yehova akamuambia Noa: “Ingia ndani ya safina wewe pamoja na nyumba yako yote, kwa sababu ni wewe nimeona kuwa mwenye haki mbele yangu kati ya kizazi hiki.+ 2 Unapaswa kujichukulia wanyama safi wa kila aina, wanyama saba-saba,*+ dume na dike yake; na wanyama wenye hawako safi wa kila aina wawili-wawili tu, dume na dike yake; 3 chukua pia viumbe vyenye kuruka vya mbinguni saba-saba,* dume na dike yake, ili kulinda uzima wa uzao wa viumbe hivyo juu ya dunia yote.+ 4 Kwa maana kisha tu siku saba (7), nitafanya mvua inyeshe+ juu ya dunia kwa siku makumi ine (40) muchana na usiku,+ na nitafuta juu ya uso wa inchi kila kiumbe chenye uzima chenye nimefanya.”+ 5 Kwa hiyo Noa akafanya mambo yote yenye Yehova alimuamuru.

6 Noa alikuwa na miaka mia sita (600) wakati maji ya garika yalikuja juu ya dunia.+ 7 Basi Noa, pamoja na wana wake, bibi yake, na bibi za wana wake, wakaingia ndani ya safina mbele ya maji ya garika kuja.+ 8 Kati ya kila aina ya munyama mwenye kuwa safi na kati ya kila aina ya munyama mwenye haiko safi na kati ya kila aina ya viumbe vyenye kuruka na kila kitu chenye kutambaa juu ya inchi,+ 9 vikaingia viwili-viwili mahali Noa alikuwa ndani ya safina, dume na dike, kama vile Mungu alikuwa amemuamuru Noa. 10 Na kisha siku saba (7) maji ya garika yakakuja juu ya dunia.

11 Katika mwaka wa mia sita (600) wa maisha ya Noa, mwezi wa pili, siku ya kumi na saba (17) ya mwezi huo, katika siku hiyo chemchemi zote za maji yenye kuenda chini sana zikafunguka na milango mikubwa ya maji mengi ya mbinguni ikafunguliwa.+ 12 Mvua ikanyesha juu ya dunia kwa siku makumi ine (40), muchana na usiku. 13 Katika siku ile ile, Noa akaingia ndani ya safina yeye pamoja na wana wake, Shemu, Hamu, na Yafeti,+ na bibi yake na bibi watatu (3) wa wana wake.+ 14 Waliingia pamoja na kila munyama wa pori kulingana na aina yake, na kila munyama wa kufugwa kulingana na aina yake, na kila munyama mwenye kutambaa juu ya dunia kulingana na aina yake, na kila kiumbe chenye kuruka kulingana na aina yake, kila ndege, kila kiumbe chenye mabawa. 15 Waliendelea kuingia mahali Noa alikuwa ndani ya safina, wawili-wawili, kila aina ya mwili wenye pumuzi ya uzima.* 16 Basi wakaingia, dume na dike wa kila aina ya mwili, kama vile Mungu alikuwa amemuamuru. Kisha Yehova akafunga mulango nyuma yake.

17 Garika ikaendelea* kwa siku makumi ine (40) juu ya dunia, na maji yakaendelea kuongezeka na kuanza kubeba safina, na safina ilikuwa inaelea juu ya dunia. 18 Maji yakajaa na kuendelea kuongezeka juu ya dunia, lakini safina ilikuwa inaelea juu ya maji. 19 Maji yakajaa sana juu ya dunia na milima yote mirefu chini ya mbingu zote ikafunikwa.+ 20 Maji yakapanda kufikia mikono* kumi na tano (15) juu ya milima.

21 Basi viumbe vyote vyenye uzima vyenye vilikuwa vinatembea juu ya dunia vikakufa+⁠—​viumbe vyenye kuruka, wanyama wa kufugwa, wanyama wa pori, na viumbe vyenye kupatikana kwa wingi, na wanadamu wote.+ 22 Kila kitu kwenye inchi kavu chenye kilikuwa na pumuzi ya uzima* katika matundu ya pua yake kikakufa.+ 23 Kwa hiyo Mungu akafuta juu ya uso wa dunia kila kitu chenye uzima, kutia ndani mwanadamu, wanyama, wanyama wenye kutambaa, na viumbe vyenye kuruka vya anga. Vyote vikafutwa juu ya dunia;+ Noa peke yake na wale wenye walikuwa pamoja naye ndani ya safina ndio waliokoka.+ 24 Na maji yakaendelea kujaa juu ya dunia kwa siku mia moja makumi tano (150).+

8 Lakini Mungu akakaza uangalifu juu ya* Noa na juu ya wanyama wote wa pori na juu ya wanyama wote wa kufugwa wenye walikuwa pamoja naye ndani ya safina,+ na Mungu akavumisha upepo juu ya dunia, na maji yakaanza kupunguka. 2 Chemchemi za maji yenye kuenda chini sana na milango mikubwa ya maji mengi ya mbinguni ikafungwa, kwa hiyo mvua kutoka mbinguni ikaacha kunyesha.*+ 3 Basi maji yakaanza kupunguka polepole juu ya dunia. Kisha siku mia moja makumi tano (150), maji yalikuwa yamepunguka. 4 Katika mwezi wa saba (7), siku ya kumi na saba (17) ya mwezi huo, safina ikasimama juu ya milima ya Ararati. 5 Na maji yakaendelea kupunguka polepole mupaka mwezi wa kumi (10). Katika mwezi wa kumi, siku ya kwanza ya mwezi huo, vichwa vya milima vikaonekana.+

6 Kwa hiyo wakati siku makumi ine (40) zilimalizika, Noa akafungua dirisha+ lenye alikuwa ametengeneza kwenye safina 7 na akatuma kunguru inje; kunguru alikuwa anaruka kuenda inje na kurudia, mupaka wakati maji yalikauka juu ya dunia.

8 Kisha wakati fulani akatuma njiwa inje ili kuona kama maji yalikuwa yamepunguka juu ya uso wa inchi. 9 Njiwa huyo hakupata mahali pa kushuka ili kupumuzika,* kwa hiyo akarudia mahali Noa alikuwa ndani ya safina kwa sababu maji yalikuwa yangali yanafunika uso wa dunia yote.+ Kwa hiyo Noa akanyoosha mukono wake na kumuingiza ndani ya safina. 10 Akangojea siku zingine saba (7), na mara ingine tena akatuma njiwa inje ya safina. 11 Wakati njiwa huyo alirudia mangaribi mahali Noa alikuwa, Noa aliona kwamba kulikuwa jani la mubichi la muzeituni katika mudomo wa njiwa huyo! Kwa hiyo Noa akajua kwamba maji yalikuwa yamepunguka juu ya dunia.+ 12 Akangojea siku zingine saba (7). Kisha akatuma njiwa huyo inje, lakini hakurudia tena mahali Noa alikuwa.

13 Sasa katika mwaka wa mia sita na moja (601),+ mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, maji yalikuwa yamekauka juu ya dunia; na Noa akaondoa kifuniko cha safina na kuona kuwa uso wa inchi ulikuwa unakauka. 14 Katika mwezi wa pili, siku ya makumi mbili na saba (27) ya mwezi huo, dunia ilikuwa imekauka.

15 Sasa Mungu akamuambia Noa: 16 “Toka ndani ya safina, wewe, bibi yako, wana wako, na bibi za wana wako.+ 17 Toka pamoja na viumbe vyote vyenye uzima vya kila aina ya mwili,+ kati ya viumbe vyote vyenye kuruka na kati ya wanyama na kati ya wanyama wenye kutambaa juu ya dunia, ili viongezeke* na kuzaa na kuwa vingi juu ya dunia.”+

18 Kwa hiyo Noa akatoka inje pamoja na wana wake,+ bibi yake, na bibi za wana wake. 19 Kila kiumbe chenye uzima, kila munyama mwenye kutambaa, kila kiumbe chenye kuruka, na kila kitu chenye kutembea juu ya dunia, kikatoka inje ya safina kulingana na familia yake.+ 20 Kisha Noa akamujengea Yehova mazabahu+ na akakamata wamoja kati ya wanyama wote wenye kuwa safi na wamoja kati ya viumbe vyote vyenye kuruka vyenye kuwa safi+ na akatoa matoleo ya kuteketezwa juu ya ile mazabahu.+ 21 Na Yehova akaanza kusikia harufu ya muzuri.* Kwa hiyo Yehova akasema katika moyo wake: “Sitalaani tena* inchi+ hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu, kwa maana muelekeo wa moyo wa mwanadamu ni mubaya kuanzia ujana wake;+ na mimi sitapiga na kuua tena kila kitu chenye uzima kama vile nimefanya.+ 22 Kuanzia sasa, dunia haitakosa hata kidogo kuwa na wakati wa kupanda mbegu na wakati wa kuvuna, baridi na joto, kipindi cha joto na kipindi cha baridi, na muchana na usiku.”+

9 Mungu akamubariki Noa na wana wake na kuwaambia: “Muzae na mukuwe wengi na mujaze dunia.+ 2 Kila kiumbe chenye uzima cha dunia, kila kiumbe chenye kuruka cha mbinguni, kila kitu chenye kutembea juu ya dunia na samaki wote wa bahari watawahofu na kuwaogopa ninyi. Wote hao wametiwa sasa katika mukono wenu.*+ 3 Kila munyama mwenye kutembea na mwenye uzima anaweza kuwa chakula chenu.+ Kama vile niliwapatia majani ya mubichi, ninawapatia wanyama hao wote.+ 4 Isipokuwa tu nyama pamoja na uzima wake*⁠—​damu yake+⁠—​hamupaswe kula.+ 5 Zaidi ya hayo, nitaomba hesabu kwa ajili ya damu ya uzima wenu.* Nitaomba hesabu kila kiumbe chenye uzima; na nitaomba hesabu kila mwanadamu kwa ajili ya uzima wa ndugu yake.+ 6 Kila mutu mwenye anamwanga damu ya mutu, damu yake mwenyewe itamwangwa na mutu,+ kwa maana Mungu alimufanya mutu kwa mufano wake.+ 7 Sasa ninyi, muzae na mukuwe wengi, mujae sana katika dunia na muongezeke sana.”+

8 Kisha Mungu akamuambia Noa na wana wake pamoja naye: 9 “Sasa ninafanya agano langu pamoja na ninyi+ na pamoja na uzao wenu kisha ninyi, 10 na pamoja na kila kiumbe chenye uzima chenye* kuwa pamoja na ninyi, ndege, wanyama, na viumbe vyote vya dunia pamoja na ninyi, vyote vyenye vilitoka ndani ya safina⁠—​kila kiumbe chenye uzima cha dunia.+ 11 Ndiyo, ninafanya agano langu pamoja na ninyi: Hakuna siku miili yote itaharibiwa* tena na maji ya garika, na hakuna siku yenye garika itaharibu tena dunia.”+

12 Na Mungu akasema tena: “Hii ndiyo alama ya agano lenye ninafanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe chenye uzima chenye* kuwa pamoja na ninyi, kwa vizazi vyote vyenye kuja. 13 Ninatia upinde wangu wa mvua katika wingu, na utakuwa alama ya agano kati yangu na dunia. 14 Kila mara wakati nitaleta wingu juu ya dunia, upinde wa mvua utaonekana katika wingu. 15 Na hakika nitakumbuka agano langu lenye nilifanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe chenye uzima cha kila aina;* na hakuna tena siku maji yatakuwa garika ili kuharibu miili yote.+ 16 Na upinde wa mvua utatokea katika wingu, na hakika nitauona na kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe chenye uzima cha kila aina,* chenye kuwa juu ya dunia.”

17 Mungu akamuambia tena Noa: “Hiyo ndiyo alama ya agano lenye ninatia kati yangu na miili yote yenye iko juu ya dunia.”+

18 Wana wa Noa wenye walitoka katika safina walikuwa Shemu, Hamu, na Yafeti.+ Kisha wakati fulani Hamu akamuzaa Kanaani.+ 19 Hao watatu (3) walikuwa wana wa Noa, na watu wote wa dunia walitokana nao na kuenea kila mahali.+

20 Sasa Noa akaanza kuwa mulimaji, na akapanda shamba la mizabibu. 21 Wakati alikunywa divai, akalewa, na akajiacha uchi ndani ya hema yake. 22 Hamu, baba ya Kanaani, akaona uchi wa baba yake, na akaambia ndugu zake wawili wenye walikuwa inje. 23 Kwa hiyo Shemu na Yafeti wakakamata nguo na wakaiweka kwenye mabega yao mbili na wakaingia kinyume-nyume katika hema. Basi wakafunika uchi wa baba yao lakini nyuso zao zilikuwa zinaangalia pembeni, nao hawakuona uchi wa baba yao.

24 Wakati Noa aliamuka kisha divai kumutoka na kujua jambo lenye mwana wake mudogo alimutendea, 25 akasema:

“Kanaani alaaniwe.+

Akuwe mutumwa wa hali ya chini kabisa wa ndugu zake.”+

26 Tena akasema:

“Yehova, Mungu wa Shemu asifiwe,

Na Kanaani akuwe mutumwa wake.+

27 Mungu amupatie Yafeti nafasi kubwa,

Na akae katika mahema ya Shemu.

Kanaani akuwe mutumwa wake pia.”

28 Noa akaendelea kuishi miaka mia tatu makumi tano (350) kisha Garika.+ 29 Basi siku zote za Noa zikakuwa miaka mia kenda makumi tano (950), kisha akakufa.

10 Hii ndiyo historia ya wana wa Noa, Shemu,+ Hamu, na Yafeti.

Walizaa wana kisha Garika.+ 2 Wana wa Yafeti walikuwa Gomeri,+ Magogu,+ Madai, Yavani, Tubali,+ Mesheki,+ na Tirasi.+

3 Wana wa Gomeri walikuwa Ashkenazi,+ Rifati, na Togarma.+

4 Wana wa Yavani walikuwa Elisha,+ Tarshishi,+ Kitimu,+ na Dodanimu.

5 Kutokana na hawa wakaaji wa visiwa walienea kila mahali katika inchi zao, kulingana na luga zao na familia zao na mataifa yao.

6 Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu,+ Putu,+ na Kanaani.+

7 Wana wa Kushi walikuwa Seba,+ Havila, Sabta, Raama,+ na Sabteka.

Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.

8 Kushi akamuzaa Nimrodi. Alikuwa wa kwanza kuwa mutu mwenye nguvu katika dunia. 9 Alikuwa muwindaji mwenye nguvu na mwenye kumupinga Yehova. Ndiyo sababu kuko musemo: “Kama vile Nimrodi, muwindaji mwenye nguvu na mwenye kumupinga Yehova.” 10 Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa* Babeli,+ Ereki,+ Akadi, na Kalne, katika inchi ya Shinari.+ 11 Kutoka katika inchi hiyo alienda Ashuru+ na kujenga Ninawi,+ Rehobot-Iri, Kala, 12 na Reseni, kati ya Ninawi na Kala: Huu ndio ule muji mukubwa.

13 Misraimu akamuzaa Ludimu,+ Anamimu, Lehabimu, Naftuhimu,+ 14 Patrusimu,+ Kasluhimu (wenye Wafilisti+ walitokana nao), na Kaftorimu.+

15 Kanaani akamuzaa Sidoni,+ muzaliwa wake wa kwanza, na Heti,+ 16 na pia Muyebusi,+ Mwamori,+ Mugirgashi, 17 Muhivi,+ Mwarkia, Musini, 18 Mwarvadi,+ Musemari, na Muhamati.+ Kisha, familia za Wakanaani zikasambaa. 19 Basi mupaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni kufikia Gerari,+ karibu na Gaza,+ kufikia Sodoma, Gomora,+ Adma, Seboimu,+ karibu na Lasha. 20 Hao ndio walikuwa wana wa Hamu kulingana na familia zao na luga zao, inchi zao na mataifa yao.

21 Shemu, babu ya wana wote wa Eberi+ na ndugu ya Yafeti muzaliwa wa kwanza,* naye pia alizaa watoto. 22 Wana wa Shemu walikuwa Elamu,+ Asihuru,+ Arpakshadi,+ Ludi, na Aramu.+

23 Wana wa Aramu walikuwa Usi, Huli, Geteri, na Mashi.

24 Arpakshadi akamuzaa Shela,+ na Shela akamuzaa Eberi.

25 Eberi alizaa wana wawili. Jina la mumoja lilikuwa Pelegi,*+ kwa sababu wakati wa maisha yake dunia ilikuwa imegawanyika.* Jina la ndugu yake lilikuwa Yoktani.+

26 Yoktani akamuzaa Almodadi, Shelefu, Hazarmaveti, Yera,+ 27 Hadoramu, Uzali, Dikla, 28 Obali, Abimaeli, Sheba, 29 Ofiri,+ Havila, na Yobabu; wote hao walikuwa wana wa Yoktani.

30 Mahali kwenye walikuwa wanaishi kulianzia Mesha mupaka Sefari, eneo lenye milima la Mashariki.

31 Hao ndio walikuwa wana wa Shemu kulingana na familia zao na luga zao, inchi zao na mataifa yao.+

32 Ni hizo zilikuwa familia za wana wa Noa kulingana na wazao wa familia zao na mataifa yao. Kutokana nao, mataifa yote yalienea katika dunia kisha Garika.+

11 Sasa dunia yote iliendelea kuwa na luga moja na maneno ya namna moja. 2 Wakati walisafiri kuelekea upande wa mashariki, walivumbua bonde tambarare katika inchi ya Shinari,+ na walianza kuishi kule. 3 Kisha wakaambiana: “Mukuje! Tutengeneze matofali na kuyachoma kwa moto.” Basi wakatumia matofali pa nafasi ya majiwe, na kabulimbo pa nafasi ya saruji.* 4 Basi wakasema: “Mukuje! Tujijengee muji na munara wenye sehemu yake ya juu itafika mbinguni, na tujifanyie jina kubwa, ili tusisambazwe juu ya uso wote wa dunia.”+

5 Kisha Yehova akashuka ili aone muji na munara wenye wana wa binadamu walikuwa wamejenga. 6 Basi Yehova akasema: “Angalia! Wao ni kikundi kimoja cha watu na wako na luga moja,+ na ni hivi wameanza kufanya. Sasa hakuna kitu wanaweza kuwa nacho katika akili yao chenye hawataweza kufanya. 7 Mukuje! Tushuke+ kule na tuvuruge luga yao ili kila mumoja wao asielewe luga ya mwingine.” 8 Kwa hiyo Yehova akawasambaza kutoka mahali pale juu ya uso wote wa dunia,+ na pole kwa pole wakaacha kujenga muji huo. 9 Ndiyo sababu muji huo uliitwa Babeli,*+ kwa sababu ni kule Yehova alivuruga luga ya dunia yote, na Yehova aliwasambaza kutoka mahali pale juu ya uso wote wa dunia.

10 Hii ndiyo historia ya Shemu.+

Shemu alikuwa na miaka mia moja (100) wakati alimuzaa Arpakshadi+ miaka mbili kisha Garika. 11 Kisha kumuzaa Arpakshadi, Shemu akaishi tena miaka mia tano (500). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.+

12 Arpakshadi akaishi miaka makumi tatu na tano (35) na kisha akamuzaa Shela.+ 13 Kisha kumuzaa Shela, Arpakshadi akaishi tena miaka mia ine na tatu (403). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.

14 Shela akaishi miaka makumi tatu (30) na kisha akamuzaa Eberi.+ 15 Kisha kumuzaa Eberi, Shela akaishi tena miaka mia ine na tatu (403). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.

16 Eberi akaishi miaka makumi tatu na ine (34) na kisha akamuzaa Pelegi.+ 17 Kisha kumuzaa Pelegi, Eberi akaishi tena miaka mia ine makumi tatu (430). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.

18 Pelegi akaishi miaka makumi tatu (30) na kisha akamuzaa Reu.+ 19 Kisha kumuzaa Reu, Pelegi akaishi tena miaka mia mbili na kenda (209). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.

20 Reu akaishi miaka makumi tatu na mbili (32) na kisha akamuzaa Serugi. 21 Kisha kumuzaa Serugi, Reu akaishi tena miaka mia mbili na saba (207). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.

22 Serugi akaishi miaka makumi tatu (30) na kisha akamuzaa Nahori. 23 Kisha kumuzaa Nahori, Serugi akaishi tena miaka mia mbili (200). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.

24 Nahori akaishi miaka makumi mbili na kenda (29) na kisha akamuzaa Tera.+ 25 Kisha kumuzaa Tera, Nahori akaishi tena miaka mia moja kumi na kenda (119). Na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.

26 Tera akaishi miaka makumi saba (70), kisha akamuzaa Abramu,+ Nahori,+ na Harani.

27 Hii ndiyo historia ya Tera.

Tera alimuzaa Abramu, Nahori, na Harani; na Harani alimuzaa Loti.+ 28 Wakati Tera baba yake alikuwa angali muzima, Harani alikufa katika inchi yake ya kizalikio, katika Uru+ ya Wakaldayo.+ 29 Abramu na Nahori walijichukulia wanamuke. Jina la bibi ya Abramu lilikuwa Sarai,+ na jina la bibi ya Nahori lilikuwa Milka,+ binti ya Harani, baba ya Milka na Iska. 30 Basi Sarai alikuwa tasa;+ hakukuwa na mutoto.

31 Kisha Tera akamuchukua Abramu mwana wake na Loti mujukuu wake,+ mwana wa Harani, na Sarai binti-mukwe wake, bibi ya Abramu mwana wake, wakatoka Uru ya Wakaldayo pamoja naye ili kuenda katika inchi ya Kanaani.+ Kisha wakati fulani wakafika Harani+ na wakaanza kukaa kule. 32 Siku za maisha ya Tera zikakuwa miaka mia mbili na tano (205). Kisha akakufa kule Harani.

12 Na Yehova akamuambia Abramu: “Toka katika inchi yako na uende mbali na watu wa jamaa yako na kutoka kwa nyumba ya baba yako mupaka kwenye inchi yenye nitakuonyesha;+ 2 Nitakufanya kuwa taifa kubwa, nitakubariki, nitafanya jina lako kuwa kubwa, na wewe utakuwa baraka.+ 3 Nitabariki wale wenye wanakubariki, na nitalaani mutu mwenye anaita ubaya juu yako,+ na familia zote za dunia hakika zitabarikiwa* kupitia wewe.”+

4 Kwa hiyo Abramu akaondoka kama vile Yehova alikuwa amemuambia, na Loti akaenda pamoja naye. Abramu alikuwa na miaka makumi saba na tano (75) wakati alitoka Harani.+ 5 Abramu akamuchukua Sarai+ bibi yake na Loti mwana wa ndugu yake+ na mali zote zenye walikuwa wamekusanya+ na watu wenye* walikuwa wamepata kule Harani, nao wakaenda katika inchi ya Kanaani.+ Wakati walifika katika inchi ya Kanaani, 6 Abramu akapita katikati ya inchi mupaka eneo la Shekemu,+ karibu na miti mikubwa ya More.+ Wakati huo Wakanaani walikuwa katika inchi hiyo. 7 Kisha Yehova akamutokea Abramu na kumuambia: “Nitapatia uzao+ wako* inchi hii.”+ Kwa hiyo Abramu akajenga mazabahu pale kwa ajili ya Yehova, mwenye alikuwa amemutokea. 8 Kisha wakati fulani akatoka pale na kuenda katika eneo lenye milima upande wa mashariki wa Beteli+ na kusimamisha hema yake, Beteli ilikuwa upande wa mangaribi na Ai+ upande wa mashariki. Akajenga kule mazabahu kwa ajili ya Yehova+ na akaanza kuitia jina la Yehova.+ 9 Kisha, Abramu akavunja kambi na kusafiri kuelekea upande wa Negebu,+ alikuwa anahamisha kambi yake kutoka mahali pamoja mupaka mahali pengine.

10 Sasa njaa ikatokea katika inchi, na Abramu akateremuka kuelekea Misri ili akae kule kwa wakati fulani,*+ kwa sababu njaa katika inchi hiyo ilikuwa kali.+ 11 Wakati alikaribia kuingia Misri, akamuambia Sarai bibi yake: “Tafazali, unisikilize. Ninajua kama uko mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri sana.+ 12 Kwa hiyo wakati Wamisri watakuona hakika watasema, ‘Huyu ni bibi yake.’ Kisha wataniua lakini wewe watakuacha muzima. 13 Tafazali sema uko dada yangu, ili mambo yaniendee muzuri kwa sababu yako, na niendelee kuishi.”+

14 Wakati tu Abramu aliingia Misri, Wamisri wakaona kwamba mwanamuke huyo alikuwa mwenye sura na umbo ya muzuri sana. 15 Na wakubwa wa Farao pia wakamuona, na wakaanza kumusifu mbele ya Farao, kwa hiyo mwanamuke huyo akapelekwa katika nyumba ya Farao. 16 Naye akamutendea Abramu muzuri kwa sababu ya Sarai, na Abramu akapata kondoo, ngombe, punda-dume na punda-dike, watumishi wanaume na watumishi wanamuke, na ngamia.+ 17 Kisha Yehova akamupiga Farao na nyumba yake kwa mapigo makubwa kwa sababu ya Sarai, bibi ya Abramu.+ 18 Kwa hiyo Farao akamuita Abramu na kumuambia: “Ni jambo gani hili lenye umenitendea? Sababu gani haukuniambia kama yeye alikuwa bibi yako? 19 Sababu gani ulisema, ‘Yeye ni dada yangu,’+ na hivyo nilikuwa karibu kumuchukua akuwe bibi yangu? Bibi yako ndiye huyu. Umuchukue na uende!” 20 Kwa hiyo Farao akapatia watu wake maagizo juu ya Abrahamu, nao wakamuacha aende pamoja na bibi yake na vyote vyenye alikuwa navyo.+

13 Kisha Abramu akapanda kutoka Misri na kuenda Negebu,+ yeye na bibi yake na vyote vyenye alikuwa navyo, pamoja na Loti. 2 Abramu alikuwa na utajiri wa mifugo, feza, na zahabu.+ 3 Alikuwa anapiga kambi kutoka mahali pamoja mupaka mahali pengine wakati alikuwa anasafiri kutoka Negebu mupaka Beteli, mupaka wakati alifika mahali hema yake ilikuwaka zamani kati ya Beteli na Ai,+ 4 kufikia mahali alikuwa amejenga mazabahu zamani. Abramu akaitia jina la Yehova pale.

5 Sasa Loti, mwenye alikuwa anasafiri pamoja na Abramu, alikuwa pia na kondoo, ngombe, na mahema. 6 Basi inchi haikuwaruhusu wote waweze kukaa pamoja; mali zao zilikuwa zimeongezeka sana na hivyo hawangeweza tena kukaa pamoja. 7 Kwa sababu hiyo, ugomvi ukatokea kati ya wachungaji wa mifugo wa Abramu na wachungaji wa mifugo wa Loti. (Wakati ule Wakanaani na Waperizi walikuwa wanakaa katika inchi hiyo.)+ 8 Kwa hiyo Abramu akamuambia Loti:+ “Tafazali, ugomvi usikuwe kati yangu na wewe na kati ya wachungaji wangu na wachungaji wako, kwa maana sisi ni ndugu. 9 Je, inchi yote haiko mbele yako? Tafazali, ujitenge na mimi. Ukienda upande wa kushoto, mimi nitaenda upande wa kuume; lakini ukienda upande wa kuume, mimi nitaenda upande wa kushoto.” 10 Kwa hiyo Loti akainua macho yake na kuona kwamba wilaya yote ya Yordani+ ilikuwa eneo lenye maji mengi (mbele Yehova aharibu Sodoma na Gomora), kama bustani ya Yehova,+ kama inchi ya Misri, mupaka Soari.+ 11 Kisha Loti akajichagulia wilaya yote ya Yordani, na Loti akahamishia kambi yake upande wa mashariki. Kwa hiyo wakatengana. 12 Abramu alikaa katika inchi ya Kanaani, lakini Loti akakaa katika miji ya wilaya hiyo.+ Mwishowe akasimamisha hema yake karibu na Sodoma. 13 Sasa watu wa Sodoma walikuwa waovu, na walikuwa wanatenda zambi nzito mbele ya Yehova.+

14 Yehova akamuambia Abramu, kisha Loti kutengana naye: “Tafazali, inua macho yako na uangalie ukiwa mahali kwenye uko, kuelekea upande wa kaskazini na wa kusini, na wa mashariki na wa mangaribi, 15 kwa sababu inchi yote yenye unaona, nitakupatia wewe na uzao wako* ikuwe uriti wa kudumu.+ 16 Na mimi nitafanya uzao wako ukuwe* kama chembe za mavumbi ya inchi, ili, kama mutu anaweza kuhesabia mavumbi ya inchi, basi uzao wako utaweza* kuhesabiwa.+ 17 Simama, tembea katika inchi kwa urefu wake na upana wake, kwa maana nitakupatia inchi hiyo.” 18 Kwa hiyo Abramu akaendelea kuishi katika mahema. Kisha wakati fulani akaenda na kukaa kati ya miti mikubwa ya Mamre,+ yenye kuwa Hebroni,+ na akajenga kule mazabahu kwa ajili ya Yehova.+

14 Sasa katika siku za Amrafeli mufalme wa Shinari,+ Arioko mufalme wa Elasari, Kedorlaoma+ mufalme wa Elamu,+ na Tidali mufalme wa Goimu, 2 wafalme hao walipigana vita na Bera mufalme wa Sodoma,+ na Birsha mufalme wa Gomora,+ Shinabu mufalme wa Adma, na Shemeberi mufalme wa Seboimu,+ na mufalme wa Bela, ni kusema, Soari. 3 Hao wote waliweka majeshi yao pamoja katika Bonde* la Sidimu,+ ni kusema, Bahari ya Chumvi.*+

4 Walikuwa wamemutumikia Kedorlaoma kwa miaka kumi na mbili (12), lakini katika mwaka wa kumi na tatu (13) waliasi. 5 Kwa hiyo, katika mwaka wa kumi na ine (14), Kedorlaoma na wafalme wenye walikuwa pamoja naye walikuja na kushinda Warefaimu katika Ashterot-karnaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi+ katika Shave-kiriataimu, 6 na Wahori+ katika mulima wao wa Seiri+ mupaka El-parani, yenye kuwa katika jangwa. 7 Kisha waligeuka na kuenda En-mishpati, ni kusema, Kadeshi,+ na wakashinda eneo lote la Waamaleki+ na pia Waamori+ wenye walikuwa wanakaa katika Hasason-tamari.+

8 Halafu, mufalme wa Sodoma akapiga mwendo, na pia mufalme wa Gomora, mufalme wa Adma, mufalme wa Seboimu, na mufalme wa Bela, ni kusema, Soari, na wakajipanga kwa ajili ya vita katika Bonde* la Sidimu, 9 ili wapigane na Kedorlaoma mufalme wa Elamu, Tidali mufalme wa Goimu, Amrafeli mufalme wa Shinari, na Arioko mufalme wa Elasari+⁠—​wafalme ine (4) ili kupigana na wafalme tano (5). 10 Sasa Bonde* la Sidimu lilikuwa linajaa mashimo yenye kuwa na kabulimbo,* na wafalme wa Sodoma na Gomora walijaribu kukimbia na waliangukia ndani, na wale wenye walibakia walikimbilia kwenye eneo lenye milima. 11 Kisha wale wenye walipata ushindi wakakamata mali zote za Sodoma na Gomora na chakula chao chote na wakaenda zao.+ 12 Pia wakamukamata Loti, mwana wa ndugu ya Abramu mwenye alikuwa anakaa Sodoma,+ na pia wakakamata mali zake, na wakaendelea na safari yao.

13 Kisha mambo hayo mutu mwenye alikuwa ameponyoka akakuja kumuambia Abramu Mwebrania. Wakati huo alikuwa anakaa kati ya miti mikubwa ya Mamre ule Mwamori,+ ndugu ya Eshkoli na Aneri.+ Wanaume hao walikuwa wamefanya mapatano na* Abramu. 14 Basi Abramu akasikia kwamba mutu wa jamaa* yake+ amekamatwa mateka. Kwa hiyo akakusanya watu wake wenye kuzoezwa kupigana vita, watumishi mia tatu kumi na munane (318) wenye walizaliwa katika nyumba yake, na akawafuatilia mupaka Dani.+ 15 Wakati wa usiku, akagawanya jeshi lake, na yeye pamoja na watumishi wake wakawashambulia na kuwashinda. Na akawafuatilia mupaka Hoba, yenye kuwa upande wa kaskazini wa Damasko. 16 Na akakomboa mali zote, na pia akamukomboa Loti mutu wa jamaa yake, mali ya Loti, wanamuke, na watu wengine.

17 Wakati Abramu alirudia kisha kumushinda Kedorlaoma na wafalme wenye walikuwa pamoja naye, mufalme wa Sodoma akaenda kukutana na Abramu kwenye Bonde* la Shave, ni kusema, Bonde la Mufalme.+ 18 Na Melkisedeki+ mufalme wa Salemu+ akaleta mukate na divai; alikuwa kuhani wa Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi.+

19 Kisha akamubariki Abramu na kusema:

“Abramu abarikiwe na Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi,

Mutengenezaji wa mbingu na dunia;

20 Na atukuzwe Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi,

Mwenye ametia wakandamizaji wako katika mikono yako!”

Na Abramu akamupatia sehemu moja ya kumi (1/10) ya kila kitu.+

21 Kisha mambo hayo mufalme wa Sodoma akamuambia Abramu: “Unipatie wale watu,* lakini ujikamatie mali hizo.” 22 Lakini Abramu akamuambia mufalme wa Sodoma: “Ninainua mukono wangu ili kuapa kwa Yehova Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi, Mutengenezaji wa mbingu na dunia, 23 kwamba sitakamata kitu chochote chenye kuwa chako, kuanzia uzi mupaka kamba ya kiatu, ili usiseme, ‘Nimemufanya Abramu kuwa tajiri.’ 24 Sitakamata kitu isipokuwa tu kile chenye vijana wamekwisha kula. Na kuhusu fungu lenye linapaswa kupewa watu wenye walienda pamoja na mimi, Aneri, Eshkoli na Mamre+⁠—​acha wakamate fungu lao.”

15 Kisha mambo hayo neno la Yehova likakuja kwa Abramu katika maono, na kusema: “Usiogope,+ Abramu. Mimi ni ngao kwako.+ Zawabu yako itakuwa kubwa sana.”+ 2 Abramu akajibu: “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, utanipatia nini, kwa sababu ninaendelea kuwa bila mutoto na ule mwenye atariti nyumba yangu ni Eliezeri,+ mutu wa Damasko?” 3 Kisha Abramu akasema tena: “Haujanipatia uzao wowote,*+ na mutu* wa nyumba yangu atakuwa muriti wangu.” 4 Lakini angalia! Yehova akamujibu kwa maneno haya, “Mutu huyu hatakuwa muriti wako, lakini mwana wako mwenyewe* ndiye atakuwa muriti wako.”+

5 Sasa akamupeleka inje na kusema: “Tafazali, angalia juu mbinguni na uhesabie nyota, kama unaweza kufanya vile.” Kisha akamuambia: “Ni vile uzao wako utakuwa.”*+ 6 Naye akakuwa na imani katika Yehova,+ na Mungu akamuhesabia hilo kuwa haki.+ 7 Kisha akaongeza hivi: “Mimi ni Yehova, mwenye alikutosha katika Uru ya Wakaldayo ili nikupatie inchi hii kuwa uriti wako.”+ 8 Basi Abramu akasema: “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, nitajua namna gani kwamba nitariti inchi hiyo?” 9 Mungu akamujibu: “Unikamatie kitoto-dike cha ngombe cha miaka tatu (3), mbuzi-dike wa miaka tatu, kondoo-dume wa miaka tatu, njiwa-tetere, na njiwa mudogo.” 10 Kwa hiyo akakamata hao wote na kuwakata vipande mbili na akaweka kila kipande kikiwa chenye kuangaliana na kingine,* lakini hakukata ndege hao. 11 Kisha ndege wenye kuwinda wakaanza kushuka juu ya mizoga hiyo, lakini Abramu alikuwa anawafukuza.

12 Wakati jua lilikaribia kushuka, usingizi muzito ukaanguka juu ya Abramu na giza kubwa na lenye kuogopesha likashuka juu yake. 13 Kisha Mungu akamuambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa* wageni katika inchi yenye haiko yao na kwamba watu wa inchi hiyo watawafanya kuwa watumwa na watawatesa kwa miaka mia ine (400).+ 14 Lakini mimi nitahukumu taifa lenye watatumikia,+ na kisha wataondoka na mali nyingi.+ 15 Sasa wewe, utaenda kwa mababu zako kwa amani; utazikwa katika uzee muzuri.+ 16 Lakini wazao wako watarudia hapa+ katika kizazi cha ine (4), kwa sababu kosa la Waamori halijafikia bado kipimo chake kamili.”+

17 Wakati jua lilikuwa limeshuka na giza kubwa kuja, tanuru yenye kutoa moshi ikatokea, na mwenge wa moto ukapita katikati ya vile vipande. 18 Siku hiyo Yehova akafanya agano pamoja na Abramu,+ na kusema: “Nitapatia uzao wako* inchi hii,+ kutoka muto wa Misri mupaka ule muto mukubwa, muto Efrati:+ 19 inchi ya Wakeni,+ Wakenizi, Wakadmoni, 20 Wahiti,+ Waperizi,+ Warefaimu,+ 21 Waamori, Wakanaani, Wagirgashi, na Wayebusi.”+

16 Basi Sarai, bibi ya Abramu hakukuwa amemuzalia watoto,+ lakini alikuwa na mutumishi Mumisri mwenye jina lake lilikuwa Hagari.+ 2 Kwa hiyo Sarai akamuambia Abramu: “Tafazali unisikilize. Yehova amenizuia kuzaa watoto. Tafazali sasa, lala na mutumishi wangu. Pengine ninaweza kupata watoto kupitia yeye.”+ Kwa hiyo, Abramu akasikiliza mambo yenye Sarai alisema. 3 Kisha Abramu kuishi katika inchi ya Kanaani kwa miaka kumi (10), Sarai, bibi ya Abramu, akamuchukua Hagari, mutumishi wake Mumisri na kumupatia bwana yake Abramu akuwe bibi yake. 4 Kwa hiyo Abramu akalala na Hagari, na akapata mimba. Wakati alijua kwamba iko* na mimba, Hagari akaanza kumuzarau bimukubwa wake.

5 Kwa hiyo Sarai akamuambia Abramu: “Ubaya wenye ninatendewa ni kosa lako. Ni mimi nilimutia mutumishi wangu katika mikono yako,* lakini wakati alijua kwamba iko* na mimba, akaanza kunizarau. Yehova ahukumu kati yangu na wewe.” 6 Kwa hiyo Abramu akamuambia Sarai: “Angalia! Mutumishi wako iko* chini ya mamlaka yako. Umutendee jambo lolote lenye unaona kuwa la muzuri.” Basi Sarai akaanza kumuonea, na Hagari akakimbia mbali naye.

7 Kisha wakati fulani malaika wa Yehova akamukuta Hagari kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi yenye ilikuwa katika njia ya kuenda Shuri.+ 8 Naye akasema: “Hagari, mutumishi wa Sarai, unatoka wapi na unaenda wapi?” Naye akajibu: “Ninakimbia mbali na bimukubwa wangu Sarai.” 9 Kisha malaika wa Yehova akamuambia: “Rudia kwa bimukubwa wako na ujinyenyekeze chini ya mukono wake.” 10 Kisha malaika wa Yehova akamuambia: “Nitafanya uzao wako ukuwe mwingi* sana, na kwa hiyo haitawezekana kuhesabia uzao huo kwa sababu ya wingi wake.”+ 11 Malaika wa Yehova akaongeza kusema: “Sasa uko na mimba, na utazaa mwana, na utamupatia jina Ishmaeli,* kwa maana Yehova ameona mateso yako. 12 Atakuwa kama punda wa pori.* Mukono wake utapigana na kila mutu; na mukono wa kila mutu utapigana naye, na atakaa akiwa mwenye kuangaliana na ndugu* zake wote.”

13 Kisha akaitia jina la Yehova, mwenye alikuwa anazungumuza naye: “Wewe ni Mungu mwenye kuona,”+ kwa maana alisema: “Je, kweli nimemuona yeye mwenye kuniona?” 14 Ndiyo sababu kisima hicho kiliitwa Beer-lahai-roi.* (Kiko kati ya Kadeshi na Beredi.) 15 Basi Hagari akamuzalia Abramu mwana, na Abramu akamupatia mwana wake, mwenye Hagari alizaa, jina Ishmaeli.+ 16 Abramu alikuwa na miaka makumi munane na sita (86) wakati Hagari alimuzaa Ishmaeli.

17 Wakati Abramu alikuwa na miaka makumi kenda na kenda (99), Yehova akamutokea Abramu na kumuambia: “Mimi ni Mungu Mweza-Yote. Tembea mbele yangu na ujionyeshe kuwa hauna kosa.* 2 Nitatia agano langu kati yangu na wewe,+ na nitakufanya uongezeke sana, tena sana.”+

3 Basi Abramu akaanguka uso chini, na Mungu akaendelea kuzungumuza naye, na kusema: 4 “Kwa upande wangu, angalia! agano langu liko pamoja na wewe,+ na hakika utakuwa baba ya mataifa mengi.+ 5 Jina lako halitakuwa tena Abramu;* jina lako litakuwa Abrahamu,* kwa sababu nitakufanya kuwa baba ya mataifa mengi. 6 Nitakufanya uzae sana, tena sana na nitakufanya kuwa mataifa mengi, na wafalme watatoka ndani yako.+

7 “Na nitatimiza agano langu kati yangu na wewe+ na uzao wako* kisha wewe katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya agano la milele, ili nikuwe Mungu wako na Mungu wa uzao wako* kisha wewe. 8 Na nitakupatia wewe na uzao wako* kisha wewe inchi yenye umeishi ndani yake ukiwa mugeni+⁠—​inchi yote ya Kanaani⁠—​ili ikuwe uriti wa kudumu, na mimi nitakuwa Mungu wao.”+

9 Tena Mungu akamuambia Abrahamu: “Sasa wewe, unapaswa kushika agano langu, wewe na uzao wako* kisha wewe katika vizazi vyao vyote. 10 Hili ndilo agano langu kati yangu na wewe, lenye wewe na uzao wako* kisha wewe mutashika: Kila mwanaume kati yenu anapaswa kutahiriwa.+ 11 Munapaswa kutahiriwa nyama ya magovi* yenu, na itakuwa alama ya agano kati yangu na ninyi.+ 12 Katika vizazi vyenu vyote, kila mwanaume kati yenu mwenye kuwa na siku munane (8) anapaswa kutahiriwa,+ kila mutu mwenye alizaliwa katika nyumba na kila mutu mwenye haiko wa uzao wako* na mwenye alinunuliwa kwa feza kutoka kwa mugeni. 13 Kila mwanaume mwenye alizaliwa katika nyumba yako na kila mwanaume mwenye alinunuliwa kwa feza zako anapaswa kutahiriwa,+ na agano langu katika miili yenu litakuwa agano la kudumu. 14 Kila mwanaume mwenye hatatahiriwa nyama ya govi* lake, mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katikati ya watu wake. Amevunja agano langu.”

15 Kisha Mungu akamuambia Abrahamu: “Kuhusu Sarai bibi yako,+ usimuite tena Sarai,* lakini jina lake litakuwa Sara.* 16 Nitamubariki na pia nitakupatia mwana kupitia yeye;+ nitamubariki Sara, na atakuwa mataifa mengi; wafalme wa vikundi vya watu watatoka ndani yake.” 17 Basi Abrahamu akaanguka uso chini na akaanza kucheka na kusema katika moyo wake:+ “Je, mwanaume wa miaka mia moja (100) atazaa mutoto, na Sara, mwanamuke wa miaka makumi kenda (90), atazaa?”+

18 Kwa hiyo Abrahamu akamuambia Mungu wa kweli: “Aa! acha Ishmaeli aishi mbele yako!”+ 19 Basi Mungu akasema: “Sara bibi yako kwa kweli atakuzalia mwana, na utamupatia jina Isaka.*+ Na mimi nitafanya agano langu pamoja naye kuwa agano la milele kwa uzao wake* kisha yeye.+ 20 Lakini kuhusu Ishmaeli, nimekusikia. Angalia! nitamubariki na nitamufanya azae na nitamufanya aongezeke sana, tena sana. Atatokeza wakubwa kumi na mbili (12), na nitamufanya kuwa taifa kubwa.+ 21 Lakini, nitafanya agano langu pamoja na Isaka,+ mwenye Sara atakuzalia mwaka kesho kwa wakati huu wenye uliwekwa.”+

22 Wakati Mungu alimaliza kuzungumuza na Abrahamu, akapanda juu na kumuacha Abrahamu. 23 Kisha Abrahamu akamuchukua Ishmaeli mwana wake na wanaume wote wenye walizaliwa katika nyumba yake na kila mutu mwenye alikuwa amemununua kwa feza, kila mwanaume katika nyumba ya Abrahamu, naye akawatahiri nyama ya magovi* yao siku hiyohiyo, kama vile Mungu alikuwa amemuambia.+ 24 Abrahamu alikuwa na miaka makumi kenda na kenda (99) wakati alitahiriwa nyama ya govi* lake.+ 25 Na Ishmaeli mwana wake alikuwa na miaka kumi na tatu (13) wakati alitahiriwa nyama ya govi* lake.+ 26 Siku hiyohiyo, Abrahamu alitahiriwa na pia Ishmaeli mwana wake. 27 Wanaume wote wa nyumba yake, kila mutu mwenye alizaliwa katika nyumba na kila mutu mwenye alinunuliwa kwa feza kutoka kwa mugeni, walitahiriwa siku hiyohiyo pamoja na Abrahamu.

18 Kisha mambo hayo, Yehova+ akamutokea kati ya miti mikubwa ya Mamre,+ wakati alikuwa amekaa kwenye muingilio wa hema wakati wa joto kali sana la muchana. 2 Akainua macho yake na akaona wanaume watatu (3) wenye walikuwa wamesimama mbali kidogo naye.+ Wakati aliwaona, akatoka kwenye muingilio wa hema na kukimbia ili kukutana nao, naye akainama mupaka chini. 3 Kisha akasema: “Yehova, kama nimekubaliwa mbele ya macho yako, tafazali usipite bila kusimama kwa mutumishi wako. 4 Tafazali, acha maji kidogo yaletwe na munawishwe miguu yenu,+ kisha mukae chini ya muti. 5 Kwa sababu mumekuja hapa kwa mutumishi wenu, muache nilete kipande cha mukate ili mupate nguvu mupya.* Kisha, munaweza kuendelea na safari yenu.” Basi wanaume hao wakasema: “Sawa. Unaweza kufanya kama vile umesema.”

6 Basi Abrahamu akaenda mbio kwenye hema mahali Sara alikuwa na kusema: “Fanya haraka! Kamata vipimo tatu (3)* vya unga muzuri, tengeneza donge, na ufanye mikate.” 7 Kisha Abrahamu akakimbia mahali mifugo yake ilikuwa na akachagua ngombe-dume mudogo, muzuri na mwenye kuwa teketeke. Akamupatia mutumishi, naye akafanya haraka ili kumutayarisha. 8 Kisha akakamata siagi na maziwa na ule ngombe-dume mudogo mwenye alikuwa ametayarisha na akaweka chakula mbele yao. Kisha akasimama pembeni yao chini ya muti wakati walikuwa wanakula.+

9 Wakasema: “Sara bibi yako+ iko* wapi?” Akajibu: “Iko* hapa ndani ya hema.” 10 Kwa hiyo mumoja wao akaendelea kusema: “Hakika nitarudia kwako mwaka kesho wakati kama huu, na angalia! bibi yako Sara atakuwa na mwana.”+ Na Sara alikuwa anasikiliza kwenye muingilio wa hema, wenye ulikuwa nyuma ya mwanaume huyo. 11 Abrahamu na Sara walikuwa wazee, walikuwa wameishi miaka mingi.+ Sara alikuwa amepita miaka ya kuzaa watoto.*+ 12 Kwa hiyo Sara akaanza kucheka yeye mwenyewe, na kusema: “Nimezeeka na bwana wangu amezeeka, je, kweli nitapata raha hii?”+ 13 Kisha Yehova akamuambia Abrahamu: “Sababu gani Sara amecheka na kusema, ‘Je, kweli mimi nitazaa hata kama nimezeeka?’ 14 Je, kuko jambo la ajabu sana kwa Yehova?+ Nitarudia kwako mwaka kesho wakati kama huu wenye uliwekwa, na Sara atakuwa na mwana.” 15 Lakini Sara akakataa, kwa kusema: “Sikucheka!” kwa sababu aliogopa. Lakini akamuambia: “Ndiyo! ulicheka.”

16 Wakati wanaume hao walisimama ili kuondoka na wakaangalia kuelekea upande wa Sodoma,+ Abrahamu alikuwa anatembea pamoja nao ili kuwasindikiza. 17 Yehova akasema: “Je, nimufiche Abrahamu jambo lenye ninataka kufanya?+ 18 Angalia, hakika Abrahamu atakuwa taifa kubwa na lenye nguvu, na mataifa yote ya dunia yatabarikiwa* kupitia yeye.+ 19 Kwa maana nimefikia kumujua ili aamuru wana wake na nyumba yake kisha yeye kushika njia ya Yehova kwa kutenda mambo yenye kuwa sawa na ya haki,+ ili Yehova atimize mambo yenye ameahidi kuhusu Abrahamu.”

20 Kisha Yehova akasema: “Malalamiko juu ya Sodoma na Gomora ni makubwa sana,+ na zambi yao ni nzito sana.+ 21 Nitashuka ili nione kama wanatenda kulingana na malalamiko yenye yalinifikia. Na kama haiko vile, nitajua jambo hilo.”+

22 Kisha wanaume hao wakatoka pale na kuelekea Sodoma, lakini Yehova+ akabakia pamoja na Abrahamu. 23 Kisha Abrahamu akamukaribia na kusema: “Je, kweli utaharibu mwenye haki pamoja na muovu?+ 24 Tuseme katika muji huo kuko watu makumi tano (50) wenye haki. Je, utawaharibu na hautasamehe mahali pale kwa sababu ya watu makumi tano wenye haki wenye wanapatikana katika muji huo? 25 Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba unaweza kutenda kwa namna hiyo kwa kumuua mwenye haki pamoja na muovu na hivyo mwenye haki apatwe na jambo lilelile lenye kumupata muovu!+ Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa juu yako.+ Je, Muamuzi wa dunia yote hatatenda jambo lenye kuwa sawa?”+ 26 Kisha Yehova akasema: “Nikipata katika Sodoma watu makumi tano (50) wenye haki katika muji huo, nitasamehe mahali pale pote kwa sababu yao.” 27 Lakini Abrahamu akajibu tena: “Tafazali, angalia, nimejaribu kusema na Yehova, hata kama mimi ni mavumbi na majivu. 28 Tuseme kunakosa watano (5) juu ya wale makumi tano (50) wenye haki. Je, utaharibu muji wote kwa sababu ya wale watano?” Akajibu: “Sitaharibu muji nikipata ndani yake watu makumi ine na tano (45).”+

29 Lakini akasema tena: “Tuseme watu makumi ine (40) wanapatikana ndani yake.” Akajibu: “Sitafanya vile kwa sababu ya wale watu makumi ine.” 30 Lakini akaendelea kusema: “Tafazali Yehova, usiwake kasirani,+ lakini acha niendelee kusema: Tuseme watu makumi tatu (30) tu ndio wanapatikana ndani yake.” Akajibu: “Sitafanya vile nikipata watu makumi tatu ndani yake.” 31 Lakini akaendelea kusema: “Tafazali, angalia, nimejaribu kusema na Yehova: Tuseme watu makumi mbili (20) tu ndio wanapatikana ndani yake.” Akajibu: “Sitaharibu muji kwa sababu ya wale watu makumi mbili.” 32 Mwishowe akasema: “Tafazali Yehova, usiwake kasirani, lakini acha niseme mara ingine tena: Tuseme watu kumi (10) tu ndio wanapatikana ndani yake.” Akajibu: “Sitaharibu muji kwa sababu ya wale watu kumi.” 33 Wakati Yehova alimaliza kusema na Abrahamu, akaenda,+ na Abrahamu akarudia kwake.

19 Wale malaika wawili wakafika Sodoma wakati wa mangaribi, na Loti alikuwa amekaa katika mulango mukubwa wa Sodoma. Wakati Loti aliwaona, akasimama ili kuenda kukutana nao na akainamisha uso wake mupaka chini.+ 2 Na akasema: “Mabwana wangu, tafazali, mugeuke na muingie katika nyumba ya mutumishi wenu na mukae usiku wote na munawishwe miguu yenu. Kisha munaweza kuamuka asubui sana na kuendelea na safari yenu.” Nao wakasema: “Hapana, tutabakia usiku wote katika kiwanja cha watu wote.” 3 Lakini akawalilia sana mupaka wakaenda pamoja naye katika nyumba yake. Kisha akawafanyia karamu, na akapika mikate yenye haina chachu, nao wakakula.

4 Mbele walale, wanaume wa muji⁠—​wanaume wa Sodoma kuanzia kijana mwanaume mupaka muzee, wote⁠—​wakajikusanya pamoja na kuzunguka nyumba. 5 Na wakaendelea kumuita Loti na kumuambia: “Wako wapi wale wanaume wenye waliingia kwako usiku wa leo? Uwalete inje ili tufanye ngono nao.”+

6 Kisha Loti akaenda inje kwenye walikuwa, kwenye muingilio, na akafunga mulango nyuma yake. 7 Akasema: “Tafazali, ndugu zangu, musitende kwa uovu. 8 Tafazali, hapa niko na mabinti wawili wenye hakuna siku wamefanya ngono na mwanaume. Tafazali, muache niwalete inje kwenu ili muwatendee jambo lolote lenye munaona kuwa muzuri. Lakini musiwatendee jambo lolote wanaume hawa, kwa maana wamekuja chini ya ulinzi wa* nyumba yangu.”+ 9 Lakini wakasema: “Utupitishe!” Na wakaendelea kusema: “Mugeni huyu mwenye kuwa peke yake alikuja kuishi hapa, na sasa anapima kutuhukumu! Sasa tutakutendea mubaya zaidi kuliko wao.” Nao wakasongamana kumuzunguka Loti na wakasonga mbele ili kuvunja mulango. 10 Kwa hiyo wale wanaume wakanyoosha mikono yao na kumuingiza Loti ndani ya nyumba, na wakafunga mulango. 11 Lakini malaika hao wakawapiga kwa upofu wanaume wenye walikuwa kwenye muingilio wa nyumba, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, na hivyo wakachoka kujaribu kutafuta muingilio wa nyumba.

12 Kisha wanaume hao wakamuambia Loti: “Je, uko na mutu mwingine hapa? Wana-wakwe zako, watoto wako wanaume, watoto wako wanamuke, na watu wako wote katika muji, uwatoshe hapa! 13 Kwa maana tutaharibu mahali hapa, kwa sababu kilio juu yao kimekuwa kikubwa sana mbele ya Yehova,+ ndiyo maana Yehova ametutuma tuharibu muji.” 14 Kwa hiyo Loti akaenda inje na kuanza kusema na wana-wakwe zake wenye wangeoa mabinti wake, na akaendelea kusema: “Musimame! Mutoke mahali hapa, kwa sababu Yehova ataharibu muji huu!” Lakini mbele ya wana-wakwe zake, alionekana kuwa anafanya muzaha.+

15 Wakati kulipambazuka,* malaika walimuambia Loti afanye haraka, kwa kusema: “Simama! Chukua bibi yako na watoto wako wanamuke wawili wenye wako hapa pamoja na wewe, ili musiharibiwe katika kosa la muji huu!”+ 16 Wakati Loti aliendelea kukawia, basi kwa sababu Yehova alimusikilia huruma,+ wale wanaume wakakamata mukono wake na mukono wa bibi yake na mikono ya watoto wake wanamuke wawili, na wakamupeleka na kumusimamisha inje ya muji.+ 17 Wakati tu walikuwa wamewapeleka sehemu za pembeni-pembeni za muji, mumoja wao akasema: “Kimbia ili kuokoa uzima wako!* Usiangalie nyuma+ na usisimame mahali popote katika wilaya!+ Kimbilia kwenye eneo lenye milima ili usiharibiwe!”

18 Kisha Loti akawaambia: “Tafazali, Yehova, hapana kule! 19 Tafazali, sasa, mutumishi wako amekubaliwa mbele ya macho yako na unanionyesha fazili nyingi* kwa kulinda uzima wangu,*+ lakini siwezi kukimbilia kwenye eneo lenye milima kwa sababu ninaogopa kama jambo la mubaya linaweza kunipata na nikufe.+ 20 Tafazali, sasa, muji huu uko karibu na ninaweza kukimbilia kule, ni muji mudogo tu. Tafazali, je, ninaweza kukimbilia kule? Ni muji mudogo tu. Halafu nitaokoka.”* 21 Kwa hiyo akamuambia Loti: “Sawa, nitakuonyesha ufikirio pia+ kwa kutokuharibu muji wenye unazungumuzia.+ 22 Fanya haraka! Kimbilia kule, kwa sababu siwezi kufanya jambo lolote mupaka ufike kule!”+ Ndiyo sababu alipatia muji huo jina Soari.*+

23 Jua lilikuwa limetokea juu ya inchi wakati Loti alifika Soari. 24 Kisha Yehova akafanya kiberiti na moto inyeshe juu ya Sodoma na Gomora⁠—​moto ulitoka kwa Yehova, ulitoka mbinguni.+ 25 Kwa hiyo akaharibu miji hiyo, ndiyo, wilaya hiyo yote, pamoja na wakaaji wote wa miji hiyo na mimea ya inchi.+ 26 Lakini bibi ya Loti, mwenye alikuwa nyuma ya Loti, akaanza kuangalia nyuma, naye akakuwa nguzo ya chumvi.+

27 Sasa Abrahamu akaamuka asubui sana na kuenda mahali alikuwa amesimama mbele ya Yehova.+ 28 Wakati aliangalia kuelekea upande wa Sodoma na Gomora na inchi yote ya wilaya hiyo, akaona jambo la kushangaza. Kulikuwa moshi muzito wenye ulikuwa unapanda kutoka katika inchi kama moshi muzito wa tanuru!+ 29 Kwa hiyo wakati Mungu aliharibu miji ya wilaya hiyo, Mungu alimukumbuka Abrahamu kwa kumutosha Loti katika miji hiyo yenye aliharibu, miji yenye Loti alikuwa ameishi ndani yake.+

30 Kisha wakati fulani Loti pamoja na mabinti wake wawili wakatoka Soari na kuanza kuishi katika eneo lenye milima,+ kwa sababu aliogopa kuishi Soari.+ Kwa hiyo akaanza kuishi katika pango pamoja na mabinti wake wawili. 31 Na muzaliwa wa kwanza akamuambia mudogo yake: “Baba yetu amezeeka, na hakuna mwanaume katika inchi hii wa kulala na sisi kulingana na desturi ya dunia yote. 32 Kuja, tumupatie baba yetu divai akunywe, na kisha tulale naye ili tuchunge uzao kutoka kwa baba yetu.”

33 Kwa hiyo usiku huo wakaendelea kumupatia baba yao divai akunywe; kisha ule muzaliwa wa kwanza akaingia na kulala na baba yake, lakini baba yake hakujua wakati binti yake alilala na wakati binti yake aliamuka. 34 Siku ya kufuata, ule muzaliwa wa kwanza akamuambia mudogo yake: “Angalia, nililala na baba yangu jana usiku. Tumupatie divai akunywe usiku wa leo pia. Kisha wewe utaingia na kulala naye, ili tuchunge uzao kutoka kwa baba yetu.” 35 Kwa hiyo usiku huo pia, wakaendelea kumupatia baba yao divai akunywe; kisha ule mudogo akaenda na kulala na baba yake, lakini baba yake hakujua wakati binti yake alilala na wakati binti yake aliamuka. 36 Kwa hiyo mabinti wote wawili wa Loti wakakuwa na mimba ya baba yao. 37 Ule muzaliwa wa kwanza akamuzaa mwana, akamupatia jina Moabu.+ Yeye ndiye baba ya Wamoabu wa leo.+ 38 Ule mudogo pia akamuzaa mwana, akamupatia jina Ben-ami. Yeye ndiye baba ya Waamoni+ wa leo.

20 Sasa Abrahamu akahamisha kambi yake kutoka kule+ mupaka inchi ya Negebu na akaanza kuishi katikati ya Kadeshi+ na Shuri.+ Wakati alikuwa anakaa* Gerari,+ 2 Abrahamu akasema tena juu ya Sara bibi yake: “Yeye ni dada yangu.”+ Kwa hiyo Abimeleki mufalme wa Gerari akatuma watu wamulete Sara na akamuchukua.+ 3 Kisha, Mungu akamutokea Abimeleki usiku katika ndoto na kumuambia: “Angalia, wewe ni kama tu umekufa kwa sababu ya mwanamuke mwenye ulichukua,+ kwa maana yeye ni mwenye kuolewa na ni bibi ya mwanaume mwingine.”+ 4 Lakini, Abimeleki alikuwa hajamukaribia.* Kwa hiyo akasema: “Yehova, je, utaua taifa lenye halina kosa kabisa?* 5 Je, Abrahamu hakuniambia, ‘Yeye ni dada yangu,’ na je, Sara pia hakusema, ‘Yeye ni ndugu yangu’? Nilifanya jambo hilo kwa moyo muzuri na kwa mikono yenye haina kosa.” 6 Basi Mungu wa kweli akamuambia katika ndoto: “Ninajua kwamba ulifanya vile kwa moyo muzuri, kwa hiyo nilikuzuia usinitendee zambi. Ndiyo sababu sikukuruhusu umuguse. 7 Sasa rudisha bibi ya mwanaume huyo, kwa maana mwanaume huyo ni nabii,+ atamulilia Mungu* kwa ajili yako+ na utaendelea kuishi. Lakini kama haumurudishe, ujue kama hakika utakufa, wewe na watu wote wa nyumba yako.”

8 Abimeleki akaamuka asubui sana na akaita watumishi wake wote na akawaambia mambo hayo yote, nao wakaogopa sana. 9 Kisha Abimeleki akamuita Abrahamu na kumuambia: “Ni jambo gani hili umetutendea? Ni zambi gani nimekutendea ili ulete juu yangu na juu ya ufalme wangu zambi kubwa kama hii? Jambo lenye umenitendea haliko sawa.” 10 Na Abimeleki akaendelea kumuambia Abrahamu: “Ulikuwa na nia gani wakati ulifanya jambo hilo?”+ 11 Abrahamu akasema: “Ilikuwa kwa sababu nilisema katika moyo wangu, ‘Hakuna kabisa woga wa Mungu mahali hapa, na wataniua kwa sababu ya bibi yangu.’+ 12 Na tena, yeye kwa kweli ni dada yangu, ni binti ya baba yangu lakini haiko binti ya mama yangu, naye akakuwa bibi yangu.+ 13 Kwa hiyo wakati Mungu alinifanya nitange-tange mbali na nyumba ya baba yangu,+ nilimuambia Sara: ‘Ni hivi utakuwa unanionyesha upendo mushikamanifu: Kila mahali kwenye tutaenda, sema hivi juu yangu, ‘Yeye ni ndugu yangu.”’”+

14 Basi Abimeleki akakamata kondoo na ngombe na watumishi wanaume na watumishi wanamuke na akamupatia Abrahamu, na Abimeleki akamurudishia Abrahamu bibi yake Sara. 15 Tena Abimeleki akasema: “Angalia, inchi yangu iko mbele yako. Kaa mahali popote kwenye unapenda.” 16 Na akamuambia Sara: “Angalia, ninamupatia ndugu yako vipande elfu moja (1 000) vya feza.+ Ni alama kwa wote wenye kuwa pamoja na wewe na mbele ya kila mutu kwamba hauna kosa, na umeondolewa lawama.” 17 Na Abrahamu akaanza kumulilia* Mungu wa kweli, na Mungu akamuponyesha Abimeleki na bibi yake na watumwa wake wanamuke, nao wakaanza kupata watoto; 18 kwa maana Yehova alikuwa amefanya wanamuke wote wa nyumba ya Abimeleki wakuwe tasa* kwa sababu ya Sara, bibi ya Abrahamu.+

21 Yehova akaelekeza uangalifu wake juu ya Sara kama vile alikuwa amesema, na Yehova akamutendea Sara jambo lenye alikuwa ameahidi.+ 2 Kwa hiyo Sara akakuwa na mimba,+ kisha akamuzalia Abrahamu mwana katika miaka yake ya uzee kwa wakati wenye uliwekwa, wenye Mungu alikuwa amemuahidi.+ 3 Abrahamu akamupatia mwana wake mwenye alizaliwa jina Isaka,+ mwenye Sara alikuwa amemuzalia. 4 Na Abrahamu akamutahiri Isaka mwana wake wakati alikuwa na umri wa siku munane (8), kama vile Mungu alikuwa amemuamuru.+ 5 Abrahamu alikuwa na miaka mia moja (100) wakati Isaka mwana wake alizaliwa. 6 Kisha Sara akasema: “Mungu ameniletea kicheko; kila mutu mwenye atasikia jambo hili atacheka pamoja na mimi.”* 7 Naye akaendelea kusema: “Ni nani angeweza kumuambia Abrahamu, ‘Sara hakika atanyonyesha watoto’? Lakini, nimemuzalia mwana katika miaka yake ya uzee.”

8 Sasa mutoto huyo akaendelea kukomaa na akaachishwa kunyonya, na Abrahamu akatayarisha karamu kubwa siku yenye Isaka aliachishwa kunyonya. 9 Lakini Sara alikuwa anaona namna mwana wa Hagari+ Mumisri, mwenye Hagari alimuzalia Abrahamu, alikuwa anamuchekelea Isaka.+ 10 Kwa hiyo Sara akamuambia Abrahamu: “Fukuza huyu mutumwa mwanamuke pamoja na mwana wake, kwa maana mwana wa huyu mutumwa mwanamuke hatakuwa muriti pamoja na mwana wangu, pamoja na Isaka!”+ 11 Lakini jambo lenye Sara alisema juu ya mwana wake lilimuchukiza sana Abrahamu.+ 12 Kisha Mungu akamuambia Abrahamu: “Usichukizwe na jambo lenye Sara anasema juu ya kijana huyo na juu ya mutumwa wako mwanamuke. Umusikilize,* kwa maana ule wenye utaitwa uzao wako utakuja* kupitia Isaka.+ 13 Na kuhusu mwana wa ule mutumwa mwanamuke,+ nitafanya pia taifa litoke ndani yake,+ kwa sababu yeye ni uzao wako.”*

14 Kwa hiyo Abrahamu akaamuka asubui sana na kukamata mukate na chupa ya ngozi ya maji na kumupatia Hagari. Akaweka vitu hivyo kwenye bega la Hagari na kisha akamuacha aende pamoja na mwana wake.+ Kwa hiyo Hagari akaondoka na kutanga-tanga katika jangwa la Beer-sheba.+ 15 Mwishowe maji yenye yalikuwa ndani ya chupa ya ngozi yakaisha, na akamusukuma kijana huyo mwanaume chini ya moja kati ya miti midogo-midogo. 16 Kisha akaenda na kukaa chini peke yake, karibu umbali wa mahali mushale unaweza kufika wakati unatupwa, kwa sababu alisema: “Sitaki kuona namna kijana huyu mwanaume atakufa.” Kwa hiyo akakaa chini mbali kidogo na akaanza kulalamika kwa sauti kubwa na kulia.

17 Basi Mungu akasikia sauti ya kijana huyo mwanaume,+ na malaika wa Mungu akamuita Hagari kutoka mbinguni na akamuambia:+ “Uko na shida gani, Hagari? Usiogope, kwa sababu Mungu amesikia sauti ya kijana pale kwenye iko.* 18 Simama, inua huyo kijana na umushike kwa mukono wako, kwa maana nitamufanya kuwa taifa kubwa.”+ 19 Kisha Mungu akafungua macho yake na akaona kisima cha maji, na akaenda na kujaza maji ndani ya chupa ya ngozi naye akamupatia kijana akunywe. 20 Na Mungu akaendelea kuwa pamoja na kijana huyo+ kadiri aliendelea kukomaa. Aliishi katika jangwa na alikuwa mupiga-mishale. 21 Akaenda kuishi katika jangwa la Parani,+ na mama yake akamuchukulia bibi katika inchi ya Misri.

22 Wakati huo Abimeleki pamoja na Fikoli mukubwa wa jeshi lake wakamuambia Abrahamu: “Mungu iko* pamoja na wewe katika kila jambo lenye unafanya.+ 23 Basi sasa uniapie hapa mbele ya Mungu kwamba hautanitendea kwa udanganyifu mimi na uzao wangu na kizazi changu, na kwamba utanitendea mimi na inchi yenye umekuwa ukiishi ndani yake kwa upendo uleule mushikamanifu wenye nimekuonyesha.”+ 24 Kwa hiyo Abrahamu akasema: “Ninaapa.”

25 Lakini, Abrahamu akamulaumu Abimeleki kuhusu kisima cha maji chenye watumishi wa Abimeleki walikuwa wamekamata kwa nguvu.+ 26 Abimeleki akajibu: “Sijue mwenye alifanya jambo hilo, haukuniambia jambo hilo, na kufikia leo nilikuwa sijasikia habari yoyote juu ya jambo hilo.” 27 Basi Abrahamu akakamata kondoo na ngombe akamupatia Abimeleki, na wao wawili wakafanya agano. 28 Wakati Abrahamu aliweka pembeni wana-kondoo dike saba (7) kutoka katika kundi, 29 Abimeleki akamuambia Abrahamu: “Sababu gani umewaweka hapa peke yao hawa wana-kondoo dike saba (7)?” 30 Kisha Abrahamu akasema: “Unapaswa kukubali hawa wana-kondoo dike saba (7) kutoka katika mukono wangu kuwa ushahidi kwamba mimi ndiye nilichimba kisima hiki.” 31 Ndiyo maana alipatia mahali pale jina Beer-sheba,*+ kwa sababu wote wawili walikuwa wamefanya kiapo mahali pale. 32 Kwa hiyo wakafanya agano+ kule Beer-sheba, kisha Abimeleki akasimama pamoja na Fikoli mukubwa wa jeshi lake, nao wakarudia katika inchi ya Wafilisti.+ 33 Kisha mambo hayo Abrahamu akapanda muti wa mukwaju kule Beer-sheba na kule akaitia jina la Yehova,+ Mungu wa milele.+ 34 Na Abrahamu akaishi* katika inchi ya Wafilisti kwa muda murefu.*+

22 Kisha mambo hayo Mungu wa kweli akamujaribu Abrahamu,+ na akamuambia: “Abrahamu!” naye akajibu: “Mimi huyu!” 2 Kisha Mungu akamuambia: “Tafazali, chukua mwana wako Isaka,+ mwana wako wa pekee mwenye unapenda sana,+ na ufunge safari kuenda kwenye inchi ya Moria+ na kule umutoe kuwa toleo la kuteketezwa juu ya mulima mumoja kati ya milima yenye nitakuonyesha.”

3 Kwa hiyo Abrahamu akaamuka asubui sana na akatandika punda wake na kuchukua watumishi wake wawili pamoja na Isaka mwana wake. Akapasua kuni kwa ajili ya toleo la kuteketezwa, na kisha akasimama na kufunga safari kuenda mahali kwenye Mungu wa kweli alimuonyesha. 4 Siku ya tatu (3), Abrahamu akainua macho na kuona kwa mbali mahali pale. 5 Sasa Abrahamu akaambia watumishi wake: “Ninyi mubakie hapa pamoja na punda, lakini mimi na kijana huyu tutaenda kule na kuabudu na tutarudia hapa kwenye muko.”

6 Kwa hiyo Abrahamu akakamata kuni kwa ajili ya toleo la kuteketezwa na akazibebesha Isaka mwana wake. Kisha akakamata moto na kisu* katika mikono yake, na wote wawili wakaenda pamoja kwa miguu. 7 Kisha Isaka akamuambia Abrahamu baba yake: “Baba yangu!” Naye akasema: “Ndiyo, mwana wangu!” Kwa hiyo Isaka akaendelea kusema: “Hapa kuko moto na kuni, lakini kondoo kwa ajili ya toleo la kuteketezwa iko* wapi?” 8 Abrahamu akajibu: “Mwana wangu, Mungu mwenyewe atatoa kondoo kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.”+ Na wote wawili wakaendelea kutembea pamoja.

9 Mwishowe wakafika mahali Mungu wa kweli alikuwa amemuonyesha, na Abrahamu akajenga mazabahu pale na akapanga kuni juu yake. Akamufunga Isaka mwana wake mikono na miguu na kumutia kwenye mazabahu juu ya zile kuni.+ 10 Kisha Abrahamu akanyoosha mukono wake na kukamata kile kisu* ili amuue mwana wake.+ 11 Lakini malaika wa Yehova akamuita kutoka mbinguni na kusema: “Abrahamu, Abrahamu!” naye akajibu: “Mimi huyu!” 12 Mwishowe akasema: “Usimuue kijana huyo, na usimutendee jambo lolote kabisa, kwa maana sasa ninajua kwamba unamuogopa Mungu kwa kuwa haukunikatalia mwana wako, mwana wako wa pekee.”+ 13 Basi Abrahamu akainua macho, na pale tu mbele yake kulikuwa kondoo-dume mwenye alikuwa amekamatwa kwa pembe zake katika miti midogo-midogo.* Kwa hiyo Abrahamu akaenda na kumukamata kondoo-dume huyo na kumutoa kuwa toleo la kuteketezwa pa nafasi ya mwana wake. 14 Abrahamu akaita mahali pale Yehova-yire.* Ndiyo sababu mupaka leo watu wangali wanasema: “Katika mulima wa Yehova mambo ya lazima yatatolewa.”+

15 Na malaika wa Yehova akamuita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni, 16 na kusema: “‘Ninaapa kwa jina langu,’ ni vile Yehova anasema,+ ‘kwa kuwa umetenda jambo hilo na haukunikatalia mwana wako, mwana wako wa pekee,+ 17 hakika nitakubariki na hakika nitafanya uzao wako ukuwe mwingi* kama nyota za mbinguni na kama chembe za muchanga pembeni ya bahari,+ na uzao wako utariti* mulango mukubwa wa* maadui wake.+ 18 Na kupitia uzao wako*+ mataifa yote ya dunia yatajipatia baraka kwa sababu umesikiliza sauti yangu.’”+

19 Kisha mambo hayo Abrahamu akarudia mahali watumishi wake walikuwa, na wakasimama na kurudia pamoja Beer-sheba;+ na Abrahamu akaendelea kuishi Beer-sheba.

20 Kisha mambo hayo Abrahamu akaambiwa: “Angalia, Milka pia amemuzalia Nahori ndugu yako wana:+ 21 Usi muzaliwa wake wa kwanza, Buzi ndugu yake, Kemueli baba ya Aramu, 22 Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu, na Betueli.”+ 23 Betueli akamuzaa Rebeka.+ Milka alimuzalia Nahori ndugu ya Abrahamu watoto hao wanaume munane (8). 24 Suria wake,* mwenye jina lake lilikuwa Reuma, yeye pia alimuzalia watoto wanaume: Teba, Gahamu, Tahashi, na Maaka.

23 Na Sara aliishi miaka mia moja makumi mbili na saba (127); hiyo ndiyo ilikuwa miaka ya maisha ya Sara.+ 2 Basi Sara akakufa kule Kiriat-arba,+ ni kusema, Hebroni,+ katika inchi ya Kanaani,+ na Abrahamu akaanza kumuombolezea na kumulia Sara. 3 Kisha Abrahamu akatoka mbele ya bibi yake mwenye alikuwa amekufa na akaambia wana wa Heti:+ 4 “Niko mugeni na muhamiaji kati yenu.+ Munipatie mahali pa kuzikia katikati yenu ili niweze kuondoa mufu wangu na kumuzika.” 5 Basi wana wa Heti wakamujibu Abrahamu: 6 “Utusikie, Bwana wangu, wewe ni mukubwa wa Mungu* kati yetu.+ Unaweza kumuzika mufu wako mahali pazuri zaidi katika maeneo yetu ya kuzikia. Hakuna mutu kati yetu mwenye atakukatalia mahali pake pa kuzikia ili usizike mufu wako.”

7 Kwa hiyo Abrahamu akasimama na kuinama mbele ya watu wa inchi, mbele ya wana wa Heti,+ 8 na kuwaambia: “Kama munakubali kuniacha niondoe mufu wangu ili kumuzika, basi munisikilize na mumuombe Efroni mwana wa Zohari 9 anipatie ninunue pango lake la Makpela; liko kwenye mwisho wa shamba lake. Anipatie ninunue shamba hilo mbele yenu kwa kiasi cha kuenea cha feza+ ili nikuwe na mahali pa kuzikia.”+

10 Sasa Efroni alikuwa amekaa kati ya wana wa Heti. Kwa hiyo Efroni Muhiti akamujibu Abrahamu katika masikio ya wana wa Heti, na mbele ya wote wenye walikuwa wanaingia katika mulango mukubwa wa muji wake,+ na kusema: 11 “Hapana, bwana wangu! Unisikilize. Ninakupatia shamba hilo pamoja na pango lenye kuwa ndani yake. Ninakupatia hiyo mbele ya wana wa watu wangu. Umuzike mufu wako.” 12 Basi Abrahamu akainama mbele ya watu wa inchi 13 na kumuambia Efroni katika masikio ya watu, na kusema: “Unisikilize, tafazali! Nitakupatia kiasi cha kuenea cha feza kwa ajili ya shamba hilo. Kamata kiasi hicho cha feza chenye ninakupatia, ili niweze kumuzika mufu wangu kule.”

14 Kisha Efroni akamujibu Abrahamu: 15 “Unisikilize, bwana wangu. Bei ya shamba hili ni shekeli* mia ine (400) za feza, lakini hiyo ni nini kati yako na mimi? Kwa hiyo umuzike mufu wako.” 16 Basi Abrahamu akamusikiliza Efroni, na Abrahamu akamupimia Efroni kiasi cha kuenea cha feza chenye alikuwa ametaja katika masikio ya wana wa Heti, shekeli* mia ine (400) za feza kulingana na uzito wenye ulikubaliwa na wafanyabiashara.+ 17 Kwa hiyo shamba la Efroni lenye lilikuwa katika Makpela, mbele ya Mamre⁠—lile shamba na lile pango lenye lilikuwa ndani yake na miti yote yenye ilikuwa katika mipaka ya shamba hilo⁠—​vikahakikishwa kuwa 18 mali ya Abrahamu yenye alinunua mbele ya wana wa Heti, mbele ya wote wenye walikuwa wanaingia katika mulango mukubwa wa muji. 19 Kisha mambo hayo Abrahamu akamuzika Sara bibi yake katika pango la shamba la Makpela mbele ya Mamre, ni kusema, Hebroni, katika inchi ya Kanaani. 20 Hivyo wana wa Heti wakamupatia Abrahamu lile shamba pamoja na lile pango lenye lilikuwa ndani yake kuwa mahali pa kuzikia.+

24 Sasa Abrahamu alikuwa muzee, alikuwa ameishi miaka mingi, na Yehova alikuwa amemubariki katika kila jambo.+ 2 Abrahamu akamuambia mutumishi wake, mwenye alikuwa na miaka mingi zaidi katika nyumba yake, mwenye alikuwa anasimamia mali yake yote:+ “Tafazali, weka mukono wako chini ya paja langu, 3 na nitakuapisha kwa jina la Yehova, Mungu wa mbingu na Mungu wa dunia, kwamba hautamuchukulia mwana wangu bibi kati ya mabinti wa Wakanaani, wenye ninaishi kati yao.+ 4 Lakini unapaswa kuenda katika inchi yangu na kwa watu wa jamaa yangu+ na kuchukua bibi kwa ajili ya mwana wangu, kwa ajili ya Isaka.”

5 Basi, ule mutumishi akamuambia: “Itakuwa namna gani kama ule mwanamuke anakataa kuja pamoja na mimi katika inchi hii? Je, ninapaswa kumurudisha mwana wako katika inchi kwenye ulitoka?”+ 6 Basi Abrahamu akamuambia: “Ukuwe muangalifu ili usimupeleke mwana wangu kule.+ 7 Yehova Mungu wa mbinguni, mwenye alinitosha katika nyumba ya baba yangu na katika inchi ya watu wa jamaa yangu+ na mwenye alizungumuza na mimi na kuniapia:+ ‘Nitapatia uzao wako*+ inchi hii,’+ atatuma malaika wake mbele yako,+ na wewe hakika utachukua kule bibi kwa ajili ya mwana wangu.+ 8 Lakini kama ule mwanamuke anakataa kuja pamoja na wewe, utakuwa huru kutokana na kiapo hiki. Lakini haupaswe kumupeleka mwana wangu kule.” 9 Basi ule mutumishi akaweka mukono wake chini ya paja la Abrahamu bwana wake na kumuapia kuhusu jambo hilo.+

10 Kwa hiyo ule mutumishi akakamata ngamia kumi (10) wa bwana wake na kuondoka, akabeba kila namna ya vitu vya muzuri vya bwana wake. Kisha akaondoka na kuenda Mesopotamia, mupaka katika muji wa Nahori. 11 Akafanya ngamia wapige magoti karibu na kisima cha maji inje ya muji. Ilikuwa karibu saa ya mangaribi, wakati wanamuke walikuwa wanatoka ili kushota maji. 12 Kisha akasema: “Yehova Mungu wa bwana wangu Abrahamu, tafazali unisaidie nipate matokeo ya muzuri leo, na uonyeshe bwana wangu Abrahamu upendo wako mushikamanifu. 13 Angalia, nimesimama karibu na chemchemi ya maji, na mabinti wa watu wa muji wanakuja kushota maji. 14 Na itokee kwamba kijana mwanamuke mwenye nitamuambia, ‘Tafazali, shusha mutungi wako wa maji ili nikunywe,’ naye aseme, ‘Kunywa, na nitapatia pia ngamia wako maji,’ huyo akuwe ndiye mwenye unachagulia mutumishi wako Isaka; na kwa jambo hilo unijulishe kwamba umemuonyesha bwana wangu upendo wako mushikamanifu.”

15 Wakati kidogo tu mbele amalize kusema, Rebeka, binti ya Betueli+ mwana wa Milka+ bibi ya Nahori,+ ndugu ya Abrahamu, akakuja akiwa na mutungi wa maji kwenye bega lake. 16 Sasa ule kijana mwanamuke alikuwa na sura na umbo ya muzuri sana, bikira; hakuna mwanaume mwenye alikuwa amefanya ngono naye. Akateremuka kwenye chemchemi, akajaza mutungi wake wa maji, na kisha akapanda. 17 Mara moja ule mutumishi akakimbia ili akutane naye na akasema: “Tafazali, unipatie maji kidogo ya mutungi wako.” 18 Naye akasema: “Kunywa, bwana wangu.” Kisha akashusha haraka mutungi wake kwenye mukono wake na akamupatia maji ya kunywa. 19 Wakati alimaliza kumupatia maji ya kunywa, akasema: “Nitashota pia maji kwa ajili ya ngamia wako mupaka wamalize kunywa.” 20 Kwa hiyo akamwanga haraka maji yote ya mutungi wake ndani ya chombo cha kuwekea maji ya kunywa ya wanyama, na akakimbia tena na tena kwenye kisima ili kushota maji, na akaendelea kushota maji ya kunywa kwa ajili ya ngamia wote. 21 Wakati huo wote ule mwanaume alikuwa kimya akimuangalia kwa mushangao, na kujiuliza kama Yehova alikuwa amefanya safari yake ikuwe na matokeo ya muzuri ao hapana.

22 Wakati ngamia walimaliza kunywa maji, ule mwanaume akamutoshea pete ya pua ya zahabu yenye uzito wa nusu shekeli* na vikomo mbili vya zahabu vyenye uzito wa shekeli* kumi (10), 23 kisha akasema: “Uniambie tafazali, wewe uko binti ya nani? Je, kuko nafasi katika nyumba ya baba yako kwenye tunaweza kulala usiku huu?” 24 Basi akamuambia: “Niko binti ya Betueli+ mwana wa Milka, mwenye Milka alimuzalia Nahori.”+ 25 Kisha akaendelea kusema: “Tuko na nyasi na chakula kingi cha wanyama wa kufugwa na pia mahali kwenye munaweza kulala usiku.” 26 Kisha ule mwanaume akainama na kushusha uso chini mbele ya Yehova 27 na akasema: “Asifiwe Yehova Mungu wa bwana wangu Abrahamu, kwa maana hajaacha kumuonyesha bwana wangu upendo wake mushikamanifu na uaminifu wake. Yehova ameniongoza mupaka kwenye nyumba ya ndugu za bwana wangu.”

28 Na ule kijana mwanamuke akakimbia kuenda kuambia nyumba ya mama yake juu ya mambo hayo. 29 Sasa Rebeka alikuwa na ndugu mwenye jina lake lilikuwa Labani.+ Kwa hiyo Labani akakimbia kuenda kukutana na ule mwanaume mwenye alikuwa inje karibu na chemchemi. 30 Wakati Labani aliona ile pete na vile vikomo kwenye mikono ya dada yake na kusikia maneno ya Rebeka dada yake, mwenye alikuwa anasema, “Ule mwanaume aliniambia hivi,” akaenda kukutana na ule mwanaume, mwenye alikuwa angali anasimama pembeni ya ngamia karibu na chemchemi. 31 Mara moja akasema: “Kuja, wewe mwenye kubarikiwa na Yehova. Sababu gani unaendelea kusimama hapa inje? Nimetayarisha nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.” 32 Basi ule mwanaume akaingia ndani ya nyumba, naye* akafungua kamba za ngamia na kupatia ngamia nyasi na chakula cha wanyama wa kufugwa na maji ya kunawa miguu yake na miguu ya wanaume wenye walikuwa pamoja naye. 33 Lakini, wakati chakula kiliwekwa mbele yake, akasema: “Sitakula mupaka niwaambie mambo yenye ninapaswa kusema.” Kwa hiyo Labani akamuambia: “Sema!”

34 Kisha akasema: “Mimi niko mutumishi wa Abrahamu.+ 35 Na Yehova amemubariki sana bwana wangu, na amemufanya kuwa tajiri sana kwa kumupatia kondoo na ngombe, feza na zahabu, watumishi wanaume na watumishi wanamuke, na ngamia na punda.+ 36 Tena, kisha kuzeeka,+ Sara bibi ya bwana wangu alimuzalia bwana wangu mwana, na bwana wangu atamupatia kila kitu chenye iko* nacho.+ 37 Kwa hiyo bwana wangu aliniapisha, na kusema: ‘Haupaswe kumuchukulia mwana wangu bibi kati ya mabinti wa Wakanaani, wenye ninaishi katika inchi yao.+ 38 Hapana, lakini utaenda mupaka kwenye nyumba ya baba yangu na kwenye familia yangu,+ na unapaswa kumuchukulia mwana wangu bibi.’+ 39 Lakini nilimuambia bwana wangu: ‘Itakuwa namna gani kama ule mwanamuke anakataa kuja pamoja na mimi?’+ 40 Aliniambia: ‘Yehova, Mungu mwenye nimetembea mbele yake,+ atamutuma malaika wake+ pamoja na wewe na hakika atafanya safari yako ikuwe na matokeo ya muzuri, na wewe unapaswa kumuchukulia mwana wangu bibi katika familia yangu na katika nyumba ya baba yangu.+ 41 Utakuwa huru kutokana na kiapo chako chenye uliapa mbele yangu kama unaenda katika familia yangu na wakatae kukupatia mwanamuke. Jambo hilo litakuweka huru usikuwe chini ya kiapo chako.’+

42 “Wakati nilifika kwenye chemchemi leo, nilisema: ‘Yehova Mungu wa bwana wangu Abrahamu, kama utafanya safari yangu ikuwe na matokeo ya muzuri, 43 angalia, nimesimama karibu na chemchemi. Jambo lenye linapaswa kutokea ni kwamba wakati kijana mwanamuke + atakuja kushota maji, nitasema: “Tafazali, acha nikunywe maji kidogo ya mutungi wako,” 44 naye ataniambia, “Kunywa, na pia nitashota maji kwa ajili ya ngamia wako.” Ule mwanamuke akuwe ndiye mwenye Yehova amechagua kwa ajili ya mwana wa bwana wangu.’+

45 “Wakati kidogo mbele nimalize kusema katika moyo wangu, Rebeka akatokea akiwa na mutungi kwenye bega lake, na akateremuka mupaka kwenye chemchemi na kuanza kushota maji. Kisha nikamuambia: ‘Tafazali, nipatie maji nikunywe.’+ 46 Kwa hiyo akashusha mutungi haraka kutoka kwenye bega lake na kusema: ‘Kunywa,+ na pia nitapatia ngamia zako maji.’ Kisha nikakunywa maji, na pia akapatia ngamia zangu maji. 47 Kisha mambo hayo nikamuuliza, ‘Wewe uko binti ya nani?’ naye akajibu, ‘Binti ya Betueli mwana wa Nahori, mwenye Milka alimuzalia Nahori.’ Kwa hiyo nikamuvalisha pete kwenye pua yake na vikomo kwenye mikono yake.+ 48 Na mimi nikainama na kushusha uso chini mbele ya Yehova na nikamusifu Yehova Mungu wa bwana wangu Abrahamu,+ mwenye aliniongoza katika njia yenye kuwa sawa ili nimuchukue binti ya ndugu ya bwana wangu kwa ajili ya mwana wake. 49 Na sasa muniambie kama munataka kumuonyesha bwana wangu upendo mushikamanifu na uaminifu; lakini kama haiko vile, muniambie, kusudi nitende kwa njia moja ao ingine.”*+

50 Kisha Labani na Betueli wakajibu: “Jambo hili limetoka kwa Yehova. Hatuwezi kukuambia ndiyo ao hapana.* 51 Rebeka ndiye huyu hapa mbele yako. Umuchukue na uende, na akuwe bibi ya mwana wa bwana wako, kama vile Yehova amesema.” 52 Wakati mutumishi wa Abrahamu alisikia maneno yao, mara moja akainama mupaka chini mbele ya Yehova. 53 Na ule mutumishi akaanza kutosha vitu vya feza na vya zahabu na nguo na kumupatia Rebeka vitu hivyo, na akamupatia ndugu yake na mama yake vitu vya muzuri. 54 Kisha mambo hayo yeye na wanaume wenye walikuwa pamoja naye wakakula na kunywa, na wakalala pale.

Wakati aliamuka asubui, akasema: “Muniruhusu niende kwa bwana wangu.” 55 Kwa hiyo ndugu na mama ya Rebeka wakasema: “Acha huyu kijana mwanamuke akae pamoja na sisi hata kwa siku kumi (10) hivi. Kisha anaweza kuenda.” 56 Lakini akawaambia: “Musinizuie, kwa maana Yehova amefanya safari yangu ikuwe na matokeo ya muzuri. Muniruhusu niende, ili nirudie kwa bwana wangu.” 57 Kwa hiyo wakasema: “Tumuite ule kijana mwanamuke na tumuulize.” 58 Wakamuita Rebeka na kumuuliza: “Je, utaenda na mutu huyu?” Akajibu: “Mimi niko tayari kuenda.”

59 Kwa hiyo wakamuruhusu Rebeka dada yao+ na mulezi wake*+ waende pamoja na mutumishi wa Abrahamu na wanaume wake. 60 Nao wakamubariki Rebeka na kumuambia: “Dada yetu, ukuwe maelfu mara elfu kumi,* na uzao wako uriti* mulango mukubwa wa* wale wenye wanawachukia.”+ 61 Kisha Rebeka na watumishi wake wanamuke wakasimama, wakapanda juu ya ngamia, na kumufuata ule mwanaume. Kwa hiyo ule mutumishi akamuchukua Rebeka na kuondoka.

62 Sasa Isaka alikuwa amekuja kupitia njia yenye kuenda Beer-lahai-roi,+ kwa maana alikuwa anaishi katika inchi ya Negebu.+ 63 Na Isaka alikuwa ameenda kutembea katika eneo la mashamba karibu na wakati giza linaingia ili kufikiri sana.*+ Wakati aliinua macho, basi, akaona ngamia wanakuja! 64 Wakati Rebeka aliinua macho, akamuona Isaka, naye akashuka haraka kutoka kwenye ngamia. 65 Kisha akamuuliza ule mutumishi: “Ni nani ule mwanaume mwenye kutembea kule katika eneo la mashamba ili kukutana na sisi?” Ule mutumishi akajibu: “Ni bwana wangu.” Kwa hiyo Rebeka akakamata kitambaa chake cha kufunika kichwa ili ajifunike. 66 Na ule mutumishi akamuelezea Isaka mambo yote yenye alikuwa amefanya. 67 Kisha mambo hayo Isaka akamupeleka Rebeka ndani ya hema ya Sara mama yake.+ Kwa hiyo akamuchukua Rebeka kuwa bibi yake; na Isaka akamupenda,+ na akapata faraja kisha kifo cha mama yake.+

25 Kisha Abrahamu akachukua tena bibi, na jina lake lilikuwa Ketura. 2 Kisha wakati fulani Ketura akamuzalia Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani,+ Ishbaki, na Shua.+

3 Yokshani akazaa Sheba na Dedani.

Wana wa Dedani walikuwa Ashurimu, Letushimu, na Leumimu.

4 Wana wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Hanoki, Abida, na Eldaa.

Hao wote walikuwa wana wa Ketura.

5 Kisha wakati fulani Abrahamu akamupatia Isaka kila kitu chenye alikuwa nacho,+ 6 lakini Abrahamu akapatia wana wa masuria* wake zawadi. Kisha, wakati alikuwa angali muzima, aliwaambia waende upande wa mashariki, mbali na Isaka mwana wake,+ katika inchi ya Mashariki. 7 Miaka ya maisha ya Abrahamu ilikuwa miaka mia moja makumi saba na tano (175). 8 Kisha Abrahamu akavuta pumuzi yake ya mwisho na akakufa katika uzee muzuri; alikuwa muzee na mwenye kutosheka, naye akakusanywa kwa watu wake.* 9 Wana wake Isaka na Ishmaeli wakamuzika katika pango la Makpela katika shamba la Efroni mwana wa Zohari Muhiti lenye kuwa mbele ya Mamre,+ 10 shamba lenye Abrahamu alinunua kwa wana wa Heti. Ni kule Abrahamu na Sara bibi yake walizikwa.+ 11 Kisha Abrahamu kufa, Mungu aliendelea kumubariki Isaka mwana wake;+ na Isaka alikuwa anaishi karibu na Beer-lahai-roi.+

12 Hii ndiyo historia ya Ishmaeli+ mwana wa Abrahamu mwenye Hagari+ Mumisri, mutumishi wa Sara, alimuzalia Abrahamu.

13 Sasa haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, kufuatana na majina yao kulingana na asili za familia zao: Muzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli alikuwa Nebayoti,+ kisha Kedari,+ Adbeeli, Mibsamu,+ 14 Mishma, Duma, Masa, 15 Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi, na Kedema. 16 Hao ndio wana wa Ishmaeli, na hayo ndiyo majina yao kulingana na makao yao na kambi zao,* wakubwa kumi na mbili (12) kulingana na ukoo wao mbalimbali.+ 17 Na Ishmaeli akaishi miaka mia moja makumi tatu na saba (137). Kisha akavuta pumuzi yake ya mwisho na akakufa, naye akakusanywa kwa watu wake.* 18 Nao wakaanza kuishi kuanzia Havila+ karibu na Shuri,+ yenye iko karibu na Misri, mupaka kufikia Ashuru. Alikaa karibu na ndugu zake wote.*+

19 Hii ndiyo historia ya Isaka mwana wa Abrahamu.+

Abrahamu alimuzaa Isaka. 20 Isaka alikuwa na miaka makumi ine (40) wakati alimuoa Rebeka, binti ya Betueli+ Mwaramu wa Padan-aramu, dada ya Labani ule Mwaramu. 21 Na Isaka akaendelea kumulilia Yehova kwa ajili ya bibi yake, kwa sababu alikuwa tasa; kwa hiyo Yehova akasikia ombi lake, na Rebeka bibi yake akakuwa na mimba. 22 Na wana wenye walikuwa ndani ya tumbo lake wakaanza kupigana,+ kwa hiyo akasema: “Kama ni hivi, sababu gani niendelee kuishi?” Basi akamuuliza Yehova. 23 Na Yehova akamuambia: “Mataifa mbili yako katika tumbo lako la uzazi,+ na vikundi mbili vya watu vitatenganishwa kutoka ndani yako;+ na taifa moja litakuwa na nguvu kuliko taifa lingine,+ na mukubwa atamutumikia mudogo.”+

24 Wakati muda wa kuzaa ulifika, angalia! mapacha walikuwa katika tumbo lake la uzazi. 25 Kisha wakati wa kwanza alitoka, mwili wake wote ulikuwa mwekundu, na ulikuwa kama nguo ya manyoya,+ basi wakamupatia jina Esau.*+ 26 Kisha ndugu yake akatoka na mukono wake ulikuwa unashika kisigino cha Esau,+ kwa hiyo Isaka akamupatia jina Yakobo.*+ Isaka alikuwa na miaka makumi sita (60) wakati Rebeka aliwazaa.

27 Kadiri wale watoto wanaume waliendelea kukomaa, Esau akakuwa fundi wa kuwinda,+ mutu wa pori, lakini Yakobo akakuwa mutu mwenye hana lawama, mwenye kukaa katika mahema.+ 28 Na Isaka alimupenda Esau kwa sababu hiyo ilimaanisha nyama ya kuwinda katika kinywa chake, lakini Rebeka alimupenda Yakobo.+ 29 Siku moja Yakobo alikuwa anatokotesha muchuzi wakati Esau alirudia kutoka katika pori akiwa amechoka. 30 Kwa hiyo Esau akamuambia Yakobo: “Haraka, tafazali, unipatie sehemu fulani ya muchuzi mwekundu* wenye uko nao pale,* kwa maana nimechoka sana!”* Ndiyo sababu jina lake lilikuwa Edomu.*+ 31 Yakobo akamuambia: “Kwanza unipatie ninunue haki yako ya muzaliwa wa kwanza!”+ 32 Na Esau akasema: “Angalia, niko karibu kufa! Haki ya kuzaliwa itanifanyia nini?” 33 Yakobo akamuambia: “Uniapie kwanza!” Basi akamuapia na kumuuzisha Yakobo haki yake ya muzaliwa wa kwanza.+ 34 Kisha Yakobo akamupatia Esau mukate na muchuzi wa dengu, naye akakula na kunywa, kisha akasimama na kuenda. Hivyo Esau akazarau haki yake ya kuzaliwa.

26 Sasa njaa ikatokea katika inchi, zaidi ya ile njaa ya kwanza yenye ilitokea katika siku za Abrahamu,+ kwa hiyo Isaka akaenda Gerari kwa Abimeleki mufalme wa Wafilisti. 2 Kisha Yehova akamutokea Isaka na kusema: “Usishuke kuenda Misri. Kaa katika inchi yenye nitakuonyesha. 3 Kaa kama mugeni katika inchi hii,+ na mimi nitaendelea kuwa pamoja na wewe na kukubariki kwa sababu nitakupatia wewe na uzao wako* inchi hizi zote,+ na nitatimiza kiapo hiki chenye nilimuapia Abrahamu baba yako:+ 4 ‘Nitafanya uzao wako uongezeke* kama nyota za mbinguni;+ na nitapatia uzao wako* inchi hizi zote;+ na kupitia uzao wako* mataifa yote ya dunia yatajipatia baraka,’+ 5 kwa sababu Abrahamu alisikiliza sauti yangu na kuendelea kufuata maagizo yangu, amri zangu, masharti yangu, na sheria zangu.”+ 6 Kwa hiyo Isaka akaendelea kuishi Gerari.+

7 Wakati wanaume wa mahali pale walikuwa wanamuuliza juu ya bibi yake, alikuwa anasema: “Huyu ni dada yangu.”+ Aliogopa kusema, “Ni bibi yangu,” kwa maana alisema, “Wanaume wa hapa wanaweza kuniua kwa sababu ya Rebeka,” kwa kuwa alikuwa na sura na umbo ya muzuri.+ 8 Kisha wakati fulani kupita, Abimeleki mufalme wa Wafilisti alikuwa anaangalia inje kupitia dirisha, na akamuona Isaka akimuonyesha mapenzi* Rebeka bibi yake.+ 9 Mara moja Abimeleki akamuita Isaka na kumuambia: “Kumbe ni bibi yako! Sababu gani ulisema, ‘Yeye ni dada yangu’?” Kwa hiyo Isaka akamuambia: “Nilisema vile kwa sababu niliogopa kwamba nitauawa kwa sababu yake.”+ 10 Lakini Abimeleki akasema tena: “Ni jambo gani hili lenye umetutendea?+ Mutu fulani kati ya watu angelala na bibi yako, na ungeleta hatia juu yetu!”+ 11 Kisha Abimeleki akaamuru watu wote, na kusema: “Mutu mwenye atamugusa mwanaume huyu na bibi yake hakika atauawa!”

12 Na Isaka akaanza kupanda mbegu katika inchi hiyo, na mwaka huo akavuna mara mia moja (100) mbegu zenye alipanda, kwa kuwa Yehova alikuwa anamubariki.+ 13 Huyu mwanaume akakuwa tajiri, na akaendelea kupata mali mupaka akakuwa tajiri sana. 14 Akapata makundi ya kondoo na makundi ya ngombe na kundi kubwa la watumishi,+ na Wafilisti wakaanza kumusikilia wivu.

15 Kwa hiyo Wafilisti wakakamata udongo na kufunika visima vyote vyenye watumishi wa baba yake walikuwa wamechimba katika siku za Abrahamu.+ 16 Kisha Abimeleki akamuambia Isaka: “Toka katika ujirani wetu, kwa sababu umekuwa na nguvu sana kuliko sisi.” 17 Kwa hiyo Isaka akatoka mahali pale na kupiga kambi katika bonde* la Gerari+ na kuanza kuishi kule. 18 Na Isaka akachimba tena visima vyenye vilikuwa vimechimbwa katika siku za Abrahamu baba yake lakini vyenye Wafilisti walikuwa wamefunika kisha Abrahamu kufa,+ na akavipatia majina yaleyale yenye baba yake alikuwa amevipatia.+

19 Wakati watumishi wa Isaka walikuwa wanachimba katika bonde,* wakapata kisima cha maji safi. 20 Na wachungaji wa Gerari wakaanza kugombana na wachungaji wa Isaka, wakisema: “Haya maji ni yetu!” Kwa hiyo akaita kile kisima Eseki,* kwa sababu walikuwa wamegombana naye. 21 Na wakaanza kuchimba kisima kingine, na wakaanza kukigombania pia. Kwa hiyo akakiita Sitna.* 22 Kisha wakati fulani akatoka mahali pale na kuchimba kisima kingine, lakini hawakukigombania. Kwa hiyo akakiita Rehoboti* na kusema: “Ni kwa sababu sasa Yehova ametupatia nafasi ya kutosha naye ametufanya tuongezeke katika inchi.”+

23 Kisha akatoka kule na kuenda Beer-sheba.+ 24 Yehova akamutokea usiku huo na kusema: “Mimi ni Mungu wa Abrahamu baba yako.+ Usiogope,+ kwa sababu niko pamoja na wewe, na nitakubariki na kufanya uzao wako uongezeke* kwa sababu ya Abrahamu mutumishi wangu.”+ 25 Kwa hiyo akajenga mazabahu kule na kuitia jina la Yehova.+ Na Isaka akasimamisha hema yake kule,+ na watumishi wake wakachimba kisima kule.

26 Kisha wakati fulani Abimeleki akakuja kumutembelea kutoka Gerari pamoja na Ahuzati mushauri wake na Fikoli mukubwa wa jeshi lake.+ 27 Isaka akawaambia: “Sababu gani mumenitembelea, wakati ninyi mulinichukia na kunifukuza katika ujirani wenu?” 28 Basi wakasema: “Tumeona waziwazi kwamba Yehova iko* pamoja na wewe.+ Kwa hiyo tulisema, ‘Tafazali, kiapo chenye masharti kikuwe kati yetu na wewe, na tufanye agano pamoja na wewe+ 29 kwamba hautatufanyia jambo lolote la mubaya kama vile sisi hatukukufanyia jambo la kukuumiza, kwa sababu tulikutendea tu mambo ya muzuri kwa kukuruhusu uende kwa amani. Sasa wewe ni mubarikiwa wa Yehova.’” 30 Kisha Isaka akawafanyia karamu, nao wakakula na kunywa. 31 Wakaamuka asubui sana na kila mumoja akamuapia mwenzake.+ Kisha Isaka akawaacha waende, nao wakaenda kwa amani.

32 Siku hiyo watumishi wa Isaka walikuja na kumuambia kuhusu kisima chenye walikuwa wamechimba,+ na wakamuambia: “Tumepata maji!” 33 Kwa hiyo akakiita Shiba. Ndiyo sababu jina la muji huo ni Beer-sheba+ mupaka leo.

34 Wakati Esau alikuwa na miaka makumi ine (40), alimuoa Yuditi binti ya Beeri Muhiti na pia Basemati binti ya Eloni Muhiti.+ 35 Waliletea Isaka na Rebeka uchungu mukubwa.*+

27 Wakati Isaka alikuwa muzee na macho yake yalikuwa yamekuwa zaifu sana asiweze kuona, akamuita Esau+ mwana wake mukubwa na kusema: “Mwana wangu!” Naye akajibu: “Mimi huyu!” 2 Na Isaka akaendelea kusema: “Nimezeeka sasa. Sijue siku ya kifo changu. 3 Kwa hiyo wakati huu, tafazali, kamata silaha zako, mufuko wako wa mishale na upinde wako, uende katika pori na uniwindie munyama wa pori.+ 4 Kisha unipikie chakula kitamu chenye ninapenda na uniletee. Kisha nitakikula ili nikubariki mbele nikufe.”

5 Lakini Rebeka alikuwa anasikiliza wakati Isaka alikuwa anazungumuza na Esau mwana wake. Na Esau akaenda katika pori ili kuwinda munyama na kumuleta.+ 6 Na Rebeka akamuambia Yakobo mwana wake:+ “Nimesikia sasa hivi baba yako anazungumuza na ndugu yako Esau, na kusema, 7 ‘Niletee munyama wa pori na unipikie chakula kitamu. Kisha nikikule ili nikubariki mbele ya Yehova mbele nikufe.’+ 8 Na sasa, mwana wangu, sikiliza kwa uangalifu na ufanye mambo yenye ninakuagiza.+ 9 Tafazali, uende, mahali mifugo iko na uniletee wana-mbuzi wawili wazuri zaidi ili niwatayarishe kuwa chakula kitamu kwa ajili ya baba yako, kama vile anapendaka. 10 Kisha umupelekee baba yako akule, ili akubariki mbele akufe.”

11 Yakobo akamuambia Rebeka mama yake: “Lakini Esau ndugu yangu ni mwanaume mwenye nywele nyingi kwenye mwili,+ na ngozi yangu iko laini. 12 Namna gani kama baba ananigusa?+ Basi hakika nitaonekana kuwa mutu mwenye kumufanyia muzaha, na nitajilitea laana kuliko kujiletea baraka.” 13 Mama yake akamuambia: “Mwana wangu, laana hiyo yenye ingekuwa juu yako ikuwe juu yangu. Fanya tu vile ninakuambia na uende, uniletee wana-mbuzi.”+ 14 Kwa hiyo akaenda na kuwakamata na kuwaleta kwa mama yake, na mama yake akatayarisha chakula kitamu, kama vile baba yake alikuwa anapenda. 15 Kisha mambo hayo Rebeka akakamata nguo za muzuri sana za Esau mwana wake mukubwa, zenye Rebeka alikuwa nazo katika nyumba, na akamuvalisha Yakobo mwana wake mudogo.+ 16 Pia akatia ngozi za wana-mbuzi hao kwenye mikono yake na pia kwenye sehemu yenye haina nywele ya shingo yake.+ 17 Kisha akamupatia Yakobo mwana wake kile chakula kitamu na mukate wenye alikuwa ametayarisha.+

18 Kwa hiyo akaingia kwa baba yake na kusema: “Baba yangu!” naye akasema: “Mimi huyu! Wewe ni nani, mwana wangu?” 19 Yakobo akamuambia baba yake: “Mimi ni Esau muzaliwa wako wa kwanza.+ Nimefanya tu kama vile uliniambia. Simama na ukae, tafazali, na ukule sehemu fulani ya nyama yenye niliwinda, ili unibariki.”*+ 20 Basi Isaka akamuambia mwana wake: “Namna gani umeipata haraka sana, mwana wangu?” Akajibu: “Kwa sababu Yehova Mungu wako aliileta kwangu.” 21 Kisha Isaka akamuambia Yakobo: “Tafazali, kuja karibu, nikuguse, mwana wangu, ili nijue kama kwa kweli wewe ni mwana wangu Esau ao hapana.”+ 22 Kwa hiyo Yakobo akaenda karibu na Isaka baba yake, naye akamugusa, kisha akasema: “Sauti ni sauti ya Yakobo, lakini mikono ni mikono ya Esau.”+ 23 Hakumutambua kwa sababu mikono yake ilikuwa na nywele nyingi kama mikono ya Esau ndugu yake. Kwa hiyo akamubariki.+

24 Kisha mambo hayo akauliza: “Wewe kweli ni mwana wangu Esau?” akajibu: “Ni mimi.” 25 Kisha akasema: “Mwana wangu, niletee sehemu fulani ya nyama yenye uliwinda ili nikule, kisha nitakubariki.”* Kwa hiyo akamuletea ile nyama na akakula, na akamuletea divai na akakunywa. 26 Kisha Isaka baba yake akamuambia: “Kuja karibu, tafazali, na unibusu, mwana wangu.”+ 27 Kwa hiyo akaenda karibu na akamubusu, na Isaka akanusa harufu ya nguo zake.+ Kisha akamubariki na kusema:

“Angalia, harufu ya mwana wangu iko kama harufu ya shamba lenye Yehova amebariki. 28 Mungu wa kweli akupatie umande wa mbinguni+ na udongo wenye mbolea wa dunia+ na nafaka nyingi na divai mupya.+ 29 Vikundi vya watu vikutumikie, na mataifa yakuinamie. Ukuwe bwana juu ya ndugu zako, na wana wa mama yako wakuinamie.+ Alaaniwe kila mutu mwenye anakulaani, na abarikiwe kila mutu mwenye anakubariki.”+

30 Sasa wakati tu Isaka alimaliza kumubariki Yakobo, na wakati Yakobo alikuwa ametoka tu mbele ya Isaka baba yake, Esau ndugu yake akarudia kutoka katika kuwinda.+ 31 Naye pia akatayarisha chakula kitamu na kumuletea baba yake, na akamuambia baba yake: “Baba yangu asimame na kula sehemu fulani ya nyama yenye mwana wake aliwinda, ili unibariki.”* 32 Basi Isaka baba yake akamuambia: “Wewe ni nani?” akajibu: “Mimi ni Esau mwana wako, muzaliwa wako wa kwanza.”+ 33 Na Isaka akaanza kutetemeka kwa nguvu sana, kwa hiyo akasema: “Ni nani, basi, mwenye aliwinda na kuniletea nyama? Niliisha kuikula mbele ufike, na nilimubariki⁠—⁠na hakika atabarikiwa!”

34 Wakati alisikia maneno ya baba yake, Esau akaanza kulia kwa sauti kubwa sana na yenye uchungu na kumuambia baba yake: “Baba yangu, unibariki, ndiyo, mimi pia!”+ 35 Lakini akamuambia: “Ndugu yako alikuja kwa udanganyifu ili apate baraka yenye ulipaswa kupata.” 36 Basi Esau akamuambia: “Je, haiko hiyo ndiyo sababu anaitwa Yakobo,* ili achukue nafasi yangu mara hizi mbili?+ Amekwisha kuchukua haki yangu ya muzaliwa wa kwanza,+ na sasa amechukua baraka yangu!”+ Kisha akaongeza: “Je, haukuniachia baraka fulani?” 37 Lakini Isaka akamujibu Esau: “Angalia, nimemuweka kuwa bwana juu yako,+ na nimemupatia ndugu zake wote kuwa watumishi wake, na nimemupatia nafaka na divai mupya ili kumutegemeza.+ Ninaweza kufanya nini tena kwa ajili yako, mwana wangu?”

38 Esau akamuambia baba yake: “Baba yangu, je, hauna hata baraka moja? Baba yangu, unibariki, ndiyo, mimi pia!” Basi Esau akalia kwa sauti kubwa na kutoa machozi.+ 39 Kwa hiyo Isaka baba yake akamujibu:

“Angalia, makao yako yatakuwa mbali na udongo wenye mbolea, mbali na umande wa mbinguni.+ 40 Na utaishi kwa upanga wako,+ na utamutumikia ndugu yako.+ Lakini wakati utachoka kuvumilia, utavunja nira yake na kuiondoa kwenye shingo yako.”+

41 Hata hivyo, Esau akamuchukia Yakobo katika moyo wake kwa sababu ya baraka yenye baba yake alikuwa amemupatia,+ na Esau akakuwa anasema katika moyo wake: “Siku za kumuombolezea baba yangu zinakaribia.+ Kisha siku hizo nitamuua Yakobo ndugu yangu.” 42 Wakati Rebeka aliambiwa maneno ya Esau mwana wake mukubwa, mara moja akamuita Yakobo mwana wake mudogo na kumuambia: “Angalia! Esau ndugu yako anapanga kukuua ili kulipiza kisasi.* 43 Sasa, mwana wangu, fanya kama vile ninakuambia. Simama na ukimbilie kwa Labani ndugu yangu kule Harani.+ 44 Uishi naye wakati fulani mupaka kasirani kali ya ndugu yako itulie, 45 mupaka kasirani ya ndugu yako kukuelekea ipunguke, naye asahau mambo yenye umemutendea. Kisha nitatuma wakuite utoke kule. Sababu gani niwapoteze ninyi wawili siku moja?”

46 Kisha mambo hayo Rebeka akakuwa anamuambia Isaka: “Ninachukia sana maisha yangu kwa sababu ya mabinti wa Heti.+ Kama siku moja Yakobo anachukua bibi kati ya mabinti wa Heti, kama mabinti hawa wa inchi hii, maisha yangu yako na faida gani?”+

28 Kwa hiyo Isaka akamuita Yakobo na akamubariki na kumuamuru, akisema: “Haupaswe kuchukua bibi kati ya mabinti wa Kanaani.+ 2 Uende mupaka Padan-aramu kwenye nyumba ya Betueli, baba ya mama yako, na uchukue bibi kule kati ya mabinti wa Labani,+ ndugu ya mama yako. 3 Mungu Mweza-Yote atakubariki na atakufanya uzae na kuongezeka, na hakika utakuwa kutaniko la vikundi vya watu.+ 4 Na atakupatia wewe baraka ya Abrahamu,+ wewe na uzao wako* pamoja na wewe, ili uriti inchi yenye umeishi ndani yake ukiwa mugeni, yenye Mungu amemupatia Abrahamu.”+

5 Kwa hiyo Isaka akamuacha Yakobo aende, naye akaenda Padan-aramu, kwa Labani mwana wa Betueli Mwaramu,+ ndugu ya Rebeka,+ mama ya Yakobo na Esau.

6 Esau akaona kwamba Isaka alikuwa amemubariki Yakobo na kumuacha aende Padan-aramu kuchukua bibi kule, na kwamba wakati alimubariki alimuamuru, “Usichukue bibi kati ya mabinti wa Kanaani,”+ 7 na kwamba Yakobo alimutii baba yake na mama yake na alienda Padan-aramu.+ 8 Basi Esau akatambua kama Isaka baba yake hakupendezwa na mabinti wa Kanaani,+ 9 kwa hiyo Esau akaenda kwa Ishmaeli na kumuchukua Mahalati binti ya Ishmaeli mwana wa Abrahamu, dada ya Nebayoti, akuwe bibi yake, kwa kuongezea juu ya wale bibi wengine wenye alikuwa nao.+

10 Yakobo akaondoka Beer-sheba na kuenda Harani.+ 11 Kisha wakati fulani akafika mahali fulani na akaamua kulala pale kwa sababu jua lilikuwa limeshuka. Kwa hiyo akakamata moja kati ya majiwe ya mahali pale na akaliweka ili apumuzishe kichwa chake juu yake na akalala pale.+ 12 Kisha akaota ndoto, na angalia! kulikuwa ngazi yenye* kusimamishwa juu ya dunia, na sehemu ya juu ya ngazi hiyo ilifika mupaka mbinguni, na malaika wa Mungu walikuwa wanapanda na kushuka kwenye ngazi hiyo.+ 13 Na angalia! Yehova alikuwa anasimama juu ya ngazi hiyo,* na alisema:

“Mimi ni Yehova Mungu wa Abrahamu baba yako na Mungu wa Isaka.+ Nitakupatia wewe na uzao wako* inchi yenye unalala juu yake.+ 14 Na hakika uzao wako utakuwa* kama mavumbi ya dunia,+ na utaenea kila mahali upande wa mangaribi, upande wa mashariki, upande wa kaskazini, na upande wa kusini, na kupitia wewe na uzao wako* familia zote za inchi hakika zitabarikiwa.*+ 15 Niko pamoja na wewe, na nitakulinda kila mahali kwenye utaenda, na nitakurudisha kwenye inchi hii.+ Sitakuacha mupaka wakati nitatimiza mambo yenye nimekuahidi.”+

16 Kisha Yakobo akaamuka katika usingizi wake na kusema: “Kwa kweli Yehova iko* mahali hapa, na sikujua jambo hilo.” 17 Naye akaogopa sana na kusema: “Hapa ni mahali kwenye kuogopesha sana! Hakika hapa ni nyumba ya Mungu,+ na huu ni mulango mukubwa wa mbinguni.”+ 18 Kwa hiyo Yakobo akaamuka asubui sana na kukamata lile jiwe lenye alikuwa amepumuzisha kichwa chake juu yake, akalisimamisha kuwa nguzo na akamwanga mafuta juu ya sehemu ya juu ya jiwe hilo.+ 19 Kwa hiyo akaita mahali pale Beteli,* lakini jina la zamani la muji huo lilikuwa Luzi.+

20 Kisha Yakobo akafanya naziri, kwa kusema: “Kama Mungu ataendelea kuwa pamoja na mimi na kunilinda katika safari yangu na kunipatia mukate wa kula na nguo za kuvaa, 21 na kama ninarudia kwa amani katika nyumba ya baba yangu, basi hakika Yehova atakuwa ameonyesha kwamba yeye ni Mungu wangu. 22 Na jiwe hili lenye nimesimamisha kuwa nguzo litakuwa nyumba ya Mungu,+ na hakika nitakupatia sehemu moja ya kumi (1/10) ya kila kitu chenye utanipatia.”

29 Kisha mambo hayo Yakobo akaendelea na safari yake na akaenda mupaka kwenye inchi ya watu wa Mashariki. 2 Basi akaona kisima katika eneo la mashamba na makundi tatu (3) ya kondoo wenye kulala pembeni ya kisima, kwa sababu wachungaji walikuwa wanazoea kuwapatia maji ya kile kisima. Kulikuwa jiwe kubwa juu ya kinywa cha kile kisima. 3 Wakati makundi yote yalikuwa yamekusanywa pale, waliviringisha jiwe na kuliondoa kwenye kinywa cha kisima, na walipatia makundi maji, kisha walirudisha lile jiwe mahali pake juu ya kinywa cha kisima.

4 Basi Yakobo akawaambia: “Ndugu zangu, ninyi ni watu wa wapi?” Wakasema: “Sisi ni watu wa Harani.”+ 5 Akawaambia: “Je, munamujua Labani+ mujukuu wa Nahori?”+ Wakajibu: Tunamujua.” 6 Akawaambia: “Iko* muzuri?” Wakajibu: “Iko* muzuri. Na angalia, Raheli binti yake+ anakuja na kondoo!” 7 Kisha akasema: “Ingali muchana. Haiko wakati wa kukusanya mifugo. Mupatie kondoo maji, na kisha muende kuwakulisha.” 8 Wakasema: “Haturuhusiwe kufanya vile mupaka makundi yote ya kondoo yakusanywe na wavingirishe jiwe na kuliondoa kwenye kinywa cha kisima. Kisha tunapatia kondoo maji.”

9 Wakati alikuwa angali anazungumuza nao, Raheli akakuja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa muchungaji. 10 Wakati Yakobo alimuona Raheli binti ya Labani ndugu ya mama yake, na kondoo wa Labani, mara moja Yakobo akaenda karibu na akaviringisha jiwe na kuliondoa kwenye kinywa cha kisima na akapatia maji kondoo wa Labani ndugu ya mama yake. 11 Kisha Yakobo akamubusu Raheli na akapandisha sauti yake na akaanza kulia. 12 Na Yakobo akaanza kumuambia Raheli kwamba yeye ni mutu wa jamaa* ya baba yake na kwamba yeye ni mwana wa Rebeka. Na Raheli akakimbia kuenda kumuambia baba yake.

13 Wakati tu Labani+ alisikia habari kuhusu Yakobo mwana wa dada yake, akakimbia ili kumupokea. Akamukumbatia na kumubusu na kumuleta katika nyumba yake. Na akaanza kumuelezea Labani mambo hayo yote. 14 Labani akamuambia: “Wewe kwa kweli ni mufupa wangu na nyama yangu.”* Kwa hiyo Yakobo akakaa na Labani mwezi muzima.

15 Kisha Labani akamuambia Yakobo: “Je, unapaswa kunitumikia bure kwa sababu tu uko mutu wa jamaa* yangu?+ Uniambie, mushahara wako utakuwa nini?”+ 16 Sasa Labani alikuwa na mabinti wawili. Jina la mukubwa lilikuwa Lea, na jina la mudogo lilikuwa Raheli.+ 17 Lakini macho ya Lea hayakukuwa yanangaa, lakini Raheli alikuwa mwanamuke mwenye kuvutia sana na mwenye sura na umbo ya muzuri sana. 18 Yakobo alikuwa amemupenda sana Raheli, kwa hiyo akamuambia Labani: “Niko tayari kukutumikia miaka saba (7) kwa ajili ya Raheli binti yako mudogo.”+ 19 Labani akasema: “Ni muzuri zaidi nikupatie ule binti kuliko kumupatia mwanaume mwingine. Endelea kuishi na mimi.” 20 Na Yakobo akatumika miaka saba (7) kwa ajili ya Raheli,+ lakini aliona miaka hiyo kama siku kidogo tu kwa sababu alimupenda Raheli.

21 Kisha Yakobo akamuambia Labani: “Unipatie bibi yangu kwa sababu siku zangu zimemalizika, na uniache nilale naye.” 22 Basi Labani akakusanya watu wote wa mahali pale na akafanya karamu. 23 Lakini wakati wa mangaribi, akamuchukua Lea binti yake na kumuleta kwa Yakobo ili alale naye. 24 Pia, Labani akamuchukua Zilpa mutumishi wake mwanamuke na kumupatia Lea binti yake ili akuwe mutumishi wake.+ 25 Asubui Yakobo akaona kumbe ilikuwa Lea! Kwa hiyo akamuambia Labani: “Ni jambo gani hili lenye umenitendea? Je, sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Sababu gani umenidanganya?”+ 26 Labani akasema: “Haiko desturi yetu kupatia mutu mwanamuke mudogo zaidi mbele ya muzaliwa wa kwanza. 27 Furahia juma moja la mwanamuke huyu. Kisha nitakupatia pia huyu mwanamuke mwingine kwa kunitumikia miaka ingine saba (7).”+ 28 Yakobo akafanya vile, akafurahia juma moja la mwanamuke huyu, kisha akamupatia Raheli binti yake akuwe bibi yake. 29 Tena, Labani akamuchukua Bilha mutumishi wake mwanamuke+ na kumupatia Raheli binti yake ili akuwe mutumishi wake.+

30 Kisha Yakobo akalala pia na Raheli, na akamupenda Raheli kuliko Lea, na akamutumikia Labani kwa miaka ingine saba (7).+ 31 Wakati Yehova aliona kwamba Lea hakukuwa anapendwa,* akamuwezesha kupata mimba,*+ lakini Raheli alikuwa tasa.+ 32 Kwa hiyo Lea akakuwa na mimba na akamuzaa mwana na kumupatia jina Rubeni,*+ kwa maana alisema: “Ni kwa sababu Yehova ameona mateso yangu,+ kwa kuwa sasa bwana yangu ataanza kunipenda.” 33 Na akakuwa tena na mimba na akamuzaa mwana na kisha akasema: “Ni kwa sababu Yehova amesikiliza, kwamba sikukuwa ninapendwa, kwa hiyo amenipatia huyu pia.” Kisha akamupatia jina Simeoni.*+ 34 Na akakuwa tena na mimba na akamuzaa mwana, kisha akasema: “Sasa bwana yangu atajiunga na mimi, kwa sababu nimemuzalia wana watatu (3).” Kwa hiyo mutoto huyo akapewa jina Lawi.*+ 35 Na akakuwa na mimba mara ingine tena na akamuzaa mwana, kisha akasema: “Mara hii nitamusifu Yehova.” Kwa hiyo akamupatia jina Yuda.*+ Kisha Lea akaacha kuzaa.

30 Wakati Raheli aliona kwamba hakumuzalia Yakobo watoto, alimusikilia wivu dada yake na akaanza kumuambia Yakobo: “Unipatie watoto, kama haunipatie nitakufa.” 2 Kwa hiyo kasirani ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli, na akasema: “Je, mimi niko Mungu, mwenye amekuzuia kupata watoto?”* 3 Kwa hiyo Raheli akasema: “Chukua Bilha mutumwa wangu mwanamuke.+ Lala naye ili anizalie watoto,* ili mimi pia nipate watoto kupitia yeye.” 4 Basi akamupatia Bilha mutumishi wake akuwe bibi yake, na Yakobo akalala naye.+ 5 Bilha akakuwa na mimba na kisha wakati fulani akamuzalia Yakobo mwana. 6 Kisha Raheli akasema: “Mungu amekuwa muamuzi wangu na pia amesikiliza sauti yangu kwa kunipatia mwana.” Ndiyo sababu alimupatia jina Dani.*+ 7 Bilha, mutumishi wa Raheli, akakuwa tena na mimba na kisha wakati fulani akamuzalia Yakobo mwana wa pili. 8 Kisha Raheli akasema: “Nimepigana mieleka kwa nguvu na dada yangu. Pia nimekuwa mushindi!” Kwa hiyo akamupatia jina Naftali.*+

9 Wakati Lea aliona kwamba ameacha kuzaa watoto, akamuchukua Zilpa mutumishi wake na kumupatia Yakobo ili Zilpa akuwe bibi yake.+ 10 Na Zilpa, mutumishi wa Lea, akamuzalia Yakobo mwana. 11 Kisha Lea akasema: “Hii ni neema!” Kwa hiyo akamupatia jina Gadi.*+ 12 Kisha, Zilpa, mutumishi wa Lea, akamuzalia Yakobo mwana wa pili. 13 Kisha Lea akasema: “Nimefurahi sana! Kwa maana hakika mabinti watanitangaza kuwa mwenye furaha.”+ Kwa hiyo akamupatia jina Asheri.*+

14 Sasa Rubeni+ alikuwa anatembea katika siku za mavuno ya ngano, na akapata matunda ya dudai katika pori. Kwa hiyo akayaletea Lea mama yake. Basi Raheli akamuambia Lea: “Tafazali, unipatie matunda fulani ya dudai ya mwana wako.” 15 Basi Lea akamuambia: “Je, ni jambo la kidogo kwamba wewe umemuchukua bwana yangu?+ Je, unataka pia kuchukua matunda ya dudai ya mwana wangu?” Kwa hiyo Raheli akasema: “Ni sawa. Yakobo atalala na wewe usiku wa leo kama unanipatia matunda ya dudai ya mwana wako.”

16 Wakati Yakobo alirudia mangaribi kutoka kwenye eneo la mashamba, Lea akaenda kumupokea na akasema: “Utalala na mimi, kwa sababu nimekukodisha moja kwa moja kwa matunda ya dudai ya mwana wangu.” Kwa hiyo akalala naye usiku huo. 17 Na Mungu akasikia na kumujibu Lea, naye akakuwa na mimba na kisha wakati fulani akamuzalia Yakobo mwana wa tano (5). 18 Kisha Lea akasema: “Mungu amenipatia mushahara* wangu kwa sababu nimemupatia bwana yangu mutumishi wangu.” Kwa hiyo akamupatia jina Isakari.*+ 19 Na Lea akakuwa na mimba mara ingine tena na kisha wakati fulani akamuzalia Yakobo mwana wa sita (6).+ 20 Kisha Lea akasema: “Mungu amenipatia zawadi, ndiyo, zawadi ya muzuri. Sasa bwana yangu atanivumilia,+ kwa sababu nimemuzalia wana sita (6).”+ Kwa hiyo akamupatia jina Zabuloni.*+ 21 Kisha, akamuzaa mutoto mwanamuke na akamupatia jina Dina.+

22 Mwishowe Mungu akamukumbuka Raheli, na akamusikia na kumujibu kwa kumuwezesha akuwe na mimba.*+ 23 Na akakuwa na mimba na akazaa mwana. Kisha akasema: “Mungu ameniondolea haya yangu!”+ 24 Kwa hiyo akamupatia jina Yosefu,*+ na akasema: “Yehova ananiongezea mwana mwingine.”

25 Kisha Raheli kumuzaa Yosefu, mara moja Yakobo akamuambia Labani: “Uniache niende kwangu na katika inchi yangu.+ 26 Unipatie bibi zangu na watoto wangu wenye nimepata kwa kukutumikia; ili niende, kwa maana unajua muzuri namna nimekutumikia.”+ 27 Kisha Labani akamuambia: “Kama nimekubaliwa mbele ya macho yako,⁠—nimetambua kupitia alama za mambo yenye yatatokea* kwamba Yehova ananibariki kwa sababu yako.” 28 Na akaongeza: “Uniambie mushahara wako utakuwa nini, na nitakupatia.”+ 29 Kwa hiyo Yakobo akamuambia: “Unajua namna nimekutumikia na namna mifugo yako imekuwa katika mikono yangu;+ 30 ulikuwa na wanyama kidogo mbele nifike, lakini mifugo yako imeongezeka na imekuwa na wanyama wengi, na Yehova amekubariki tangu wakati nilifika. Sasa ni wakati gani nitafanya jambo fulani kwa ajili ya nyumba yangu mwenyewe?”+

31 Kisha akasema: “Nikupatie nini?” Yakobo akasema: “Hautanipatia kitu chochote! Ukinifanyia jambo hili moja, nitaanza tena kuchunga kundi lako na kulilinda.+ 32 Nitapita katika kundi lako lote leo. Tia pembeni kila kondoo mwenye madoa-madoa na mwenye alama zenye rangi na kila kondoo wa rangi ya kahawa kati ya wana-kondoo dume na mbuzi-dike mumoja mwenye alama zenye rangi na mwenye madoa-madoa kati ya mbuzi-dike. Kuanzia sasa, watakuwa mushahara wangu.+ 33 Na haki yangu itasema* kwa ajili yangu siku utakuja kuangalia mushahara wangu; kila mwenye hana madoa-madoa na mwenye hana alama zenye rangi kati ya mbuzi-dike na kila mwenye hana rangi ya kahawa kati ya wana-kondoo dume atakuwa ameibwa kama atapatikana pamoja na mimi.”

34 Basi Labani akasema: “Ni sawa! Ikuwe kama vile unasema.”+ 35 Basi siku hiyo, akatia pembeni mbuzi-dume wenye mistari-mistari na wenye alama zenye rangi na mbuzi-dike wote wenye madoa-madoa na wenye alama zenye rangi, kila mwenye alikuwa na rangi nyeupe kidogo na wa rangi ya kahawa kati ya wana-kondoo dume, na akawapatia wana wake ili wawachunge. 36 Kisha mambo hayo Labani akaenda mbali na Yakobo, mwendo wa siku tatu (3), na Yakobo alikuwa anachunga makundi yenye yalibakia ya Labani.

37 Kisha Yakobo akakamata fimbo za mubichi za muti wa mulubna, muti wa lozi, na muti wa mwaramoni, na akaondoa ngozi ili kutia madoa meupe kwenye fimbo hizo kwa kufanya sehemu nyeupe za fimbo hizo zionekane. 38 Kisha akaweka zile fimbo zenye alikuwa ameondoa ngozi mbele ya kundi, katika mifereji, katika vyombo vya kuwekea maji ya kunywa ya wanyama, kwenye makundi yalikuja kunywa maji, ili wanyama wakuwe na hamu ya kupandana mbele ya fimbo hizo wakati walikuwa wanakuja kunywa maji.

39 Kwa hiyo makundi yalikuwa yanapata hamu ya kupandana mbele ya zile fimbo, na makundi yalikuwa yanazaa wanyama wenye mistari-mistari, madoa-madoa, na alama zenye rangi. 40 Kisha Yakobo akatenganisha wana-kondoo dume na akageuza nyuso za wanyama ziangaliane na wanyama wenye mistari-mistari na wote wenye rangi ya kahawa kati ya makundi ya Labani. Kisha akatenganisha makundi yake mwenyewe na hakuyachanganya pamoja na makundi ya Labani. 41 Kila mara wakati wanyama wenye nguvu walipata hamu ya kupandana, Yakobo alikuwa anaweka zile fimbo katika mifereji mbele ya macho ya makundi, ili wanyama hao wapandane karibu na zile fimbo. 42 Lakini wakati wanyama walikuwa wazaifu, hakuweka zile fimbo mahali pale. Kwa hiyo sikuzote wanyama wazaifu walikuwa wa Labani, lakini wale wenye nguvu walikuwa wa Yakobo.+

43 Na mwanaume huyu akakuwa tajiri sana, na akakuwa na makundi mengi, watumishi wanaume na watumishi wanamuke na ngamia na punda.+

31 Kisha Yakobo akasikia mambo yenye wana wa Labani walikuwa wanasema: “Yakobo amekamata kila kitu chenye kilikuwa cha baba yetu, na amepata utajiri wote huu kutokana na mali yenye ilikuwa ya baba yetu.”+ 2 Wakati Yakobo alikuwa anaangalia uso wa Labani, aliona kwamba mutazamo wake kumuelekea haukukuwa kama vile ulikuwa zamani.+ 3 Mwishowe Yehova akamuambia Yakobo: “Rudia katika inchi ya baba zako na kwa watu wa jamaa yako,+ na nitaendelea kuwa pamoja na wewe.” 4 Kisha Yakobo akatumia Raheli na Lea ujumbe ili wakuje kwenye eneo la mashamba mahali kundi lake lilikuwa, 5 na akawaambia:

“Nimeona kwamba mutazamo wa baba yenu kunielekea umebadilika,+ lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja na mimi.+ 6 Ninyi wenyewe munajua hakika kwamba nimemutumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote.+ 7 Na baba yenu amejaribu kunidanganya na kubadilisha mushahara wangu mara kumi (10); lakini Mungu hakumuruhusu aniumize. 8 Kila mara wakati alisema, ‘Wanyama wenye madoa-madoa watakuwa mushahara wako,’ kundi lote lilizaa wanyama wenye madoa-madoa; na kila mara wakati alisema, ‘Wanyama wenye mistari-mistari watakuwa mushahara wako,’ kundi lote lilizaa wanyama wenye mistari-mistari.+ 9 Kwa hiyo Mungu aliendelea kukamata mifugo ya baba yenu na kunipatia. 10 Siku moja, wakati kundi lilikuwa na hamu ya kupandana, niliinua macho yangu na kuona katika ndoto kwamba mbuzi-dume wenye walikuwa wanapanda kundi walikuwa wenye mistari-mistari, madoa-madoa, na alama zenye rangi.+ 11 Kisha malaika wa Mungu wa kweli akaniita katika ndoto, ‘Yakobo!’ nikasema, ‘Mimi huyu.’ 12 Na akaendelea kusema, ‘Tafazali, inua macho yako, na uone kwamba mbuzi-dume wote wenye kupanda kundi ni wenye mistari-mistari, madoa-madoa, na alama zenye rangi, kwa maana nimeona mambo yote yenye Labani anakutendea.+ 13 Mimi ni Mungu wa kweli wa Beteli,+ mahali kwenye ulitia nguzo mafuta na kufanya naziri kwangu.+ Sasa simama, toka katika inchi hii, na urudie katika inchi yako ya kizalikio.’”+

14 Kwa hiyo Raheli na Lea wakamujibu: “Je, kungali fungu lolote lenye tunaweza kuriti katika nyumba ya baba yetu? 15 Je, yeye hatuone kama wageni, kwa sababu ametuuzisha na ameendelea kutumia feza zote zenye zilitolewa kwa ajili yetu?+ 16 Utajiri wote wenye Mungu amekamata kwa baba yetu ni wetu na wa watoto wetu.+ Kwa hiyo, basi, fanya kila kitu chenye Mungu amekuambia ufanye.”+

17 Kwa hiyo Yakobo akasimama na akapandisha watoto wake na bibi zake juu ya ngamia,+ 18 na akaanza kupeleka mifugo yake na mali zote zenye alikuwa amekusanya,+ mifugo yake yenye alikuwa amekusanya kule Padan-aramu, ili kuenda kwa Isaka baba yake katika inchi ya Kanaani.+

19 Sasa wakati Labani alikuwa ameenda kukata manyoya ya kondoo wake, Raheli aliiba sanamu za terafimu*+ zenye zilikuwa za baba yake.+ 20 Tena, Yakobo akamucheza akili Labani ule Mwaramu, kwa maana hakumuambia kwamba alikuwa anaondoka. 21 Na akakimbia na kuvuka ule Muto,*+ yeye na vyote vyenye alikuwa navyo. Kisha akaelekea upande wa eneo lenye milima la Gileadi.+ 22 Siku ya tatu (3), Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia. 23 Kwa hiyo Labani akachukua ndugu zake* na kumufuatilia Yakobo kwa safari ya siku saba (7) na akamupata katika eneo lenye milima la Gileadi. 24 Kisha Mungu akamutokea Labani ule Mwaramu+ katika ndoto wakati wa usiku+ na kumuambia: “Ukuwe muangalifu juu ya mambo yenye utamuambia Yakobo, kama ni ya muzuri ao ya mubaya.”+

25 Kwa hiyo Labani akafika karibu na Yakobo, Yakobo alikuwa amesimamisha hema yake katika mulima na Labani alikuwa amepiga kambi pamoja na ndugu zake katika eneo lenye milima la Gileadi. 26 Kisha Labani akamuambia Yakobo: “Umefanya nini? Sababu gani umenicheza akili na kupeleka mabinti wangu kama watu wenye walikamatwa mateka kwa upanga? 27 Sababu gani ulikimbia kwa uficho na kunicheza akili na haukuniambia? Kama ungeniambia, ningekuaga kwa furaha na nyimbo, kwa ngoma ya kidogo* na kinubi. 28 Lakini haukunipatia nafasi ya kubusu wajukuu* wangu na mabinti wangu. Umetenda kwa upumbavu. 29 Niko na uwezo wa kukuumiza, lakini Mungu wa baba yenu alizungumuza na mimi usiku wa jana, alisema, ‘Ukuwe muangalifu juu ya mambo yenye utamuambia Yakobo, kama ni ya muzuri ao ya mubaya.’+ 30 Sasa umeenda kwa sababu umekuwa ukitamani sana kurudia kwenye nyumba ya baba yako, lakini sababu gani umeiba miungu yangu?”+

31 Yakobo akamujibu Labani: “Ni kwa sababu niliogopa, kwa maana nilisema katika moyo wangu, ‘Unaweza kuninyanganya mabinti wako.’ 32 Mutu mwenye utapata na miungu yako, atauawa. Chunguza vitu vyenye niko navyo mbele ya hawa ndugu zetu, na ukamate kitu chochote chenye kuwa chako.” Lakini Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameiba miungu hiyo. 33 Kwa hiyo Labani akaingia katika hema ya Yakobo na hema ya Lea na hema ya wale watumwa wanamuke wawili,+ lakini hakuipata. Kisha akatoka katika hema ya Lea na kuingia katika hema ya Raheli. 34 Wakati huo, Raheli alikuwa amekamata zile sanamu za terafimu na kuziweka ndani ya kitunga chenye mwanamuke anaikalia juu ya ngamia, na alikuwa anaziikalia. Kwa hiyo Labani akatafuta-tafuta katika hema yote lakini hakuzipata. 35 Kisha Raheli akamuambia baba yake: “Usikasirike, bwana wangu, kwa sababu siwezi kusimama mbele yako, kwa maana nimepatwa na kitu chenye wanamuke wanazoea kupata.”+ Kwa hiyo akatafuta-tafuta kwa uangalifu lakini hakupata zile sanamu za terafimu.+

36 Basi Yakobo akakasirika na kuanza kumulaumu Labani. Kisha Yakobo akamuambia Labani: “Nimefanya kosa gani, na nimetenda zambi gani ili unifuatilie kwa ukali? 37 Sasa kwa kuwa umetafuta-tafuta katika vitu vyangu vyote, umepata kitu gani chenye kuwa cha nyumba yako? Ukiweke hapa mbele ya ndugu zangu na ndugu zako, na waamue kati ya sisi wawili. 38 Miaka hii makumi mbili (20) yenye nimekuwa pamoja na wewe, hakuna siku mimba za kondoo wako na mbuzi wako zimeharibika,+ na hakuna siku nimekula kondoo-dume wa kundi lako. 39 Sikukuletea munyama mwenye alipasuliwa na wanyama wa pori.+ Nilikuwa ninalipa hasara ya munyama huyo mimi mwenyewe. Ikuwe munyama aliibwa muchana ao aliibwa usiku, ulikuwa unaniomba nimulipe. 40 Jua lilinichoma wakati wa muchana, na baridi ilinipiga wakati wa usiku, na macho yangu yalikuwa yanakosa usingizi.+ 41 Nimeishi miaka makumi mbili (20) katika nyumba yako. Nimekutumikia miaka kumi na ine (14) ili unipatie mabinti wako wawili na miaka sita (6) ya kuchunga kundi lako, na ulibadilisha mushahara wangu mara kumi (10).+ 42 Kama Mungu wa baba yangu,+ Mungu wa Abrahamu na ule Mwenye Isaka anaogopa,*+ hangekuwa upande wangu, ungeniacha niende mikono wazi. Mungu ameona mateso yangu na kazi ya jasho ya mikono yangu, ndiyo sababu alikukaripia usiku wenye umepita.”+

43 Kisha Labani akamujibu Yakobo: “Mabinti hawa ni mabinti wangu na watoto hawa ni watoto wangu na kundi hili ni kundi langu, na kila kitu chenye unaona ni changu mimi na mabinti wangu. Namna gani ninaweza kuumiza mabinti hawa leo ao kuumiza watoto wenye wao wamezaa? 44 Sasa, kuja tufanye agano, mimi na wewe, na agano hilo litakuwa ushahidi kati yetu.” 45 Kwa hiyo Yakobo akakamata jiwe na akalisimamisha kama nguzo.+ 46 Kisha Yakobo akaambia ndugu zake: “Muokote majiwe!” Na wakakamata majiwe na kufanya rundo. Kisha wakakula mahali pale juu ya lile rundo la majiwe. 47 Na Labani akaanza kuita lile rundo Yegar-sahaduta,* lakini Yakobo akaliita Galeedi.*

48 Kisha Labani akasema: “Rundo hili la majiwe ni ushahidi kati yangu na wewe leo.” Ndiyo sababu aliita lile rundo Galeedi,+ 49 na pia Munara wa Mulinzi, kwa sababu alisema: “Yehova aendelee kuchungulia kati yako na mimi wakati tutakuwa hatuonane. 50 Ukitesa mabinti wangu ao ukianza kuchukua bibi wengine kuongezea juu ya mabinti wangu, hata kama hakuna mutu mwenye kuwa pamoja na sisi, kumbuka kwamba Mungu atakuwa shahidi kati yako na mimi.” 51 Labani akaendelea kumuambia Yakobo: “Hili hapa ni rundo la majiwe, na hii ni nguzo yenye nimesimamisha kati yako na mimi. 52 Rundo hili la majiwe ni ushahidi, na nguzo hii pia ni kitu chenye kutoa ushahidi,+ kwamba mimi sitapita rundo hili la majiwe ili kuja kukuumiza na wewe hautapita rundo hili la majiwe na nguzo hii ili kuja kuniumiza. 53 Mungu wa Abrahamu+ na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba yao, akuwe muamuzi kati yetu.” Na Yakobo akaapa kwa jina la ule Mwenye Isaka baba yake anaogopa.*+

54 Kisha mambo hayo Yakobo akatoa zabihu katika mulima na akaalika ndugu zake wakule mukate. Kwa hiyo wakakula na wakalala usiku huo katika mulima. 55 Lakini, Labani akaamuka asubui sana, akabusu wajukuu* wake+ na mabinti wake na kuwabariki.+ Kisha Labani akaondoka na kurudia kwake.+

32 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake, na malaika wa Mungu wakakutana naye. 2 Wakati tu aliwaona, Yakobo akasema: “Hii ni kambi ya Mungu!” Kwa hiyo akaita mahali pale Mahanaimu.*

3 Kisha Yakobo akatuma wajumbe wamutangulie kuenda kwa Esau ndugu yake katika inchi ya Seiri,+ eneo* la Edomu,+ 4 na akawaamuru: “Ni hivi mutamuambia bwana wangu, Esau, ‘Mutumishi wako Yakobo anasema hivi: “Nimeishi* na Labani wakati murefu mupaka sasa.+ 5 Na nimepata ngombe-dume, punda, kondoo, na watumishi wanaume na watumishi wanamuke,+ na ninatuma ujumbe huu ili kumujulisha bwana wangu, kusudi nikubaliwe mbele ya macho yako.”’”

6 Kisha wakati fulani wajumbe hao wakarudia kwa Yakobo, na kusema: “Tulikutana na ndugu yako Esau, na sasa anakuja ili kukutana na wewe, na iko* na wanaume mia ine (400).”+ 7 Na Yakobo akaogopa sana na akakuwa na wasiwasi.+ Kwa hiyo akagawanya watu wenye walikuwa pamoja naye, na pia makundi, ngombe, na ngamia, katika kambi mbili. 8 Akasema: “Esau akishambulia kikundi kimoja, kikundi kingine kitaponyoka.”

9 Kisha Yakobo akasema: “Ee Mungu wa baba yangu Abrahamu na Mungu wa baba yangu Isaka, Ee Yehova, wewe mwenye kuniambia, ‘Rudia katika inchi yako na kwa watu wa jamaa yako, na mimi nitakutendea mema,’+ 10 sistahili upendo wote mushikamanifu na uaminifu wote wenye umemuonyesha mutumishi wako,+ kwa maana nilikuwa tu na fimbo wakati nilivuka muto huu Yordani lakini sasa nimekuwa kambi mbili.+ 11 Ninakuomba,+ uniokoe, katika mukono wa ndugu yangu Esau, kwa maana ninaogopa kwamba anaweza kuja na kunishambulia mimi,+ na pia mama na watoto wao. 12 Lakini umesema: ‘Hakika nitakutendea mambo ya muzuri, na nitafanya uzao wako ukuwe mwingi* kama chembe za muchanga wa bahari, zenye haziwezi kuhesabiwa kwa sababu ya ziko nyingi sana.’”+

13 Na Yakobo akalala pale usiku huo. Kisha akakamata sehemu fulani ya mali zake ili amupatie zawadi Esau ndugu yake:+ 14 mbuzi-dike mia mbili (200), mbuzi-dume makumi mbili (20), kondoo-dike mia mbili, na kondoo-dume makumi mbili, 15 ngamia makumi tatu (30) wenye kunyonyesha vitoto vyao, ngombe makumi ine (40), ngombe-dume kumi (10), punda-dike makumi mbili (20), na punda-dume kumi wenye kukomaa.+

16 Akapatia watumishi wake wanyama hao, kundi moja kisha lingine, na akaambia watumishi wake: “Munitangulie na muvuke mbele yangu, na munapaswa kuacha nafasi kati ya kundi moja na kundi lenye kufuata.” 17 Pia akamuamuru ule wa kwanza: “Kama Esau ndugu yangu anakutana na wewe na kuuliza, ‘Wewe uko mutumishi wa nani, na unaenda wapi, na wale wanyama wenye kuwa mbele yako ni wa nani?’ 18 basi unapaswa kumuambia, ‘Ni wa mutumishi wako Yakobo. Ni zawadi yenye ilitumwa kwa bwana wangu, kwa Esau,+ na angalia! yeye mwenyewe iko* nyuma yetu pia.’” 19 Na akamuamuru pia mutumishi wa pili, wa tatu (3), na wale wote wenye walikuwa wanafuata yale makundi: “Ni vile mutamuambia Esau wakati mutakutana naye. 20 Na pia munapaswa kusema, ‘Mutumishi wako Yakobo iko* nyuma yetu.’” Kwa maana alisema katika moyo wake: ‘Kama ninamutuliza kwa kutuma zawadi initangulie,+ basi wakati nitamuona, pengine atanipokea muzuri.’ 21 Kwa hiyo zawadi hizo zikavuka na kumutangulia, lakini yeye mwenyewe akalala katika kambi usiku huo.

22 Kisha wakati fulani katika usiku huo, akasimama na kuchukua bibi zake wawili+ na watumishi wake wanamuke wawili+ na wana wake wadogo kumi na moja (11) na akavuka nafasi ya kuvukia ya Yaboki.+ 23 Kwa hiyo akawachukua na kuwavukisha muto mudogo,* na akavukisha kila kitu chenye alikuwa nacho.

24 Mwishowe Yakobo akabakia peke yake. Kisha mwanaume mumoja akaanza kupigana mieleka naye mupaka wakati kulipambazuka.*+ 25 Wakati ule mwanaume aliona kwamba Yakobo amemushinda, akamugusa tundu la maungio ya kiuno; na tundu la maungio ya kiuno cha Yakobo likateguka wakati alikuwa anapigana mieleka naye.+ 26 Kisha ule mwanaume akasema: “Uniache niende, kwa maana kumepambazuka.”* Lakini Yakobo akasema: “Sitakuacha uende mupaka unibariki.”+ 27 Kwa hiyo akamuambia: “Jina lako nani?” akajibu: “Yakobo.” 28 Kisha akamuambia: “Jina lako halitakuwa tena Yakobo lakini Israeli,*+ kwa maana umeshindana na Mungu+ na wanadamu na mwishowe umeshinda.” 29 Yakobo akamuuliza: “Tafazali, uniambie jina lako.” Lakini, akasema: “Sababu gani unauliza jina langu?”+ Kisha akamubariki pale. 30 Kwa hiyo Yakobo akaita mahali pale Penieli,*+ kwa sababu alisema, “Nimemuona Mungu uso kwa uso, lakini uzima wangu ulilindwa.”*+

31 Na jua likaanza kuangaza juu ya Yakobo wakati alipita karibu na Penueli,* lakini alikuwa anatembea kwa kukokota muguu* kwa sababu ya kiuno chake.+ 32 Ndiyo maana mupaka leo wana wa Israeli hawazoee kula mushipa wa paja,* wenye kuwa kwenye tundu la maungio ya kiuno, kwa sababu mwanaume huyo aligusaka tundu la maungio ya kiuno cha Yakobo karibu na mushipa wa paja.

33 Sasa Yakobo akainua macho yake na kumuona Esau anakuja, na wanaume mia ine (400) walikuwa pamoja naye.+ Kwa hiyo akagawanya watoto kati ya Lea, Raheli, na wale watumishi wanamuke wawili.+ 2 Akaweka wale watumishi wanamuke na watoto wao mbele,+ kisha Lea na watoto wake,+ na Raheli+ na Yosefu nyuma yao. 3 Kisha yeye mwenyewe akapita mbele yao na kuinama mupaka chini mara saba (7) wakati alimukaribia ndugu yake.

4 Lakini Esau akakimbia ili kukutana naye, akamukumbatia na kumubusu, nao wakaanza kulia. 5 Wakati aliinua macho yake na kuona wanamuke na watoto, akasema: “Ni nani hawa wenye kuwa pamoja na wewe?” Yakobo akamuambia: “Hawa ni watoto wenye Mungu amemupatia mutumishi wako.”+ 6 Basi watumishi wanamuke wakaenda mbele pamoja na watoto wao na kuinama chini, 7 na Lea pia akaenda mbele pamoja na watoto wake, nao wakainama chini. Kisha Yosefu akaenda mbele pamoja na Raheli, nao wakainama chini.+

8 Esau akasema: “Kambi yote hii ya wasafiri yenye nimekutana nayo iko na kusudi gani?”+ Yakobo akajibu: “Ili kukubaliwa mbele ya macho ya bwana wangu.”+ 9 Kisha Esau akasema: “Niko na mali nyingi sana, ndugu yangu.+ Bakia na mali yako.” 10 Lakini Yakobo akasema: “Hapana, tafazali. Kama nimekubaliwa mbele ya macho yako, unapaswa kukubali zawadi ya mukono wangu, kwa sababu nimeileta ili nione uso wako. Na nimeona uso wako kama vile kuona uso wa Mungu, kwa sababu umenipokea kwa furaha.+ 11 Tafazali, kamata zawadi ya baraka yenye ililetwa kwako,+ kwa sababu Mungu amenibariki na niko na kila kitu chenye ninahitaji.”+ Na akaendelea kumukaza, mupaka akaikamata.

12 Kisha wakati fulani Esau akasema: “Tuondoke na tuende, na mimi nikutangulie.” 13 Lakini Yakobo akamuambia: “Bwana wangu anajua kwamba watoto ni wazaifu+ na niko na kondoo na ngombe wenye kunyonyesha vitoto vyao. Ikiwa wanapelekwa haraka-haraka sana kwa siku moja, basi kundi lote litakufa. 14 Tafazali, bwana wangu atangulie mutumishi wake, lakini mimi nitaendelea na safari polepole kwa mwendo wa mifugo na wa watoto mupaka wakati nitafika kwa bwana wangu kule Seiri.”+ 15 Kisha Esau akasema: “Tafazali, uniruhusu niache watu wangu fulani pamoja na wewe.” Yakobo akasema, “Sababu gani ufanye vile? Ninaomba tu nikubaliwe mbele ya macho ya bwana wangu.” 16 Basi siku hiyo Esau akasafiri na kurudia Seiri.

17 Na Yakobo akasafiri mupaka Sukoti,+ na akajijengea nyumba na kutengeneza vibanda kwa ajili ya mifugo yake. Ndiyo sababu aliita mahali pale Sukoti.*

18 Kisha kutoka Padan-aramu,+ Yakobo akafika salama kwenye muji wa Shekemu+ katika inchi ya Kanaani,+ na akapiga kambi karibu na ule muji. 19 Kisha akanunua sehemu ya shamba ya wana wa Hamori, baba ya Shekemu, kwa vipande mia moja (100) vya feza,+ akasimamisha hema yake pale. 20 Akasimamisha mazabahu mahali pale na kuipatia jina Mungu, Mungu wa Israeli.+

34 Sasa Dina, binti ya Yakobo mwenye Lea alimuzalia,+ alikuwa anazoea kutembelea* vijana wanamuke wa inchi.+ 2 Wakati Shekemu mwana wa Hamori Muhivi,+ mukubwa wa inchi, alimuona, akamukamata na kulala naye na kumulala kinguvu. 3 Na akashikamana* sana na Dina, binti ya Yakobo, na akamupenda ule kijana mwanamuke na alikuwa anaongea naye kwa kumushawishi.* 4 Mwishowe Shekemu akamuambia Hamori+ baba yake: “Unichukulie huyu kijana mwanamuke ili akuwe bibi yangu.”

5 Wakati Yakobo alisikia kwamba Shekemu alikuwa amemuchafua Dina binti yake, wana wake walikuwa pamoja na mifugo yake katika eneo la mashamba. Kwa hiyo Yakobo alibakia kimya mupaka wakati wana wake walirudia. 6 Kisha wakati fulani Hamori, baba ya Shekemu, akaenda kuzungumuza na Yakobo. 7 Lakini wana wa Yakobo wakasikia jambo hilo na mara moja wakarudia kutoka katika eneo la mashamba. Wakaumia katika mioyo yao na wakakasirika sana kwa sababu Shekemu alikuwa ameletea Israeli haya kwa kulala na binti ya Yakobo,+ jambo lenye halikupaswa kufanywa.+

8 Hamori akazungumuza nao, na kusema: “Mwana wangu Shekemu anamupenda sana* binti yenu. Tafazali mumupatie binti yenu ili akuwe bibi yake, 9 na mufanye mapatano ya ndoa* na sisi. Mutupatie mabinti wenu, na ninyi muchukue mabinti wetu kwa ajili yenu wenyewe.+ 10 Munaweza kukaa pamoja na sisi, na inchi itakuwa wazi mbele yenu. Mukae na mufanye biashara ndani yake na mufanye makao yenu ndani yake.” 11 Kisha Shekemu akamuambia baba ya Dina na ndugu zake: “Muache nikubaliwe mbele ya macho yenu, na nitawapatia kila kitu chenye mutaniomba. 12 Munaweza kuniomba kiasi kikubwa sana cha mali ya kuoa na zawadi.+ Niko tayari kutoa kila kitu chenye mutaniambia. Lakini, munipatie tu ule kijana mwanamuke akuwe bibi yangu.”

13 Na wana wa Yakobo wakamujibu kwa udanganyifu Shekemu na Hamori baba yake, kwa sababu Shekemu alikuwa amemuchafua Dina dada yao. 14 Wakawaambia: “Hatuwezi hata kidogo kufanya jambo kama hilo, kupatia dada yetu mwanaume mwenye hatahiriwe,*+ kwa sababu hilo ni jambo la haya kwetu. 15 Tunaweza kukubali tu kwa sharti hili: kwamba mukuwe kama sisi na mutahiri wanaume wenu wote.+ 16 Halafu tutawapatia mabinti wetu, na sisi tutachukua mabinti wenu kwa ajili yetu, na tutakaa pamoja na ninyi na tutakuwa kikundi kimoja cha watu. 17 Lakini kama hamutusikilize na kutahiriwa, basi tutamuchukua binti yetu na kuenda.”

18 Maneno yao yakamufurahisha Hamori+ na Shekemu mwana wake.+ 19 Ule kijana mwanaume hakukawia kutimiza mambo yenye walimuomba,+ kwa sababu alimufurahia sana binti ya Yakobo, na alikuwa mwenye kuheshimiwa zaidi katika nyumba yote ya baba yake.

20 Kwa hiyo Hamori na Shekemu mwana wake wakaenda kwenye mulango mukubwa wa muji na kuzungumuza na wanaume wa muji wao,+ na kusema: 21 “Wanaume hawa wanapenda kuishi kwa amani pamoja na sisi. Muwaache wakae katika inchi na wafanye biashara ndani yake, kwa kuwa inchi hii ni kubwa kabisa na watapata mahali pa kuishi. Tunaweza kuchukua mabinti wao wakuwe bibi zetu, na tunaweza kuwapatia mabinti wetu.+ 22 Lakini wanaume hawa watakubali kuishi pamoja na sisi na tutakuwa kikundi kimoja cha watu kwa sharti hili: kila mwanaume kati yetu atahiriwe kama vile wao wanatahiriwa.+ 23 Sasa, je, mali zao, utajiri wao, na mifugo yao yote havitakuwa vyetu? Kwa hiyo tukubali sharti lao ili wakae pamoja na sisi.” 24 Watu wote wenye walikuwa wanatoka inje kupitia mulango mukubwa wa muji wakamusikiliza Hamori na Shekemu mwana wake, na wanaume wakatahiriwa, wale wote wenye walikuwa wanatoka inje kupitia mulango mukubwa wa muji.

25 Lakini, siku ya tatu (3), wakati walikuwa wangali na maumivu, wana wawili wa Yakobo, Simeoni na Lawi, ndugu za Dina,+ wakakamata kila mumoja upanga wake na kuingia kwa uficho katika muji na wakamuua kila mwanaume.+ 26 Wakamuua kwa upanga Hamori na Shekemu mwana wake, kisha wakamuchukua Dina kutoka katika nyumba ya Shekemu na wakaenda. 27 Wana wengine wa Yakobo wakafika na kuona wanaume wenye kuuawa na wakanyanganya vitu vya muji huo kwa sababu walikuwa wamemuchafua dada yao.+ 28 Wakakamata makundi yao, mifugo yao, punda wao, na kila kitu chenye kilikuwa katika muji na katika eneo la mashamba. 29 Walikamata pia mali zao zote, wakakamata watoto wao wadogo na bibi zao, na kunyanganya kila kitu katika zile nyumba.

30 Basi Yakobo akaambia Simeoni na Lawi:+ “Mumeniletea shida kubwa* na kunifanya ninuke mubaya mbele ya wakaaji wa inchi hii, kwa Wakanaani na Waperizi. Mimi sina watu wengi, na hakika watakusanyika pamoja ili kunishambulia na nitaharibiwa, mimi na nyumba yangu.” 31 Lakini wakasema: “Je, kuko mutu mwenye anapaswa kumutendea dada yetu kama kahaba?”

35 Kisha mambo hayo Mungu akamuambia Yakobo: “Simama, upande kuenda Beteli+ na ukae kule, na kule umujengee mazabahu Mungu wa kweli, mwenye alikutokea wakati ulikuwa unamukimbia Esau ndugu yako.”+

2 Basi Yakobo akaambia watu wa nyumba yake na wote wenye walikuwa pamoja naye: “Muondoe miungu ya kigeni yenye kuwa katikati yenu,+ na mujisafishe na kubadilisha nguo zenu, 3 kisha tusimame na kupanda kuenda Beteli. Kule nitamujengea mazabahu Mungu wa kweli, mwenye alinijibu katika siku ya taabu yangu na mwenye amekuwa pamoja na mimi kila mahali* kwenye nilienda.”+ 4 Kwa hiyo wakamupatia Yakobo miungu yote ya kigeni yenye walikuwa nayo na mahereni ya masikio yenye ilikuwa katika masikio yao, na Yakobo akazika* vitu vyote hivyo chini ya muti mukubwa wenye ulikuwa karibu na Shekemu.

5 Wakati walisafiri, woga wa Mungu uliangukia miji yenye iliwazunguka, kwa hiyo watu wa miji hiyo hawakufuatilia wana wa Yakobo. 6 Mwishowe Yakobo akafika Luzi,+ ni kusema, Beteli, katika inchi ya Kanaani, yeye na watu wote wenye walikuwa pamoja naye. 7 Akajenga mazabahu mahali pale na kupaita El-beteli,* kwa sababu Mungu wa kweli alikuwa amemutokea mahali pale wakati alikuwa anamukimbia ndugu yake.+ 8 Kisha wakati fulani Debora,+ mulezi wa Rebeka, akakufa na kuzikwa chini ya muti wa mwaloni karibu na Beteli. Basi akaita muti huo Alon-bakuti.*

9 Mungu akamutokea Yakobo mara ingine tena wakati alikuwa anatoka Padan-aramu na akamubariki. 10 Mungu akamuambia: “Jina lako ni Yakobo.+ Jina lako halitakuwa tena Yakobo, lakini sasa jina lako litakuwa Israeli.” Na Mungu akaanza kumuita Israeli.+ 11 Mungu akaendelea kumuambia: “Mimi ni Mungu Mweza-Yote.+ Zaa na uongezeke. Mataifa na kutaniko la mataifa yatatoka ndani yako,+ na wafalme watatoka ndani yako.*+ 12 Na kuhusu inchi yenye nimepatia Abrahamu na Isaka, nitakupatia wewe inchi hiyo, na nitaipatia uzao wako* kisha wewe.”+ 13 Kisha Mungu akapanda juu na kumuacha mahali kwenye alikuwa amezungumuza naye.

14 Kwa hiyo Yakobo akasimamisha nguzo mahali pale kwenye Mungu alikuwa amezungumuza naye, nguzo ya majiwe, na akamwanga toleo la kinywaji juu yake.+ 15 Na Yakobo akaendelea kupaita Beteli mahali pale kwenye Mungu alikuwa amezungumuza naye.+

16 Kisha wakaondoka Beteli. Na wakati walikuwa wangali mbali kidogo na Efrati, Raheli akaanza kuzaa, na alizaa kwa magumu sana. 17 Lakini wakati alikuwa anazaa kwa shida, mwanamuke wa kuzalisha akamuambia: “Usiogope, kwa maana utazaa mwana huyu pia.”+ 18 Basi kwa kuwa uzima wake ulikuwa unatoka* (kwa maana alikuwa anakufa) akamupatia jina Ben-oni,* lakini baba yake akamupatia jina Benyamini.*+ 19 Kwa hiyo Raheli akakufa na kuzikwa katika njia ya kuenda Efrati, ni kusema, Betlehemu.+ 20 Yakobo akasimamisha nguzo juu ya kaburi la Raheli; hiyo ndiyo nguzo ya kaburi la Raheli mupaka leo.

21 Kisha mambo hayo Israeli akaendelea na safari na akasimamisha hema yake mbali kidogo kisha kupita munara wa Ederi. 22 Siku moja, wakati Israeli alikuwa anakaa katika inchi hiyo, Rubeni akaenda na akalala na Bilha suria* wa baba yake, na Israeli akasikia habari hiyo.+

Basi Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili (12). 23 Wana wa Lea walikuwa Rubeni,+ muzaliwa wa kwanza wa Yakobo, kisha Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, na Zabuloni. 24 Wana wa Raheli walikuwa Yosefu na Benyamini. 25 Na wana wa Bilha, mutumishi wa Raheli, walikuwa Dani na Naftali. 26 Na wana wa Zilpa, mutumishi wa Lea, walikuwa Gadi na Asheri. Hawa ndio wana wa Yakobo wenye alizaa kule Padan-aramu.

27 Mwishowe Yakobo akafika mahali Isaka baba yake alikuwa anaishi kule Mamre,+ kule Kiriath-arba, ni kusema, Hebroni, kwenye Abrahamu na pia Isaka walikuwa wameishi kama wageni.+ 28 Isaka aliishi miaka mia moja makumi munane (180).+ 29 Kisha Isaka akavuta pumuzi yake ya mwisho na akakufa na kukusanywa kwa watu wake,* kisha kuishi maisha ya murefu na yenye kuwa muzuri;* na wana wake Esau na Yakobo wakamuzika.+

36 Hii ndiyo historia ya Esau, ni kusema, Edomu.+

2 Esau alichukua bibi zake kati ya mabinti wa Kanaani: Ada+ binti ya Eloni Muhiti;+ na Oholibama+ binti ya Ana, mujukuu wa Sibeoni Muhivi; 3 na Basemati,+ binti ya Ishmaeli, dada ya Nebayoti.+

4 Ada akamuzalia Esau, Elifazi, naye Basemati akamuzaa Reueli,

5 na Oholibama akamuzaa Yeushi, Yalamu, na Kora.+

Hao ndio wana wa Esau, wenye alizaa katika inchi ya Kanaani. 6 Kisha mambo hayo Esau akachukua bibi zake, watoto wake wanaume, watoto wake wanamuke, na watu wote wa* nyumba yake, mifugo yake na wanyama wake wengine wote, na mali yote yenye alikuwa amekusanya+ katika inchi ya Kanaani na akahamia katika inchi ingine mbali kidogo na Yakobo ndugu yake.+ 7 Kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana na haikuwezekana waishi pamoja, na inchi yenye walikuwa wanaishi ndani yake* haikukuwa na nafasi kwa ajili ya wao wote kwa sababu ya mifugo yao. 8 Kwa hiyo Esau akaanza kuishi katika eneo lenye milima la Seiri.+ Esau ni Edomu.+

9 Na hii ndiyo historia ya Esau baba ya Edomu katika eneo lenye milima la Seiri.+

10 Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, bibi ya Esau; Reueli mwana wa Basemati, bibi ya Esau.+

11 Wana wa Elifazi walikuwa Temani,+ Omari, Sefo, Gatamu, na Kenasi.+ 12 Timna akakuwa suria* wa Elifazi, mwana wa Esau. Kisha wakati fulani akamuzalia Elifazi, Amaleki.+ Hao ndio wana wa Ada, bibi ya Esau.

13 Hawa ndio wana wa Reueli: Nahati, Zera, Shamma, na Miza. Hao ndio walikuwa wana wa Basemati,+ bibi ya Esau.

14 Hawa ndio walikuwa wana wa Oholibama binti ya Ana, mujukuu wa Sibeoni, bibi ya Esau: Yeushi, Yalamu, na Kora.

15 Hawa ndio mashehe* wa wana wa Esau:+ Wana wa Elifazi, muzaliwa wa kwanza wa Esau: Shehe Temani, Shehe Omari, Shehe Sefo, Shehe Kenasi,+ 16 Shehe Kora, Shehe Gatamu, na Shehe Amaleki. Hao ndio mashehe wa Elifazi+ katika inchi ya Edomu. Hao ndio wana wa Ada.

17 Hawa ndio wana wa Reueli, mwana wa Esau: Shehe Nahati, Shehe Zera, Shehe Shama, na Shehe Miza. Hao ndio mashehe wa Reueli katika inchi ya Edomu.+ Hao ndio wana wa Basemati, bibi ya Esau.

18 Mwishowe hawa ndio wana wa Oholibama, bibi ya Esau: Shehe Yeushi, Shehe Yalamu, na Shehe Kora. Hao ndio mashehe wa Oholibama binti ya Ana, bibi ya Esau.

19 Hao ndio wana wa Esau, na hao ndio mashehe wao. Esau ni Edomu.+

20 Hawa ndio wana wa Seiri, Muhori, wakaaji wa inchi hiyo:+ Lotani, Shobali, Sibeoni, na Ana,+ 21 Dishoni, Ezeri, na Dishani.+ Hao ndio mashehe wa ule Muhori, wana wa Seiri, katika inchi ya Edomu.

22 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemamu, na dada ya Lotani alikuwa Timna.+

23 Hawa ndio wana wa Shobali: Alvani, Manahati, Ebali, Shefo, na Onamu.

24 Hawa ndio wana wa Sibeoni:+ Aya na Ana. Huyu ndiye Ana mwenye alipata chemchemi za maji ya moto katika jangwa wakati alikuwa anachunga punda wa Sibeoni baba yake.

25 Hawa ndio watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama binti ya Ana.

26 Hawa ndio wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Itrani, na Kerani.+

27 Hawa ndio wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.

28 Hawa ndio wana wa Dishani: Usi na Arani.+

29 Hawa ndio mashehe wa Wahori: Shehe Lotani, Shehe Shobali, Shehe Sibeoni, Shehe Ana, 30 Shehe Dishoni, Shehe Ezeri, na Shehe Dishani.+ Hao ndio mashehe wa Wahori kulingana na mashehe wao katika inchi ya Seiri.

31 Sasa hawa ndio wafalme wenye walitawala katika inchi ya Edomu+ mbele ya mufalme yeyote kutawala juu ya Waisraeli.*+ 32 Bela mwana wa Beori alitawala Edomu, na jina la muji wake lilikuwa Dinhaba. 33 Wakati Bela alikufa, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akaanza kutawala pa nafasi yake. 34 Wakati Yobabu alikufa, Hushamu kutoka katika inchi ya Watemani akaanza kutawala pa nafasi yake. 35 Wakati Hushamu alikufa, Hadadi mwana wa Bedadi, mwenye alishinda Wamidiani+ katika eneo* la Moabu akaanza kutawala pa nafasi yake, na jina la muji wake lilikuwa Aviti. 36 Wakati Hadadi alikufa, Samla kutoka Masreka akaanza kutawala pa nafasi yake. 37 Wakati Samla alikufa, Shauli kutoka Rehoboti pembeni ya ule Muto akaanza kutawala pa nafasi yake. 38 Wakati Shauli alikufa, Baal-hanani mwana wa Akbori akaanza kutawala pa nafasi yake. 39 Wakati Baal-hanani mwana wa Akbori alikufa, Hadari akaanza kutawala pa nafasi yake. Jina la muji wake lilikuwa Pau, na jina la bibi yake lilikuwa Mehetabeli binti ya Matredi binti ya Mezahabu.

40 Basi haya ndiyo majina ya mashehe wa Esau kulingana na familia zao, kulingana na maeneo yao: Shehe Timna, Shehe Alva, Shehe Yeteti,+ 41 Shehe Oholibama, Shehe Ela, Shehe Pinoni, 42 Shehe Kenasi, Shehe Temani, Shehe Mibsari, 43 Shehe Magdieli, na Shehe Iramu. Hao ndio mashehe wa Edomu kulingana na makao yao katika inchi yenye waliriti.+ Huyu ndiye Esau baba ya Edomu.+

37 Yakobo akaendelea kukaa katika inchi ya Kanaani, mahali baba yake alikuwa ameishi kama mugeni.+

2 Hii ndiyo historia ya Yakobo.

Wakati Yosefu+ alikuwa na miaka kumi na saba (17), alikuwa anachunga kundi+ pamoja na wana wa Bilha+ na wana wa Zilpa,+ bibi za baba yake. Na Yosefu akamuletea baba yao habari ya mubaya juu yao. 3 Sasa Israeli alimupenda Yosefu kuliko wana wake wengine wote+ kwa sababu alikuwa mwana wa uzee wake, na alimushoneshea kanzu ya pekee.* 4 Wakati ndugu zake waliona kwamba baba yao alimupenda zaidi kuliko ndugu zake wote, wakaanza kumuchukia na hawakukuwa wanazungumuza naye kwa amani.

5 Kisha wakati fulani Yosefu aliota ndoto na akaielezea ndugu zake,+ na wakapata sababu ingine ya kumuchukia. 6 Aliwaambia: “Tafazali musikilize ndoto yenye niliota. 7 Tulikuwa tunafunga mafungu ya nafaka katikati ya shamba, halafu fungu langu la nafaka likainuka na kusimama wima, na mafungu yenu ya nafaka yakazunguka na kuinamia fungu langu la nafaka.”+ 8 Ndugu zake wakamuambia: “Je, kweli utajifanya kuwa mufalme juu yetu na kututawala?”+ Kwa hiyo wakapata sababu ingine ya kumuchukia, kwa sababu ya ndoto zake na mambo yenye alisema.

9 Kisha mambo hayo akaota tena ndoto ingine, na akaielezea ndugu zake: “Nimeota ndoto ingine. Mara hii jua na mwezi na nyota kumi na moja (11) zilikuwa zinaniinamia.”+ 10 Kisha akamuelezea baba yake ndoto hiyo na pia ndugu zake, na baba yake akamukemea na kumuambia: “Hii ndoto yako iko na maana gani? Je, kweli mimi na mama yako pamoja na ndugu zako tutakuja na kuinama mupaka chini mbele yako?” 11 Na ndugu zake wakaanza kumusikilia wivu,+ lakini baba yake akaendelea kuweka maneno hayo katika akili yake.

12 Sasa ndugu zake wakaenda kukulisha kundi la baba yao karibu na Shekemu.+ 13 Kisha wakati fulani Israeli akamuambia Yosefu: “Je, ndugu zako hawako wanachunga makundi karibu na Shekemu? Kuja, na nikutume mahali wako.” Basi Yosefu akamuambia: “Niko tayari!” 14 Kwa hiyo akamuambia: “Tafazali, uende uone kama ndugu zako wako salama. Uone kama kundi liko katika hali gani, na uniletee habari.” Basi akamutuma kutoka bonde* la Hebroni,+ naye akaelekea upande wa Shekemu. 15 Kisha wakati fulani mwanaume fulani alikutana naye wakati alikuwa anazunguka-zunguka katika shamba. Mwanaume huyo akamuuliza: “Uko unatafuta nini?” 16 Akasema: “Niko natafuta ndugu zangu. Tafazali uniambie wako wanachunga makundi wapi?” 17 Ule mwanaume akaendelea kusema: “Wameondoka hapa, kwa maana niliwasikia wanasema, ‘Tuende Dotani.’” Kwa hiyo akawafuata ndugu zake na akawakuta Dotani.

18 Sasa wakamuona kwa mbali, na mbele afike karibu nao, wakaanza kufanya mupango wa kumuua. 19 Kwa hiyo wakaambiana: “Angalia! Ule mwota-ndoto anakuja!+ 20 Mukuje sasa, tumuue na tumutupe ndani ya moja ya mashimo ya maji, na tutasema kwamba munyama mukali wa pori alimupasua-pasua. Kisha tuone ndoto zake zitakuwa namna gani.” 21 Wakati Rubeni+ alisikia maneno hayo, akajaribu kumuokoa kutoka katika mikono yao. Kwa hiyo akasema: “Tusiondoe uzima wake.”*+ 22 Rubeni akawaambia: “Musimwange damu.+ Mumutupe ndani ya shimo hili la maji lenye kuwa katika jangwa, lakini musimuumize.”*+ Alitaka kumuokoa kutoka katika mikono yao ili amurudishe kwa baba yake.

23 Kwa hiyo wakati tu Yosefu alifika mahali ndugu zake walikuwa, wakamuvua ile kanzu, ile kanzu ya pekee yenye alikuwa anavaa,+ 24 na wakamukamata na kumutupa ndani ya lile shimo la maji. Wakati huo lile shimo lilikuwa bila kitu ndani; halikukuwa na maji.

25 Kisha wakakaa ili wakule chakula. Wakati waliinua macho, kulikuwa musururu wa Waishmaeli+ wenye ulikuwa unatoka Gileadi. Ngamia wao walibeba ubani mweusi, zeri, na ngozi ya muti yenye utomvu,+ na walikuwa wanaenda Misri. 26 Basi Yuda akaambia ndugu zake: “Tutapata faida gani ikiwa tunamuua ndugu yetu na kufunika damu yake?+ 27 Mukuje sasa, tumuuzishe+ kwa Waishmaeli, na tusiweke mukono wetu juu yake. Kwa vyovyote, yeye ni ndugu yetu na nyama yetu.” Kwa hiyo wakamusikiliza ndugu yao. 28 Na wakati wale wafanyabiashara Wamidiani+ walikuwa wanapita, wakamutosha Yosefu katika shimo la maji na wakamuuzisha kwa wale Waishmaeli kwa vipande makumi mbili (20) vya feza.+ Wale wanaume wakamupeleka Yosefu Misri.

29 Kisha wakati fulani wakati Rubeni alirudia kwenye lile shimo la maji na kuona kwamba Yosefu hakukuwa ndani ya lile shimo la maji, akapasua nguo zake. 30 Wakati alirudia mahali ndugu zake walikuwa, mara moja akasema: “Mutoto haiko! Na mimi⁠—​nitafanya nini?”

31 Kwa hiyo wakakamata kanzu ya Yosefu na wakachinja mbuzi-dume na wakatumbukiza-tumbukiza ile kanzu katika damu hiyo. 32 Kisha mambo hayo wakamutumia baba yao ile kanzu ya pekee na kusema: “Hii ndiyo tumepata. Tafazali chunguza hii uone kama ni ya mwana wako ao hapana.”+ 33 Kisha akaichunguza na mara moja akasema: “Ni kanzu ya mwana wangu! Munyama mukali wa pori anapaswa kuwa amemupasua-pasua! Hakika Yosefu amepasuliwa vipande-vipande!” 34 Basi Yakobo akapasua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia kuzunguka kiuno chake na akamuombolezea mwana wake kwa siku nyingi. 35 Na watoto wake wote wanaume na watoto wake wote wanamuke wakajaribu sana kumufariji, lakini aliendelea kukataa kufarijiwa, akisema: “Nitashuka ndani ya Kaburi*+ nikiombolezea mwana wangu!” Na baba yake akaendelea kumulilia.

36 Basi Wamidiani wakamuuzisha Yosefu Misri kwa Potifa, ofisa wa makao ya Farao+ na mukubwa wa walinzi.+

38 Wakati huo, Yuda akaacha ndugu zake na kuenda kusimamisha hema yake karibu na mwanaume mumoja Mwadulamu mwenye aliitwa Hira. 2 Yuda akaona kule binti mumoja Mukanaani+ mwenye aliitwa Shua. Kwa hiyo akamukamata na kulala naye, 3 na akakuwa na mimba. Kisha wakati fulani akamuzaa mwana, na Yuda akamupatia jina Eri.+ 4 Akakuwa tena na mimba na akazaa mwana na akamupatia jina Onani. 5 Kisha akazaa tena mwana na akamupatia jina Shela. Huyo* alikuwa katika muji wa Akzibu+ wakati Shua alizaa Shela.

6 Kisha wakati fulani, Yuda akamuchukulia Eri muzaliwa wake wa kwanza bibi, na jina lake lilikuwa Tamari.+ 7 Lakini Eri, muzaliwa wa kwanza wa Yuda, alimuchukiza Yehova; kwa hiyo Yehova akamuua. 8 Basi Yuda akamuambia Onani: “Lala na bibi ya ndugu yako na ufanye ndoa ya mutu na shemeki yake pamoja na Tamari na utokeze uzao kwa ajili ya ndugu yako.”+ 9 Lakini Onani alijua kwamba uzao huo haungeonwa kuwa wake.+ Kwa hiyo wakati alilala na bibi ya ndugu yake, alimwanga mbegu zake za uzazi* chini ili asimuinulie ndugu yake uzao.+ 10 Jambo lenye alifanya lilikuwa mubaya mbele ya macho ya Yehova, kwa hiyo akamuua pia.+ 11 Yuda akamuambia Tamari binti-mukwe wake: “Kaa ukiwa mujane katika nyumba ya baba yako mupaka Shela mwana wangu akomae,” kwa maana Yuda alisema katika moyo wake: ‘Yeye pia anaweza kufa kama vile ndugu zake.’+ Kwa hiyo Tamari akaenda na kuishi katika nyumba ya baba yake.

12 Wakati fulani ukapita, na bibi ya Yuda, binti ya Shua,+ akakufa. Yuda akamaliza kipindi cha kuomboleza, na kisha akaenda Timna+ mahali watu wake wa kukata manyoya ya kondoo walikuwa, alienda kule pamoja na Hira rafiki yake Mwadulamu.+ 13 Tamari akaambiwa: “Baba-mukwe wako anapanda kuenda Timna ili kukata manyoya ya kondoo wake.” 14 Basi akatosha nguo zake za ujane na akajifunika uso na pia akajifunika kwa kitambaa kikubwa na akakaa kwenye muingilio wa Enaimu, muji wenye kuwa kwenye barabara ya kuenda Timna, kwa maana aliona kwamba Shela alikuwa amekomaa na bado hakukuwa amepewa kwa Shela ili akuwe bibi yake.+

15 Wakati Yuda alimuona, mara moja akafikiri ni kahaba, kwa sababu alikuwa amejifunika uso. 16 Kwa hiyo akapita karibu naye pembeni ya barabara na kumuambia: “Tafazali, uniruhusu, nilale na wewe,” kwa maana hakujua kwamba alikuwa binti-mukwe wake.+ Lakini, Tamari akasema: “Utanipatia nini ili ulale na mimi?” 17 Akasema: “Nitatuma mwana-mbuzi kutoka katika mifugo yangu.” Lakini Tamari akasema: “Utawekesha kitu gani mupaka wakati utatuma mwana-mbuzi huyo?” 18 Yuda akaendelea kusema: “Unapenda nikuwekeshe kitu gani?” akasema: “Pete yako ya kutia muhuri,+ kamba yako na fimbo yenye kuwa katika mukono wako.” Kisha akamupatia vile vitu na akalala naye, na Tamari akakuwa na mimba ya Yuda. 19 Kisha mambo hayo Tamari akasimama na akaenda na kutosha kitambaa chake kikubwa na kuvaa nguo zake za ujane.

20 Na Yuda akatuma mwana-mbuzi kupitia rafiki yake Mwadulamu,+ ili kukamata vitu vyenye aliwekesha katika mukono wa ule mwanamuke, lakini hakumupata. 21 Akauliza watu wa muji huo, kwa kusema: “Iko* wapi ule kahaba wa hekalu katika Enaimu pembeni ya barabara?” Lakini wakasema: “Hakujakuwaka kahaba wa hekalu mahali hapa.” 22 Mwishowe akarudia kwa Yuda na kusema: “Sikumupata, na watu wa mahali pale walisema, ‘Hakujakuwaka kahaba wa hekalu mahali hapa.’” 23 Kwa hiyo Yuda akasema: “Muache avikamate vikuwe vyake, ili watu wasituzarau. Kwa vyovyote, nimetuma huyu mwana-mbuzi, lakini haukumupata.”

24 Lakini, kisha miezi tatu (3) hivi, Yuda aliambiwa: “Tamari binti-mukwe wako amefanya ukahaba, na pia amepata mimba katika ukahaba wake.” Basi Yuda akasema: “Mumutie inje na ateketezwe kwa moto.”+ 25 Wakati walikuwa wanamupeleka inje, akatuma ujumbe huu kwa baba-mukwe wake: “Mwanaume mwenye vitu hivi ndiye alinipatia mimba.” Kisha Tamari akaongeza kusema: “Tafazali chunguza uone ni nani mwenye pete hii ya kutia muhuri na kamba hii na fimbo hii.”+ 26 Kisha Yuda akachunguza vitu hivyo na kusema: “Yeye ni mwenye haki zaidi kuliko mimi, kwa sababu sikumupatia Shela mwana wangu akuwe bwana yake.”+ Na kisha mambo hayo, Yuda hakufanya ngono naye tena.

27 Wakati muda wake wa kuzaa ulifika, kulikuwa mapacha katika tumbo lake la uzazi. 28 Wakati alikuwa anazaa, mutoto mumoja alitia mukono wake inje, na mara moja mwanamuke wa kuzalisha akakamata uzi ya rangi nyekundu yenye kungaa na kuifunga kuzunguka mukono wa mutoto huyo, akisema: “Ni huyu alitoka wa kwanza.” 29 Lakini wakati tu alirudisha mukono wake nyuma, ndugu yake akatoka, na mara moja mwanamuke wa kuzalisha akasema: “Mbona umejipasulia njia kwa nguvu!” Kwa hiyo akapewa jina Perezi.*+ 30 Kisha ndugu yake akatoka, uzi ya rangi nyekundu yenye kungaa ilikuwa inafungwa kuzunguka mukono wake, na akapewa jina Zera.+

39 Sasa Yosefu akapelekwa Misri.+ Na Mumisri mumoja mwenye aliitwa Potifa,+ ofisa wa makao ya Farao na mwenye alikuwa mukubwa wa walinzi, akamununua kutoka kwa Waishmaeli+ wenye walikuwa wamemuleta kule. 2 Lakini Yehova alikuwa pamoja na Yosefu.+ Kwa hiyo mambo yakamuendea muzuri na akawekwa juu ya nyumba ya bwana wake, ule Mumisri. 3 Na bwana wake akaona kama Yehova alikuwa pamoja naye na kama Yehova alikuwa anafanya kila jambo lenye Yosefu alifanya liendeke muzuri.

4 Yosefu akaendelea kukubaliwa mbele ya macho ya bwana wake, na akakuwa mutumishi wake mwenyewe. Kwa hiyo Potifa akamuweka juu ya nyumba yake, na akamuweka asimamie vitu vyake vyote. 5 Tangu wakati Potifa alimuweka kuwa musimamizi wa nyumba yake na wa vitu vyake vyote, Yehova aliendelea kubariki nyumba ya ule Mumisri kwa sababu ya Yosefu, na Yehova akabariki vitu vyote vyenye Potifa alikuwa navyo katika nyumba na katika eneo la mashamba.+ 6 Mwishowe akaacha kila kitu chenye kilikuwa chake katika mikono ya Yosefu, na Potifa hakukuwa anahangaikia kitu kingine isipokuwa chakula chenye alikuwa anakula. Tena, Yosefu akakuwa mwanaume mwenye umbo ya muzuri na sura ya kupendeza.

7 Kisha mambo hayo, bibi ya bwana wake akaanza kumuangalia na kumutamani sana Yosefu na kusema: “Lala na mimi.” 8 Lakini akakataa na kumuambia bibi ya bwana wake: “Angalia, bwana wangu haangaikie kile ninafanya katika nyumba hii, na ameweka vitu vyake vyote katika mikono yangu. 9 Hakuna mwenye kuwa mukubwa zaidi kuliko mimi katika nyumba hii, na bwana wangu hakunikataza kitu chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe uko bibi yake. Kwa hiyo ninaweza namna gani kufanya ubaya huu mukubwa na kwa kweli nimutendee Mungu zambi?”+

10 Kwa hiyo kila siku alikuwa anasema na Yosefu, lakini Yosefu hakukubali hata kidogo kulala naye wala kubakia pamoja naye. 11 Lakini siku moja wakati Yosefu aliingia katika nyumba ili kufanya kazi yake, wafanyakazi wote wa nyumba hawakukuwa katika nyumba. 12 Kisha akakamata kwa nguvu nguo ya Yosefu na kusema: “Lala na mimi!” Lakini Yosefu akaacha nguo yake katika mukono wake na kukimbia inje. 13 Wakati tu aliona kwamba Yosefu amemuachia nguo yake na kukimbia inje, 14 akaanza kuita wanaume wa nyumba yake na kuwaambia: “Muangalie! Alituletea mwanaume huyu Mwebrania ili kutufanya tukuwe kitu cha kuchekwa. Alikuja ili kulala na mimi, lakini nilianza kulalamika kwa sauti yangu yote. 15 Kisha wakati tu alisikia ninasema kwa sauti kubwa na kulalamika, akaacha nguo yake pembeni yangu na kukimbia inje.” 16 Kisha mambo hayo akaweka nguo ya Yosefu pembeni yake mupaka wakati bwana wake alirudia katika nyumba yake.

17 Kisha akamuambia Potifa jambo lilelile, kwa kusema: “Ule mutumishi Mwebrania mwenye ulituletea alikuja karibu na mimi ili kunifanya kuwa kitu cha kuchekwa. 18 Lakini wakati tu nilipandisha sauti na kuanza kulalamika, aliacha nguo yake pembeni yangu na kukimbia inje.” 19 Wakati tu bwana wa Yosefu alisikia maneno yenye bibi yake alimuambia, kwa kusema: “Hayo ndiyo mambo yenye mutumishi wako alinitendea,” kasirani yake ikawaka. 20 Kwa hiyo bwana wa Yosefu akamukamata na kumutia katika gereza, mahali wafungwa wa mufalme walikuwa wamefungwa, na Yosefu akabakia kule katika gereza.+

21 Lakini Yehova aliendelea kuwa pamoja na Yosefu na akaendelea kumuonyesha upendo mushikamanifu na kumufanya akubaliwe mbele ya macho ya ofisa mukubwa wa gereza.+ 22 Kwa hiyo ofisa mukubwa wa gereza akamuweka Yosefu kuwa musimamizi wa wafungwa wote katika gereza, na kila kitu chenye wafungwa walikuwa wanafanya ndani ya gereza, ni yeye alikuwa anaagiza kifanywe.+ 23 Ule ofisa mukubwa wa gereza hakukuwa anaangalia kitu chochote chenye kilikuwa katika mikono ya Yosefu, kwa sababu Yehova alikuwa pamoja na Yosefu na Yehova alifanya kila jambo lenye Yosefu alifanya liendeke muzuri.+

40 Kisha mambo hayo, mukubwa wa wanyweshaji+ wa mufalme wa Misri na mukubwa wa watengenezaji wa mikate walimutendea zambi bwana wao, mufalme wa Misri. 2 Kwa hiyo Farao akakasirikia wale maofisa wawili, mukubwa wa wanyweshaji na mukubwa wa watengenezaji wa mikate,+ 3 na akawatia katika gereza la nyumba ya mukubwa wa walinzi,+ kwenye Yosefu alikuwa amefungwa.+ 4 Kisha mukubwa wa walinzi akamupatia Yosefu mugao wa kuwa pamoja nao na kuwahangaikia,+ na wakabakia katika gereza kwa wakati* fulani.

5 Munyweshaji na mutengenezaji wa mikate wa mufalme wa Misri, wenye walikuwa wanafungwa katika gereza, kila mumoja aliota ndoto usiku uleule, na kila ndoto ilikuwa na mafasirio yake. 6 Asubui ya kufuata, wakati Yosefu aliingia na kuwaona, walionekana kuwa wenye huzuni. 7 Kwa hiyo akauliza wale wafanyakazi maofisa wa Farao wenye walikuwa wamefungwa pamoja naye katika nyumba ya bwana wake: “Sababu gani nyuso zenu ziko na huzuni leo?” 8 Basi wakamuambia: “Kila mumoja wetu aliota ndoto, lakini hakuna mutu wa kutufasiria maana yake.” Yosefu akawaambia: “Je, mafasirio hayatoke kwa Mungu?+ Tafazali, munielezee ndoto zenu.”

9 Kwa hiyo mukubwa wa wanyweshaji akamuelezea Yosefu ndoto yake, akamuambia: “Katika ndoto yangu, kulikuwa muzabibu mbele yangu. 10 Na kwenye ule muzabibu, kulikuwa matawi tatu (3), na wakati ulikuwa unatoa machipukizi, ulitoa maua, na mafungu-mafungu yake yakatoa zabibu zenye kuivya. 11 Na kikombe cha Farao kilikuwa katika mukono wangu, na nikakamata zabibu na kuzikamulia ndani ya kikombe cha Farao. Kisha pale nikatia kile kikombe katika mukono wa Farao.” 12 Kisha Yosefu akamuambia: “Haya ndiyo mafasirio yake: yale matawi tatu (3) ni siku tatu. 13 Kisha siku tatu (3), Farao atakutosha katika gereza,* atakurudisha katika kazi yako,+ na utaweka kikombe cha Farao katika mukono wake kama vile ulikuwa unafanya zamani wakati ulikuwa munyweshaji wake.+ 14 Lakini, unapaswa kunikumbuka wakati mambo yatakuendea muzuri. Tafazali unionyeshe upendo mushikamanifu na unitaje mbele ya Farao, ili nitoke hapa. 15 Kwa kweli, nilikamatwa katika inchi ya Waebrania,+ na sijafanya hapa jambo lolote lenye linaweza kuacha wanitie katika gereza.”*+

16 Wakati mukubwa wa watengenezaji wa mikate aliona kwamba Yosefu alikuwa amefasiria jambo fulani la muzuri, akamuambia: “Mimi pia nilikuwa katika ndoto yangu, na kulikuwa vitunga tatu (3) vya mikate ya mweupe juu ya kichwa changu, 17 na ndani ya kitunga cha juu, kulikuwa vitu vya muzuri vya kila namna vyenye vilipikwa kwa ajili ya Farao, na kulikuwa ndege wenye walikuwa wanakula vitu hivyo katika kitunga juu ya kichwa changu. 18 Kisha Yosefu akajibu, “Haya ndiyo mafasirio yake: Vile vitunga tatu (3) ni siku tatu. 19 Kisha siku tatu (3), Farao atakukata kichwa na kukutundika kwenye muti, na ndege watakula mwili wako.”+

20 Sasa siku ya tatu (3) ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Farao,+ na alifanya karamu kwa ajili ya watumishi wake wote, na akatosha katika gereza* mukubwa wa wanyweshaji na mukubwa wa watengenezaji wa mikate mbele ya watumishi wake. 21 Na akamurudisha mukubwa wa wanyweshaji katika kazi yake ya munyweshaji, na akaendelea kumupatia Farao kikombe. 22 Lakini akamutundika mukubwa wa watengenezaji wa mikate, kama vile Yosefu alikuwa amewafasiria.+ 23 Hata hivyo, ule mukubwa wa wanyweshaji hakumukumbuka Yosefu; aliendelea kumusahau.+

41 Kisha miaka mbili, Farao akaota ndoto+ kwamba alikuwa anasimama pembeni ya Muto Nile. 2 Na pale, ngombe saba (7) wazuri na wenye kunenepa walikuwa wanatoka katika muto, na walikuwa wanakula majani ya Muto Nile.+ 3 Kulikuwa ngombe wengine saba (7) wenye sura ya mubaya na wenye kukonda wenye walikuwa wanatoka katika Muto Nile, na walisimama pembeni ya wale ngombe wenye kunenepa pembeni ya Muto Nile. 4 Kisha wale ngombe wenye sura ya mubaya, na wenye kukonda wakaanza kula wale ngombe saba (7) wenye sura ya muzuri, wenye kunenepa. Basi Farao akaamuka.

5 Kisha akalala tena na akaota ndoto ingine. Kulikuwa masuke saba (7) ya nafaka yenye yalikuwa juu ya tawi moja, yenye kujaa na ya muzuri.+ 6 Na kisha masuke hayo kulikuwa masuke mengine saba (7) ya nafaka yenye yalikuwa yanaota na yalikuwa membamba na yenye kukaushwa na upepo wa mashariki. 7 Na masuke hayo membamba ya nafaka yakaanza kumeza yale masuke saba (7) ya nafaka yenye kujaa na ya muzuri. Basi Farao akaamuka na akatambua kwamba ilikuwa ndoto.

8 Lakini asubui, roho ya Farao ikavurugika sana. Kwa hiyo akaita makuhani wote wenye kufanya uchawi wa Misri na watu wake wote wenye hekima. Farao akawaelezea ndoto zake, lakini hakuna mwenye aliweza kumufasiria Farao maana ya ndoto zake.

9 Basi mukubwa wa wanyweshaji akamuambia Farao, na kusema: “Ninaungama zambi zangu leo. 10 Farao alikasirikia watumishi wake. Kwa hiyo alinitia katika gereza ya nyumba ya mukubwa wa walinzi, mimi na mukubwa wa watengenezaji wa mikate.+ 11 Kisha mambo hayo sisi wote wawili tukaota ndoto usiku mumoja. Kila mumoja wetu aliota ndoto yake na kila ndoto ilikuwa na mafasirio yake.+ 12 Na tulikuwa katika gereza pamoja na kijana mumoja Mwebrania, mutumishi wa mukubwa wa walinzi.+ Wakati tulimuelezea ndoto zetu,+ alitufasiria maana ya kila ndoto. 13 Mambo yote yalifanyika kama vile alikuwa ametufasiria. Mimi nilirudishwa kwenye kazi yangu, lakini ule mwanaume mwingine alitundikwa.”+

14 Kwa hiyo Farao akatuma watu wamulete Yosefu;+ na wakamutosha haraka katika gereza.*+ Akajinyoa na kubadilisha nguo zake na akaingia mbele ya Farao. 15 Kisha Farao akamuambia Yosefu: “Niliota ndoto, lakini hakuna mutu wa kuifasiria. Sasa nimesikia wanasema juu yako kwamba unaweza kusikia ndoto na kuifasiria.”+ 16 Basi Yosefu akamujibu Farao: “Haiko mimi! Mungu ndiye atasema kuhusu hali ya muzuri ya Farao.”+

17 Farao akaendelea kusema na Yosefu: “Katika ndoto yangu nilikuwa ninasimama pembeni ya Muto Nile. 18 Na pale, ngombe saba (7) wenye sura ya muzuri, wenye kunenepa, walikuwa wanatoka katika Muto Nile, na walianza kula majani ya Muto Nile.+ 19 Na kisha hao kulitokea ngombe wengine saba (7), wazaifu na wenye sura ya mubaya na wenye kukonda. Hakuna siku nimeona ngombe wenye sura ya mubaya hivyo katika inchi yote ya Misri. 20 Na ngombe hao wenye kukonda, wabaya wakaanza kula wale ngombe saba (7) wa kwanza wenye kunenepa. 21 Lakini wakati walimaliza kuwakula, hakuna mwenye angeweza kutambua kwamba walikuwa wamewakula, kwa sababu sura yao ilikuwa mubaya kama vile pale mwanzo. Kisha nikaamuka.

22 “Kisha niliona katika ndoto yangu masuke saba (7) ya nafaka yakiota kwenye tawi moja, yalikuwa yenye kujaa na ya muzuri.+ 23 Kisha masuke hayo kuliota masuke mengine saba (7) ya nafaka ya kukauka, membamba, na yenye kukaushwa na upepo wa mashariki. 24 Kisha yale masuke membamba ya nafaka yakaanza kumeza yale masuke saba (7) ya muzuri ya nafaka. Kwa hiyo nikaelezea makuhani wenye kufanya uchawi ndoto hiyo,+ lakini hakuna mwenye aliweza kunifasiria maana yake.”+

25 Kisha Yosefu akamuambia Farao: “Ndoto za Farao ni moja na ni ileile. Mungu wa kweli amemuambia Farao mambo yenye atafanya.+ 26 Wale ngombe saba (7) wazuri ni miaka saba. Pia, yale masuke saba ya muzuri ya nafaka ni miaka saba. Ndoto zako ni moja na ni ileile. 27 Wale ngombe saba (7) wenye kukonda na wabaya wenye walipanda kisha wale ngombe wazuri ni miaka saba, na yale masuke saba ya nafaka yenye hayana kitu, yenye yalikaushwa na upepo wa mashariki, itakuwa miaka saba ya njaa. 28 Ni vile nilimuambia Farao: Mungu wa kweli amemufanya Farao aone mambo yenye Atafanya.

29 “Kutakuwa miaka saba (7) ya chakula kingi katika inchi yote ya Misri. 30 Lakini kisha miaka hiyo, kutatokea miaka saba (7) ya njaa, na chakula kingi chote chenye kilikuwa katika inchi ya Misri hakika kitasahauliwa, na njaa itaharibu inchi.+ 31 Na chakula kingi chenye kilikuwa katika inchi hakitakumbukwa tena kwa sababu ya njaa yenye itatokea kisha, kwa maana itakuwa kali sana. 32 Ndoto hiyo ilitolewa mara mbili kwa Farao kwa sababu jambo hilo limefanywa imara kabisa na Mungu wa kweli, na Mungu wa kweli atalitimiza hivi karibuni.

33 “Kwa hiyo basi Farao atafute mwanaume mwenye akili na hekima na amuweke juu ya inchi ya Misri. 34 Farao akamate hatua na aweke waangalizi katika inchi, na akusanye sehemu moja ya tano (1/5) ya mazao ya Misri wakati wa ile miaka saba (7) ya chakula kingi.+ 35 Na waangalizi hao wakusanye chakula chote wakati wa ile miaka ya muzuri yenye inakuja, na warundike nafaka chini ya usimamizi wa Farao, yenye itakuwa chakula chenye kitawekwa katika miji na kulindwa kule.+ 36 Chakula hicho kitakuwa akiba ya inchi kwa ajili ya ile miaka saba (7) ya njaa yenye itatokea katika inchi ya Misri, ili inchi isiangamie kwa sababu ya ile njaa.”+

37 Wazo hilo likaonekana kuwa la muzuri kwa Farao na kwa watumishi wake wote. 38 Kwa hiyo Farao akawaambia watumishi wake: “Je, kunaweza kupatikana mutu mwingine kama huyu mwenye kuwa na roho ya Mungu ndani yake?” 39 Kisha Farao akamuambia Yosefu: “Kwa kuwa Mungu amekuwezesha kujua mambo yote hayo, hakuna mutu mwenye akili na hekima kama wewe. 40 Wewe mwenyewe utasimamia nyumba yangu, na watu wangu wote watakutii katika kila jambo.+ Ni katika cheo changu cha mufalme tu* ndiyo nitakuwa mukubwa zaidi kuliko wewe.” 41 Na Farao akaendelea kumuambia Yosefu: “Angalia, ninakuweka juu ya inchi yote ya Misri.”+ 42 Kisha Farao akatosha kwenye mukono wake pete yake ya kutia muhuri na kuiweka kwenye mukono wa Yosefu na akamuvalisha nguo za kitani kizuri na mukufu wa zahabu kwenye shingo yake. 43 Zaidi ya hayo, Farao akamupandisha katika gari la pili la heshima lenye alikuwa nalo, na watu walikuwa wanasema kwa sauti kubwa mbele yake, “Avrekh!”* Kwa hiyo Farao akamuweka juu ya inchi yote ya Misri.

44 Tena Farao akamuambia Yosefu: “Mimi ni Farao, lakini bila ruhusa yako, hakuna mutu mwenye ataweza kufanya jambo lolote* katika inchi yote ya Misri.”+ 45 Kisha Farao akamupatia Yosefu jina Zafenat-panea na akamupatia Asenati+ binti ya Potifera kuhani wa Oni* akuwe bibi yake. Na Yosefu akaanza kusimamia* inchi ya Misri.+ 46 Yosefu alikuwa na miaka makumi tatu (30)+ wakati alisimama mbele ya* Farao mufalme wa Misri.

Kisha Yosefu akatoka mbele ya Farao na akatembea katika inchi yote ya Misri. 47 Na katika ile miaka saba (7) ya chakula kingi, inchi iliendelea kuzaa chakula kwa wingi. 48 Na aliendelea kukusanya chakula chote cha ile miaka saba (7) katika inchi ya Misri, na alikuwa anarundika chakula hicho katika miji. Katika kila muji alikuwa anakusanya chakula katika maeneo ya mashamba yenye kuzunguka muji huo. 49 Yosefu akaendelea kurundika nafaka nyingi sana, kama muchanga wa bahari, mupaka, mwishowe, wakaacha kuipima kwa sababu haikuweza kupimwa.

50 Mbele ya ule mwaka wa njaa kufika, Asenati, binti ya Potifera kuhani wa Oni* alimuzalia Yosefu wana wawili.+ 51 Yosefu akamupatia muzaliwa wa kwanza jina Manase,*+ kwa sababu alisema, “Mungu amenifanya nisahau taabu yangu yote na nyumba yote ya baba yangu.” 52 Na alipatia ule wa pili jina Efraimu,*+ kwa sababu alisema, “Mungu amenifanya nizae katika inchi ya taabu yangu.”+

53 Kisha ile miaka saba (7) ya chakula kingi katika inchi ya Misri ikaisha,+ 54 na ile miaka saba (7) ya njaa ikaanza, kama vile Yosefu alikuwa amesema.+ Hiyo njaa ikaenea katika inchi zote, lakini katika inchi yote ya Misri kulikuwa mukate.*+ 55 Mwishowe, inchi yote ya Misri ikakuwa na njaa, na watu wakaanza kumulilia Farao awapatie mukate.+ Kisha Farao akaambia Wamisri wote: “Muende kwa Yosefu, na mufanye jambo lolote lenye atawaambia.”+ 56 Hiyo njaa ikaendelea katika uso wote wa dunia.+ Kisha Yosefu akaanza kufungua madepo yote ya nafaka yenye yalikuwa kati yao na kuuzisha nafaka hiyo kwa Wamisri,+ kwa sababu hiyo njaa ilipiga sana inchi ya Misri. 57 Zaidi ya hayo, watu wa dunia yote wakakuja Misri ili kununua chakula kwa Yosefu, kwa sababu hiyo njaa ilikuwa imepiga sana dunia yote.+

42 Wakati Yakobo alipata habari kama kuko nafaka katika Misri,+ akaambia wana wake: “Sababu gani munaendelea tu kuangaliana?” 2 Akaongeza kusema: “Nimesikia kama kuko nafaka katika Misri. Mushuke kule na mutununulie nafaka, ili tuendelee kuishi na tusikufe.”+ 3 Kwa hiyo ndugu kumi (10) za Yosefu+ wakashuka ili kununua nafaka kule Misri. 4 Lakini Yakobo hakumutuma Benyamini,+ ndugu ya Yosefu, pamoja na ndugu zake wengine, kwa sababu alisema: “Pengine jambo fulani lenye kuleta kifo linaweza kumufikia.”+

5 Kwa hiyo wana wa Israeli wakaenda pamoja na watu wengine wenye walikuwa wanaenda kununua, kwa sababu njaa ilikuwa imeenea katika inchi ya Kanaani.+ 6 Yosefu ndiye alikuwa mutu mwenye mamlaka juu ya inchi,+ na ni yeye alikuwa anauzisha nafaka kwa watu wote wa dunia.+ Kwa hiyo ndugu za Yosefu wakafika na kuinamisha nyuso zao mupaka chini mbele yake.+ 7 Wakati Yosefu aliona ndugu zake, akawatambua mara moja, lakini alijifanya wasimutambue.+ Kwa hiyo akazungumuza nao kwa ukali na kusema: “Mumetoka wapi?” wakasema: “Tumetoka katika inchi ya Kanaani ili kununua chakula.”+

8 Basi Yosefu akatambua ndugu zake, lakini wao hawakumutambua. 9 Mara moja Yosefu akakumbuka ndoto zenye alikuwa ameota juu yao,+ na akawaambia: “Ninyi muko wapelelezi! Mumekuja kuona maeneo yenye uzaifu ya* inchi!” 10 Kisha wakamuambia: “Hapana, bwana wangu, lakini watumishi wako wamekuja kununua chakula. 11 Sisi wote tuko wana wa mutu mumoja. Tuko watu wenye haki. Watumishi wako hawako wapelelezi.” 12 Lakini akawaambia: “Haiko vile! Mumekuja kuona maeneo yenye uzaifu ya inchi!” 13 Basi wakasema: “Watumishi wako ni ndugu kumi na mbili (12).+ Tuko wana wa mutu mumoja+ katika inchi ya Kanaani, na ndugu yetu mudogo zaidi amebakia pamoja na baba yetu,+ lakini mwingine haiko tena.”+

14 Lakini, Yosefu akawaambia: “Ni kama vile nilisema⁠—⁠‘Muko wapelelezi!’ 15 Mutajaribiwa kwa njia hii: Kama vile hakika Farao anaishi, hamutatoka hapa mupaka ndugu yenu mudogo zaidi afike hapa.+ 16 Mumutume mumoja wenu amulete ndugu yenu, lakini ninyi wengine mutabakia katika kifungo. Katika njia hiyo, maneno yenu yatajaribiwa ili kuona kama muko munasema kweli. Na ikiwa haiko vile, basi, kama vile hakika Farao anaishi, ninyi muko wapelelezi.” 17 Basi akawatia katika kifungo kwa siku tatu (3).

18 Yosefu akawaambia hivi siku ya tatu (3): “Mufanye hivi ili muishi, kwa maana ninamuogopa Mungu. 19 Kama muko watu wanyoofu, mumoja wa ndugu zenu abakie mufungwa katika nyumba yenu ya kifungo, lakini ninyi wengine munaweza kuenda na kubeba nafaka ili kupunguza njaa katika nyumba zenu.+ 20 Kisha muniletee ndugu yenu mudogo zaidi, ili maneno yenu yaonekane kuwa ya kweli na ninyi hamutakufa.” Nao wakafanya vile.

21 Nao wakaambiana: “Hakika tuko tunapewa azabu kwa sababu ya ndugu yetu,+ kwa kuwa tuliona taabu yake* wakati alituomba tumuonyeshe huruma, lakini hatukusikiliza. Ndiyo maana musiba huu umetufikia.” 22 Kisha Rubeni akawajibu: “Je, sikuwaambia, ‘Musimutendee mutoto zambi,’ lakini hamukukuwa munanisikiliza?+ Sasa hakika damu yake iko inaombwa.”+ 23 Lakini hawakujua kwamba Yosefu alikuwa anaelewa, kwa sababu kulikuwa mutafsiri katikati yao. 24 Kwa hiyo akaenda mbali nao na kuanza kulia.+ Wakati alirudia na kuzungumuza nao tena, akamukamata Simeoni+ kati yao na kumufunga mbele ya macho yao.+ 25 Kisha Yosefu akatoa amri ili mifuko yao ijazwe nafaka na feza za kila mumoja zirudishwe ndani ya gunia lake na wapewe vyakula kwa ajili ya safari. Ni vile walifanyiwa.

26 Kwa hiyo wakabebesha punda wao nafaka zao na kutoka pale. 27 Wakati mumoja wao alifungua gunia lake ili akulishe punda wake wakiwa mahali pa kulala usiku, aliona feza zake katika kinywa cha mufuko wake. 28 Basi akawaambia ndugu zake: “Feza zangu zimerudishwa, na ziko hapa katika mufuko wangu!” Kisha mioyo yao ikazimia, na wakitetemeka, waliangaliana na kusema: “Ni jambo gani hili lenye Mungu ametutendea?”

29 Wakati walifika kwa Yakobo baba yao katika inchi ya Kanaani, wakamuambia mambo yote yenye yaliwapata, wakasema: 30 “Ule mwanaume mwenye kuwa bwana wa inchi hiyo alizungumuza na sisi kwa ukali+ na alisema kama sisi tuko tunapeleleza inchi. 31 Lakini tulimuambia, ‘Sisi tuko watu wenye haki. Hatuko wapelelezi.+ 32 Sisi tuko ndugu kumi na mbili (12),+ wana wa baba yetu. Mumoja wetu haiko tena,+ na ule mudogo zaidi iko* sasa pamoja na baba yetu katika inchi ya Kanaani.’+ 33 Lakini ule mwanaume mwenye kuwa bwana wa inchi hiyo alituambia, ‘Kwa njia hii nitajua kwamba muko watu wenye haki. Muache mumoja wa ndugu zenu pamoja na mimi.+ Kisha mukamate kitu fulani ili kupunguza njaa katika nyumba zenu na muende.+ 34 Na muniletee ndugu yenu mudogo zaidi, ili niweze kujua kwamba ninyi hamuko wapelelezi lakini muko watu wenye haki. Kisha nitawarudishia ndugu yenu, na munaweza kufanya biashara katika inchi.’”

35 Wakati walikuwa wanaondoa vitu vyenye vilikuwa ndani ya magunia yao, mufuko wa feza ulikuwa ndani ya gunia la kila mumoja wao. Wakati wao na baba yao waliona mifuko yao ya feza, wakaogopa. 36 Mara moja Yakobo baba yao akawaambia: “Ni mimi munafanya nikose watoto!+ Yosefu haiko tena,+ na Simeoni haiko tena,+ na munataka kumukamata Benyamini! Ni mimi mambo yote hayo yanaangukia!” 37 Lakini Rubeni akamuambia baba yake: “Unaweza kuua wana wangu wawili kama simulete kwako.+ Unipatie yeye, na nitamurudisha kwako.”+ 38 Lakini Yakobo akasema: “Mwana wangu hatashuka pamoja na ninyi, sababu ndugu yake amekufa na amebakia yeye peke yake.+ Kama jambo fulani lenye kuleta kifo linamufikia katika safari yenye mutafanya, basi hakika mutashusha imvi zangu katika Kaburi*+ kwa huzuni.”+

43 Sasa njaa ilikuwa kali katika inchi.+ 2 Kwa hiyo wakati walimaliza kula nafaka yenye walikuwa wametosha Misri,+ baba yao akawaambia: “Murudie kule na mutununulie chakula kidogo.” 3 Kisha Yuda akamuambia: “Ule mwanaume alituonya waziwazi, ‘Hamutaona uso wangu tena kama ndugu yenu haiko pamoja na ninyi.’+ 4 Kama unatutuma pamoja na ndugu yetu, tutashuka na kukununulia chakula. 5 Lakini kama haumutume, hatutashuka, kwa sababu ule mutu alituambia, ‘Hamutaona uso wangu tena kama ndugu yenu haiko pamoja na ninyi.’”+ 6 Na Israeli+ akauliza: “Sababu gani muliniletea shida hii kwa kumuambia ule mwanaume kama muko na ndugu mwingine?” 7 Wakajibu: “Ule mwanaume alituuliza moja kwa moja juu ya familia yetu na watu wa jamaa yetu, kwa kusema, ‘Je, baba yenu angali muzima? Je, muko na ndugu mwingine?’ na tulimuambia mambo hayo.+ Namna gani tungejua kama angeweza kusema, ‘Mushuke pamoja na ndugu yenu’?”+

8 Kisha Yuda akamulilia Israeli baba yake: “Tuma kijana huyu pamoja na mimi,+ na utuache tuende ili tuweze kuishi na tusikufe+⁠—​sisi na wewe na watoto wetu.+ 9 Nitahakikisha iko* salama.+ Utamuomba katika mikono yangu. Kama simurudishe kwako na kumuleta kwako, nitakuwa nimekutendea zambi kwa wakati wote. 10 Lakini kama hatungekuwa tumekawia, kufikia sasa tungekuwa tumefika kule na kurudia mara mbili.”

11 Kwa hiyo Israeli baba yao akawaambia: “Ikiwa inapaswa kuwa vile, basi mufanye hivi: Mubebe vitu vya muzuri zaidi vya inchi katika mifuko* yenu na muvipelekee ule mwanaume kuwa zawadi:+ zeri kidogo,+ asali kidogo, ubani mweusi, ngozi ya muti yenye utomvu,+ kungu, na lozi. 12 Mubebe kiasi cha feza mara mbili; na pia murudishe feza zenye ziliwekwa kwenye kinywa cha mifuko yenu.+ Pengine walikosea. 13 Mumuchukue ndugu yenu na muende, murudie kwa ule mwanaume. 14 Mungu Mweza-Yote amuchochee mwanaume huyo awaonyeshe huruma, ili amuachilie na kuwapatia ule ndugu yenu mwingine na Benyamini. Lakini kwa upande wangu, kama ni lazima nikose watoto, nitakosa watoto!”+

15 Kwa hiyo wale wanaume wakakamata zawadi hiyo, na wakakamata kiasi cha feza mara mbili katika mikono yao na pia Benyamini. Kisha wakasimama na kushuka mupaka Misri na wakasimama tena mbele ya Yosefu.+ 16 Wakati Yosefu alimuona Benyamini pamoja nao, mara moja akamuambia ule mwanaume mwenye alikuwa anasimamia nyumba yake: “Peleka wanaume hawa katika nyumba yangu na uchinje wanyama na kutayarisha chakula, kwa maana wanaume hawa wanapaswa kula chakula cha muchana pamoja na mimi.” 17 Bila kukawia ule mwanaume akafanya kama vile Yosefu alikuwa amemuambia,+ na akawapeleka katika nyumba ya Yosefu. 18 Lakini wale wanaume wakaogopa wakati walipelekwa katika nyumba ya Yosefu, na wakaanza kusema: “Tumeletwa hapa kwa sababu ya zile feza zenye zilirudishwa katika mifuko yetu wakati wenye ulipita. Sasa watatushambulia na kutufanya watumwa na kukamata punda zetu!”+

19 Kwa hiyo wakamuendea ule mwanaume mwenye alikuwa anasimamia nyumba ya Yosefu na wakazungumuza naye kwenye muingilio wa ile nyumba. 20 Wakasema: “Utusamehe, bwana wangu! Tulikuja hapa mara ya kwanza ili kununua chakula.+ 21 Lakini wakati tulifika mahali pa kulala na kuanza kufungua mifuko yetu, kumbe, feza za kila mumoja wetu zilikuwa katika kinywa cha mufuko wake, feza zetu pamoja na uzito wake wote.+ Kwa hiyo tungependa kuzirudisha sisi wenyewe. 22 Na tumeleta feza zingine ili kununua chakula. Hatujue ni nani mwenye aliweka feza zetu katika mifuko yetu.”+ 23 Kisha akasema: “Ni sawa. Musiogope. Mungu wenu na Mungu wa baba yenu aliweka mali katika mifuko yenu. Nilikuwa nimekwisha kupokea feza zenu.” Kisha mambo hayo akamutosha Simeoni inje na kumuleta kwao.+

24 Kisha ule mwanaume akawaingiza katika nyumba ya Yosefu na akawapatia maji ya kunawa miguu yao, na akawapatia chakula kwa ajili ya punda wao. 25 Na wakatayarisha zawadi+ ya kumupatia Yosefu wakati atakuja muchana, kwa maana walikuwa wamesikia kwamba watakula chakula pale.+ 26 Wakati Yosefu aliingia katika nyumba, wakamupelekea zawadi yao na wakainamisha uso mupaka chini mbele yake.+ 27 Kisha mambo hayo akawauliza hali yao na kusema: “Baba yenu ule muzee mwenye mulisema juu yake iko* namna gani? Angali muzima?”+ 28 Basi wakasema: “Mutumishi wako baba yetu iko* muzuri. Angali muzima.” Kisha wakainama na kushusha uso chini.+

29 Wakati aliinua macho na kumuona Benyamini ndugu yake, mwana wa mama yake,+ akasema: “Je, huyu ndiye ndugu yenu mudogo zaidi mwenye muliniambia juu yake?”+ Akaongeza kusema: “Mungu akuonyeshe wema, mwana wangu.” 30 Halafu Yosefu akafanya haraka, kwa maana alilemewa na hisia kwa sababu ya ndugu yake, na akatafuta mahali pa kulilia. Kwa hiyo akaingia katika chumba chenye hakikukuwa na watu na akaanza kutoa machozi kule.+ 31 Kisha kunawa uso wake na kutoka katika chumba, akiwa sasa amejizuia, akasema: “Mulete chakula.” 32 Wakamuletea chakula chake peke yake na ndugu zake chakula chao peke yao, na Wamisri wenye walikuwa pamoja naye wakakula peke yao, kwa maana Wamisri hawangeweza kula chakula pamoja na Waebrania; kwa sababu hilo ni jambo lenye kuchukiza kwa Wamisri.+

33 Ndugu zake walikuwa wamekaa mbele yake, kuanzia muzaliwa wa kwanza kulingana na haki yake ya muzaliwa wa kwanza+ mupaka ule mudogo zaidi kulingana na miaka yake, na walikuwa wanaangaliana kwa mushangao. 34 Yosefu akaendelea kutuma chakula kutoka kwenye meza yake mupaka kwenye meza zao, lakini aliongeza chakula cha Benyamini mara tano (5) zaidi ya chakula cha wale wengine wote.+ Kwa hiyo wakaendelea kufanya karamu na kunywa pamoja naye mupaka wakati walishiba.

44 Kisha wakati fulani Yosefu akaamuru ule mwanaume mwenye alikuwa anasimamia nyumba yake: “Jaza mifuko ya wanaume hawa chakula kingi kwa kadiri yenye wanaweza kubeba, na uweke feza za kila mumoja wao katika kinywa cha mufuko wake.+ 2 Lakini unapaswa kuweka kikombe changu, kile kikombe cha feza, katika kinywa cha mufuko wa ule mudogo zaidi, pamoja na feza za nafaka yake.” Kwa hiyo akafanya kama vile Yosefu alikuwa amemuagiza.

3 Asubui wakati mwangaza ulikuwa umetokea, wanaume hao waliruhusiwa kuondoka pamoja na punda wao. 4 Wakati walikuwa hawajaenda mbali na muji, Yosefu akamuambia ule mwanaume mwenye alikuwa anasimamia nyumba yake: “Simama! Ufuatilie wanaume hao! Wakati utawafikia, uwaambie, ‘Sababu gani mumelipa ubaya kwa wema? 5 Je, haiko kikombe hiki bwana wangu anakunywia ndani na kutumia ili kusoma kwa ufundi alama za mambo yenye yatatokea? Mumetenda jambo la uovu.’”

6 Kwa hiyo akawafikia na kuwaambia maneno hayo. 7 Lakini wakamuambia: “Sababu gani bwana wangu anasema jambo kama hilo? Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba watumishi wako wafanye jambo kama hilo. 8 Kwa sababu, feza zenye tulipata katika kinywa cha mifuko yetu tulikurudishia kutoka inchi ya Kanaani.+ Namna gani basi, tunaweza kuiba feza ao zahabu ya nyumba ya bwana wako? 9 Ikiwa kinapatikana kwa mumoja wa watumwa wako, akufe kabisa, na sisi wengine tutakuwa pia watumwa wa bwana wangu.” 10 Kwa hiyo akasema: “Ikuwe kama vile munasema: Ule mwenye atapatikana na kikombe hicho atakuwa mutumwa wangu, lakini ninyi wengine hamutakuwa na kosa.” 11 Basi kila mumoja wao akashusha haraka mufuko wake chini na kuufungua. 12 Akatafuta-tafuta kwa uangalifu, akaanzia kwa ule mukubwa zaidi na kumalizia kwa ule mudogo zaidi. Mwishowe kikombe kikapatikana katika mufuko wa Benyamini.+

13 Kisha wakapasua nguo zao, na kila mumoja wao akainua muzigo wake na kuurudisha juu ya punda wake na wakarudia katika muji. 14 Wakati Yuda+ na ndugu zake waliingia katika nyumba ya Yosefu, alikuwa angali pale; na wakaanguka chini mbele yake.+ 15 Yosefu akawaambia: “Ni jambo gani hili lenye mumefanya? Je, hamukujua kwamba mutu kama mimi anaweza kusoma kwa ufundi alama za mambo yenye yatatokea?”+ 16 Yuda akajibu: “Tumuambie bwana wangu nini? Tuseme nini? Na namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye haki? Mungu wa kweli amefunua kosa la watumwa wako.+ Sasa sisi tuko watumwa wa bwana wangu, sisi na ule mwenye kikombe kilipatikana katika mukono wake!” 17 Lakini, akasema: “Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba nifanye vile. Mutu mwenye kikombe kilipatikana katika mukono wake ni yeye atakuwa mutumwa wangu.+ Lakini ninyi wengine, muende kwa amani kwa baba yenu.”

18 Sasa Yuda akamukaribia na kusema: “Ninakuomba, bwana wangu, tafazali acha mutumwa wako aseme neno moja katika masikio ya bwana wangu, na usimukasirikie mutumwa wako, kwa sababu wewe uko kama Farao.+ 19 Bwana wangu aliuliza watumwa wake, ‘Je, muko na baba ao ndugu?’ 20 Kwa hiyo tulimuambia bwana wangu, ‘Tuko na baba mwenye kuzeeka na mutoto mumoja wa uzee wake, mudogo zaidi.+ Lakini ndugu yake alikufa,+ kwa hiyo yeye ndiye mwana peke yake mwenye amebakia wa mama yake,+ na baba yake anamupenda.’ 21 Kisha uliambia watumwa wako, ‘Mumulete ili nimuone.’+ 22 Lakini tuliambia bwana wangu, ‘Kijana huyo hawezi kuacha baba yake. Akimuacha, hakika baba yake atakufa.’+ 23 Kisha uliambia watumwa wako, ‘Kama ndugu yenu mudogo zaidi hashuke pamoja na ninyi, hamutaona tena uso wangu.’+

24 “Kwa hiyo tulipanda kwa mutumwa wako baba yangu na tukamuambia maneno ya bwana wangu. 25 Kisha wakati fulani baba yetu alisema, ‘Murudie na mutununulie chakula kidogo.’+ 26 Lakini tulisema, ‘Hatuwezi kushuka kule. Kama ndugu yetu mudogo zaidi iko* pamoja na sisi tutashuka, kwa sababu hatuwezi kuona uso wa mwanaume ule kama ndugu yetu mudogo zaidi haiko pamoja na sisi.’+ 27 Kisha mutumwa wako baba yangu akatuambia, ‘Munajua muzuri kama bibi yangu alinizalia tu wana wawili.+ 28 Lakini mumoja wao aliniacha na nikasema: “Anapaswa kuwa amepasuliwa vipande-vipande!”+ na mupaka sasa sijamuona. 29 Kama munamuondoa huyu pia mbele ya macho yangu na kama jambo lenye kuleta kifo linamufikia, hakika mutashusha imvi zangu katika Kaburi*+ nikiwa katika huzuni.’+

30 “Na sasa ikiwa ninarudia kwa mutumwa wako baba yangu bila kijana huyu kuwa pamoja na sisi, kwa maana uzima wake mwenyewe umeshikamana* na uzima wa kijana huyu, 31 kisha wakati tu ataona kwamba kijana haiko pale, atakufa, na watumwa wako hakika watashusha imvi za mutumwa wako baba yetu katika Kaburi* kwa huzuni. 32 Mutumwa wako alimuhakikishia baba yangu kwa ajili ya kijana huyu, kwa kusema, ‘Kama simurudishe kwako, basi nitakuwa nimemutendea baba yangu zambi milele.’+ 33 Kwa hiyo basi, acha mutumwa wako abakie na akuwe mutumwa wa bwana wangu pahali pa kijana huyu, ili kijana huyu aweze kurudia pamoja na ndugu zake. 34 Namna gani nitaweza kurudia kwa baba yangu bila kijana huyu kuwa pamoja na mimi? Siwezi kuvumilia kuona wakati musiba huo utamufikia baba yangu!”

45 Wakati huo Yosefu hakuweza tena kujizuia mbele ya watumishi wake wote.+ Kwa hiyo akasema kwa sauti kubwa: “Mutoshe kila mutu mbele yangu!” Hakuna mutu mwingine mwenye alibakia pamoja naye wakati Yosefu alijitambulisha mwenyewe kwa ndugu zake.+

2 Kisha akaanza kulia kwa sauti kubwa mupaka Wamisri wakasikia na nyumba ya Farao ikasikia. 3 Mwishowe Yosefu akaambia ndugu zake: “Mimi ni Yosefu. Je, baba yangu angali muzima?” Lakini ndugu zake hawakuweza kumujibu, kwa maana walishituka sana kwa sababu yake. 4 Kwa hiyo Yosefu akaambia ndugu zake: “Tafazali, munikaribie.” Basi wakamukaribia.

Kisha akasema: “Mimi ni Yosefu ndugu yenu, mwenye muliuzisha apelekwe Misri.+ 5 Lakini sasa musihuzunike na kila mumoja asimulaumu mwenzake kwa sababu muliniuzisha huku; kwa sababu Mungu alinituma mbele yenu ili kulinda uzima.+ 6 Huu ni mwaka wa pili wa njaa katika inchi,+ na kungali miaka tano (5) yenye hakutakuwa kulima wala kuvuna. 7 Lakini Mungu alinituma mbele yenu ili kulinda mabaki kwa ajili yenu+ juu ya dunia* na kuwaokoa kwa wokovu mukubwa. 8 Kwa hiyo basi, haiko ninyi ndio mulinituma huku, lakini ni Mungu wa kweli, ili aniweke kuwa mushauri mukubwa* wa Farao na bwana kwa ajili ya nyumba yake yote na mutawala juu ya inchi yote ya Misri.+

9 “Murudie haraka kwa baba yangu, na munapaswa kumuambia, ‘Mwana wako Yosefu anasema: “Mungu ameniweka kuwa bwana juu ya Misri yote.+ Shuka ukuje kwangu. Usikawie.+ 10 Unapaswa kukaa katika inchi ya Gosheni,+ mahali kwenye utakuwa karibu na mimi⁠—​wewe, wana wako, wajukuu wako, makundi yako, mifugo yako, na kila kitu chenye uko nacho. 11 Nitakupatia chakula kule, kwa maana kungali miaka tano (5) ya njaa.+ Kama haiko vile, utakuwa maskini, wewe na nyumba yako na kila kitu chenye uko nacho.’” 12 Ninyi na ndugu yangu Benyamini munajionea na macho yenu wenyewe kwamba ni mimi ninazungumuza na ninyi.+ 13 Kwa hiyo munapaswa kumuambia baba yangu kuhusu utukufu wangu katika Misri na kila kitu chenye mumeona. Sasa mufanye haraka na mumulete baba yangu hapa.”

14 Kisha akamukumbatia Benyamini ndugu yake na akaanza kulia, na Benyamini akalia na mikono ya Yosefu ilikuwa imezunguka shingo ya Benyamini.+ 15 Na akabusu ndugu zake wote na akalia juu ya shingo zao, na kisha mambo hayo ndugu zake wakazungumuza naye.

16 Habari ikafika katika nyumba ya Farao: “ Ndugu za Yosefu wamekuja!” Habari hiyo ikamufurahisha Farao na watumishi wake. 17 Kwa hiyo Farao akamuambia Yosefu: “Ambia ndugu zako, ‘Mufanye hivi: Mubebeshe wanyama wenu mizigo na muende katika inchi ya Kanaani, 18 na muchukue baba yenu na watu wa nyumba zenu na mukuje hapa kwangu. Nitawapatia vitu vya muzuri vya inchi ya Misri, na mutakula* sehemu yenye utajiri mukubwa zaidi ya* inchi.’+ 19 Na unaamuriwa kuwaambia:+ ‘Mufanye hivi: Mukamate magari ya kukokotwa+ ya inchi ya Misri kwa ajili ya watoto wenu na bibi zenu, na munapaswa kumuleta baba yenu juu ya moja ya magari hayo na kuja hapa.+ 20 Musikuwe na wasiwasi juu ya mali zenu,+ kwa maana vitu vya muzuri zaidi vya inchi ya Misri ni vyenu.’”

21 Na wana wa Israeli wakafanya vile, na Yosefu akawapatia magari ya kukokotwa kama vile Farao aliamuru, na akawapatia chakula kwa ajili ya safari. 22 Akapatia kila mumoja wao nguo za kubadilisha, lakini akamupatia Benyamini vipande mia tatu (300) vya feza na nguo tano (5) za kubadilisha.+ 23 Na akamutumia baba yake vitu hivi: punda kumi (10) wenye kubeba vitu vya muzuri vya Misri na punda-dike kumi wenye kubeba nafaka na mikate na vyakula vingine kwa ajili ya safari ya baba yake. 24 Kwa hiyo akaacha ndugu zake waende, na wakati walikuwa wanaondoka, akawaambia: “Musigombane katika njia.”+

25 Kisha wakaondoka Misri na kufika katika inchi ya Kanaani kwa Yakobo baba yao. 26 Kisha wakamuambia: “Yosefu angali muzima, na yeye ndiye mutawala juu ya inchi yote ya Misri!”+ Lakini moyo wake haukushituka kabisa kwa sababu hakuwaamini.+ 27 Wakati waliendelea kumuambia maneno yote yenye Yosefu alikuwa amewaambia na wakati aliona magari ya kukokotwa yenye Yosefu alikuwa ametuma ili yamubebe, roho ya Yakobo ikaanza kufufuka. 28 Mara moja Israeli akasema: “Inatosha! Mwana wangu Yosefu angali muzima! Ninapaswa kuenda na kumuona mbele nikufe!”+

46 Kwa hiyo Israeli akakamata yote yenye alikuwa nayo* na akaondoka. Wakati alifika Beer-sheba,+ akamutolea zabihu Mungu wa Isaka, baba yake.+ 2 Kisha Mungu akazungumuza na Israeli usiku katika maono na kusema: “Yakobo, Yakobo!” naye akajibu: “Mimi huyu!” 3 Akasema: “Mimi ni Mungu wa kweli, Mungu wa baba yako.+ Usiogope kushuka kuenda Misri, kwa maana nitakufanya kuwa taifa kubwa kule.+ 4 Mimi mwenyewe nitashuka pamoja na wewe kule Misri, na mimi mwenyewe nitakurudisha tena kutoka kule,+ na Yosefu ataweka mukono wake juu ya macho yako.”*+

5 Kisha mambo hayo Yakobo akaondoka Beer-sheba, na wana wa Israeli wakamubeba Yakobo baba yao na watoto wao na bibi zao katika magari ya kukokotwa yenye Farao alikuwa ametuma ili kumubeba Yakobo. 6 Walienda pamoja na mifugo yao na mali zao, zenye walikuwa wamekusanya katika inchi ya Kanaani. Na mwishowe wakaingia katika Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye. 7 Alienda Misri pamoja na wana wake na wajukuu wake wanaume, watoto wake wanamuke na wajukuu wake wanamuke⁠—​uzao wake wote.

8 Sasa haya ndiyo majina ya wana wa Israeli wenye waliingia Misri,+ Yakobo na wana wake: muzaliwa wa kwanza wa Yakobo alikuwa Rubeni.+

9 Wana wa Rubeni walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+

10 Wana wa Simeoni+ walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli+ mwana wa mwanamuke Mukanaani.

11 Wana wa Lawi+ walikuwa Gershoni, Kohati, na Merari.+

12 Wana wa Yuda+ walikuwa Eri, Onani, Shela,+ Perezi,+ na Zera.+ Lakini, Eri na Onani walikufa katika inchi ya Kanaani.+

Wana wa Perezi walikuwa Hezroni na Hamuli.+

13 Wana wa Isakari walikuwa Tola, Puva, Iobu, na Shimroni.+

14 Wana wa Zabuloni+ walikuwa Seredi, Eloni, na Yahleeli.+

15 Hao ndio wana wa Lea, wenye alimuzalia Yakobo kule Padan-aramu, na pia Dina binti yake.+ Watoto wake wote wanaume na watoto wake wote wanamuke walikuwa* makumi tatu na tatu (33).

16 Wana wa Gadi+ walikuwa Zifioni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi, na Areli.+

17 Wana wa Asheri+ walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, Beria, na dada yao alikuwa Sera.

Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli.+

18 Hao ndio wana wa Zilpa,+ mwenye Labani alimupatia Lea binti yake. Zilpa alimuzalia Yakobo watu* kumi na sita (16).

19 Wana wa Raheli, bibi ya Yakobo, walikuwa Yosefu+ na Benyamini.+

20 Katika inchi ya Misri, Asenati+ binti ya Potifera kuhani wa Oni,* alimuzalia Yosefu wana hawa: Manase+ na Efraimu.+

21 Wana wa Benyamini+ walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera,+ Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu,+ na Ardi.+

22 Hao ndio wana wenye Raheli alimuzalia Yakobo: wote walikuwa watu* kumi na ine (14).

23 Mwana* wa Dani+ alikuwa Hushimu.+

24 Wana wa Naftali+ walikuwa Yahzeeli, Guni, Yezeri, na Shilemu.+

25 Hao ndio wana wa Bilha, mwenye Labani alimupatia Raheli binti yake. Bilha alimuzalia Yakobo hawa: watu* saba (7) kwa ujumla.

26 Wale wote wenye walikuwa* wazao wa Yakobo na wenye waliingia Misri pamoja naye walikuwa makumi sita na sita (66), bila kuhesabu bibi za wana wa Yakobo.+ 27 Wana wa Yosefu wenye walizaliwa katika Misri walikuwa wawili.* Watu wote wa* nyumba ya Yakobo wenye waliingia Misri walikuwa makumi saba (70).+

28 Yakobo akamutuma Yuda+ atangulie na kumuambia Yosefu kwamba alikuwa katika njia kuenda Gosheni. Wakati waliingia katika inchi ya Gosheni,+ 29 Yosefu akaagiza gari lake litayarishwe na akapanda kuenda kumupokea Israeli baba yake kule Gosheni. Wakati alijitambulisha kwa baba yake, mara moja akamukumbatia* baba yake na kulia kwa wakati fulani.* 30 Kisha Israeli akamuambia Yosefu: “Sasa niko tayari kufa; nimeona uso wako na kujua kwamba ungali muzima.”

31 Kisha Yosefu akaambia ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake: “Muache nipande kuenda kumujulisha Farao+ na kumuambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumba ya baba yangu wenye walikuwa katika inchi ya Kanaani wamekuja hapa kwangu.+ 32 Watu hao ni wachungaji,+ na wanafuga mifugo,+ na wameleta makundi yao na mifugo yao na kila kitu chenye wako nacho.’+ 33 Wakati Farao atawaita na kuwauliza, ‘Munafanya kazi gani?’ 34 munapaswa kusema, ‘Watumishi wako wamefuga mifugo tangu ujana wao mupaka sasa, sisi na mababu zetu,’+ ili muweze kuishi katika inchi ya Gosheni,+ kwa maana kila muchungaji wa kondoo ni chukizo kwa Wamisri.”+

47 Kwa hiyo Yosefu akaenda na kumujulisha Farao:+ “Baba yangu na ndugu zangu wamekuja kutoka katika inchi ya Kanaani na makundi yao na mifugo yao na kila kitu chenye wako nacho, na sasa wako katika inchi ya Gosheni.”+ 2 Yosefu akachukua ndugu zake tano (5) na kuwatambulisha kwa Farao.+

3 Farao akaambia ndugu zake: “Munafanya kazi gani?” Wakamujibu Farao: “Watumishi wako ni wachungaji wa kondoo, sisi na mababu zetu.”+ 4 Kisha wakamuambia Farao: “Tumekuja ili kukaa kama wageni katika inchi+ kwa sababu hakuna malisho kwa ajili ya kundi la watumishi wako, kwa maana njaa iko kali katika inchi ya Kanaani.+ Kwa hiyo tafazali acha watumishi wako wakae katika inchi ya Gosheni.”+ 5 Basi Farao akamuambia Yosefu: “Baba yako na ndugu zako wamekuja hapa kwenye uko. 6 Inchi ya Misri iko katika mikono yako. Patia baba yako na ndugu zako makao katika sehemu ya muzuri zaidi ya inchi.+ Uwaache wakae katika inchi ya Gosheni, na kama unajua wanaume fulani kati yao wenye kuwa na uwezo, uwaweke wasimamie mifugo yangu.”

7 Kisha Yosefu akamuingiza Yakobo baba yake na kumutambulisha kwa Farao, na Yakobo akamubariki Farao. 8 Farao akamuuliza Yakobo: “Uko na miaka ngapi?” 9 Yakobo akamuambia Farao: “Miaka ya kuhama-hama kwangu* iko miaka mia moja makumi tatu (130). Miaka ya maisha yangu imekuwa kidogo na yenye taabu,+ nayo haijafikia hesabu ya miaka ya maisha ya mababu zangu wakati walikuwa wanahama-hama.”*+ 10 Kisha mambo hayo Yakobo akamubariki Farao na kuondoka.

11 Kwa hiyo Yosefu akamupatia baba yake na ndugu zake makao, na akawapatia mali katika inchi ya Misri, katika eneo la muzuri sana la inchi, katika inchi ya Ramesesi,+ kama vile Farao alikuwa ameamuru. 12 Na Yosefu akaendelea kupatia chakula* baba yake na ndugu zake na watu wote wa nyumba ya baba yake, kulingana na hesabu ya watoto wao.

13 Sasa inchi yote haikukuwa na chakula,* kwa sababu njaa ilikuwa kali sana, na inchi ya Misri na inchi ya Kanaani zikakuwa zaifu kwa sababu ya ile njaa.+ 14 Yosefu alikuwa anakusanya feza zote zenye zilipatikana katika inchi ya Misri na katika inchi ya Kanaani kwa ajili ya nafaka yenye watu walikuwa wananunua,+ na Yosefu alikuwa anazipeleka katika nyumba ya Farao. 15 Kisha wakati fulani feza za inchi ya Misri na za inchi ya Kanaani zikaisha, na Wamisri wote wakaanza kuenda kwa Yosefu na kusema: “Utupatie chakula! Sababu gani tukufe mbele ya macho yako kwa sababu feza zetu zimeisha?” 16 Kisha Yosefu akasema: “Kama feza zenu zimeisha, mulete mifugo yenu na nitawapatia chakula kwa kubadilishana na mifugo yenu.” 17 Kwa hiyo wakaanza kumuletea Yosefu mifugo yao, na Yosefu akaendelea kuwapatia chakula kwa kubadilishana na farasi zao, makundi na mifugo, na punda, na akaendelea kuwapatia chakula kwa kubadilishana na mifugo yao yote katika mwaka huo.

18 Wakati mwaka huo ulimalizika, walianza kuja tena kwake mwaka wenye ulifuata na kusema: “Hatutamuficha bwana wangu kwamba feza na makundi ya wanyama wa kufugwa vimekwisha kupewa bwana wangu. Hatukubakia na kitu kwa ajili ya bwana wangu isipokuwa tu miili yetu na mashamba yetu. 19 Sababu gani tukufe mbele ya macho yako, sisi na mashamba yetu? Utununue sisi na mashamba yetu kwa kubadilishana na chakula, na sisi pamoja na mashamba yetu tutakuwa watumwa wa Farao. Utupatie mbegu ili tuweze kuishi na tusikufe na ili mashamba yetu yasikae bila kitu.” 20 Basi Yosefu akamununulia Farao mashamba yote ya Wamisri kwa sababu kila Mumisri aliuzisha shamba lake, kwa maana njaa ilikuwa kali sana; na inchi ikakuwa ya Farao.

21 Kisha akahamisha watu na kuwapeleka katika miji, kuanzia mwisho mumoja wa eneo la Misri mupaka ule mwisho mwingine.+ 22 Ni mashamba ya makuhani tu ndiyo hakununua,+ kwa sababu chakula cha makuhani kilikuwa kinatoka kwa Farao na makuhani waliishi kwa kutegemea chakula chenye Farao aliwapatia. Ndiyo sababu wao hawakuuzisha mashamba yao. 23 Kisha Yosefu akaambia watu: “Muangalie, leo nimewanunua ninyi na mashamba yenu kwa ajili ya Farao. Mukamate mbegu, na munapaswa kuzipanda katika mashamba. 24 Wakati zitazaa, mutamupatia Farao sehemu moja ya tano (1/5),+ lakini sehemu ine (4) zitakuwa zenu ili zikuwe mbegu kwa ajili ya mashamba na chakula kwa ajili yenu na wale wenye kuwa katika nyumba zenu na kwa ajili ya watoto wenu ili wakule.” 25 Kwa hiyo wakasema: “Umelinda uzima wetu.+ Acha tukubaliwe mbele ya macho ya bwana wangu, na sisi tutakuwa watumwa wa Farao.”+ 26 Kisha Yosefu akaifanya ikuwe amri, yenye ingali inafanya kazi mupaka leo juu ya Misri, kwamba sehemu moja ya tano (1/5) ni ya Farao. Ni mashamba ya makuhani tu ndiyo hayakukuwa ya Farao.+

27 Israeli akaendelea kukaa katika inchi ya Misri, katika inchi ya Gosheni,+ na wakafanya makao yao kule na wakazaa na kuongezeka sana.+ 28 Na Yakobo akaishi katika inchi ya Misri kwa miaka kumi na saba (17), na hivyo siku zote za maisha yake zikakuwa miaka mia moja makumi ine na saba (147).+

29 Wakati wa kufa kwa Israeli ulikaribia,+ kwa hiyo akamuita Yosefu mwana wake na kumuambia: “Kama sasa, nimekubaliwa mbele ya macho yako, tafazali weka mukono wako chini ya paja langu, na unionyeshe upendo mushikamanifu na uaminifu. Tafazali, usinizike Misri.+ 30 Wakati nitakufa, unapaswa kunichukua kutoka Misri na kunizika katika kaburi la mababu zangu.”+ Basi, Yosefu akasema: “Nitafanya kama vile unasema.” 31 Kisha Yakobo akasema: “Uniapie.” Kwa hiyo akamuapia.+ Basi Israeli akainama kwenye kichwa cha kitanda chake.+

48 Kisha mambo hayo, Yosefu akaambiwa: “Angalia, baba yako anaendelea kuwa muzaifu.” Basi akachukua wana wake wawili Manase na Efraimu pamoja naye.+ 2 Kisha Yakobo akaambiwa: “Mwana wako Yosefu amekuja kukuona.” Kwa hiyo Israeli akakusanya nguvu zake na kukaa kwenye kitanda chake. 3 Na Yakobo akamuambia Yosefu:

“Mungu Mweza-Yote alinitokea kule Luzi katika inchi ya Kanaani na akanibariki.+ 4 Na aliniambia, ‘Nitakufanya uzae, na nitakufanya kuwa watu wengi, na nitakufanya kuwa kutaniko la vikundi vya watu,+ na nitapatia uzao wako* inchi hii kisha wewe kuwa uriti wa kudumu.’+ 5 Sasa wana wako wawili wenye ulizaa katika inchi ya Misri mbele nifike kwako ni wangu.+ Efraimu na Manase watakuwa wangu kama vile Rubeni na Simeoni ni wangu.+ 6 Lakini watoto wenye utazaa kisha wao watakuwa wako. Wataitwa kwa jina la ndugu zao katika uriti wao.+ 7 Lakini mimi, wakati nilikuwa ninatoka Padani, Raheli alikufa+ pembeni yangu katika inchi ya Kanaani, wakati kulikuwa kungali safari murefu mbele ya kufika Efrati.+ Kwa hiyo nikamuzika kwenye njia ya kuenda Efrati, ni kusema, Betlehemu.”+

8 Kisha Israeli akaona wana wa Yosefu na akauliza: “Hawa ni nani?” 9 Kwa hiyo Yosefu akamuambia baba yake: “Hawa ni wana wangu wenye Mungu amenipatia mahali hapa.”+ Basi Yakobo akasema: “Tafazali, uwalete karibu na mimi ili niwabariki.”+ 10 Sasa macho ya Israeli yalikuwa yamefifia kwa sababu ya uzee, na hakuweza kuona. Kwa hiyo Yosefu akawaleta karibu na Yakobo, na Yakobo akawabusu na kuwakumbatia. 11 Israeli akamuambia Yosefu: “Sikuwaza kwamba ningeona uso wako tena,+ lakini Mungu ameniwezesha kuona uzao wako* pia.” 12 Kisha Yosefu akawaondoa kwenye magoti ya Israeli, na akainamisha uso wake mupaka chini.

13 Sasa Yosefu akachukua wote wawili, Efraimu+ kwa mukono wake wa kuume ili akuwe kwenye mukono wa kushoto wa Israeli na Manase+ kwa mukono wake wa kushoto ili akuwe kwenye mukono wa kuume wa Israeli, na akawaleta karibu naye. 14 Lakini Israeli akanyoosha mukono wake wa kuume na kuuweka juu ya kichwa cha Efraimu, hata kama yeye ndiye alikuwa mudogo, na akaweka mukono wake wa kushoto juu ya kichwa cha Manase. Aliweka mikono yake vile kimakusudi, kwa sababu Manase ndiye alikuwa muzaliwa wa kwanza.+ 15 Kisha akamubariki Yosefu na kusema:+

“Mungu wa kweli mwenye baba zangu Isaka na Abrahamu walitembea mbele yake,+

Mungu wa kweli mwenye amekuwa akinichunga maisha yangu yote mupaka leo,+

16 Malaika mwenye amekuwa akiniokoa katika misiba yangu yote,+ abariki vijana hawa.+

Jina langu liitwe juu yao na jina la baba zangu, Abrahamu na Isaka,

Waongezeke na kuwa wengi katika dunia.”+

17 Wakati Yosefu aliona kwamba baba yake ameweka mukono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakufurahi, kwa hiyo akajaribu kushika mukono wa baba yake ili auondoe juu ya kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase. 18 Yosefu akamuambia baba yake: “Hapana vile, baba yangu, kwa sababu huyu ndiye muzaliwa wa kwanza.+ Weka mukono wako wa kuume juu ya kichwa chake.” 19 Lakini baba yake akaendelea kukataa na kusema: “Ninajua, mwana wangu, ninajua. Yeye pia atakuwa kikundi cha watu, na yeye pia atakuwa mukubwa. Lakini, ndugu yake mudogo atakuwa mukubwa kuliko yeye,+ na uzao wake utakuwa mwingi* sawasawa kabisa na mataifa mengi.”+ 20 Kwa hiyo akaendelea kuwabariki siku hiyo,+ kwa kusema:

“Israeli ataje jina lenu wakati wanatangaza baraka, wakisema,

‘Mungu akufanye kuwa kama Efraimu na Manase.’”

Hivyo akaendelea kumuweka Efraimu mbele ya Manase.

21 Kisha Israeli akamuambia Yosefu: “Angalia, niko karibu kufa,+ lakini hakika Mungu ataendelea kuwa pamoja na ninyi na atawarudisha katika inchi ya mababu zenu.+ 22 Lakini mimi, ninakupatia sehemu moja zaidi ya inchi* kuliko ndugu zako, yenye nilikamata katika mukono wa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”

49 Na Yakobo akaita wana wake na kusema: “Mujikusanye pamoja ili niwaambie mambo yenye yatawapata katika kipindi cha mwisho cha zile siku. 2 Mujikusanye na kusikiliza, ninyi wana wa Yakobo, ndiyo, mumusikilize Israeli baba yenu.

3 “Rubeni,+ wewe ni muzaliwa wangu wa kwanza,+ nguvu zangu na mwanzo wa nguvu zangu za uzazi, ulikuwa na heshima nyingi na nguvu nyingi. 4 Kwa sababu ya kukosa kujizuia kama maji yenye musukosuko, hautakuwa mukubwa, kwa maana ulipanda juu ya kitanda cha baba yako.+ Wakati huo ulichafua kitanda changu. Alipanda kabisa juu ya kitanda hicho!

5 “Simeoni na Lawi ni ndugu.+ Silaha zao za kuchinja ni vyombo vya jeuri.+ 6 Usiingie katika kikundi chao, Ee nafsi* yangu. Usijiunge na mukusanyiko wao, Ee heshima yangu,* kwa sababu katika kasirani yao waliua watu,+ na walikata mishipa ya magoti ya ngombe-dume ili kujifurahisha. 7 Hasira yao ilaaniwe, kwa sababu haina huruma, na kasirani yao kali, kwa sababu ni kali sana.+ Niwatawanye katika Yakobo, na niwasambaze katika Israeli.+

8 “Sasa wewe, Yuda,+ ndugu zako watakusifu.+ Mukono wako utakuwa juu ya shingo ya maadui wako.+ Wana wa baba yako watainama mbele yako.+ 9 Yuda ni mwana-simba.+ Mwana wangu, utapanda kutoka kwenye mawindo. Ameshutama na kujinyoosha kama simba, na kama simba, ni nani anaweza kupima kumuamusha? 10 Fimbo ya ufalme haitatoka kwa Yuda,+ wala fimbo ya kamanda kutoka katikati ya miguu yake, mupaka wakati Shilo* atakuja,+ na vikundi vya watu vitamutii yeye.+ 11 Atafunga punda wake kwenye muti wa muzabibu na mwana-punda wake kwenye muti muzuri wa muzabibu, atafua nguo zake katika divai na nguo yake katika damu ya zabibu. 12 Macho yake ni mekundu sana kwa sababu ya divai, na meno yake ni meupe kwa sababu ya maziwa.

13 “Zabuloni+ atakaa pembeni ya bahari, karibu na mahali kwenye mashua* zinatia nanga,*+ na mupaka wake wa mbali utakuwa kuelekea Sidoni.+

14 “Isakari+ ni punda mwenye mifupa migumu, mwenye kulala katikati ya mifuko mbili ya kiti chenye kuwa juu ya punda. 15 Na ataona kwamba mahali pa kupumuzikia ni pazuri na kwamba inchi inapendeza. Atainamisha bega lake ili abebe muzigo na atakubali kufanya kazi ya kulazimishwa.

16 “Dani+ atahukumu watu wake akiwa mumoja wa makabila ya Israeli.+ 17 Dani akuwe nyoka pembeni ya barabara, kama nyoka-kipiri mwenye pembe kando ya njia, mwenye kuuma visigino vya farasi na hivyo mupandaji wake anaangukia nyuma.+ 18 Nitangojea wokovu wako, Ee Yehova.

19 “Kuhusu Gadi,+ kikundi cha wanyanganyi kitamushambulia, lakini yeye atawashambulia kwenye visigino vyao.+

20 “Mukate wa Asheri+ utakuwa mwingi,* naye atatoa chakula chenye kustahili kukuliwa na mufalme.+

21 “Naftali+ ni paa mwembamba. Anasema maneno yenye kupendeza.+

22 “Yosefu+ ni chipukizi la muti wenye kuzaa matunda, muti wenye kuzaa matunda pembeni ya chemchemi ya maji, wenye matawi yenye kusambaa juu ya ukuta. 23 Lakini wapiga-mishale waliendelea kumusumbua na kumutupia mishale na waliendelea kumuwekea chuki.+ 24 Lakini upinde wake ulibakia mahali pake,+ na mikono yake iliendelea kuwa na nguvu na myepesi.+ Hilo lilitokana na mikono ya mwenye nguvu wa Yakobo, lilitokana na muchungaji, jiwe la Israeli. 25 Ametoka* kwa Mungu wa baba yako, na atakusaidia, na iko* pamoja na Mweza-Yote, na atakubariki kwa baraka za mbingu zenye kuwa juu, kwa baraka zenye kuwa chini kabisa,+ kwa baraka za maziwa ya mama na tumbo la uzazi.* 26 Baraka za baba yako zitakuwa kubwa kuliko baraka za milima ya milele, kuliko vitu vyenye kutamanika vya milima midogo yenye kudumu.+ Baraka zitaendelea kuwa juu ya kichwa cha Yosefu, kwenye sehemu ya juu ya katikati ya kichwa cha ule mwenye alitengwa na ndugu zake.+

27 “Benyamini+ ataendelea kupasua kama imbwa wa pori.+ Asubui atakula mawindo, na mangaribi atagawanya vitu vyenye vinachukuliwa katika vita.”+

28 Hayo ndiyo makabila kumi na mbili (12) ya Israeli, na hayo ndiyo maneno yenye baba yao aliwaambia wakati alikuwa anawabariki. Alipatia kila mumoja wao baraka yenye kumustahili.+

29 Kisha mambo hayo akawapatia maagizo haya: “Niko karibu kukusanywa kwa watu wangu.*+ Munizike pamoja na baba zangu katika pango lenye kuwa katika shamba la Efroni Muhiti,+ 30 pango lenye kuwa katika shamba la Makpela mbele ya Mamre katika inchi ya Kanaani, shamba lenye Abrahamu alinunua kwa Efroni Muhiti ili likuwe mahali pa kuzikia. 31 Ni kule walizika Abrahamu na Sara bibi yake.+ Ni kule walizika Isaka+ na Rebeka bibi yake na ni kule nilimuzika Lea. 32 Shamba hilo pamoja na pango lenye kuwa ndani yake lilinunuliwa kwa wana wa Heti.”+

33 Basi Yakobo akamaliza kuwapatia wana wake maagizo hayo. Kisha akaweka tena miguu yake juu ya kitanda na akavuta pumuzi yake ya mwisho na akakusanywa kwa watu wake.*+

50 Kisha Yosefu akajitupa juu ya baba yake+ na akalia juu yake na kumubusu. 2 Kisha Yosefu akaamuru watumishi wake, wanganga, wamupakae baba yake dawa ili asioze.+ Kwa hiyo waganga hao wakamupakaa Israeli dawa ili asioze, 3 na wakatumia siku makumi ine (40) za kuenea kwa ajili yake, kwa maana huu ndio muda kamili wenye ulitumiwa ili kumupakaa mutu dawa ili asioze, na Wamisri wakaendelea kutoa machozi kwa ajili yake kwa siku makumi saba (70).

4 Wakati siku za kumuombolezea ziliisha, Yosefu akawaambia watu wa makao* ya Farao, kwa kusema: “Kama nimekubaliwa mbele ya macho yenu, mumupatie Farao ujumbe huu: 5 ‘Baba yangu aliniapisha,+ kwa kusema: “Angalia! Niko karibu kufa.+ Unapaswa kunizika katika kaburi langu,+ lenye nimechimba katika inchi ya Kanaani.”+ Tafazali, acha niende kumuzika baba yangu, kisha nitarudia.’” 6 Farao akajibu: “Uende na umuzike baba yako kama vile alikuapisha.”+

7 Kwa hiyo Yosefu akaenda kumuzika baba yake, na watumishi wote wa Farao wakaenda pamoja naye, wazee+ wa makao ya Farao na wazee wote wa inchi ya Misri 8 na watu wote wa nyumba ya Yosefu na ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake.+ Waliacha tu katika inchi ya Gosheni watoto wao wadogo na makundi yao na mifugo yao. 9 Magari+ na wapanda-farasi walienda pamoja naye; na kambi ilikuwa kubwa sana. 10 Kisha wakafika kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Atadi, katika eneo la Yordani, na wakaomboleza sana kule na kulia kwa uchungu, na akaendelea kumuombolezea baba yake kwa siku saba (7). 11 Wakaaji wa inchi, Wakanaani, wakawaona wakiomboleza kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka cha Atadi, mara moja wakasema: “Haya ni maombolezo makubwa ya Wamisri!” Ndiyo sababu mahali pale paliitwa Abel-misraimu,* penye kuwa katika eneo la Yordani.

12 Kwa hiyo wana wa Yakobo wakamufanyia kama vile alikuwa amewaagiza.+ 13 Wana wake wakamupeleka mupaka katika inchi ya Kanaani na wakamuzika katika pango la shamba la Makpela, shamba lenye kuwa mbele ya Mamre na lenye Abrahamu alinunua kwa Efroni Muhiti ili likuwe mahali pa kuzikia.+ 14 Kisha kumuzika baba yake, Yosefu akarudia Misri pamoja na ndugu zake na wale wote wenye walienda pamoja naye ili kumuzika baba yake.

15 Wakati ndugu za Yosefu waliona kwamba baba yao amekufa, wakasema: “Pengine Yosefu anatuwekea chuki na pengine atatulipiza uovu wote wenye tulimutendea.”+ 16 Kwa hiyo wakatuma ujumbe huu kwa Yosefu: “Baba yako alitoa amri hii mbele akufe: 17 ‘Mutamuambia Yosefu hivi: “Tafazali, ninakuomba usamehe kosa la ndugu zako na zambi yenye walifanya kwa kukuumiza kwa namna hiyo.”’ Sasa, tafazali, usamehe kosa la watumishi wa Mungu wa baba yako.” Na Yosefu akalia wakati walizungumuza naye. 18 Kisha ndugu zake wakakuja na kuinama mbele yake na kusema: “Sisi hapa sasa tuko watumwa wako!”+ 19 Yosefu akawaambia: “Musiogope. Je, mimi niko pahali pa Mungu? 20 Hata kama mulitaka kuniumiza,+ Mungu alikuwa na nia ya kufanya mambo yageuke kuwa ya muzuri na kulinda uzima wa watu wengi, kama vile munaona leo.+ 21 Kwa hiyo sasa musiogope. Nitaendelea kuwapatia ninyi na watoto wenu chakula.”+ Hivyo akawafariji na akazungumuza nao kwa njia ya kuwatuliza.

22 Na Yosefu akaendelea kukaa Misri, yeye pamoja na watu wa nyumba ya baba yake, na Yosefu akaishi miaka mia moja na kumi (110). 23 Yosefu akaona kizazi cha tatu (3) cha wana wa Efraimu,+ pia wana wa Makiri,+ mwana wa Manase. Walizaliwa kwenye magoti ya Yosefu.* 24 Mwishowe Yosefu akaambia ndugu zake: “Niko karibu kufa, lakini Mungu hatakosa kuelekeza uangalifu wake juu yenu,+ na hakika atawatosha katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi yenye aliapia Abrahamu, Isaka, na Yakobo.”+ 25 Kwa hiyo Yosefu akaapisha wana wa Israeli, kwa kusema: “Mungu hatakosa kuelekeza uangalifu wake juu yenu. Munapaswa kutosha mifupa yangu hapa na kuenda nayo.”+ 26 Na Yosefu akakufa na miaka mia moja na kumi (110), na wakafanya mipango ili mwili wake upakaliwe dawa kusudi usioze,+ na akatiwa katika sanduku kule Misri.

Ao “maji yenye mawimbi makubwa.”

Ao “roho ya Mungu.”

Ao “nafsi zenye.”

Ao “nafsi zote zenye kutembea na kujaa katika maji kulingana na aina zake.”

Ao “nafsi zenye uzima kulingana na aina zake.”

Ao “wanyama wenye kutembea,” inaonekana ni kutia ndani wanyama wenye kutambaa na aina za wanyama wenye kuwa tofauti na aina zingine.

Ao “uzima wa nafsi; nafsi yenye uzima.”

Tnn., “jeshi lake lote.”

Andiko la kwanza kutaja jina la pekee la Mungu, יהוה (YHWH ). Angalia Nyongeza A4.

Ao “uso wa udongo.”

Ao “nafsi.” Kiebrania, neʹphesh, maana yake “kiumbe chenye kupumua.” Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “na kuwa vichwa ine.”

Ulimbo ni umajimaji wa muti wenye kukamatana ao kunata-nata.

Ao “Tigri.”

Ao “nafsi.”

Ao “ataendelea kukaa.”

Ao “mwenye kujihazari; mwerevu.”

Ao “chuki.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu yake.”

Ao “Atachubua; Atapiga.”

Ao “utamuchubua, utamuponda.”

Maana yake “Mutu wa Udongo; Binadamu; Mwanadamu.”

Ao “chakula.”

Maana yake “Mwenye Kuishi.”

Ao “mupaka wakati wenye hauna kipimo.”

Ao “nimetokeza.”

Tnn., “uso wake ukaanguka.”

Ao “hautainuliwa?”

Ao “eko.”

Tnn., “nguvu zake.”

Tnn., “kutoka kwenye uso wa udongo.”

Ao “inchi ya Nodi.”

Ao “filimbi.”

Maana yake “Mwenye Amechaguliwa; Mwenye Amewekwa.”

Tnn., “mbegu ingine.”

Ao “Adamu; Wanadamu.”

Tnn., “ule Mungu.” Angalia Maana ya Maneno.

Pengine maana yake ni “Pumuziko; Faraja.”

Huu ni usemi wa Kiebrania wenye kumaanisha wana wa Mungu ambao ni malaika.

Ao, “kwa sababu anatenda kulingana na mwili.”

Pengine maana yake ni “Waangushaji,” ni kusema, watu wenye kuangusha wengine chini. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “akahuzunika.”

Ao “akaumia katika moyo wake.”

Ao “bila lawama.”

Tnn., “vizazi vyake.”

Ao “kila mutu alikuwa ameharibu.”

Ao “goudron.”

Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.

Katika Kiebrania ni tsoʹhar. Wengine wanawaza kwamba tsoʹhar ni sehemu ya juu ya safina yenye kulala ao kupengama kwa kipimo cha mukono mumoja, kuliko kuwa tundu ao dirisha la kuingiza mwangaza.

Ao “roho ya uzima.”

Ao pengine, “wanyama 14 wakiwa wawili-wawili wa kila munyama mwenye kuwa safi.”

Ao pengine, “wanyama 14 wakiwa wawili-wawili wa viumbe vyenye kuruka vya anga.”

Ao “roho ya uzima.”

Ao “ikaendelea kuja.”

Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.

Ao “pumuzi ya roho ya uzima.”

Tnn., “akamukumbuka.”

Ao “ikazuiwa.”

Ao “pa kutia kikanyangio cha muguu wake.”

Ao “vijae.”

Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

Ao “Sitaita tena mabaya juu ya.”

Ao “wametiwa chini ya mamlaka yenu.”

Ao “nafsi yake.”

Ao “damu ya nafsi yenu.”

Ao “nafsi yenye uzima yenye.”

Ao “kitu chochote chenye uzima kitaharibiwa.”

Ao “nafsi yenye uzima yenye.”

Ao “kila nafsi yenye uzima ya miili yote.”

Ao “kila nafsi yenye uzima ya miili yote.”

Ao “Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa.”

Ao pengine, “na ndugu mukubwa wa Yafeti.”

Maana yake “Mugawanyiko.”

Ao “wakaaji wa dunia walikuwa wamegawanyika.”

Ao “mortier.”

Maana yake “Muvurugo.”

Ao “zitajipatia baraka.”

Ao “nafsi zenye.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “ili akae kule akiwa mugeni.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu yako ikuwe.”

Tnn., “mbegu yako itaweza.”

Ao “Eneo Tambarare la Chini.”

Ni kusema, Bahari Yenye Kufa.

Ao “Eneo Tambarare la Chini.”

Ao “Eneo Tambarare la Chini.”

Ao “mortier.”

Ao “washirika wa.”

Tnn., “ndugu.”

Ao “Eneo Tambarare la Chini.”

Ao “zile nafsi.”

Tnn., “mbegu yoyote.”

Tnn., “mwana.”

Tnn., “ule mwenye kutoka katika viuno vyako.”

Ao “mbegu yako itakuwa.”

Ao “akaweka kila kipande ili kilingane na kingine.”

Ao “mbegu yako itakuwa.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “eko.”

Tnn., “katika kifua chako.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “mbegu yako ikuwe mingi.”

Maana yake “Mungu Anasikia.”

Ao “aina fulani ya punda wa pori,” hata kama watu fulani wanawaza kwamba ni pundamilia (zèbre). Inawezekana maneno hayo yanazungumuzia mutazamo wa kujitegemea.

Ao pengine “naye atakaa katika uadui na ndugu zake wote.”

Maana yake “Kisima cha Mwenye Kuishi Mwenye Ananiona.”

Ao “hauna lawama.”

Maana yake “Baba Iko Juu (Ametukuzwa).”

Maana yake “Baba ya Watu Wengi; Baba ya Wengi.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu yako.”

Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.

Tnn., “mbegu yako.”

Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.

Ao “nafsi hiyo inapaswa.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Pengine maana yake ni “Mugomvi.”

Maana yake “Mwanamuke wa Kifalme.”

Maana yake “Kicheko.”

Tnn., “mbegu yake.”

Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.

Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.

Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.

Tnn., “mutie moyo wenu nguvu.”

Tnn., “Vipimo 3 vya sea.” Sea moja ilikuwa sawa na litre 7.33 (vibaba 6.66). Angalia Nyongeza B14.

Ao “eko.”

Ao “Eko.”

Tnn., “Kawaida ya wanamuke ilikuwa imeacha kwa ajili ya Sara.”

Ao “yatajipatia baraka.”

Tnn., “kivuli cha.”

Ni kusema, wakati mwangaza wa asubui ulianza kutokea.

Ao “nafsi yako.”

Ao “upendo mushikamanifu.”

Ao “nafsi yangu.”

Ao “nafsi yangu itaendelea kuishi.”

Maana yake “Udogo.”

Ao “anaishi akiwa mugeni.”

Ni kusema, alikuwa hajafanya ngono naye.

Ao “lenye haki.”

Ao “ataomba dua.”

Ao “kuomba dua kwa.”

Ao “alikuwa amefunga kabisa kila tumbo la uzazi la nyumba ya Abimeleki.”

Ao pengine, “atanicheka.”

Tnn., “Sikiliza sauti yake.”

Ao “mbegu yako itakuja.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Pengine maana yake “Kisima cha Kiapo” ao “Kisima cha Wale Saba.”

Ao “akaishi akiwa mugeni.”

Tnn., “siku nyingi.”

Ao “kisu cha kuchinjia.”

Ao “eko.”

Ao “kisu cha kuchinjia.”

Ao “kichaka.”

Maana yake “Yehova Atatoa; Yehova Ataishugulikia.”

Tnn., “mbegu yako ikuwe nyingi.”

Ao “mbegu yako itariti.”

Ao “miji ya.”

Tnn., “mbegu yako.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao pengine, “mukubwa zaidi.”

Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

Tnn., “mbegu yako.”

Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

Pengine ni Labani.

Ao “eko.”

Tnn., “kusudi nigeukie kwenye mukono wa kuume ao wa kushoto.”

Ao “Hatuwezi kukuambia jambo la mubaya ao la muzuri.”

Ni kusema, mulezi huyo alikuwa sasa mutumishi wake.

Ao “ukuwe mama ya maelfu ya makumi ya maelfu.”

Ao “mbegu yako iriti.”

Ao “miji ya.”

Ao “kutafakari.”

Angalia Maana ya Maneno.

Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.

Ao “kambi zao zenye kuzungukwa na kuta.”

Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.

Ao pengine, “Aliishi katika uadui na ndugu zake wote.”

Maana yake “Mwenye Nywele Nyingi Kwenye Mwili.”

Maana yake “Mwenye Kushika Kisigino; Mwenye Kukamata Nafasi ya Mwingine.”

Ao “unipatie kitu chekundu cha kumeza.”

Tnn., “chekundu, chekundu kile.”

Ao “niko na njaa sana.”

Maana yake “Chekundu.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “mbegu yako iongezeke.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “akimukumbatia.”

Ao “bonde la muto.”

Ao “bonde la muto.”

Maana yake “Ugomvi.”

Maana yake “Mashitaka.”

Maana yake “Nafasi Kubwa.”

Ao “mbegu yako iongezeke.”

Ao “eko.”

Tnn., “uchungu wa roho.”

Ao “nafsi yako inibariki.”

Ao “nafsi yangu itakubariki.”

Ao “nafsi yako inibariki.”

Maana yake “Mwenye Kushika Kisigino; Mwenye Kuchukua Nafasi ya Mwingine.”

Ao “anajifariji kwa kupanga kukuua.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “kipandio chenye.”

Ao “kipandio hicho.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “mbegu yako itakuwa.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “zitajipatia baraka.”

Ao “eko.”

Maana yake “Nyumba ya Mungu.”

Ao “Eko.”

Ao “Eko.”

Tnn., “ndugu.”

Ao “uko na uhusiano wa damu pamoja na mimi.”

Tnn., “ndugu.”

Tnn., “alikuwa anachukiwa.”

Tnn., “akafungua tumbo lake la uzazi.”

Maana yake “Angalia, Mwana!”

Maana yake “Kusikia.”

Maana yake “Kujiunga; Yenye Kushikamana.”

Maana yake “Mwenye Kusifiwa; Kitu cha Kusifiwa.”

Ao “amefunga tumbo lako la uzazi?”

Tnn., “azae kwenye magoti yangu.”

Maana yake “Muamuzi.”

Maana yake “Mieleka Yangu.”

Maana yake “Neema.”

Maana yake “Mwenye Furaha; Furaha.”

Ao “mushahara wa mutu mwenye alikodishwa.”

Maana yake “Yeye Ni Mushahara.”

Maana yake “Kuachilia.”

Tnn., “na Mungu akamusikiliza na kufungua tumbo lake la uzazi.”

Kifupi cha jina Yosifia, lenye maana yake ni “Yah Aongeze (Azidishe).”

Ao “kupitia mambo yenye kuwa hakika.”

Ao “unyoofu wangu utasema.”

Ao “miungu ya familia; sanamu.”

Ni kusema, Efrati.

Ao “watu wa jamaa yake.”

Ao “tari.”

Tnn., “wana.”

Tnn., “kwa woga wa Isaka.”

Neno la Kiaramu lenye maana yake ni “Rundo la Ushahidi.”

Neno la Kiebrania lenye maana yake ni “Rundo la Ushahidi.”

Tnn., “kwa woga wa Isaka baba yake.”

Tnn., “wana.”

Maana yake “Kambi Mbili.”

Tnn., “pori.”

Ao “Nimeishi kama mugeni.”

Ao “eko.”

Ao “mbegu yako itakuwa nyingi.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “bonde la muto.”

Ni kusema, wakati mwangaza wa asubui ulianza kutokea.

Ni kusema, mwangaza wa asubui umeanza kutokea.

Maana yake “Mwenye Kushindana (Mwenye Kuendelea Kufanya Jambo) na Mungu” ao “Mungu Anashindana.”

Maana yake “Uso wa Mungu.”

Ao “nafsi yangu ililindwa.”

Ao “Penieli.”

Ao “kwa kuchechemea.”

Tnn., “kamba ya mushipa wa paja.”

Maana yake “Vibanda.”

Ao “kuenda kuona.”

Ao “nafsi yake ikashikamana.”

Tnn., “alikuwa anasema kwenye moyo wa ule kijana mwanamuke.”

Ao “Nafsi ya mwana wangu Shekemu inashikamana na.”

Ao “na muoane.”

Tnn., “mwenye kuwa na govi.” Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.

Ao “kutengwa.”

Ao “katika njia.”

Ao “akaficha.”

Maana yake “Mungu wa Beteli.”

Maana yake “Muti wa Mwaloni wa Kilio.”

Tnn., “watatoka katika viuno vyako.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “nafsi yake ilikuwa inatoka.”

Maana yake “Mwana wa Maombolezo Yangu.”

Maana yake “Mwana wa Mukono wa Kuume.”

Angalia Maana ya Maneno.

Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.

Tnn., “akiwa amezeeka na kujaa siku.”

Ao “nafsi zote za.”

Ao “wanaishi ndani yake kama wageni.”

Angalia Maana ya Maneno.

Shehe alikuwa mukubwa wa kabila.

Tnn., “wana wa Israeli.”

Tnn., “shamba.”

Ao “nguo ya murefu yenye kupendeza.”

Ao “eneo tambarare la chini.”

Ao “Tusipige nafsi yake.”

Ao “musimuue.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ni kusema, Yuda.

Ao “shahawa zake.”

Ao “Eko.”

Maana yake “Mupasuko,” pengine inamaanisha kupasuka kwa musamba. Musamba ni sehemu ya katikati ya mwili yenye inaunganisha mapaja na kiwiliwili.

Tnn., “siku.”

Tnn., “atainua kichwa chako.”

Tnn., “tangi; shimo.”

Tnn., “akainua kichwa cha.”

Tnn., “tangi; shimo.”

Ao “Ni kuhusiana na ufalme tu.”

Inawezekana ni neno lenye linaamuru watu waonyeshe heshima kubwa.

Tnn., “kuinua mukono ao muguu wake.”

Ni kusema, Heliopolisi.

Ao “kutembea katika.”

Ao “alianza kutumikia.”

Ni kusema, Heliopolisi.”

Maana yake “Mwenye Kufanya Jambo Lisahauliwe; Mwenye Kufanya Mwingine Asahau.”

Maana yake “Kuzaa Mara Mbili.”

Ao “chakula.”

Ao “uzaifu wa.”

Ao “taabu ya nafsi yake.”

Ao “eko.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “eko.”

Ao “vyombo.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “nafsi yake mwenyewe imeshikamana.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “katika inchi.”

Tnn., “kama baba.”

Ao “mutaishi kwa kutegemea.”

Ao “unono wa.”

Ao “watu wote wenye walikuwa wake.”

Ni kusema, atayafunga wakati Yakobo atakufa.

Ao “Nafsi zote za watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke zilikuwa.”

Ao “nafsi.”

Ni kusema, Heliopolisi.

Ao “nafsi.”

Tnn., “Wana.”

Ao “nafsi.”

Ao “Nafsi zote zenye zilikuwa.”

Ao “nafsi mbili.”

Ao “nafsi zote za.”

Tnn., “akamuangukia kwenye shingo yake.”

Ao “akalia kwenye shingo yake tena na tena.”

Ao “kukaa kama mugeni.”

Ao “wanakaa kama wageni.”

Tnn., “mukate.”

Tnn., “mukate.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu yako.”

Ao “mbegu yake itakuwa nyingi.”

Ao “sehemu moja yenye muteremuko.” Tnn., “bega moja.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao pengine, “muelekeo wangu.”

Maana yake “Ule Mwenye Ni Yake; Ule Mwenye Ni Mali Yake.”

Ao “mashua za maji; bateaux.”

Nanga ni jiwe ao chuma chenye kufungwa kwa kamba ao kwa munyororo na kuingizwa ndani ya maji ili mashua isibebwe na maji.

Ao “Chakula cha Asheri kitakuwa kingi.”

Ni kusema, Yosefu.

Ao “eko.”

Tnn., “baraka za maziwa na tumbo la uzazi.”

Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.

Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.

Ao “watu wa nyumba.”

Maana yake “Maombolezo ya Wamisri.”

Ni kusema, walitendewa kama wana na walipendelewa sana.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine