Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • nwt Mambo ya Walawi 1:1-27:34
  • Mambo ya Walawi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo ya Walawi
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Mambo ya Walawi

MAMBO YA WALAWI

1 Na Yehova akamuita Musa na kusema naye kutoka katika hema ya mukutano,+ na kumuambia: 2 “Sema na Waisraeli* na uwaambie, ‘Ikiwa mutu yeyote kati yenu anataka kumutolea Yehova toleo kutoka kati ya wanyama wa kufugwa, munapaswa kumutolea toleo lenu kutoka katika mifugo na kundi.+

3 “‘Kama toleo lake ni toleo la kuteketezwa kutoka katika mifugo, anapaswa kutoa munyama dume mwenye hana kasoro.+ Anapaswa kumutoa kwa kupenda kwake mwenyewe+ mbele ya Yehova kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 4 Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha toleo hilo la kuteketezwa, na litakubaliwa kwa ajili yake ili kufunika zambi kwa ajili yake.

5 “‘Kisha ngombe-dume huyo mudogo atachinjwa mbele ya Yehova, na wana wa Haruni, makuhani,+ wataleta damu ya munyama huyo na kuinyunyiza* kwenye pande zote za mazabahu,+ yenye kuwa kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 6 Toleo la kuteketezwa linapaswa kuondolewa ngozi na kukatwa vipande-vipande.+ 7 Wana wa Haruni, makuhani, wanapaswa kuweka moto kwenye mazabahu+ na kupanga kuni kwenye moto huo. 8 Wana wa Haruni, makuhani, watapanga vile vipande vya toleo+ pamoja na kichwa na mafuta* juu ya kuni zenye kuwa kwenye moto wa mazabahu. 9 Matumbotumbo na miguu yake itasafishwa na maji, na kuhani atachoma vitu hivyo vyote ili vitoe moshi juu ya mazabahu vikiwa toleo la kuteketezwa, toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye harufu ya kumupendeza* Yehova.+

10 “‘Kama munyama mwenye anatoa kwa ajili ya toleo la kuteketezwa anatoka katika kundi,+ kati ya wana-kondoo dume ao mbuzi, anapaswa kutoa dume mwenye hana kasoro.+ 11 Atachinjwa kwenye upande wa kaskazini wa mazabahu mbele ya Yehova, na wana wa Haruni, makuhani, watanyunyiza* damu yake kwenye pande zote za mazabahu.+ 12 Atamukata vipande-vipande, na kuhani atapanga vipande vyake pamoja na kichwa chake na mafuta yake* juu ya kuni zenye kuwa kwenye moto wa mazabahu. 13 Atasafisha matumbotumbo na miguu yake kwa maji, na kuhani atavileta vyote na kuvichoma ili vitoe moshi juu ya mazabahu. Ni toleo la kuteketezwa, toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye harufu ya kumupendeza* Yehova.

14 “‘Lakini, kama anatoa ndege kuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya Yehova, atatoa toleo lake kutoka kati ya njiwa-tetere ao njiwa wadogo.+ 15 Kuhani atamutoa juu ya mazabahu na atamuvunja shingo na kuacha kichwa kikininginia na atamuchoma ili atoe moshi kwenye mazabahu, lakini damu yake itamwangwa pembeni ya mazabahu. 16 Atatosha kifuko cha chakula chenye kuwa katika koo yake pamoja na manyoya yake na kutupa vitu hivyo karibu na mazabahu, upande wa mashariki, mahali pa kuweka majivu.*+ 17 Atamupasua kwenye mabawa yake bila kumukata vipande mbili. Kisha kuhani atamuchoma ili atoe moshi kwenye mazabahu juu ya kuni zenye kuwa juu ya moto. Ni toleo la kuteketezwa, toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye harufu ya kumupendeza* Yehova.

2 “‘Sasa kama mutu anamutolea Yehova toleo la nafaka,+ toleo lake linapaswa kuwa unga muzuri, na anapaswa kumwanga mafuta juu yake na kutia ubani juu yake.+ 2 Kisha atalipeleka kwa wana wa Haruni, makuhani, na kuhani atakamata mukono mumoja wa unga huo muzuri na mafuta na ubani wake wote, na atauchoma ili utoe moshi juu ya mazabahu ukiwa toleo la kumbukumbu,+ toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye harufu ya kumupendeza* Yehova. 3 Nafaka yoyote yenye inabakia ya toleo la nafaka itakuwa ya Haruni na wana wake,+ ni kitu kitakatifu sana+ kutoka katika matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto.

4 “‘Kama mutu anatoa toleo la nafaka lenye limepikwa katika jiko, linapaswa kuwa la unga muzuri, mikate ya muviringo yenye haina chachu na yenye kuchanganywa na mafuta ao mikate myembamba yenye haina chachu yenye imepakwa mafuta.+

5 “‘Kama toleo lako ni toleo la nafaka kutoka kwenye kikaangio,+ linapaswa kuwa unga muzuri wenye hauna chachu, wenye ulichanganywa na mafuta. 6 Litavunjwa vipande-vipande, na utamwanga mafuta juu yake.+ Ni toleo la nafaka.

7 “‘Kama toleo lako ni toleo la nafaka lenye lilipikwa ndani ya chungu ya kukaangia, linapaswa kufanywa kwa unga muzuri pamoja na mafuta. 8 Utamuletea Yehova toleo la nafaka lenye lilitengenezwa na vitu hivyo, na litapelekwa kwa kuhani, naye atalipeleka karibu na mazabahu. 9 Na kuhani atakamata sehemu fulani ya toleo hilo la nafaka kama toleo la kumbukumbu+ na kulichoma ili litoe moshi juu ya mazabahu. Ni toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye harufu ya kumupendeza* Yehova.+ 10 Nafaka yoyote yenye kubakia ya toleo la nafaka ni ya Haruni na wana wake, ni kitu kitakatifu sana kutoka katika matoleo ya Yehova yenye kutolewa kwa njia ya moto.+

11 “‘Toleo lolote la nafaka lenye munamutolea Yehova halipaswe kuwa na chachu,+ kwa maana hamupaswe kuchoma chachu ao asali ili itoe moshi ikiwa toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.

12 “‘Munaweza kumutolea Yehova vitu hivyo vikiwa matunda ya kwanza,+ lakini havipaswe kuletwa kwenye mazabahu vikiwa harufu ya muzuri.*

13 “‘Kila toleo la nafaka lenye unatoa linapaswa kukolezwa na chumvi; na haupaswe kukubali chumvi ya agano la Mungu ikosekane katika toleo lako la nafaka. Kila toleo lenye unatoa, utalitoa pamoja na chumvi.+

14 “‘Kama unamutolea Yehova toleo la nafaka la matunda ya kwanza yenye kukomaa, utatoa nafaka mupya* yenye kukaangwa kwa moto, chenga-chenga za nafaka mupya zenye zilipondwa, kuwa toleo la nafaka la matunda yako ya kwanza yenye kukomaa.+ 15 Utatia mafuta juu yake na kuweka ubani juu yake. Ni toleo la nafaka. 16 Kuhani atalichoma kama toleo la kumbukumbu ili litoe moshi,+ ni kusema, sehemu fulani ya chenga-chenga za nafaka pamoja na mafuta na ubani wake wote. Ni toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.

3 “‘Kama toleo lake ni zabihu ya ushirika*+ na kama linatoka katika mifugo, ikuwe munyama dume ao dike, anapaswa kumutolea Yehova munyama mwenye hana kasoro. 2 Anapaswa kuweka mukono wake juu ya kichwa cha toleo lake, na litachinjwa kwenye muingilio wa hema ya mukutano; na wana wa Haruni, makuhani, watanyunyiza* damu yake kwenye pande zote za mazabahu. 3 Atatoa sehemu ya zabihu hiyo ya ushirika kuwa toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto:+ mafuta+ yenye kufunika matumbotumbo, mafuta yote yenye kuzunguka matumbotumbo, 4 na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yenye kuwa karibu na viuno. Ataondoa pia mafuta yenye kuwa juu ya maini pamoja na figo.+ 5 Wana wa Haruni watachoma vitu hivyo ili vitoe moshi kwenye mazabahu juu ya toleo la kuteketezwa lenye kuwa juu ya kuni zenye kuwa juu ya moto;+ ni toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye harufu ya kumupendeza* Yehova.+

6 “‘Kama toleo lenye anamutolea Yehova kuwa zabihu ya ushirika linatoka katika kundi, atatoa munyama dume ao dike mwenye hana kasoro.+ 7 Kama anatoa kondoo-dume mudogo kuwa toleo lake, basi atamutoa mbele ya Yehova. 8 Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha toleo lake, na litachinjwa mbele ya hema ya mukutano. Wana wa Haruni, makuhani, watanyunyiza* damu yake kwenye pande zote za mazabahu. 9 Atatoa mafuta kutoka katika zabihu ya ushirika ili kuwa toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+ Ataondoa mukia wote wenye mafuta karibu na uti wa mugongo, mafuta yenye kufunika matumbotumbo, mafuta yote yenye kuzunguka matumbotumbo, 10 na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yenye kuwa karibu na viuno. Ataondoa pia mafuta yenye kuwa juu ya maini pamoja na figo.+ 11 Na kuhani atachoma vitu hivyo ili vitoe moshi juu ya mazabahu kama chakula,* ni toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+

12 “‘Kama toleo lake ni mbuzi, basi atamutoa mbele ya Yehova. 13 Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha mbuzi huyo, na atachinjwa mbele ya hema ya mukutano, na wana wa Haruni watanyunyiza* damu yake kwenye pande zote za mazabahu. 14 Sehemu yenye atamutolea Yehova kwa njia ya moto ni mafuta yenye kufunika matumbotumbo, mafuta yote yenye kuzunguka matumbotumbo,+ 15 na figo zake mbili na mafuta yake yenye kuwa karibu na viuno. Atatoa pia mafuta yenye kuwa juu ya maini pamoja na figo. 16 Kuhani atachoma vitu hivyo ili vitoe moshi juu ya mazabahu kama chakula,* ni toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye harufu ya muzuri.* Mafuta yote ni ya Yehova.+

17 “‘Ni sheria ya kudumu kwa ajili ya vizazi vyenu, katika makao yenu yote: Hamupaswe kula mafuta yoyote wala damu yoyote.’”+

4 Yehova akaendelea kumuambia Musa: 2 “Ambia Waisraeli, ‘Kama mutu anatenda zambi bila kukusudia+ kwa kufanya jambo lolote kati ya mambo yenye Yehova ameamuru kwamba hayapaswe kufanywa:

3 “‘Kama kuhani mwenye kutiwa mafuta+ anafanya zambi+ na kuleta hatia juu ya watu, basi anapaswa kumutolea Yehova ngombe-dume mudogo mwenye hana kasoro kuwa toleo la zambi kwa ajili ya zambi yenye alifanya.+ 4 Ataleta ngombe-dume huyo kwenye muingilio wa hema ya mukutano+ mbele ya Yehova na kuweka mukono wake juu ya kichwa cha ngombe-dume huyo, na atachinja ngombe-dume huyo mbele ya Yehova.+ 5 Kisha kuhani mwenye kutiwa mafuta+ atakamata sehemu fulani ya damu ya ngombe-dume huyo na kuileta ndani ya hema ya mukutano; 6 na kuhani ataingiza kidole chake ndani ya damu hiyo+ na kunyunyiza* sehemu fulani ya damu hiyo mara saba (7)+ mbele ya Yehova, mbele ya pazia la mahali patakatifu. 7 Pia, kuhani atatia sehemu fulani ya damu hiyo kwenye pembe za mazabahu ya uvumba wenye marashi,+ mazabahu yenye kuwa mbele ya Yehova katika hema ya mukutano; na atamwanga damu yote yenye ilibakia ya ngombe-dume huyo kwenye musingi wa mazabahu ya toleo la kuteketezwa,+ yenye kuwa kwenye muingilio wa hema ya mukutano.

8 “‘Kisha ataondoa mafuta yote ya ngombe-dume huyo wa toleo la zambi, na pia mafuta yenye kufunika matumbotumbo na mafuta yenye kuzunguka matumbotumbo, 9 na figo mbili pamoja na mafuta yake yenye kuwa karibu na viuno. Na ataondoa mafuta yenye kuwa juu ya maini pamoja na figo.+ 10 Zitakuwa sehemu zilezile zenye zinaondolewa kwenye ngombe-dume wa zabihu ya ushirika.+ Na kuhani atazichoma ili zitoe moshi juu ya mazabahu ya toleo la kuteketezwa.

11 “‘Lakini ngozi ya ngombe-dume huyo na nyama yake yote pamoja na kichwa chake, miguu yake, matumbotumbo yake, na mavi yake+⁠— 12 sehemu zote zenye kubakia za ngombe-dume huyo⁠—​atafanya zipelekwe mahali safi sehemu za pembeni-pembeni ya kambi, mahali kwenye majivu* yanatupwa, na ataziteketeza kwa moto juu ya kuni.+ Zinapaswa kuteketezwa kwa moto mahali kwenye majivu yanatupwa.

13 “‘Sasa kama mukusanyiko wote wa Israeli umekuwa na hatia kwa kufanya zambi bila kukusudia,+ lakini kutaniko halikujua kwamba walikuwa wamefanya jambo lenye Yehova aliwaamuru wasifanye,+ 14 na sasa zambi hiyo inajulikana, kutaniko linapaswa kutoa ngombe-dume mudogo kwa ajili ya toleo la zambi na kumuleta mbele ya hema ya mukutano. 15 Wazee wa mukusanyiko wataweka mikono yao juu ya kichwa cha ngombe-dume huyo mbele ya Yehova, na ngombe-dume huyo atachinjwa mbele ya Yehova.

16 “‘Kisha kuhani mwenye kutiwa mafuta ataleta sehemu fulani ya damu ya ngombe-dume huyo katika hema ya mukutano. 17 Na kuhani ataingiza kidole chake ndani ya damu hiyo na kunyunyiza* sehemu fulani ya damu hiyo mara saba (7) mbele ya Yehova, mbele ya pazia.+ 18 Kisha atatia sehemu fulani ya damu hiyo kwenye pembe za mazabahu+ yenye kuwa mbele ya Yehova, katika hema ya mukutano; na damu yote yenye ilibakia ataimwanga kwenye musingi wa mazabahu ya toleo la kuteketezwa, yenye kuwa kwenye muingilio wa hema ya mukutano.+ 19 Ataondoa mafuta yake yote na kuyachoma ili yatoe moshi juu ya mazabahu.+ 20 Atamufanya ngombe-dume huyo kama vile alimufanya ule ngombe-dume wa toleo la zambi. Ni vile atamufanya, na kuhani atafunika zambi kwa ajili yao,+ nao watasamehewa. 21 Atafanya ngombe-dume huyo apelekwe sehemu za pembeni-pembeni ya kambi na kumuteketeza kwa moto kama vile aliteketeza kwa moto ngombe-dume wa kwanza.+ Ni toleo la zambi kwa ajili ya kutaniko.+

22 “‘Wakati mukubwa+ anatenda zambi bila kukusudia kwa kufanya moja kati ya mambo yenye Yehova Mungu wake ameamuru kwamba hayapaswe kufanywa na anakuwa na hatia, 23 ao kama amefikia kujua zambi yenye alitenda kinyume cha amri, basi anapaswa kuleta mwana-mbuzi dume mwenye hana kasoro kuwa toleo lake. 24 Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha mwana-mbuzi huyo na kumuchinjia mahali kwenye toleo la kuteketezwa linachinjwa mbele ya Yehova.+ Ni toleo la zambi. 25 Kuhani atakamata kwa kidole chake sehemu fulani ya damu ya toleo la zambi na kuitia kwenye pembe+ za mazabahu ya toleo la kuteketezwa, na damu yenye inabakia ya mwana-mbuzi huyo ataimwanga kwenye musingi wa mazabahu ya toleo la kuteketezwa.+ 26 Atachoma mafuta yake yote ili yatoe moshi juu ya mazabahu kama vile yale mafuta ya zabihu ya ushirika;+ na kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mutu huyo, na atasamehewa zambi hiyo.

27 “‘Kama mutu yeyote katikati ya watu wa inchi anatenda zambi bila kukusudia na kuwa na hatia kwa kufanya moja kati ya mambo yenye Yehova anaamuru kwamba hayapaswe kufanywa,+ 28 ao kama amefikia kujua zambi yenye ametenda, basi anapaswa kuleta mwana-mbuzi dike mwenye hana kasoro kuwa toleo lake kwa ajili ya zambi yenye ametenda. 29 Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha toleo la zambi na kuchinja toleo la zambi mahali palepale kuwa toleo la kuteketezwa.+ 30 Kuhani atakamata kwa kidole chake sehemu fulani ya damu ya munyama huyo na kuitia kwenye pembe za mazabahu ya toleo la kuteketezwa, na damu yote yenye inabakia ataimwanga kwenye musingi wa mazabahu.+ 31 Ataondoa mafuta yake yote,+ kama vile mafuta yanaondolewa katika munyama wa zabihu ya ushirika,+ na kuhani atayachoma ili yatoe moshi juu ya mazabahu yakiwa harufu ya kumupendeza* Yehova; na kuhani atafunika zambi kwa ajili yake, na atasamehewa.

32 “‘Lakini kama anatoa mwana-kondoo kuwa toleo lake la zambi, anapaswa kuleta mwana-kondoo dike mwenye hana kasoro. 33 Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha toleo la zambi na kumuchinja kuwa toleo la zambi katika mahali kwenye toleo la kuteketezwa linachinjwa.+ 34 Kuhani atakamata kwa kidole chake sehemu fulani ya damu ya munyama huyo wa toleo la zambi na kuitia kwenye pembe za mazabahu ya toleo la kuteketezwa,+ na damu yote yenye inabakia ataimwanga kwenye musingi wa mazabahu. 35 Ataondoa mafuta yake yote kama vile mafuta ya mwana-kondoo dume wa zabihu ya ushirika yanaondolewa, na kuhani atayachoma ili yatoe moshi kwenye mazabahu juu ya matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto;+ na kuhani atafunika zambi kwa ajili yake kwa sababu ya zambi yenye ametenda, na atasamehewa.+

5 “‘Kama mutu* anafanya zambi kwa sababu amesikia mwito wa waziwazi wa kutoa ushahidi*+ naye ni shahidi ao amejionea ao amepata kujua kuhusu jambo hilo, lakini hatoe habari, basi atajibu kwa sababu ya kosa lake.

2 “‘Ao wakati mutu anagusa kitu chochote chenye hakiko safi, ikuwe muzoga wa munyama wa pori, muzoga wa munyama wa kufugwa, ao kiumbe chenye hakiko safi chenye kupatikana kwa wingi,+ mutu huyo haiko safi na amekuwa na hatia hata kama hatambue jambo hilo. 3 Ao kama mutu anagusa uchafu wa mwanadamu bila kujua+⁠—​kitu chochote chenye hakiko safi ambacho kinaweza kumufanya asikuwe safi⁠—​na anafikia kujua jambo hilo, basi amekuwa na hatia.

4 “‘Ao kama mutu* anaapa bila kufikiri kwamba atafanya jambo fulani⁠—​ikuwe kufanya jambo la muzuri ao kufanya jambo la mubaya, hata likuwe jambo gani⁠—​na hakukuwa anajua vile, lakini kisha anatambua kwamba ameapa bila kufikiri, amekuwa na hatia.*+

5 “‘Kama anafikia kuwa na hatia katika moja kati ya mambo hayo, basi anapaswa kuungama+ namna gani amefanya zambi. 6 Pia atamuletea Yehova toleo la hatia kwa ajili ya zambi yenye alifanya,+ ni kusema, munyama dike kutoka katika kundi, mwana-kondoo dike ao mwana-mbuzi dike, kwa ajili ya toleo la zambi. Kisha kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mutu huyo.

7 “‘Lakini, kama hana uwezo wa kupata kondoo, atamuletea Yehova njiwa-tetere wawili ao njiwa wawili wadogo+ kuwa toleo lake la hatia kwa ajili ya zambi yake, ndege mumoja kwa ajili ya toleo la zambi na ndege mwingine kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.+ 8 Atawaleta kwa kuhani, na kuhani atatoa ndege mumoja kwanza kwa ajili ya toleo la zambi na atamuvunja shingo na kuacha kichwa kikininginia, lakini asikikate kabisa. 9 Atanyunyiza* sehemu fulani ya damu ya toleo hilo la zambi pembeni ya mazabahu, lakini damu yenye kubakia itamwangwa kwenye musingi wa mazabahu.+ Ni toleo la zambi. 10 Atamutoa ule ndege mwingine kuwa toleo la kuteketezwa kulingana na utaratibu wa kawaida;+ na kuhani atafunika zambi kwa ajili yake kwa sababu ya zambi yenye amefanya, naye atasamehewa.+

11 “‘Sasa kama hana uwezo wa kupata njiwa-tetere wawili ao njiwa wawili wadogo, atatoa sehemu moja ya kumi (1/10) ya kipimo cha efa moja*+ ya unga muzuri ili kuwa toleo la zambi. Hapaswe kuongeza mafuta ao kutia ubani juu ya unga huo kwa sababu ni toleo la zambi. 12 Atauleta kwa kuhani, na kuhani atakamata mukono mumoja wa unga huo kuwa toleo la kumbukumbu na atauchoma ili utoe moshi kwenye mazabahu juu ya matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto. Ni toleo la zambi. 13 Kuhani atafunika zambi kwa ajili yake kwa sababu ya zambi yenye ametenda, yoyote kati ya zambi hizo, naye atasamehewa.+ Sehemu yenye kubakia ya toleo hilo itakuwa ya kuhani,+ kama vile toleo la nafaka.’”+

14 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 15 “Kama mutu anajiendesha kwa njia ya kukosa uaminifu kwa kutenda zambi bila kukusudia kwa kuvunja sheria kuhusu vitu vitakatifu vya Yehova,+ atamuletea Yehova kondoo-dume mwenye hana kasoro kutoka katika kundi ili akuwe toleo la hatia;+ samani yake itapimwa kwa shekeli* za feza kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.*+ 16 Na atalipia zambi yenye ametendea mahali patakatifu, na pia ataongeza sehemu moja ya tano (1/5) ya samani ya vitu hivyo.+ Atamupatia kuhani, ili kuhani afunike zambi+ kwa ajili yake kupitia ule kondoo-dume wa toleo la hatia, naye atasamehewa.+

17 “Kama mutu anatenda* zambi kwa kufanya moja kati ya mambo yenye Yehova ameamuru kwamba hayapaswe kufanywa, hata kama hajue jambo hilo, iko* tu na hatia na atajibu kwa sababu ya kosa lake.+ 18 Atamuletea kuhani kondoo-dume mwenye hana kasoro kutoka katika kundi kulingana na samani yenye ilikadiriwa, kwa ajili ya toleo la hatia.+ Kisha kuhani atafunika zambi kwa ajili yake kwa sababu ya kosa la bila kukusudia lenye alifanya bila kujua, naye atasamehewa. 19 Ni toleo la hatia. Hakika amekuwa na hatia ya kutenda zambi juu ya Yehova.”

6 Yehova akaendelea kumuambia Musa: 2 “Kama mutu anatenda* zambi na anajiendesha kwa njia ya kukosa uaminifu kwa Yehova+ kwa kumudanganya jirani yake kuhusu kitu fulani chenye alipewa ili akichunge,+ ao kitu fulani chenye aliachiwa katika mukono wake, ao akimwiba ao kumupunja jirani yake, 3 ao anapata kitu chenye kilipotea na anadanganya kuhusu kitu hicho, na kama anaapa kwa uongo kuhusu zambi yoyote kama hiyo yenye anaweza kutenda,+ anapaswa kufanya hivi: 4 Kama ametenda zambi na iko* na hatia, anapaswa kurudisha kitu chenye aliiba, kitu chenye alinyanganya, kitu chenye alikamata kwa kupunja, kitu chenye alipewa ili akichunge, ao kitu chenye kilipotea chenye alipata, 5 ao kitu chochote chenye aliapia kwa uongo, na anapaswa kutoa malipo kamili kwa ajili ya kitu hicho,+ na kuongeza juu yake sehemu moja ya tano ya samani ya kitu hicho. Atapatia mwenye kitu hicho ile sehemu moja ya tano (1/5) siku yenye hatia yake itahakikishwa. 6 Na atamuletea kuhani kondoo-dume mwenye hana kasoro kuwa toleo lake la hatia kwa Yehova kutoka katika kundi kulingana na samani yenye ilikadiriwa, kwa ajili ya toleo la hatia.+ 7 Kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mutu huyo mbele ya Yehova, na mutu huyo atasamehewa kosa lolote lenye pengine alifanya na hivyo akakuwa na hatia.”+

8 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 9 “Amuru Haruni na wana wake na kusema, ‘Hii ndiyo sheria kuhusu toleo la kuteketezwa:+ Toleo la kuteketezwa litabakia kwenye moto juu ya mazabahu usiku wote mupaka asubui, na moto utaendelea kuwashwa kwenye mazabahu ili usizimike. 10 Kuhani atavaa nguo yake ya ukuhani ya kitani,+ na atavaa kapitula* ya kitani+ kwenye mwili wake. Kisha ataondoa majivu*+ ya toleo la kuteketezwa yenye moto ulikuwa umeteketeza juu ya mazabahu na kuyaweka pembeni ya mazabahu. 11 Kisha atatosha nguo zake+ na kuvaa nguo zingine, na atapeleka majivu hayo mahali safi inje ya kambi.+ 12 Moto utaendelea kuwaka juu ya mazabahu. Haupaswe kuzimika. Kila asubui kuhani atateketeza kuni+ kwenye moto huo na kupanga toleo la kuteketezwa juu yake, na atachoma mafuta ya zabihu za ushirika ili yatoe moshi juu ya moto huo.+ 13 Moto utaendelea kuwaka kila wakati juu ya mazabahu. Haupaswe kuzimika.

14 “‘Sasa hii ndiyo sheria kuhusu toleo la nafaka:+ Ninyi wana wa Haruni mutamutolea Yehova toleo hilo mbele ya mazabahu. 15 Mumoja wao atakamata mukono mumoja wa huo unga muzuri wa toleo la nafaka na sehemu fulani ya mafuta yake na ubani wote wenye kuwa juu ya toleo hilo la nafaka, na atauchoma ili utoe moshi juu ya mazabahu kama harufu ya muzuri* ya toleo la kumbukumbu kwa Yehova.+ 16 Haruni na wana wake watakula unga wenye utabakia.+ Unga huo utatengenezwa kuwa mikate yenye haina chachu na itakuliwa katika mahali patakatifu. Wataikula katika kiwanja cha hema ya mukutano.+ 17 Hautapikwa pamoja na kitu chochote chenye kuwa na chachu.+ Nimeutoa huo kuwa fungu lao kutoka katikati ya matoleo yangu yenye yanatolewa kwa njia ya moto.+ Ni kitu kitakatifu sana,+ kama lile toleo la zambi na kama lile toleo la hatia. 18 Kila mwanaume kati ya wana wa Haruni atakula unga huo.+ Ni posho lao la kudumu katika vizazi vyenu vyote kutoka katikati ya matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto.+ Kila kitu chenye kinagusa matoleo hayo kitakuwa kitakatifu.’”

19 Yehova akasema tena na Musa: 20 “Hili ni toleo lenye Haruni na wana wake watamutolea Yehova siku yenye Haruni atatiwa mafuta:+ sehemu moja ya kumi (1/10) ya kipimo cha efa* moja+ ya unga muzuri kuwa toleo la nafaka lenye linatolewa kwa ukawaida,+ nusu ya unga huo asubui na nusu ya unga huo mangaribi. 21 Utachanganywa na mafuta na kupikwa kwenye kikaangio.+ Mutauchanganya muzuri na mafuta na kuuleta ukiwa vipande-vipande vyenye vimepikwa vya toleo la nafaka lenye harufu ya kumupendeza* Yehova. 22 Kuhani mwenye kutiwa mafuta mwenye atakamata nafasi ya Haruni kutoka kati ya wana wake+ atatoa toleo hilo. Ni sharti la kudumu: Litachomwa likiwa toleo nzima ili litoe moshi mbele ya Yehova. 23 Kila toleo la nafaka la kuhani linapaswa kuwa toleo nzima. Halipaswe kukuliwa.”

24 Yehova akasema tena na Musa na kumuambia: 25 “Sema na Haruni na wana wake: ‘Hii ni sheria kuhusu toleo la zambi:+ Toleo la zambi litachinjiwa+ pia mahali kwenye toleo la kuteketezwa linachinjwa mbele ya Yehova. Ni kitu kitakatifu sana. 26 Kuhani mwenye anatoa munyama huyo kwa ajili ya zambi atamukula.+ Atakuliwa katika mahali patakatifu, katika kiwanja cha hema ya mukutano.+

27 “‘Kila kitu chenye kinagusa nyama ya munyama huyo kitakuwa kitakatifu, na kama mutu ananyunyiza* sehemu fulani ya damu ya munyama huyo kwenye nguo yake, mutafulia katika mahali patakatifu kitu chenye damu imenyunyizwa* juu yake. 28 Chombo cha udongo chenye nyama hiyo ilitokoteshwa ndani yake kitavunjwa-vunjwa. Lakini kama ilitokoteshwa katika chombo cha shaba, basi chombo hicho kitaparuzwa na kusafishwa na maji.

29 “‘Kila mwanaume kati ya makuhani ataikula.+ Ni kitu kitakatifu sana.+ 30 Lakini, toleo lolote la zambi halitakuliwa kama sehemu fulani ya damu ya toleo hilo imeletwa katika hema ya mukutano ili kufunika zambi katika mahali patakatifu.+ Litateketezwa kwa moto.

7 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu toleo la hatia:+ Ni kitu kitakatifu sana. 2 Toleo la hatia litachinjwa mahali kwenye matoleo ya kuteketezwa yanachinjwa, na damu yake+ itanyunyizwa* kwenye pande zote za mazabahu.+ 3 Atatoa mafuta yote ya munyama huyo,+ pamoja na mukia wake wenye mafuta, mafuta yenye kufunika matumbotumbo, 4 na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yenye kuwa karibu na viuno. Ataondoa pia mafuta yenye kuwa juu ya maini pamoja na figo.+ 5 Kuhani atavichoma ili vitoe moshi juu ya mazabahu vikiwa toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+ Ni toleo la hatia. 6 Kila mwanaume kati ya makuhani atakula toleo hilo,+ na linapaswa kukuliwa katika mahali patakatifu. Ni toleo takatifu sana.+ 7 Sheria kuhusu toleo la zambi inatumika pia kuhusu toleo la hatia; toleo hilo ni la kuhani mwenye anafunika zambi kupitia toleo hilo.+

8 “‘Wakati kuhani anatoa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya mutu fulani, ngozi+ ya toleo la kuteketezwa lenye waliletea kuhani itakuwa yake.

9 “‘Kila toleo la nafaka lenye linapikwa katika jiko ao kupikwa ndani ya chungu ao kwenye kikaangio+ ni la kuhani mwenye analitoa. Litakuwa lake.+ 10 Lakini kila toleo la nafaka lenye linachanganywa na mafuta+ ao lenye kukauka+ litakuwa la wana wote wa Haruni; kila mumoja wao atapokea fungu sawasawa.

11 “‘Sasa hii ni sheria ya zabihu ya ushirika+ yenye mutu anaweza kumutolea Yehova: 12 Kama anaitoa ili kuonyesha shukrani,+ atatoa zabihu hiyo ya shukrani pamoja na mikate ya muviringo yenye haina chachu yenye imechanganywa na mafuta, mikate myembamba yenye haina chachu yenye imepakwa mafuta, na mikate ya muviringo yenye imetengenezwa na unga muzuri, wenye umechanganywa muzuri kabisa na kutiwa mafuta. 13 Atatoa toleo lake pamoja na mikate ya muviringo yenye iko na chachu na zabihu ya shukrani ya zabihu zake za ushirika. 14 Atatoa mukate mumoja kutoka katika kila toleo kuwa fungu takatifu kwa Yehova; litakuwa la kuhani mwenye ananyunyiza* damu ya zabihu za ushirika.+ 15 Nyama ya zabihu ya shukrani ya zabihu zake za ushirika inapaswa kukuliwa siku yenye anatoa zabihu yake ya shukrani. Hapaswe kuweka nyama yoyote ya zabihu hiyo mupaka asubui.+

16 “‘Kama zabihu ya toleo lake ni naziri+ ao ni toleo la kujipendea,+ inapaswa kukuliwa siku yenye anatoa zabihu yake, na sehemu yenye ilibakia ya zabihu hiyo inaweza pia kukuliwa siku yenye inafuata. 17 Lakini nyama yoyote ya zabihu hiyo yenye itabakia mupaka siku ya tatu inapaswa kuteketezwa kwa moto.+ 18 Hata hivyo, kama nyama yoyote ya zabihu yake ya ushirika inakuliwa siku ya tatu (3), ule mwenye anaitoa hatakubaliwa. Haitamuletea faida yoyote; ni kitu chenye kuchukiza, na mutu mwenye atakula sehemu fulani ya zabihu hiyo atajibu* kwa sababu ya kosa lake.+ 19 Nyama yenye inagusa kitu chochote chenye hakiko safi haipaswe kukuliwa. Inapaswa kuteketezwa kwa moto. Kila mutu mwenye kuwa safi anaweza kula nyama yenye kuwa safi.

20 “‘Lakini mutu yeyote mwenye haiko safi na anakula nyama ya zabihu ya ushirika, yenye kuwa ya Yehova, mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katikati ya watu wake.+ 21 Kama mutu anagusa* kitu chochote chenye hakiko safi, ikuwe uchafu wa mwanadamu+ ao munyama mwenye haiko safi+ ao kitu chochote chenye kuchukiza chenye hakiko safi,+ na anakula sehemu fulani ya nyama ya zabihu ya ushirika, yenye kuwa ya Yehova, mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katikati ya watu wake.’”

22 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 23 “Sema na Waisraeli, ‘Hamupaswe kula mafuta yoyote+ ya ngombe-dume ao ya mwana-kondoo dume ao ya mbuzi. 24 Mafuta ya munyama mwenye alipatikana amekufa na mafuta ya munyama mwenye aliuawa na munyama mwingine yanaweza kutumiwa kwa kusudi lingine lolote, lakini hamupaswe kuyakula hata kidogo.+ 25 Kwa maana mutu yeyote mwenye anakula mafuta ya munyama mwenye anatoa kuwa toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto anapaswa kuondolewa* katikati ya watu wake.

26 “‘Hamupaswe kula damu yoyote+ kila mahali kwenye munaishi, ikuwe damu ya ndege ao ya wanyama. 27 Mutu yeyote mwenye anakula damu yoyote anapaswa* kuondolewa*+ katikati ya watu wake.”

28 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 29 “Sema na Waisraeli, ‘Mutu yeyote mwenye anamuletea Yehova zabihu yake ya ushirika atamuletea Yehova sehemu ya toleo hilo kutoka katika zabihu yake ya ushirika.+ 30 Ataleta katika mikono yake mwenyewe mafuta+ pamoja na kifua kuwa toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, na atatikisa toleo hilo mbele na nyuma likiwa toleo la kutikiswa+ mbele ya Yehova. 31 Kuhani atachoma mafuta hayo ili yatoe moshi juu ya mazabahu,+ lakini kifua kitakuwa cha Haruni na wana wake.+

32 “‘Mutamupatia kuhani muguu wa kuume ukiwa fungu takatifu kutoka katika zabihu zenu za ushirika.+ 33 Muguu wa kuume utakuwa fungu la mwana wa Haruni mwenye atatoa damu ya zabihu za ushirika na mafuta.+ 34 Kwa maana ninakamata kifua cha toleo la kutikiswa na muguu wa lile fungu takatifu kutoka katikati ya zabihu za ushirika za Waisraeli, na ninapatia vitu hivyo Haruni kuhani na wana wake. Ni sharti la kudumu kwa Waisraeli.+

35 “‘Hilo lilikuwa fungu kutoka katika matoleo ya kuteketezwa ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto, lenye liliwekwa pembeni kwa ajili ya makuhani, kwa ajili ya Haruni na wana wake, katika siku yenye aliwaleta karibu ili wamutumikie Yehova wakiwa makuhani.+ 36 Yehova aliamuru wapewe fungu hilo kutoka kwa Waisraeli katika siku yenye aliwatia mafuta.+ Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyao.’”

37 Hii ndiyo sheria kuhusu toleo la kuteketezwa,+ toleo la nafaka,+ toleo la zambi,+ toleo la hatia,+ zabihu ya kuweka katika madaraka,+ na zabihu ya ushirika,+ 38 kama vile Yehova alimuamuru Musa kwenye Mulima Sinai+ katika siku yenye aliamuru Waisraeli wamutolee Yehova matoleo yao katika jangwa la Sinai.+

8 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Chukua Haruni na wana wake,+ zile nguo,+ yale mafuta ya kutia mafuta,+ ule ngombe-dume wa toleo la zambi, wale kondoo-dume wawili, na kile kitunga cha mikate yenye haina chachu,+ 3 na ukusanye mukusanyiko wote pamoja kwenye muingilio wa hema ya mukutano.”

4 Basi Musa akafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru, na mukusanyiko wote ukakusanyika kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 5 Sasa Musa akaambia mukusanyiko: “Hili ndilo jambo lenye Yehova ameamuru tufanye.” 6 Kwa hiyo Musa akamuleta Haruni na wana wake karibu na akawanawisha kwa maji.+ 7 Kisha akamuvalisha kanzu,+ akamufunga kitambaa cha kufunga kiuno,+ akamuvalisha ile koti yenye haina mikono,+ na akamuvalisha efodi+ na kumufunga mukaba* wa efodi wenye kusukwa,+ akaufunga kwa kukaza juu ya Haruni. 8 Halafu akamuvalisha kifuko cha kifua+ na akatia Urimu na Tumimu+ ndani ya kifuko hicho. 9 Kisha akatia kilemba+ juu ya kichwa chake, na kutia lile bamba lenye kungaa la zahabu upande wa mbele wa kilemba hicho, ile alama takatifu ya kuwekwa pembeni kwa ajili ya kusudi la pekee,*+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.

10 Kisha Musa akakamata yale mafuta ya kutia mafuta na akatia mafuta ile tabenakulo na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake+ na akavitakasa. 11 Kisha kufanya vile akanyunyiza* sehemu fulani ya mafuta hayo juu ya mazabahu mara saba (7) na akatia mafuta mazabahu na vyombo vyake vyote na beseni na kitu cha kuweka beseni juu yake ili kuvitakasa. 12 Mwishowe akamwanga juu ya kichwa cha Haruni sehemu fulani ya mafuta hayo ya kutia mafuta na akamutia mafuta ili kumutakasa.+

13 Halafu Musa akaleta wana wa Haruni karibu na akawavalisha kanzu na akawafunga vitambaa vya kufunga kwenye kiuno na akawavalisha kitu cha kuvaa kwenye kichwa,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.

14 Kisha akaleta ngombe-dume wa toleo la zambi, na Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha ngombe-dume huyo wa toleo la zambi.+ 15 Musa akamuchinja na akakamata damu yake+ kwa kidole chake na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu pande zote, na akatakasa mazabahu kutokana na zambi, lakini damu yenye ilibakia akaimwanga kwenye musingi wa mazabahu, ili kuitakasa kwa ajili ya kufunika zambi juu yake. 16 Kisha akakamata mafuta yote yenye kuwa juu ya matumbotumbo, mafuta yenye kuwa juu ya maini, na figo mbili pamoja na mafuta yake, na Musa akachoma vitu hivyo ili vitoe moshi juu ya mazabahu.+ 17 Kisha akafanya sehemu zenye zilibakia za ngombe-dume huyo, ngozi yake, nyama yake, na mavi yake, ziteketezwe kwa moto inje ya kambi,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.

18 Sasa akaleta kondoo-dume wa toleo la kuteketezwa karibu, na Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo-dume huyo.+ 19 Kisha Musa akamuchinja na kunyunyiza* damu yake kwenye pande zote za mazabahu. 20 Akakata kondoo-dume huyo vipande-vipande, na Musa akachoma kichwa, vile vipande, na yale mafuta* ili yatoe moshi. 21 Akasafisha matumbotumbo na miguu kwa maji, na Musa akachoma kondoo-dume muzima ili atoe moshi juu ya mazabahu. Lilikuwa toleo la kuteketezwa lenye harufu ya muzuri.* Lilikuwa toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.

22 Kisha akaleta kondoo-dume wa pili, kondoo wa kuweka katika madaraka ya ukuhani,+ na Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo-dume huyo.+ 23 Musa akamuchinja na akakamata sehemu fulani ya damu yake na kuipakaa kwenye sehemu ya chini ya sikio la kuume la Haruni na kwenye kidole kikubwa cha mukono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha muguu wake wa kuume. 24 Kisha Musa akaleta wana wa Haruni mbele na akapakaa sehemu fulani ya damu hiyo kwenye sehemu za chini za masikio yao ya kuume na kwenye vidole vikubwa vya mikono yao ya kuume na kwenye vidole vikubwa vya miguu yao ya kuume; lakini Musa alinyunyiza* damu yenye ilibakia kwenye pande zote za mazabahu.+

25 Kisha akakamata yale mafuta, ule mukia wenye mafuta, mafuta yote yenye kuwa juu ya matumbotumbo, yale mafuta yenye kuwa juu ya maini, zile figo mbili na mafuta yake, na muguu wa kuume.+ 26 Akakamata katika kitunga cha mikate yenye haina chachu chenye kilikuwa mbele ya Yehova mukate mumoja wa muviringo wenye hauna chachu,+ mukate mumoja wa muviringo wenye mafuta,+ na mukate mumoja mwembamba. Kisha akatia mikate hiyo juu ya vipande vya mafuta na juu ya muguu wa kuume. 27 Kisha kufanya vile akatia vitu hivyo vyote katika mikono ya Haruni na mikono ya wana wake na akaanza kuvitikisa mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova. 28 Kisha Musa akavikamata kutoka katika mikono yao na kuvichoma ili vitoe moshi kwenye mazabahu juu ya toleo la kuteketezwa. Vitu hivyo vilikuwa zabihu ya kuwaweka katika madaraka yao, zabihu yenye harufu ya muzuri.* Lilikuwa toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.

29 Kisha Musa akakamata kifua na kukitikisa mbele na nyuma kikiwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova.+ Sehemu hiyo ya kondoo-dume wa kuwaweka katika madaraka yao ilikuwa fungu la Musa, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.+

30 Na Musa akakamata sehemu fulani ya mafuta ya kutia mafuta+ na sehemu fulani ya damu yenye ilikuwa kwenye mazabahu na kuinyunyiza* juu ya Haruni na nguo zake na juu ya wana wake na nguo zao. Kwa hiyo akamutakasa Haruni na nguo zake na wana wake+ na nguo zao.+

31 Kisha Musa akamuambia Haruni na wana wake: “Mutokoteshe+ nyama hiyo kwenye muingilio wa hema ya mukutano, na muikule pale pamoja na mikate yenye kuwa katika kitunga cha kuwaweka katika madaraka yenu, kama vile niliamuriwa, ‘Haruni na wana wake wataikula.’+ 32 Nyama na mikate yenye itabakia, mutaiteketeza kwa moto.+ 33 Hamupaswe kutoka inje ya muingilio wa hema ya mukutano kwa siku saba (7), mupaka siku za kuwaweka ninyi katika madaraka zimalizike, kwa sababu itachukua siku saba ili kuwaweka ninyi kuwa makuhani.*+ 34 Yehova alituamuru tufanye mambo yenye tumefanya leo ili kufunika zambi kwa ajili yenu.+ 35 Mutabakia kwenye muingilio wa hema ya mukutano muchana na usiku kwa siku saba (7),+ na mutafanya mambo yenye Yehova amewaomba mufanye+ ili musikufe; kwa maana ni vile nimeamuriwa.”

36 Na Haruni na wana wake wakafanya mambo yote yenye Yehova alikuwa ameamuru kupitia Musa.

9 Siku ya munane (8),+ Musa akamuita Haruni na wana wake na wazee wa Israeli. 2 Akamuambia Haruni: “Ujikamatie kitoto-dume cha ngombe kwa ajili ya toleo la zambi+ na kondoo-dume kwa ajili ya toleo la kuteketezwa, wanyama wenye hawana kasoro, na uwatoe mbele ya Yehova. 3 Lakini utaambia Waisraeli, ‘Mukamate mbuzi-dume kwa ajili ya toleo la zambi na kitoto-dume cha ngombe na mwana-kondoo dume, wote wa mwaka mumoja, wenye hawana kasoro, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa, 4 na ngombe-dume na kondoo-dume kwa ajili ya zabihu za ushirika,+ ili kuwatoa kuwa zabihu mbele ya Yehova, na pia toleo la nafaka+ lenye kuchanganywa na mafuta, kwa sababu leo Yehova atawatokea ninyi.’”+

5 Kwa hiyo wakapeleka mbele ya hema ya mukutano vitu vyenye Musa alikuwa ameamuru. Kisha mukusanyiko wote ukakaribia na kusimama mbele ya Yehova. 6 Na Musa akasema: “Ni hivi Yehova ameamuru mufanye, ili utukufu wa Yehova uwatokee ninyi.”+ 7 Kisha Musa akamuambia Haruni: “Uende karibu na mazabahu na utoe toleo lako la zambi+ na toleo lako la kuteketezwa, na ufunike zambi kwa ajili yako mwenyewe+ na kwa ajili ya nyumba yako; na utoe toleo la watu,+ na ufunike zambi kwa ajili yao,+ kama vile Yehova ameamuru.”

8 Haruni akaenda mara moja karibu na mazabahu na akachinja kile kitoto-dume cha ngombe cha toleo la zambi chenye kilikuwa kwa ajili yake mwenyewe.+ 9 Kisha wana wa Haruni wakamuletea damu,+ na akaingiza kidole chake katika damu hiyo na akaitia kwenye pembe za mazabahu, na damu yenye ilibakia akaimwanga kwenye musingi wa mazabahu.+ 10 Akachoma mafuta na figo na mafuta yenye kuwa juu ya maini kutoka katika toleo la zambi ili vitoe moshi juu ya mazabahu, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.+ 11 Na akateketeza kwa moto nyama na ngozi inje ya kambi.+

12 Kisha akachinja toleo la kuteketezwa, na wana wa Haruni wakamupatia damu, na akainyunyiza* kwenye pande zote za mazabahu.+ 13 Wakamupatia vipande vya toleo la kuteketezwa pamoja na kichwa, na akavichoma ili vitoe moshi juu ya mazabahu. 14 Pia, akasafisha matumbotumbo na miguu na akachoma vitu hivyo juu ya toleo la kuteketezwa ili vitoe moshi juu ya mazabahu.

15 Kisha akatoa toleo la watu na akakamata ule mbuzi wa toleo la zambi mwenye alikuwa kwa ajili ya watu na akamuchinja na kutoa toleo la zambi kama vile alifanya na ule wa kwanza. 16 Na akatoa toleo la kuteketezwa na akalitoa kwa kufuata utaratibu wa kawaida.+

17 Kisha akatoa toleo la nafaka;+ akajaza sehemu fulani ya toleo hilo katika mukono wake na akalichoma ili litoe moshi juu ya mazabahu, zaidi ya toleo la kuteketezwa la asubui.+

18 Kisha mambo hayo Haruni akachinja ule ngombe-dume na kondoo-dume wa zabihu ya ushirika mwenye alikuwa kwa ajili ya watu. Kisha wana wa Haruni wakamupatia damu, na akainyunyiza* kwenye pande zote za mazabahu.+ 19 Lakini vipande vya mafuta vya ngombe-dume,+ mukia wenye mafuta wa kondoo-dume, mafuta yenye kufunika viungo vya ndani, na figo, na mafuta yenye kuwa juu ya maini,+ 20 walitia vipande hivyo vyote vya mafuta juu ya vifua, kisha akachoma vipande hivyo vyenye mafuta ili vitoe moshi juu ya mazabahu.+ 21 Lakini, Haruni akatikisa vifua na muguu wa kuume mbele na nyuma kuwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova, kama vile Musa alikuwa ameamuru.+

22 Halafu Haruni akainua mikono yake kuelekea watu na akawabariki+ na akashuka chini kisha kutoa toleo la zambi na toleo la kuteketezwa na zabihu za ushirika. 23 Mwishowe Musa na Haruni wakaingia katika hema ya mukutano na wakatoka inje na kubariki watu.+

Halafu utukufu wa Yehova ukatokea watu wote,+ 24 na moto ukashuka kutoka kwa Yehova+ na ukaanza kuteketeza lile toleo la kuteketezwa na vile vipande vya mafuta vyenye vilikuwa kwenye mazabahu. Wakati watu wote waliona jambo hilo, wakaanza kupiga vigelegele na wakaanguka uso chini.+

10 Kisha wakati fulani, Nadabu na Abihu,+ wana wa Haruni, wakakamata kila mumoja wao chetezo chake na wakatia moto ndani yake na kutia uvumba+ juu yake. Halafu wakaanza kutoa mbele ya Yehova moto wenye hauruhusiwe,+ wenye alikuwa hajawaamuru wafanye. 2 Basi moto ukashuka kutoka kwa Yehova na kuwateketeza,+ kwa hiyo wakakufa mbele ya Yehova.+ 3 Musa akamuambia Haruni: “Yehova amesema hivi: ‘Nitatakaswa kati ya wale wenye kuwa karibu na mimi,+ na nitatukuzwa mbele ya watu wote.’” Na Haruni akabakia kimya.

4 Kwa hiyo Musa akaita Mishaeli na Elsafani, wana wa Uzieli,+ ndugu ya baba ya Haruni, na akawaambia: “Mukuje hapa, mutoshe ndugu zenu mbele ya mahali patakatifu na muwapeleke inje ya kambi.” 5 Kwa hiyo wakakaribia na wakabeba wanaume hao wakiwa na kanzu zao na kuwapeleka inje ya kambi, kama vile Musa alikuwa amewaambia.

6 Kisha Musa akaambia Haruni na wana wake wengine, Eleazari na Itamari: “Musiache nywele zenu katika hali ya ovyo-ovyo na musipasue nguo zenu,+ ili musikufe na ili Mungu asikasirikie mukusanyiko wote. Ndugu zenu wa nyumba yote ya Israeli wataombolezea wale wenye Yehova ameua kwa moto. 7 Hamupaswe kuenda inje ya muingilio wa hema ya mukutano ili musikufe, kwa sababu mafuta ya Yehova ya kutia mafuta yako juu yenu.”+ Kwa hiyo wakafanya kama vile Musa alisema.

8 Kisha Yehova akamuambia Haruni: 9 “Usikunywe divai ao pombe yoyote, wewe na wana wako, wakati munaingia katika hema ya mukutano,+ ili musikufe. Ni sheria ya kudumu kwa ajili ya vizazi vyenu. 10 Hii ni kwa sababu ya kufanya tofauti kati ya kitu kitakatifu na kitu chenye hakiko kitakatifu na kati ya kitu safi na kitu chenye hakiko safi,+ 11 na ili kufundisha Waisraeli wote masharti yote yenye Yehova amewaambia kupitia Musa.”+

12 Kisha Musa akaambia Haruni na wana wake wenye walibakia, Eleazari na Itamari: “Mukamate toleo la nafaka lenye lilibakia kutoka katikati ya matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto na mukule toleo hilo kama mikate yenye haina chachu karibu na mazabahu,+ kwa sababu ni kitu kitakatifu sana.+ 13 Munapaswa kula toleo hilo katika mahali patakatifu,+ kwa sababu ni posho lako na posho la wana wako kutoka katikati ya matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto, kwa maana ni vile nimeamuriwa. 14 Pia, mutakula kifua cha toleo la kutikiswa na muguu wa fungu takatifu+ mukiwa mahali safi, wewe na watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke,+ kwa sababu vitu hivyo vimetolewa ili kuwa posho lako na posho la wana wako kutoka katikati ya zabihu za ushirika za Waisraeli. 15 Wataleta muguu wa fungu takatifu na kifua cha toleo la kutikiswa pamoja na matoleo ya mafuta yenye yanatolewa kwa njia ya moto, ili kutikisa toleo la kutikiswa mbele na nyuma mbele ya Yehova; hilo litakuwa posho la kudumu kwa ajili yako na kwa ajili ya wana wako,+ kama vile Yehova ameamuru.”

16 Na Musa akatafuta sana ule mbuzi wa toleo la zambi,+ na akavumbua kwamba alikuwa ameteketezwa kwa moto. Kwa hiyo akakasirikia sana Eleazari na Itamari, wana wa Haruni wenye walibakia, na akasema: 17 “Sababu gani hamukukula toleo la zambi mukiwa mahali patakatifu,+ kwa kuwa ni kitu kitakatifu sana na amewapatia toleo hilo ili muweze kujibu kwa ajili ya kosa la mukusanyiko na ili mufunike zambi kwa ajili yao mbele ya Yehova? 18 Muangalie! Damu yake haijaletwa ndani ya mahali patakatifu.+ Mulipaswa kabisa kula toleo hilo katika mahali patakatifu, kama vile niliamuriwa.” 19 Haruni akamujibu Musa: “Angalia! Leo walimutolea Yehova toleo lao la zambi na toleo lao la kuteketezwa,+ na bado mambo haya yamenipata. Kama ningekula toleo la zambi leo, je, jambo hilo lingemupendeza Yehova?” 20 Wakati Musa alisikia maneno hayo, akatosheka.

11 Kisha Yehova akaambia Musa na Haruni: 2 “Ambia Waisraeli, ‘Hivi ndivyo viumbe vya dunia vyenye munaweza kula:+ 3 Kila munyama mwenye kwato* yenye kupasuka katikati na mwenye mupasuko kamili katika kwato zake na mwenye anacheua anaweza kukuliwa.

4 “‘Lakini hamupaswe kula wanyama hawa wenye wanacheua ao wenye kwato yenye kupasuka katikati: ngamia kwa sababu anacheua lakini hana kwato* yenye kupasuka katikati. Yeye haiko safi kwenu.+ 5 Pia wibari,+ kwa sababu anacheua lakini kwato* yake haipasuke katikati. Yeye haiko safi kwenu. 6 Pia sungura, kwa sababu anacheua lakini kwato* yake haipasuke katikati. Yeye haiko safi kwenu. 7 Pia nguruwe,+ kwa sababu iko* na kwato* yenye kupasuka katikati na mupasuko kamili katika kwato lakini hacheue. Yeye haiko safi kwenu. 8 Hamupaswe kula sehemu yoyote ya nyama yao wala kugusa mizoga yao. Hao hawako safi kwenu.+

9 “‘Hawa ndio munaweza kula katikati ya kila kitu chenye kuwa ndani ya maji: Kiumbe chochote chenye kuwa ndani ya maji chenye kuwa na mapezi* na magamba, ikuwe ndani ya bahari ao ndani ya mito, hicho munaweza kula.+ 10 Lakini kitu chochote ndani ya bahari na ndani ya mito chenye hakina mapezi* na magamba, kati ya viumbe vyote vyenye kupatikana kwa wingi na kila kiumbe kingine chenye uzima chenye kuwa ndani ya maji, ni chukizo kwenu. 11 Ndiyo, vitakuwa vyenye kuchukiza sana kwenu, na hamupaswe kula sehemu yoyote ya nyama yavyo,+ na munapaswa kuchukia sana mizoga yavyo. 12 Kila kitu ndani ya maji chenye hakina mapezi* na magamba ni chukizo kwenu.

13 “‘Hivi ndivyo viumbe vyenye kuruka vyenye munapaswa kuchukia sana; havipaswe kukuliwa, kwa sababu ni chukizo: tai,+ furukombe, tumbusi mweusi,+ 14 mwewe mwekundu na kila aina ya mwewe mweusi, 15 kila aina ya kunguru, 16 mbuni, bundi, shakwe, kila aina ya kipanga, 17 bundi mudogo, munandi, bundi mwenye masikio ya murefu, 18 bata-maji, mwari, tumbusi, 19 korongo, kila aina ya kulastara, hudihudi, na popo. 20 Kila kiumbe chenye mabawa* chenye kupatikana kwa wingi na chenye kutambaa kwa miguu yote ine (4) ni chukizo kwenu.

21 “‘Kati ya viumbe vyenye kupatikana kwa wingi vyenye vinatambaa kwa miguu yote ine (4), munaweza kula tu vile vyenye miguu mbili yenye kuunganishwa yenye ni mirefu kuliko miguu yao ingine ili kuruka juu ya udongo. 22 Kati ya hivyo munaweza kula: kila aina ya nzige wenye kuhama-hama, nzige wengine wenye kukuliwa,+ senene, na panzi. 23 Viumbe vingine vyote vyenye mabawa vyenye kupatikana kwa wingi na vyenye kuwa na miguu ine (4) ni chukizo kwenu. 24 Kupitia viumbe hivyo mutajichafua. Kila mutu mwenye anagusa mizoga ya viumbe hivyo hatakuwa safi mupaka mangaribi.+ 25 Kila mutu mwenye anabeba mizoga ya viumbe hivyo anapaswa kufua nguo zake;+ hatakuwa safi mupaka mangaribi.

26 “‘Kila munyama mwenye kwato* yenye kupasuka katikati lakini mwenye hana mupasuko kamili na hacheue haiko safi kwenu. Kila mutu mwenye anagusa wanyama hao hatakuwa safi.+ 27 Kila kiumbe chenye uzima chenye kutembea kwa miguu yenye makucha kati ya viumbe vyenye kutembea kwa miguu ine (4) hakiko safi kwenu. Kila mutu mwenye anagusa mizoga ya viumbe hivyo hatakuwa safi mupaka mangaribi. 28 Mutu yeyote mwenye atabeba mizoga ya viumbe hivyo anapaswa kufua nguo zake,+ na hatakuwa safi mupaka mangaribi.+ Viumbe hivyo haviko safi kwenu.

29 “‘Hivi ndivyo viumbe vya dunia vyenye kupatikana kwa wingi vyenye haviko safi kwenu: fuko, panya,+ kila aina ya mujusi, 30 mujusi kafiri, mujusi mukubwa, mujusi mwenye kuishi ndani ya maji, mujusi mwenye kuishi ndani ya muchanga, na kinyonga.* 31 Viumbe hivyo vyenye kupatikana kwa wingi haviko safi kwenu.+ Kila mutu mwenye anagusa mizoga yavyo hatakuwa safi mupaka mangaribi.+

32 “‘Sasa kila kitu chenye viumbe hivyo vinaangukia wakati vinakufa hakitakuwa safi, ikuwe chombo cha mbao, nguo, ngozi, ao kipande cha nguo ya gunia. Kila chombo chenye kinatumiwa kinapaswa kuzamishwa ndani ya maji, na hakitakuwa safi mupaka mangaribi; kisha kitakuwa safi. 33 Kama vinaangukia ndani ya chombo cha udongo, munapaswa kukivunja-vunja, na kila kitu chenye kilikuwa ndani ya chombo hicho hakitakuwa safi.+ 34 Chakula chochote chenye kinamwangikiwa na maji yenye kutoka katika chombo hicho hakitakuwa safi, na kila kinywaji chenye kuwa ndani ya chombo hicho hakitakuwa safi. 35 Kila kitu chenye mizoga ya viumbe hivyo inaangukia hakitakuwa safi. Ikuwe jiko la mukubwa ao jiko la kidogo, linapaswa kuvunjwa-vunjwa. Vitu hivyo haviko safi, na sikuzote havitakuwa safi kwenu. 36 Ni chemchemi na tangi la kuwekea maji tu ndivyo vitaendelea kuwa safi, lakini kila mutu mwenye anagusa mizoga ya viumbe hivyo hatakuwa safi. 37 Kama mizoga ya viumbe hivyo inaanguka juu ya mbegu ya mumea yenye itapandwa, mbegu hiyo iko safi. 38 Lakini kama maji yanatiwa juu ya mbegu na kama sehemu ya mizoga ya viumbe hivyo inaanguka juu ya mbegu hiyo, mbegu hiyo haiko safi kwenu.

39 “‘Sasa kama munyama mwenye munatumia kwa ajili ya chakula anakufa, mutu yeyote mwenye anagusa muzoga wa munyama huyo hatakuwa safi mupaka mangaribi.+ 40 Kila mutu mwenye anakula sehemu yoyote ya muzoga wa munyama huyo anapaswa kufua nguo zake, na hatakuwa safi mupaka mangaribi.+ Kila mutu mwenye anabeba muzoga wa munyama huyo anapaswa kufua nguo zake, na hatakuwa safi mupaka mangaribi. 41 Kila kiumbe chenye kupatikana kwa wingi ni chukizo.+ Hakipaswe kukuliwa. 42 Hamupaswe kula kila kiumbe chenye kutambaa kwa tumbo, kila kiumbe chenye kutembea kwa miguu yote ine (4), ao viumbe vyote vyenye kupatikana kwa wingi vyenye viko na miguu mingi, kwa sababu viumbe hivyo ni chukizo.+ 43 Musijifanye* kuwa chukizo kupitia kila kiumbe chenye kupatikana kwa wingi, na musijichafue na kuwa watu wenye hawako safi kutokana na viumbe hivyo.+ 44 Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wenu,+ na munapaswa kujitakasa na kuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni mutakatifu.+ Kwa hiyo hamupaswe kujichafua* kupitia kila kiumbe chenye kupatikana kwa wingi chenye kutembea juu ya dunia. 45 Kwa maana mimi ni Yehova, mwenye kuwaongoza kutoka katika inchi ya Misri ili nijionyeshe kuwa Mungu wenu,+ na munapaswa kuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni mutakatifu.+

46 “‘Hii ni sheria kuhusu wanyama, viumbe vyenye kuruka, kila kiumbe chenye uzima chenye* kutambaa ndani ya maji, na kuhusu kila kiumbe chenye* kupatikana kwa wingi juu ya dunia, 47 ili kufanya tofauti kati ya kitu chenye hakiko safi na kitu chenye kiko safi na kati ya viumbe vyenye uzima vyenye vinaweza kukuliwa na vyenye haviwezi kukuliwa.’”+

12 Yehova akaendelea kusema na Musa: 2 “Ambia Waisraeli, ‘Kama mwanamuke anapata mimba na anazaa mutoto mwanaume, mwanamuke huyo hatakuwa safi kwa siku saba (7), atakuwa tu kama vile anakuwaka katika siku zake za kuona mwezi.*+ 3 Siku ya munane (8), nyama ya govi* la mutoto huyo itatahiriwa.+ 4 Mwanamuke huyo ataendelea kujitakasa kutokana na ile damu kwa siku makumi tatu na tatu (33) zenye zitafuata. Hapaswe kugusa kitu chochote kitakatifu, na hapaswe kuingia katika mahali patakatifu mupaka wakati atamaliza siku za utakaso wake.

5 “Kama anazaa mutoto mwanamuke, mwanamuke huyo hatakuwa safi kwa siku kumi na ine (14), atakuwa kama vile anakuwaka katika siku zake za kuona mwezi.* Ataendelea kujitakasa kutokana na ile damu kwa siku makumi sita na sita (66) zenye zitafuata. 6 Wakati siku zake za utakaso kwa ajili ya mutoto mwanaume ao mutoto mwanamuke zitamalizika, atamuletea kuhani mwana-kondoo dume katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa+ na njiwa mudogo ao njiwa-tetere kwa ajili ya toleo la zambi kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 7 Kuhani atatoa toleo hilo mbele ya Yehova na kufunika zambi kwa ajili ya mwanamuke huyo, na atakuwa safi kutokana na mutiririko wake wa damu. Hii ni sheria kuhusu mwanamuke mwenye anazaa mutoto mwanaume ao mutoto mwanamuke. 8 Lakini kama hawezi kupata kondoo, basi anapaswa kukamata njiwa-tetere wawili ao njiwa wawili wadogo,+ mumoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa na mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, na kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mwanamuke huyo, na atakuwa safi.’”

13 Yehova akaendelea kusema na Musa na Haruni, na kumuambia: 2 “Kama mutu iko* na uvimbe kwenye ngozi yake, kigaga,* ao doa lenye linaweza kuwa ugonjwa wa ukoma+ kwenye ngozi yake,* basi anapaswa kupelekwa kwa Haruni kuhani ao kwa mumoja wa wana wake, makuhani.+ 3 Kuhani atachunguza sehemu yenye ugonjwa kwenye ngozi yake. Kama nywele za sehemu hiyo yenye ugonjwa zimegeuka kuwa mweupe na ugonjwa huo unaonekana kuwa umeingia sana chini ya ngozi, huo ni ugonjwa wa ukoma. Kuhani atauchunguza na kutangaza kwamba mutu huyo haiko safi. 4 Lakini kama doa kwenye ngozi yake liko mweupe na linaonekana kuwa limeingia sana chini ya ngozi na nywele hazijageuka kuwa mweupe, basi kuhani atamuweka mutu huyo mwenye ameambukizwa mbali na watu kwa siku saba (7).+ 5 Kisha kuhani atamuchunguza siku ya saba (7), na kama inaonekana kwamba ugonjwa huo haukuendelea na haujaenea kwenye ngozi, kuhani atamuweka mbali na watu kwa siku zingine saba.

6 “Kuhani anapaswa kumuchunguza tena siku ya saba (7), na kama ugonjwa huo umeanza kufifia na haujaenea kwenye ngozi, kuhani atamutangaza kuwa safi;+ kilikuwa kigaga* tu. Kisha mutu huyo atafua nguo zake na kuwa safi. 7 Lakini kama kigaga hicho kimeenea* kabisa kwenye ngozi kisha mutu huyo kuonekana mbele ya kuhani ili kuhakikisha utakaso wake, basi ataenda kujionyesha tena* mbele ya kuhani. 8 Kuhani atachunguza kigaga* hicho, na kama kimeenea kwenye ngozi, basi kuhani atatangaza kwamba mutu huyo haiko safi. Ni ukoma.+

9 “Kama ugonjwa wa ukoma unatokea juu ya mwili wa mutu, basi anapaswa kupelekwa mbele ya kuhani, 10 na kuhani atamuchunguza.+ Kama kuko uvimbe mweupe kwenye ngozi na umegeuza nywele kuwa mweupe na kuko kidonda chenye kuwa wazi+ katika uvimbe huo, 11 huo ni ukoma wa muda murefu kwenye ngozi ya mutu huyo, na kuhani atatangaza kwamba mutu huyo haiko safi. Hapaswe kumuweka mbali na watu,+ kwa sababu haiko safi. 12 Sasa kama ukoma unaenea kwenye ngozi yote na ukoma unamufunika mutu kwa ugonjwa kuanzia kichwa mupaka miguu, kwa kadiri kuhani anaweza kuona, 13 na kuhani amemuchunguza na kuona kwamba ukoma umefunika ngozi yake yote, basi atatangaza kwamba mutu huyo mwenye ugonjwa iko* safi.* Ngozi yote imegeuka kuwa mweupe, na yeye iko* safi. 14 Lakini kila mara wakati kidonda chenye kuwa wazi kinaonekana katika ngozi, hatakuwa safi. 15 Wakati kuhani anaona kidonda hicho chenye kuwa wazi, atatangaza kwamba mutu huyo haiko safi.+ Kidonda hicho chenye kuwa wazi hakiko safi. Ni ukoma.+ 16 Lakini kama kidonda hicho chenye kuwa wazi kinageuka tena kuwa cheupe, basi mutu huyo ataenda kwa kuhani. 17 Kuhani atamuchunguza,+ na kama kidonda hicho kimegeuka kuwa cheupe, basi kuhani atatangaza mutu huyo mwenye ameambukizwa kuwa safi. Yeye iko* safi.

18 “Kama mutu anakuwa na jipu kwenye ngozi yake na linapona, 19 lakini mahali pake panatokea uvimbe mweupe ao doa la rangi nyekundu-nyeupe, basi anapaswa kujionyesha kwa kuhani. 20 Kuhani atachunguza doa hilo,+ na kama linaonekana kuwa limeingia sana chini ya ngozi na nywele za sehemu hiyo zimegeuka kuwa mweupe, basi kuhani atatangaza kwamba mutu huyo haiko safi. Ni ugonjwa wa ukoma wenye umetokea katika jipu. 21 Lakini kama kuhani anachunguza na anaona kwamba hakuna nywele mweupe katika doa hilo na halijaingia sana chini ya ngozi na linaonekana kuwa limefifia, basi kuhani atamuweka mbali na watu kwa siku saba (7).+ 22 Na kama doa hilo limeenea waziwazi kwenye ngozi, basi kuhani atatangaza kwamba mutu huyo haiko safi. Ni ugonjwa. 23 Lakini kama doa hilo linabakia nafasi moja na halijaenea, ni jipu tu linavimba, na kuhani atamutangaza mutu huyo kuwa safi.+

24 “Ao kama mutu iko* na kovu lenye lilitokana na moto na kovu hilo la mubichi linageuka rangi na kuwa doa nyekundu-nyeupe ao mweupe, 25 basi kuhani atachunguza doa hilo. Kama nywele katika doa hilo zimegeuka kuwa mweupe na linaonekana kuwa limeingia sana chini ya ngozi, ni ukoma wenye umetokea katika kovu, na kuhani atatangaza kwamba mutu huyo haiko safi. Ni ugonjwa wa ukoma. 26 Lakini kama kuhani anachunguza doa hilo na anaona kwamba hakuna nywele mweupe katika doa hilo na halijaingia sana chini ya ngozi na limefifia, basi kuhani atamuweka mutu huyo mbali na watu kwa siku saba (7).+ 27 Kuhani atamuchunguza siku ya saba (7), na kama doa hilo limeenea waziwazi kwenye ngozi, basi kuhani atatangaza kwamba mutu huyo haiko safi. Ni ugonjwa wa ukoma. 28 Lakini kama doa hilo linabakia nafasi moja na halienee kwenye ngozi na limefifia, ni kovu tu linavimba, na kuhani atatangaza kwamba mutu huyo iko* safi, kwa sababu ni kovu linavimba.

29 “Kama mwanaume ao mwanamuke anapata ugonjwa kwenye kichwa ao kwenye kidevu, 30 kuhani atachunguza ugonjwa huo.+ Kama unaonekana kuwa umeingia sana chini ya ngozi na nywele za sehemu hiyo ziko na rangi ya manjano na ziko mwembamba, basi kuhani atatangaza kwamba mutu huyo haiko safi; ni ugonjwa wa ngozi ya kichwa ao kidevu. Ni ukoma wa kichwa ao wa kidevu. 31 Lakini kama kuhani anaona kwamba ugonjwa huo hauonekane kuwa umeingia sana chini ya ngozi na hakuna nywele mweusi ndani yake, kuhani anapaswa kumuweka mutu huyo mwenye ugonjwa mbali na watu kwa siku saba (7).+ 32 Kuhani atachunguza ugonjwa huo siku ya saba (7), na kama nafasi yenye ugonjwa haijaenea ao hakujakuwa nywele za rangi ya manjano kwenye nafasi hiyo na inaonekana kuwa nafasi hiyo yenye ugonjwa haijaingia sana chini ya ngozi, 33 mutu huyo anapaswa kunyolewa, lakini hatanyolewa nafasi hiyo yenye ugonjwa. Kisha kuhani atamuweka mutu huyo mwenye ugonjwa mbali na watu kwa siku saba (7).

34 “Kuhani atachunguza tena nafasi hiyo yenye ugonjwa siku ya saba (7), na kama ugonjwa huo wa ngozi ya kichwa na wa ndevu umeenea kwenye ngozi na hauonekane kuwa umeingia sana chini ya ngozi, basi kuhani anapaswa kutangaza kwamba mutu huyo iko* safi, na mutu huyo atafua nguo zake na kuwa safi. 35 Lakini kama ugonjwa huo unaenea waziwazi kwenye ngozi kisha utakaso wake, 36 kuhani atamuchunguza, kama ugonjwa huo umeenea kwenye ngozi, kuhani hana lazima ya kuchunguza kama kuko nywele za rangi ya manjano; mutu huyo haiko safi. 37 Lakini kama uchunguzi unaonyesha kwamba ugonjwa huo haujaenea na nywele mweusi zimeota nafasi hiyo, ugonjwa huo umepona. Mutu huyo iko* safi, na kuhani atamutangaza kuwa safi.+

38 “Kama mwanaume ao mwanamuke anakuwa na madoa kwenye ngozi* na madoa hayo ni meupe, 39 kuhani atamuchunguza.+ Kama madoa hayo hayako meupe sana, ni vipele vyenye havina hatari vyenye vimetokea kwenye ngozi. Mutu huyo iko* safi.

40 “Kama mwanaume anapoteza nywele za kichwa chake na anakuwa na upara, yeye iko* safi. 41 Kama anapoteza nywele sehemu ya mbele ya kichwa chake na anakuwa na upara nafasi hiyo, yeye iko* safi. 42 Lakini kama mutu anakuwa na kidonda chenye rangi nyekundu-nyeupe kwenye sehemu yenye upara ya ngozi ya kichwa chake ao kwenye paji lake la uso, ni ukoma wenye unatokea kwenye ngozi ya kichwa chake ao kwenye paji lake la uso. 43 Kuhani atamuchunguza, na kama ugonjwa huo kwenye sehemu yenye upara juu ya kichwa chake ao paji lake la uso uko na uvimbe wa rangi nyekundu-nyeupe na ikiwa unaonekana kama ukoma kwenye ngozi yake, 44 mutu huyo iko* na ukoma. Yeye haiko safi, kuhani anapaswa kutangaza kwamba mutu huyo haiko safi kwa sababu ya ugonjwa kwenye kichwa chake. 45 Kuhusu mutu mwenye ugonjwa wa ukoma, nguo zake zinapaswa kupasuliwa na nywele zake zinapaswa kuachwa katika hali ya ovyo-ovyo na anapaswa kufunika masharubu* yake na kusema hivi kwa sauti: ‘Siko safi, siko safi!’ 46 Hatakuwa safi wakati wote wenye atakuwa na ugonjwa huo. Kwa sababu haiko safi, ataishi mbali na watu. Makao yake yatakuwa inje ya kambi.+

47 “Kama ugonjwa wa ukoma unaambukiza nguo, ikuwe nguo ya sufu ao ya kitani, 48 ikuwe katika nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini* ao katika nyuzi zenye kutoka kushoto kuenda kuume za* kitani ao za manyoya ya kondoo, ao katika ngozi ao katika kitu chochote chenye kilitengenezwa na ngozi, 49 na kama doa la rangi ya manjano-kijani ao doa nyekundu la ugonjwa huo linaambukiza nguo, ngozi, nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini,* nyuzi zenye kutoka kushoto kuenda kuume,* ao kitu chochote cha ngozi, ni ambukizo la ukoma, na linapaswa kuonyeshwa kwa kuhani. 50 Kuhani atachunguza ugonjwa huo, na anapaswa kuweka ugonjwa huo mbali na watu kwa siku saba (7).+ 51 Wakati atachunguza ugonjwa huo siku ya saba (7) na kuona kwamba umeenea katika nguo, katika nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini,* katika nyuzi zenye kutoka kushoto kuenda kuume,* ao katika ngozi (ikuwe ngozi hiyo inatumiwa kwa kusudi gani), huo ni ukoma hatari, na kitu hicho hakiko safi.+ 52 Anapaswa kuteketeza kwa moto nguo hiyo ao nyuzi hizo za murefu zenye kutoka juu kuenda chini* ao nyuzi hizo zenye kutoka kushoto kuenda kuume* katika manyoya ya kondoo ao katika kitani ao kitu chochote cha ngozi chenye ugonjwa huo umetokea juu yake, kwa sababu huo ni ukoma hatari. Kitu hicho kinapaswa kuteketezwa kwa moto.

53 “Lakini kama kuhani anachunguza na ugonjwa huo haujaenea katika nguo ao katika nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini* ao katika nyuzi zenye kutoka kushoto kuenda kuume* ao katika kitu chochote cha ngozi, 54 basi kuhani ataamuru wasafishe kitu hicho chenye kiliambukizwa, na atakiweka mbali na watu kwa siku zingine saba (7). 55 Kisha kuhani atachunguza kitu chenye kiliambukizwa kisha kitu hicho kusafishwa kabisa. Kama ambukizo hilo linaonekana kuwa halijabadilika, hata kama ugonjwa huo haujaenea, kitu hicho hakiko safi. Munapaswa kukiteketeza katika moto kwa sababu kimekuliwa na ukoma, ikuwe kuanzia ndani ao inje.

56 “Lakini kama kuhani amekichunguza na sehemu yenye iliambukizwa imefifia kisha kitu hicho kusafishwa kabisa, basi atatosha sehemu yenye iliambukizwa katika nguo hiyo ao katika ngozi hiyo ao katika nyuzi hizo za murefu zenye kutoka juu kuenda chini* huo ao katika nyuzi hizo zenye kutoka kushoto kuenda kuume.* 57 Hata hivyo, kama ugonjwa huo unatokea tena kwenye sehemu ingine ya nguo ao katika nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini* ao katika nyuzi zenye kutoka kushoto kuenda kuume* ao katika kitu chochote cha ngozi, basi ugonjwa huo ni wenye kuenea, na munapaswa kuteketeza katika moto kitu chochote chenye kiliambukizwa.+ 58 Lakini wakati ambukizo hilo haliko tena katika nguo ao nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini* ao katika nyuzi zenye kutoka kushoto kuenda kuume* ao katika kitu chochote cha ngozi chenye munasafisha, basi kitu hicho kinapaswa kusafishwa mara ya pili, na kitakuwa safi.

59 “Hii ni sheria kuhusu ugonjwa wa ukoma katika nguo ya manyoya ya kondoo ao ya kitani, ao katika nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini* ao katika nyuzi zenye kutoka kushoto kuenda kuume,* ao katika kitu chochote cha ngozi; ili kutangaza kuwa kiko safi ao hakiko safi.”

14 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Hii ndiyo inapaswa kuwa sheria kuhusu mutu mwenye ukoma katika siku yenye utakaso wake unahakikishwa, wakati anapelekwa kwa kuhani.+ 3 Kuhani ataenda inje ya kambi na kumuchunguza. Kama mutu huyo mwenye ukoma amepona ukoma wake, 4 kuhani atamuamuru alete ndege wawili wenye kuwa safi wenye ni wazima, muti wa mwerezi, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na hisopo ili atakaswe.+ 5 Kuhani ataamuru ndege mumoja achinjwe ndani ya chombo cha udongo, juu ya maji yenye yalishotwa kwenye muto. 6 Lakini anapaswa kukamata ule ndege mwenye kuwa muzima na muti wa mwerezi, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na hisopo, na kutumbukiza vitu hivyo pamoja ndani ya damu ya ndege mwenye alichinjwa juu ya maji yenye yalishotwa kwenye muto. 7 Kisha kuhani atanyunyiza* damu hiyo mara saba (7) juu ya mutu mwenye kujitakasa kutokana na ukoma na atamutangaza kuwa safi, na atamuachilia ule ndege mwenye kuwa muzima aruke na kuenda katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba.+

8 “Mutu mwenye kujitakasa anapaswa kufua nguo zake na kunyoa nywele zake zote na kuoga ndani ya maji, na atakuwa safi. Kisha, anaweza kurudia katika kambi, lakini atakaa inje ya hema yake kwa siku saba (7). 9 Siku ya saba (7) anapaswa kunyoa nywele zote juu ya kichwa chake na kidevu chake na kope zake. Kisha kunyoa nywele zake zote, atafua nguo zake na kuoga ndani ya maji, kisha atakuwa safi.

10 “Siku ya munane (8), atakamata wana-kondoo dume wawili wenye hawana kasoro, mwana-kondoo dike+ katika mwaka wake wa kwanza mwenye hana kasoro, na sehemu tatu za kumi (3/10) za kipimo cha efa* ya unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kuwa toleo la nafaka,+ na logi moja* ya mafuta;+ 11 na kuhani mwenye kumutangaza kuwa safi ataleta mutu huyo mwenye anajitakasa, pamoja na matoleo hayo, mbele ya Yehova kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 12 Kuhani huyo atakamata ule mwana-kondoo dume na kumutoa kuwa toleo la hatia+ pamoja na logi moja ya mafuta, na atavitikisa mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova.+ 13 Kisha atachinjia mwana-kondoo huyo mahali kwenye toleo la zambi na toleo la kuteketezwa linazoea kuchinjwa,+ katika mahali patakatifu, kwa sababu, sawa na toleo la zambi, toleo la hatia ni la kuhani.+ Ni kitu kitakatifu sana.+

14 “Kisha kuhani atakamata sehemu fulani ya damu ya toleo la hatia, na kuhani ataitia kwenye sehemu ya chini ya sikio la kuume la mutu mwenye anajitakasa na kwenye kidole kikubwa cha mukono wake wa kuume na kidole kikubwa cha muguu wake wa kuume. 15 Na kuhani atakamata sehemu fulani ya ile logi ya mafuta+ na kuimwanga katika kiganja chake mwenyewe cha mukono wa kushoto. 16 Kisha kuhani ataingiza kidole chake cha mukono wa kuume katika mafuta yenye kuwa katika kiganja chake cha mukono wa kushoto na atanyunyiza* sehemu fulani ya mafuta hayo mara saba (7) kwa kidole chake mbele ya Yehova. 17 Kisha kuhani atatia sehemu fulani ya mafuta yenye yalibakia katika kiganja chake cha mukono kwenye sehemu ya chini ya sikio la kuume la mutu mwenye anajitakasa na kwenye kidole kikubwa cha mukono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha muguu wake wa kuume juu ya damu ya toleo la hatia. 18 Kuhani atatia mafuta yenye yalibakia katika kiganja chake cha mukono kwenye kichwa cha mutu mwenye anajitakasa, na kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mutu huyo mbele ya Yehova.+

19 “Kuhani atatoa toleo la zambi+ na kufunika zambi kwa ajili ya mutu mwenye anajitakasa kutokana na uchafu wake, na kisha atachinja toleo la kuteketezwa. 20 Kuhani atatoa toleo la kuteketezwa na toleo la nafaka+ kwenye mazabahu, na kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mutu huyo,+ naye atakuwa safi.+

21 “Lakini, kama mutu huyo ni maskini na hana mapato ya kuenea, basi atakamata mwana-kondoo dume mumoja kuwa toleo la hatia kwa ajili ya toleo la kutikiswa, ili kufunika zambi kwa ajili yake mwenyewe, na pia sehemu moja ya kumi (1/10) ya kipimo cha efa* ya unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta ili ukuwe toleo la nafaka, na logi moja ya mafuta, 22 na njiwa-tetere wawili ao njiwa wawili wadogo, kulingana na mapato yake. Ndege mumoja atatolewa kuwa toleo la zambi na mwingine kuwa toleo la kuteketezwa.+ 23 Siku ya munane (8),+ atawaleta kwa kuhani kwenye muingilio wa hema ya mukutano mbele ya Yehova ili utakaso wake uhakikishwe.+

24 “Kuhani atakamata mwana-kondoo dume wa toleo la hatia+ na logi moja ya mafuta, na kuhani atavitikisa mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova.+ 25 Kisha atamuchinja kondoo-dume mudogo wa toleo la hatia, na kuhani atakamata sehemu fulani ya damu ya toleo la hatia na kuitia kwenye sehemu ya chini ya sikio la kuume la mutu mwenye anajitakasa na kwenye kidole kikubwa cha mukono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha muguu wake wa kuume.+ 26 Kuhani atamwanga sehemu fulani ya mafuta hayo katika kiganja chake mwenyewe cha mukono wa kushoto,+ 27 na kisha atanyunyiza* kwa kidole cha mukono wake wa kuume sehemu fulani ya mafuta yenye kuwa katika kiganja cha mukono wake wa kushoto mara saba (7) mbele ya Yehova. 28 Na kuhani atatia sehemu fulani ya mafuta yenye kuwa katika kiganja chake cha mukono kwenye sehemu ya chini ya sikio la kuume la mutu mwenye anajitakasa na kwenye kidole kikubwa cha mukono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha muguu wake wa kuume kwenye sehemu zilezile zenye alitia damu ya toleo la hatia. 29 Kisha kuhani atatia mafuta yenye ilibakia katika kiganja chake cha mukono juu ya kichwa cha mutu mwenye anajitakasa, ili kufunika zambi kwa ajili ya mutu huyo mbele ya Yehova.

30 “Atatoa njiwa-tetere mumoja kati ya wale wawili ao njiwa mumoja mudogo kati ya wale wawili, kulingana na mapato yake,+ 31 ule mumoja mwenye anaweza kupata, kuwa toleo la zambi na ule mwingine kuwa toleo la kuteketezwa+ pamoja na toleo la nafaka; na kuhani atafunika zambi kwa ajili ya ule mutu mwenye anajitakasa mbele ya Yehova.+

32 “Hii ni sheria kuhusu mutu mwenye ugonjwa wa ukoma ulikuwa ndani yake lakini hana mapato wakati utakaso wake unahakikishwa.”

33 Kisha Yehova akaambia Musa na Haruni: 34 “Wakati mutaingia katika inchi ya Kanaani,+ yenye ninawapatia kuwa mali yenu,+ na kama ninaambukiza nyumba fulani katika inchi yenu na ugonjwa wa ukoma,+ 35 basi mwenye nyumba hiyo anapaswa kuenda na kumuambia kuhani, ‘Ambukizo fulani limetokea ndani ya nyumba yangu.’ 36 Kuhani atatoa amri waondoe vitu vyote vyenye kuwa ndani ya nyumba hiyo mbele hajakuja kulichunguza, ili asitangaze kila kitu chenye kuwa katika nyumba hiyo kuwa hakiko safi; na kisha kufanya vile ataingia ndani ili kuchunguza nyumba hiyo. 37 Atachunguza sehemu yenye iliambukizwa, na kama kuta za nyumba hiyo zimeambukizwa na sehemu zenye kuingia ndani za rangi ya manjano-kijani ao za rangi nyekundu na kama sehemu hizo zimeingia sana ndani ya ukuta, 38 basi kuhani atatoka ndani ya nyumba hiyo na kuenda mupaka kwenye muingilio wa nyumba hiyo na ataifunga kwa siku saba (7).+

39 “Kisha kuhani atarudia siku ya saba (7) na kufanya uchunguzi. Kama ambukizo limeenea ndani ya kuta za nyumba hiyo, 40 basi kuhani atatoa amri, na majiwe yenye yaliambukizwa yanapaswa kuondolewa na kutupwa inje ya muji mahali kwenye hakuko safi. 41 Kisha atatoa amri ili nyumba hiyo ikwaruzwe ndani pande zote, na lipu* na saruji* yenye itaondolewa inapaswa kutupwa inje ya muji mahali kwenye hakuko safi. 42 Kisha wataingiza majiwe mengine mahali pa majiwe yenye yaliondolewa, na anapaswa kutumia saruji* ingine na kufanya nyumba hiyo ipigwe lipu.*

43 “Lakini, kama ambukizo hilo linarudia na kutokea tena ndani ya nyumba hiyo kisha majiwe kubomolewa na nyumba hiyo kukwaruzwa na kupigwa tena lipu,* 44 basi kuhani ataingia ndani ya nyumba hiyo na kulichunguza. Kama ambukizo limeenea ndani ya nyumba, huo ni ukoma hatari+ ndani ya nyumba. Nyumba hiyo haiko safi. 45 Basi atatoa amri ili nyumba hiyo ibomolewe⁠—​majiwe yake, mbao zake, na lipu* yote na saruji* yote ya nyumba hiyo⁠—​na vitu hivyo vitapelekwa inje ya muji mahali kwenye hakuko safi.+ 46 Lakini kila mutu mwenye ataingia ndani ya nyumba hiyo siku yoyote yenye itakuwa imefungwa+ hatakuwa safi mupaka mangaribi;+ 47 na kila mutu mwenye analala katika nyumba hiyo anapaswa kufua nguo zake na kila mutu mwenye anakula chakula katika nyumba hiyo anapaswa kufua nguo zake.

48 “Lakini, kama kuhani anakuja na anaona kwamba ambukizo halijaenea katika nyumba kisha nyumba hiyo kupigwa tena lipu,* basi kuhani atatangaza nyumba hiyo kuwa safi, kwa sababu ambukizo hilo limepona. 49 Ili kutakasa nyumba hiyo kutokana na uchafu,* kuhani atakamata ndege mbili, muti wa mwerezi, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na hisopo.+ 50 Atachinja ndege mumoja ndani ya chombo cha udongo juu ya maji yenye yalishotwa kwenye muto. 51 Kisha atakamata ule muti wa mwerezi, ile hisopo, kile kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na ule ndege mwenye kuwa muzima na kutumbukiza vitu hivyo ndani ya damu ya ndege mwenye alichinjwa na ndani ya maji yenye yalishotwa kwenye muto, na anapaswa kunyunyiza* damu hiyo kuelekea nyumba hiyo mara saba (7).+ 52 Na atatakasa nyumba hiyo kutokana na uchafu* kwa kutumia damu ya ule ndege, yale maji yenye yalishotwa kwenye muto, ule ndege mwenye kuwa muzima, ule muti wa mwerezi, ile hisopo, na kile kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa. 53 Kisha atamuachilia ndege mwenye kuwa muzima aruke na kuenda katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba inje ya muji na atafunika zambi kwa ajili ya nyumba hiyo, nayo itakuwa safi.

54 “Hii ndiyo sheria kuhusu kila aina ya ukoma: ugonjwa wa ngozi ya kichwa ao wa ndevu,+ 55 ukoma wa nguo+ ao wa nyumba,+ 56 na kuhusu uvimbe, vigaga,* na madoa,+ 57 ili kuamua ni wakati gani kitu fulani hakiko safi ao ni wakati gani kitu fulani kiko safi.+ Hii ndiyo sheria kuhusu ukoma.”+

15 Yehova akaendelea kusema na Musa na Haruni, na kumuambia: 2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Kama mwanaume iko* na mutiririko katika kiungo chake cha uzazi,* mutiririko huo unamufanya asikuwe safi.+ 3 Hatakuwa safi kwa sababu ya mutiririko huo, ikuwe mutiririko huo unaendelea kutoka katika viungo vyake vya uzazi ao mutiririko huo unazuiwa kutoka, anaendelea kuwa mwenye haiko safi.

4 “‘Kitanda chochote chenye mutu mwenye kuwa na mutiririko analalia hakitakuwa safi, na kila kitu chenye anaikalia hakitakuwa safi. 5 Mutu mwenye anagusa kitanda cha mutu huyo anapaswa kufua nguo zake, na anapaswa kuoga ndani ya maji na hatakuwa safi mupaka mangaribi.+ 6 Kila mutu mwenye anakaa kwenye kitu chenye mutu mwenye kuwa na mutiririko aliikalia anapaswa kufua nguo zake, na kuoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi. 7 Kila mutu mwenye anagusa mutu mwenye iko* na mutiririko anapaswa kufua nguo zake, kuoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi. 8 Kama mutu mwenye kuwa na mutiririko anamutemea mate mutu mwenye kuwa safi, mutu huyo mwenye alitemewa mate anapaswa kufua nguo zake, kuoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi. 9 Kitu chochote cha* kuikalia juu ya mugongo wa munyama chenye mutu mwenye kuwa na mutiririko ataikalia hakitakuwa safi. 10 Kila mutu mwenye atagusa kitu chochote chenye mutu huyo aliikalia hatakuwa safi mupaka mangaribi, na kila mutu mwenye atabeba vitu hivyo atafua nguo zake, ataoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi. 11 Kama mutu mwenye kuwa na mutiririko+ hakunawa mikono yake ndani ya maji na anamugusa mutu fulani, basi mutu huyo mwenye aliguswa anapaswa kufua nguo zake, kuoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi. 12 Chombo cha udongo chenye mutu mwenye kuwa na mutiririko anagusa kinapaswa kuvunjwa-vunjwa, na chombo chochote cha mbao kinapaswa kusafishwa na maji.+

13 “‘Wakati mutiririko unaacha kutoka na mutu huyo anakuwa safi kutokana na mutiririko huo, basi atahesabia siku saba (7) kwa ajili ya utakaso wake, na anapaswa kufua nguo zake, kuoga ndani ya maji yenye yalishotwa kwenye muto, naye atakuwa safi.+ 14 Siku ya munane (8), anapaswa kukamata njiwa-tetere wawili ao njiwa wawili wadogo+ na kuenda mbele ya Yehova kwenye muingilio wa hema ya mukutano na kumupatia kuhani ndege hao. 15 Na kuhani atatoa ndege hao, mumoja kuwa toleo la zambi na mwingine kuwa toleo la kuteketezwa, na kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mutu huyo mbele ya Yehova kwa sababu ya mutiririko wake.

16 “‘Sasa kama mwanaume anatokwa na mbegu za uzazi,* anapaswa kuoga mwili wake wote ndani ya maji na hatakuwa safi mupaka mangaribi.+ 17 Anapaswa kufua nguo yoyote kwa maji na ngozi yoyote yenye mbegu za uzazi ziko* juu yake, na haitakuwa safi mupaka mangaribi.

18 “‘Wakati mwanaume analala na mwanamuke na anatokwa na mbegu za uzazi,* wanapaswa kunawa miili yao ndani ya maji na hawatakuwa safi mupaka mangaribi.+

19 “‘Kama mwanamuke iko* na mutiririko wa damu katika mwili wake, ataendelea kuwa katika uchafu wa siku zake za kuona mwezi* kwa siku saba (7).+ Kila mutu mwenye anamugusa hatakuwa safi mupaka mangaribi.+ 20 Kila kitu chenye analalia wakati wa uchafu wa siku zake za kuona mwezi* hakitakuwa safi, na kila kitu chenye anaikalia hakitakuwa safi.+ 21 Kila mutu mwenye anagusa kitanda cha mwanamuke huyo anapaswa kufua nguo zake, kuoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi. 22 Kila mutu mwenye anagusa kitu chochote chenye mwanamuke huyo aliikalia anapaswa kufua nguo zake, kuoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi. 23 Kama alikaa juu ya kitanda ao juu ya kitu kingine, kugusa kitu hicho kutafanya mutu asikuwe safi mupaka mangaribi.+ 24 Na kama mwanaume analala na mwanamuke huyo na uchafu wa siku zake za kuona mwezi* unakuja juu ya mwanaume huyo,+ basi hatakuwa safi kwa siku saba (7), na kitanda chochote chenye mwanaume huyo analalia hakitakuwa safi.

25 “‘Wakati mutiririko wa damu wa mwanamuke unatiririka kwa siku nyingi+ wakati haiko siku zake za kawaida za kuona mwezi,*+ ao kama anakuwa na mutiririko kwa wakati murefu kuliko siku zake za kawaida za kuona mwezi, hatakuwa safi katika siku zote za mutiririko wake, kama vile inakuwa katika siku za uchafu wake wa kuona mwezi. 26 Kila kitanda chenye analalia wakati wa siku za mutiririko wake kitakuwa kama kitanda cha uchafu wa siku zake za kuona mwezi,*+ na kila kitu chenye anaikalia hakitakuwa safi kama vile uchafu wa siku zake za kuona mwezi. 27 Kila mutu mwenye anagusa vitu hivyo hatakuwa safi, na anapaswa kufua nguo zake, kuoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi.+

28 “‘Lakini, wakati anakuwa safi kutokana na mutiririko wake, atahesabia siku saba (7), na kisha atakuwa safi.+ 29 Siku ya munane (8), atakamata njiwa-tetere wawili ao njiwa wawili wadogo,+ na atawapelekea kuhani kwenye muingilio wa hema ya mukutano.+ 30 Kuhani atamutoa ndege mumoja kwa ajili ya toleo la zambi na ndege mwingine kwa ajili ya toleo la kuteketezwa, na kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mwanamuke huyo mbele ya Yehova kwa sababu ya mutiririko wake wenye hauko safi.+

31 “‘Kwa hiyo munapaswa kufanya Waisraeli wajitenge mbali na uchafu wao, ili wasikufe katika uchafu wao kwa kuchafua tabenakulo yangu, yenye kuwa katikati yao.+

32 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu mwanaume mwenye kuwa na mutiririko, mwanaume mwenye haiko safi kwa sababu ya kutokwa na mbegu za uzazi,*+ 33 mwanamuke katika uchafu wa siku zake za kuona mwezi,+ kila mwanaume ao mwanamuke mwenye kuwa na mutiririko kutoka katika mwili,+ na mwanaume mwenye analala na mwanamuke mwenye haiko safi.’”

16 Yehova akasema na Musa kisha kifo cha wana wawili wa Haruni wenye walikufa kwa sababu ya kumukaribia Yehova.+ 2 Yehova akamuambia Musa: “Ambia Haruni ndugu yako kwamba asikuwe anaingia tu wakati wowote katika mahali patakatifu+ ndani ya pazia,+ mbele ya kifuniko cha Sanduku, ili asikufe,+ kwa sababu nitatokea katika wingu+ juu ya kifuniko hicho.+

3 “Hivi ndivyo vitu vyenye Haruni anapaswa kuleta wakati anaingia katika mahali patakatifu: ngombe-dume mudogo kwa ajili ya toleo la zambi+ na kondoo-dume kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.+ 4 Anapaswa kuvaa kanzu takatifu ya kitani,+ na kapitula* za kitani+ zinapaswa kufunika mwili wake,* na anapaswa kujifunga kitambaa cha kujifunga kiuno cha kitani+ na kuvaa kilemba cha kitani kwenye kichwa chake.+ Hayo ni nguo takatifu.+ Ataoga ndani ya maji+ na kuvaa nguo hizo.

5 “Anapaswa kukamata kutoka katika mukusanyiko wa Waisraeli+ wana-mbuzi dume wawili kwa ajili ya toleo la zambi na kondoo-dume mumoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.

6 “Kisha Haruni anapaswa kumutoa ule ngombe-dume wa toleo la zambi, mwenye kuwa kwa ajili yake mwenyewe, na atafunika zambi kwa ajili yake mwenyewe+ na kwa ajili ya nyumba yake.

7 “Kisha atakamata wale mbuzi wawili na kuwasimamisha mbele ya Yehova kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 8 Haruni atapiga kura juu ya mbuzi hao wawili, kura moja kwa ajili ya Yehova na ingine kwa ajili ya Azazeli.* 9 Haruni atamutoa ule mbuzi mwenye alichaguliwa kwa kura+ kwa ajili ya Yehova na atamufanya kuwa toleo la zambi. 10 Lakini ule mbuzi mwenye alichaguliwa kwa kura kwa ajili ya Azazeli anapaswa kupelekwa akiwa muzima kusudi asimame mbele ya Yehova ili kufunika zambi juu yake, kusudi aachiliwe aende katika pori kwa ajili ya Azazeli.+

11 “Haruni atamutoa ule ngombe-dume wa toleo la zambi, mwenye kuwa kwa ajili yake mwenyewe, na atafunika zambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya nyumba yake; kisha atamuchinja ule ngombe-dume wa toleo la zambi, mwenye kuwa kwa ajili yake mwenyewe.+

12 “Kisha atakamata chetezo+ chenye kujaa makaa yenye kuwaka kwenye mazabahu+ mbele ya Yehova na mikono mbili yenye kujaa uvumba muzuri wenye marashi,+ na ataleta vitu hivyo ndani ya pazia.+ 13 Pia atatia uvumba huo juu ya moto mbele ya Yehova,+ na wingu la uvumba huo litafunika kifuniko cha Sanduku,+ chenye kuwa juu ya Ushuhuda,+ ili asikufe.

14 “Atakamata sehemu fulani ya damu ya ngombe-dume+ na kuinyunyiza* kwa kidole chake mbele ya kifuniko upande wa mashariki, na atanyunyiza* kwa kidole chake sehemu fulani ya damu hiyo mara saba (7) mbele ya kifuniko hicho.+

15 “Kisha atamuchinja ule mbuzi wa toleo la zambi, mwenye kuwa kwa ajili ya watu,+ na kuleta damu yake ndani ya pazia+ na kufanya na damu yake+ kama vile alifanya na damu ya ule ngombe-dume; atanyunyiza* damu hiyo kuelekea kifuniko na mbele ya kifuniko.

16 “Anapaswa kufunika zambi kwa ajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya matendo ya uchafu ya Waisraeli na kwa sababu ya makosa yao na zambi zao,+ na ni vile anapaswa kufanya kwa ajili ya hema ya mukutano, lenye kuwa kati yao katikati ya matendo yao ya uchafu.

17 “Hakuna mutu mwingine mwenye anapaswa kuwa ndani ya hema ya mukutano kuanzia wakati Haruni ataingia katika mahali patakatifu ili kufunika zambi mupaka wakati ataenda inje. Atafunika zambi kwa ajili yake mwenyewe na nyumba yake,+ na kwa ajili ya kutaniko lote la Israeli.+

18 “Kisha atatoka inje na kuenda kwenye mazabahu,+ yenye kuwa mbele ya Yehova, na atafunika zambi kwa ajili ya mazabahu hiyo, na atakamata sehemu fulani ya damu ya ule ngombe-dume na sehemu fulani ya damu ya ule mbuzi na kuitia kwenye pembe za mazabahu pande zote. 19 Pia atanyunyiza* sehemu fulani ya damu hiyo kwa kidole chake mara saba (7) juu ya mazabahu na atasafisha mazabahu hiyo na kuitakasa kwa sababu ya matendo ya uchafu ya Waisraeli.

20 “Wakati atakuwa amemaliza kufunika zambi+ kwa ajili ya mahali patakatifu na hema ya mukutano na mazabahu,+ atamutoa pia ule mbuzi mwenye kuwa muzima.+ 21 Haruni ataweka mikono yake mbili juu ya kichwa cha ule mbuzi mwenye kuwa muzima na kuungama juu yake makosa yote ya Waisraeli na maovu yao yote na zambi zao zote, na ataziweka juu ya kichwa cha ule mbuzi+ na kumutuma katika jangwa kupitia mukono wa mutu mwenye alichaguliwa ili kufanya vile.* 22 Ule mbuzi atabeba juu yake mwenyewe makosa yao yote+ mupaka katika eneo la jangwa,+ na mutu huyo atamuachilia ule mbuzi aende katika jangwa.+

23 “Kisha Haruni ataingia katika hema ya mukutano na kutosha zile nguo za kitani zenye alivaa wakati aliingia katika mahali patakatifu, na atazitia pale chini. 24 Anapaswa kuoga ndani ya maji+ katika mahali patakatifu na kuvaa nguo zake;+ kisha atatoka inje na kutoa toleo lake la kuteketezwa+ na toleo la watu la kuteketezwa+ na kufunika zambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu.+ 25 Atachoma mafuta ya toleo la zambi ili yatoe moshi juu ya mazabahu.

26 “Ule mutu mwenye alipeleka mbuzi kwa ajili ya Azazeli+ anapaswa kufua nguo zake na kuoga ndani ya maji, na kisha anaweza kurudia katika kambi.

27 “Na ule ngombe-dume wa toleo la zambi na ule mbuzi wa toleo la zambi, wenye damu yao ililetwa katika mahali patakatifu ili kufunika zambi, watapelekwa inje ya kambi, na ngozi zao, nyama yao na mavi yao vitateketezwa ndani ya moto.+ 28 Mutu mwenye anateketeza vitu hivyo ndani ya moto anapaswa kufua nguo zake na kuoga ndani ya maji, na kisha anaweza kurudia katika kambi.

29 “Hii itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yenu: Katika mwezi wa saba (7), siku ya kumi (10) ya mwezi huo, munapaswa kujitesa,* na hamupaswe kufanya kazi yoyote,+ ikuwe mwenyeji ao mugeni mwenye anaishi kati yenu. 30 Siku hiyo zambi itafunikwa+ kwa ajili yenu, ili kuwatangaza kuwa safi. Mutasafishwa zambi zenu zote mbele ya Yehova.+ 31 Ni sabato ya pumuziko kamili kwa ajili yenu, na munapaswa kujitesa.*+ Ni sheria ya kudumu.

32 “Kuhani mwenye kutiwa mafuta+ na kuwekwa katika madaraka* ili atumike akiwa kuhani+ pa nafasi ya baba yake+ atafunika zambi na kuvaa zile nguo za kitani,+ zile nguo takatifu.+ 33 Atafunika zambi kwa ajili ya patakatifu,+ hema ya mukutano,+ na mazabahu;+ na atafunika zambi kwa ajili ya makuhani na kwa ajili ya watu wote wa kutaniko.+ 34 Hiyo itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yenu,+ ili kufunika zambi kwa ajili ya Waisraeli kuhusu zambi zao zote mara moja kila mwaka.”+

Kwa hiyo Haruni akafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.

17 Yehova akaendelea kusema na Musa: 2 “Sema na Haruni na wana wake na Waisraeli wote na uwaambie, ‘Yehova ameamuru hivi:

3 “‘“Kama mutu yeyote wa nyumba ya Israeli anachinja ngombe-dume ao mwana-kondoo dume ao mbuzi ndani ya kambi ao kama anamuchinja inje ya kambi, 4 kuliko kumuleta kwenye muingilio wa hema ya mukutano ili kumutoa kuwa toleo kwa Yehova mbele ya tabenakulo ya Yehova, mutu huyo atakuwa na hatia ya damu. Amemwanga damu na mutu huyo anapaswa kuondolewa* katikati ya watu wake. 5 Itakuwa vile ili Waisraeli wamuletee Yehova zabihu, zenye wanatoa kwa sasa katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba, wamuletee kuhani zabihu hizo kwenye muingilio wa hema ya mukutano. Wanapaswa kumutolea Yehova zabihu hizo zikiwa zabihu za ushirika.+ 6 Na kuhani atanyunyiza* damu ya zabihu hizo juu ya mazabahu ya Yehova kwenye muingilio wa hema ya mukutano na atachoma mafuta yake ili yatoe moshi na kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova.+ 7 Kwa hiyo hawapaswe tena kutoa zabihu kwa pepo wachafu wenye kufanana mbuzi,*+ wenye wanafanya nao ukahaba.+ Hiyo itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yenu katika vizazi vyenu vyote.”’

8 “Unapaswa kuwaambia, ‘Kila mutu wa nyumba ya Israeli ao kila mugeni mwenye anaishi katikati yenu mwenye atatoa toleo la kuteketezwa ao zabihu 9 na hailete kwenye muingilio wa hema ya mukutano ili kuitolea Yehova anapaswa kuondolewa* katikati ya watu wake.+

10 “‘Kama mutu yeyote wa nyumba ya Israeli ao mugeni yeyote mwenye anaishi katikati yenu anakula damu ya namna yoyote,+ hakika nitakunja uso wangu juu ya mutu huyo mwenye anakula* damu, na nitamuondoa* katikati ya watu wake. 11 Kwa maana uzima wa mwili uko* katika damu,+ na mimi mwenyewe nimeitoa kwenye mazabahu+ kwa ajili yenu* ili mufunike zambi kwa ajili yenu wenyewe, kwa maana damu ndiyo inafunika zambi+ kupitia uzima wenye* kuwa ndani yake. 12 Ndiyo sababu nimewaambia Waisraeli: “Hakuna mutu* katikati yenu mwenye anapaswa kula damu, na hakuna mugeni mwenye anaishi katikati yenu+ mwenye anapaswa kula damu.”+

13 “‘Kama mutu fulani katikati ya Waisraeli ao mugeni fulani mwenye anaishi katikati yenu anawinda na anakamata munyama wa pori ao ndege mwenye anaweza kukuliwa, anapaswa kumwanga damu yake chini+ na kuifunika kwa mavumbi. 14 Kwa maana uzima wa* kila namna ya mwili ni damu yake, kwa sababu uzima uko* ndani ya damu. Kwa hiyo, niliambia Waisraeli: “Hamupaswe kula damu ya namna yoyote ya mwili kwa sababu uzima wa* kila namna ya mwili uko katika damu yake. Kila mutu mwenye anakula damu ataondolewa.”*+ 15 Kama mutu fulani, ikuwe mwenyeji ao mugeni, anakula munyama mwenye alipatikana amekufa ao mwenye alipasuliwa na munyama wa pori,+ basi anapaswa kufua nguo zake na kuoga ndani ya maji na hatakuwa safi mupaka mangaribi;+ kisha atakuwa safi. 16 Lakini kama hafue nguo hizo na haoge mwili wake, atajibu kwa sababu ya kosa lake.’”+

18 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.+ 3 Hamupaswe kujiendesha kama vile wanajiendesha katika inchi ya Misri, kwenye mulikuwa munaishi, na hamupaswe kufanya mambo yenye wanafanya katika inchi ya Kanaani, kwenye ninawapeleka.+ Na hamupaswe kufuata sheria zao. 4 Munapaswa kutimiza maamuzi yangu ya hukumu, na munapaswa kushika amri zangu na kuzifuata.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu. 5 Munapaswa kushika sheria zangu na maamuzi yangu ya hukumu; kila mutu mwenye anafanya vile ataishi kupitia mambo hayo.+ Mimi ni Yehova.

6 “‘Mutu yeyote kati yenu asimukaribie mutu yeyote wa jamaa yake ya karibu ili kufanya ngono* naye.+ Mimi ni Yehova. 7 Haupaswe kufanya ngono na baba yako, na haupaswe kufanya ngono na mama yako. Yeye ni mama yako, na haupaswe kufanya ngono naye.

8 “‘Haupaswe kufanya ngono na bibi ya baba yako.+ Kufanya vile ni kumuletea baba yako haya.*

9 “‘Haupaswe kufanya ngono na dada yako, ikuwe mutoto mwanamuke wa baba yako ao mutoto mwanamuke wa mama yako, ikuwe amezaliwa katika nyumba ileile ao amezaliwa inje ya nyumba ile.+

10 “‘Haupaswe kufanya ngono na binti ya mwana wako ao binti ya binti yako, kwa sababu wao ni uchi wako mwenyewe.

11 “‘Haupaswe kufanya ngono na mutoto mwanamuke wa bibi ya baba yako, uzao wa baba yako, kwa sababu yeye ni dada yako.

12 “‘Haupaswe kufanya ngono na dada ya baba yako. Iko* na uhusiano wa damu pamoja na baba yako.+

13 “‘Haupaswe kufanya ngono na dada ya mama yako, kwa sababu iko* na uhusiano wa damu pamoja na mama yako.

14 “‘Haupaswe kumuletea ndugu ya baba yako haya* kwa kufanya ngono na bibi yake. Yeye ni shangazi* yako.+

15 “‘Haupaswe kufanya ngono na binti-mukwe wako.+ Yeye ni bibi ya mwana wako, na haupaswe kufanya ngono naye.

16 “‘Haupaswe kufanya ngono na bibi ya ndugu yako,+ kwa sababu kufanya vile ni kumuletea ndugu yako haya.*

17 “‘Haupaswe kufanya ngono na mwanamuke pamoja na binti yake.+ Haupaswe kukamata binti ya mwana wake na binti ya binti yake ili kulala naye. Wao ni watu wa jamaa yake ya karibu; ni tendo chafu.*

18 “‘Haupaswe kuchukua mwanamuke pamoja na dada yake ili akuwe bibi-mushindani wake+ na kufanya ngono naye wakati dada yake angali muzima.

19 “‘Haupaswe kumukaribia mwanamuke wakati wa uchafu wake wa kuona mwezi ili kufanya ngono naye.+

20 “‘Haupaswe kufanya ngono na bibi ya mwanaume mwenzako,* kufanya vile ni kujichafua.+

21 “‘Haupaswe kuruhusu muzao wako yeyote atolewe zabihu kwa Moleki.+ Haupaswe kuchafua jina la Mungu wako kwa njia hiyo.+ Mimi ni Yehova.

22 “‘Haupaswe kulala na mwanaume kama vile unalala na mwanamuke.+ Hilo ni tendo lenye kuchukiza.

23 “‘Mwanaume hapaswe kufanya ngono na munyama ili kujichafua kwa tendo hilo; wala mwanamuke hapaswe kujitoa kwa munyama ili kufanya ngono naye.+ Kufanya vile ni kuvunja sheria ya asili.

24 “‘Musijichafue kwa jambo lolote kati ya mambo hayo, kwa maana mataifa yenye ninafukuza kutoka mbele yenu yamejichafua kupitia mambo hayo yote.+ 25 Ndiyo maana inchi hiyo haiko safi, na nitaleta azabu juu ya inchi hiyo kwa sababu ya kosa lake, na inchi hiyo itatapika wakaaji wake.+ 26 Lakini ninyi munapaswa kushika sheria zangu na maamuzi yangu ya hukumu,+ na hamupaswe kufanya jambo lolote kati ya mambo hayo yenye kuchukiza, ikuwe mwenyeji ao mugeni mwenye kuishi kati yenu.+ 27 Kwa maana watu wenye waliishi katika inchi hiyo mbele yenu walifanya mambo hayo yote yenye kuchukiza,+ na sasa inchi hiyo haiko safi. 28 Basi inchi hiyo haitawatapika kwa sababu ya kuichafua kama vile itatapika mataifa yenye yaliwatangulia. 29 Kama mutu anafanya jambo lolote kati ya mambo hayo yenye kuchukiza, wote wenye kufanya mambo hayo wanapaswa* kuondolewa* katikati ya watu wao. 30 Munapaswa kushika mambo yenye nimewaomba kwa kukataa kufuata desturi zozote zenye kuchukiza ambazo zilifuatwa mbele yenu,+ ili musijichafue kupitia desturi hizo. Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

19 Yehova akasema tena na Musa, na kumuambia: 2 “Sema na kutaniko lote la Waisraeli na uwaambie, ‘Munapaswa kuwa watakatifu, kwa sababu mimi, Yehova Mungu wenu, ni mutakatifu.+

3 “‘Kila mumoja wenu anapaswa kumuheshimia* mama yake na baba yake,+ na munapaswa kushika sabato zangu.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu. 4 Musiendee miungu yenye haina mafaa yoyote+ ao kujitengenezea sanamu za miungu ya metali yenye kuyeyushwa.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.

5 “‘Sasa kama munamutolea Yehova zabihu ya ushirika,+ munapaswa kuitoa kwa njia yenye itafanya mukubaliwe.+ 6 Inapaswa kukuliwa siku yenye munaitoa na kesho yake, lakini yenye itabakia mupaka siku ya tatu (3) inapaswa kuteketezwa ndani ya moto.+ 7 Lakini, kama sehemu yoyote ya zabihu hiyo inakuliwa siku ya tatu (3), ni kitu chenye kuchukiza chenye hakitakubaliwa. 8 Mutu mwenye anaikula atajibu kwa sababu ya kosa lake kwa maana amechafua kitu kitakatifu cha Yehova, na mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katikati ya watu wake.

9 “‘Wakati munavuna mavuno ya inchi yenu, haupaswe kuvuna mavuno yote ya mipaka ya shamba lako na haupaswe kuokota masalio ya mavuno yako.+ 10 Pia, usikusanye masalio ya shamba lako la mizabibu wala usiokote zabibu zenye kusambaa za shamba lako la mizabibu. Unapaswa kuziachia maskini*+ na wakaaji wageni. Mimi ni Yehova Mungu wenu.

11 “‘Hamupaswe kuiba,+ hamupaswe kudanganya,+ na hamupaswe kutendeana kwa uongo. 12 Hamupaswe kuapa kwa uongo katika jina langu+ na hivyo kuchafua jina la Mungu wenu. Mimi ni Yehova. 13 Haupaswe kumupunja mwenzako,+ na haupaswe kunyanganya.+ Haupaswe kubakia na mushahara wa mufanyakazi usiku wote mupaka asubui.+

14 “‘Haupaswe kumulaani* kiziwi wala kuweka kizuizi mbele ya kipofu,+ na unapaswa kumuogopa Mungu wako.+ Mimi ni Yehova.

15 “‘Haupaswe kuhukumu kwa njia yenye haiko ya haki. Haupaswe kubagua maskini ao kuonyesha upendeleo kwa matajiri.+ Unapaswa kumuhukumu mwenzako kwa haki.

16 “‘Haupaswe kuzunguka-zunguka ili kueneza maneno ya kuchongea kati ya watu wako.+ Haupaswe kuweka uzima wa* mwenzako katika hatari.*+ Mimi ni Yehova.

17 “‘Haupaswe kumuchukia ndugu yako katika moyo wako.+ Unapaswa kumukaripia mwenzako,+ ili usichukue zambi pamoja naye.

18 “‘Haupaswe kulipiza kisasi+ wala kuwekea kinyongo wana wa watu wako, na unapaswa kumupenda mwenzako kama wewe mwenyewe.+ Mimi ni Yehova.

19 “‘Munapaswa kushika sheria zangu: Haupaswe kufanya wanyama wako wa kufugwa wa aina moja wazae pamoja na wanyama wa kufugwa wa aina ingine. Haupaswe kupanda mbegu za aina mbili katika shamba lako,+ na haupaswe kuvaa nguo yenye ilitengenezwa na nyuzi za aina mbili zenye kuchanganywa pamoja.+

20 “‘Sasa kama mwanaume analala na mwanamuke na anafanya ngono naye na mwanamuke huyo ni mutumishi mwenye amewekwa kwa ajili ya mwanaume mwingine, lakini mwanamuke huyo hajakombolewa ao kupewa uhuru wake, kunapaswa kuwa azabu. Lakini, hawapaswe kuuawa, kwa sababu mwanamuke huyo alikuwa hajawekwa huru. 21 Mwanaume huyo anapaswa kumuletea Yehova toleo lake la hatia kwenye muingilio wa hema ya mukutano, kondoo-dume wa toleo la hatia.+ 22 Kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mwanaume huyo kupitia kondoo-dume wa toleo la hatia mbele ya Yehova kwa sababu ya zambi yenye alifanya, na atasamehewa zambi yenye alifanya.

23 “‘Wakati mutaingia katika inchi hiyo na kupanda muti wowote kwa ajili ya chakula, munapaswa kuona matunda yake kuwa machafu na yenye kukatazwa. Kwa miaka tatu (3) yatakuwa yenye kukatazwa.* Hayapaswe kukuliwa. 24 Lakini katika mwaka wa ine (4), matunda yake yote yatakuwa matakatifu kwa ajili ya kushangilia mbele ya Yehova.+ 25 Kisha katika mwaka wa tano (5), munaweza kula matunda yake ili kuongeza mazao yake kwenye mavuno yenu. Mimi ni Yehova Mungu wenu.

26 “‘Hamupaswe kula kitu chochote chenye kuwa na damu.+

“‘Hamupaswe kutafuta alama za mambo yenye yatatokea ao kufanya uchawi.+

27 “‘Hamupaswe kunyoa* nywele zenye kuwa kwenye kila upande wa kichwa chenu ao kuharibu umbo ya pembeni-pembeni ya ndevu zenu.+

28 “‘Hamupaswe kujikata-kata katika mwili wenu kwa ajili ya mutu mwenye amekufa,*+ na hamupaswe kujitia alama za machanjo. Mimi ni Yehova.

29 “‘Usimuletee binti yako haya kwa kumufanya kuwa kahaba,+ ili inchi isifanye ukahaba na kujaa matendo yenye kupotoka.+

30 “‘Munapaswa kushika sabato zangu,+ na munapaswa kuheshimia* patakatifu pangu. Mimi ni Yehova.

31 “‘Musiendee watu wenye kupashana habari na pepo wachafu,+ na musitafute shauri kwa watu wenye kutabiri matukio+ ili musijichafue kupitia watu hao. Mimi ni Yehova Mungu wenu.

32 “‘Unapaswa kusimama mbele ya kichwa chenye imvi,+ na unapaswa kumuheshimia mutu mwenye kuzeeka,+ na unapaswa kumuogopa Mungu wako.+ Mimi ni Yehova.

33 “‘Kama mugeni anaishi pamoja na ninyi katika inchi yenu, hamupaswe kumutesa.+ 34 Mugeni mwenye anaishi pamoja na ninyi mutamuona kama mwenyeji kati yenu;+ na unapaswa kumupenda kama vile unajipenda mwenyewe, kwa maana mulikuwa wakaaji wageni katika inchi ya Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.

35 “‘Hamupaswe kutumia vipimo vya uongo ili kupima urefu, uzito, ao ujazo.*+ 36 Munapaswa kutumia mizani* yenye kuwa sawa, vipimo vyenye kuwa sawa, kipimo chenye kuwa sawa cha vitu vyenye kukauka,* na kipimo chenye kuwa sawa cha vitu vya majimaji.*+ Mimi ni Yehova Mungu wenu, mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri. 37 Kwa hiyo munapaswa kushika sheria zangu zote na maamuzi yangu yote ya hukumu, na munapaswa kuyafuata.+ Mimi ni Yehova.’”

20 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Utaambia Waisraeli, ‘Mwanaume yeyote wa Israeli na mugeni yeyote mwenye anaishi katika Israeli mwenye atamutoa muzao wake yeyote kwa Moleki anapaswa kabisa kuuawa.+ Watu wa inchi wanapaswa kumuua kwa kumupiga majiwe. 3 Mimi mwenyewe nitakunja uso wangu juu ya mutu huyo, na nitamuondoa* katikati ya watu wake, kwa sababu amemutoa mumoja wa wazao wake kwa Moleki na amechafua mahali pangu patakatifu+ na kuchafua jina langu takatifu. 4 Kama watu wa inchi wanafunga macho yao kwa makusudi juu ya jambo lenye mutu huyo anafanya wakati anamutoa muzao wake kwa Moleki na hawamuue,+ 5 basi mimi mwenyewe hakika nitakunja uso wangu juu ya mutu huyo na familia yake.+ Nitamuondoa* katikati ya watu wake, yeye pamoja na watu wote wenye walijiunga naye katika kufanya ukahaba na Moleki.

6 “‘Kuhusu mutu mwenye anaendea* watu wenye kupashana habari na pepo wachafu+ na watu wenye kutabiri matukio+ ili kufanya ukahaba pamoja nao, hakika nitageukia mutu huyo* na kumuondoa* katikati ya watu wake.+

7 “‘Munapaswa kujitakasa na kuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni Yehova Mungu wenu. 8 Na munapaswa kushika sheria zangu na kuzifuata.+ Mimi ni Yehova, mwenye anawatakasa.+

9 “‘Kama mutu yeyote anamulaani* baba yake ao mama yake, anapaswa kabisa kuuawa.+ Kwa kuwa amemulaani baba yake ao mama yake, damu yake iko juu yake.

10 “‘Sasa kuhusu mwanaume mwenye anafanya uzinifu na bibi ya mwanaume mwingine: Mwanaume mwenye anafanya uzinifu na bibi ya mwenzake anapaswa kabisa kuuawa, ule mwanaume muzinifu na pia ule mwanamuke muzinifu.+ 11 Mwanaume mwenye analala na bibi ya baba yake amemuletea baba yake haya.*+ Wote wawili wanapaswa kabisa kuuawa. Damu yao iko juu yao. 12 Kama mwanaume analala na binti-mukwe wake, wote wawili wanapaswa kabisa kuuawa. Wamevunja sheria ya asili. Damu yao iko juu yao.+

13 “‘Kama mwanaume analala na mwanaume mwenzake kama vile mutu analala na mwanamuke, wote wawili wamefanya kitu chenye kuchukiza.+ Wanapaswa kabisa kuuawa. Damu yao iko juu yao.

14 “‘Kama mwanaume anachukua mwanamuke na mama yake, hilo ni tendo chafu.*+ Wanapaswa kumuteketeza yeye na wao ndani ya moto,+ ili mwenendo huo muchafu usiendelee kati yenu.

15 “‘Kama mwanaume anafanya ngono na munyama, anapaswa kabisa kuuawa, na munapaswa kumuua munyama huyo.+ 16 Kama mwanamuke anamukaribia munyama yeyote ili kufanya ngono naye,+ munapaswa kumuua mwanamuke huyo na munyama huyo. Wanapaswa kabisa kuuawa. Damu yao iko juu yao.

17 “‘Kama mwanaume anafanya ngono na dada yake, binti ya baba yake ao binti ya mama yake, na anaona uchi wake, na dada yake anaona uchi wake, hilo ni jambo la haya sana.+ Wanapaswa kuondolewa* mbele ya macho ya wana wao. Amemuletea dada yake haya.* Anapaswa kujibu kwa sababu ya kosa lake.

18 “‘Kama mwanaume anafanya ngono na mwanamuke mwenye iko* katika siku zake za kuona mwezi* na anafanya naye ngono, mwanaume huyo na mwanamuke huyo wamefunua mutiririko wa damu yake.+ Wote wawili wanapaswa kuondolewa* katikati ya watu wao.

19 “‘Haupaswe kufanya ngono na dada ya mama yako ao na dada ya baba yako, kwa sababu kufanya vile ni kumuletea haya mutu mwenye iko* na uhusiano wa damu pamoja na wewe.+ Wanapaswa kujibu kwa sababu ya kosa lao. 20 Mwanaume mwenye analala na bibi ya ndugu ya baba yake amemuletea ndugu ya baba yake haya.*+ Wanapaswa kujibu kwa sababu ya zambi yao. Watakufa bila kuzaa mutoto. 21 Kama mwanaume anachukua bibi ya ndugu yake, hilo ni jambo lenye kuchukiza sana.+ Amemuletea ndugu yake haya.* Hawatazaa mutoto.

22 “‘Munapaswa kushika sheria zangu zote na maamuzi yangu yote ya hukumu+ na kuyatenda,+ ili inchi kwenye ninawapeleka muishi isiwatapike.+ 23 Hamupaswe kufuata sheria za mataifa yenye ninafukuza kutoka mbele yenu;+ kwa sababu yamefanya mambo hayo yote, na ninachukia mataifa hayo.+ 24 Ndiyo sababu niliwaambia: “Mutariti inchi yao, na nitawapatia inchi hiyo ikuwe mali yenu, inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu, mwenye amewatenga na vikundi vingine vya watu.”+ 25 Munapaswa kufanya tofauti kati ya munyama mwenye kuwa safi na mwenye haiko safi na ndege mwenye haiko safi na mwenye kuwa safi;+ hamupaswe kujifanya kuwa wenye* kuchukiza kupitia munyama ao ndege ao kitu chochote chenye kutambaa juu ya udongo chenye nimetenga ili mukione kuwa hakiko safi.+ 26 Munapaswa kuwa watakatifu mbele yangu, kwa sababu mimi, Yehova, niko mutakatifu,+ na ninawatenga na vikundi vingine vya watu ili mukuwe watu wangu.+

27 “‘Kila mwanaume ao mwanamuke mwenye kupashana habari na pepo wachafu ao mwenye kutabiri matukio* anapaswa kabisa kuuawa.+ Watu wanapaswa kuwaua kwa kuwapiga majiwe. Damu yao iko juu yao.’”

21 Yehova akaendelea kumuambia Musa: “Sema na wana wa Haruni, makuhani, na uwaambie, ‘Mutu yeyote asijichafue kwa ajili ya mutu mwenye alikufa* kati ya watu wake.+ 2 Lakini anaweza kufanya vile kwa ajili ya mutu wa karibu mwenye iko* na uhusiano wa damu pamoja naye, kwa ajili ya mama yake, baba yake, mutoto wake mwanaume, mutoto wake mwanamuke, ndugu yake, 3 na anaweza kujichafua kwa ajili ya dada yake kama ni bikira wa jamaa yake ya karibu na hajaolewa. 4 Hapaswe kujichafua na kujifanya asikuwe safi kwa ajili ya mwanamuke mwenye kuwa na bwana katikati ya watu wake. 5 Hawapaswe kujifanyia upara kwenye vichwa vyao+ ao kunyoa mwisho-mwisho wa ndevu zao ao kujikata-kata mwili.+ 6 Wanapaswa kuwa watakatifu mbele ya Mungu wao,+ na hawapaswe kuchafua jina la Mungu wao,+ kwa sababu wanatoa matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto, mukate wa* Mungu wao, na wanapaswa kuwa watakatifu.+ 7 Hawapaswe kumuoa kahaba,+ mwanamuke mwenye amechafuliwa, ao mwanamuke mwenye ndoa yake imevunjika,+ kwa sababu kuhani ni mutakatifu mbele ya Mungu wake. 8 Munapaswa kumutakasa kuhani,+ kwa sababu ni yeye anatoa mukate wa Mungu wenu. Munapaswa kumuona kuwa mutakatifu, kwa sababu mimi, Yehova, mwenye anawatakasa ninyi, niko mutakatifu.+

9 “‘Sasa kama binti ya kuhani anajichafua kwa kufanya ukahaba, anamuchafua baba yake. Anapaswa kuteketezwa ndani ya moto.+

10 “‘Kuhani mukubwa mwenye kuwa katikati ya ndugu zake, mwenye mafuta ya kutia mafuta yamemwangwa kwenye kichwa chake+ na mwenye amewekwa katika madaraka* ili avae nguo za ukuhani,+ hapaswe kuacha nywele zake katika hali ya ovyo-ovyo ao kupasua nguo zake.+ 11 Hapaswe kumukaribia mutu yeyote mwenye amekufa;*+ hapaswe hata kujichafua kwa ajili ya baba yake ao mama yake. 12 Hapaswe kutoka patakatifu na hapaswe kuchafua patakatifu pa Mungu wake,+ kwa sababu ile alama ya kuwekwa pembeni kwa ajili ya kusudi la pekee, yale mafuta ya Mungu wake ya kutia mafuta,+ yako juu yake. Mimi ni Yehova.

13 “‘Anapaswa kuoa mwanamuke mwenye kuwa bikira.+ 14 Hapaswe kuoa mwanamuke mujane, mwanamuke mwenye ndoa yake imevunjika, mwenye amechafuliwa, ao kahaba; lakini anapaswa kuchukua bikira katikati ya watu wake ili akuwe bibi yake. 15 Hapaswe kuchafua uzao wake* kati ya watu wake,+ kwa sababu mimi ni Yehova, mwenye kumutakasa.’”

16 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 17 “Ambia Haruni, ‘Mutu yeyote wa uzao wako* katika vizazi vyao vyote mwenye kuwa na kasoro asikaribie ili kutoa mukate wa Mungu wake. 18 Kama kuko mutu fulani mwenye kuwa na kasoro, hapaswe kukaribia: mutu mwenye kuwa kipofu ao kilema wa miguu ao mwenye kuwa na uso wenye kuharibika* ao mwenye kiungo kimoja kirefu sana, 19 mutu mwenye kuvunjika muguu ao mwenye kuvunjika mukono, 20 ao mwenye mugongo wenye kujikunja ao mutu mudogo sana,* ao mutu mwenye kasoro ya macho ao mwenye ukurutu wa ngozi* ao mwenye imba ao mwenye mapumbu yenye kuharibika.+ 21 Mutu yeyote wa uzao wa* Haruni kuhani mwenye kuwa na kasoro hatakaribia ili kutoa matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto. Kwa sababu iko* na kasoro, hapaswe kukaribia ili kutoa mukate wa Mungu wake. 22 Anaweza kula mukate wa Mungu wake kutoka kati ya vitu vitakatifu sana+ na kutoka kati ya vitu vitakatifu.+ 23 Lakini, hapaswe kukaribia pazia,+ na hapaswe kukaribia mazabahu,+ kwa sababu iko* na kasoro ndani yake; na hapaswe kuchafua patakatifu pangu,+ kwa kuwa mimi ni Yehova, mwenye kuwatakasa.’”+

24 Basi Musa akasema na Haruni na wana wake na Waisraeli wote.

22 Yehova akasema tena na Musa, na kumuambia: 2 “Ambia Haruni na wana wake kama wanapaswa kuwa waangalifu kuhusu namna wanashugulikia* vitu vitakatifu vya Waisraeli na wasichafue jina langu takatifu+ kuhusu vitu vyenye wanatakasa kwa ajili yangu.+ Mimi ni Yehova. 3 Uwaambie, ‘Katika vizazi vyenu vyote, muzao wenu yeyote mwenye, wakati haiko safi, anakaribia vitu vitakatifu vyenye Waisraeli wanatakasa kwa ajili ya Yehova, mutu huyo ataondolewa* mbele yangu.+ Mimi ni Yehova. 4 Muzao yeyote wa Haruni mwenye ukoma+ ao mwenye kuwa na mutiririko+ asikule vitu vitakatifu mupaka wakati atakuwa safi,+ wala mutu mwenye anagusa mutu yeyote ambaye amekuwa muchafu kupitia mutu mwenye amekufa,*+ wala mutu mwenye anatokwa na mbegu za uzazi,*+ 5 wala mutu mwenye anagusa kiumbe chenye hakiko safi chenye kupatikana kwa wingi+ wala mwenye anagusa mutu mwenye haiko safi kwa sababu yoyote na mwenye anaweza kumuchafua.+ 6 Mutu mwenye anagusa kitu chochote katikati ya vitu hivyo hatakuwa safi mupaka mangaribi na hapaswe kula kitu chochote katikati ya vitu vitakatifu, lakini anapaswa kuoga mwili wake ndani ya maji.+ 7 Wakati jua litakuwa limeshuka, atakuwa safi, na kisha anaweza kula vitu fulani kati ya vitu vitakatifu kwa sababu ni chakula chake.+ 8 Pia, hapaswe kula munyama yeyote mwenye alipatikana amekufa ao kitu chochote chenye kilipasuliwa na wanyama wa pori na kuwa muchafu kupitia kitu hicho.+ Mimi ni Yehova.

9 “‘Wanapaswa kutimiza mambo yenye ninawaomba, ili wasifanye zambi kwa sababu ya mambo hayo na kufa kwa sababu ya mambo hayo kwa kuwa walikuwa wanachafua mambo hayo. Mimi ni Yehova, mwenye kuwatakasa.

10 “‘Mutu mwenye haruhusiwe* hapaswe kula kitu chochote kitakatifu.+ Hakuna mugeni wa kuhani ao mufanyakazi wa kulipwa mwenye anapaswa kula kitu chochote kitakatifu. 11 Lakini kama kuhani anamununua mutu* kwa feza zake, mutu huyo anaweza kula vitu hivyo. Vilevile watumwa wenye walizaliwa katika nyumba yake wanaweza kula chakula chake.+ 12 Kama binti ya kuhani anaolewa na mwanaume mwenye haiko kuhani,* binti huyo hapaswe kula muchango wa vitu vitakatifu. 13 Lakini kama binti ya kuhani anakuwa mujane ao ndoa yake inavunjika na kama hana mutoto na anarudia katika nyumba ya baba yake kama vile katika ujana wake, anaweza kula sehemu fulani ya chakula cha baba yake;+ lakini mutu yeyote mwenye haruhusiwe* hapaswe kula chakula hicho.

14 “‘Sasa kama mutu anakula kitu kitakatifu bila kujua, anapaswa kuongeza sehemu moja ya tano (1/5) juu ya samani ya kitu hicho na kumupatia kuhani toleo takatifu.+ 15 Kwa hiyo makuhani hawapaswe kuchafua vitu vitakatifu vya Waisraeli vyenye wanamutolea Yehova muchango+ 16 na kuwafanya wapate azabu kwa ajili ya hatia yao kwa sababu ya kula vitu vyao vitakatifu; kwa maana mimi ni Yehova, mwenye kuwatakasa.’”

17 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 18 “Sema na Haruni na wana wake na Waisraeli wote na uwaambie, ‘Wakati Mwisraeli ao mukaaji mugeni katika Israeli anamutolea Yehova toleo la kuteketezwa+ ili kutimiza naziri zake ao kutoa toleo la kujipendea,+ 19 anapaswa kutoa munyama wa kiume mwenye hana kasoro+ kutoka katika mifugo, wana-kondoo dume, ao mbuzi, ili akubaliwe. 20 Hamupaswe kutoa kitu chochote chenye kasoro,+ kwa sababu hakitafanya mukubaliwe.

21 “‘Kama mutu anamutolea Yehova zabihu ya ushirika+ ili kutimiza naziri ao kama anaitoa kuwa toleo la kujipendea, inapaswa kuwa munyama mwenye hana kasoro kutoka katika mifugo ao kundi, ili akubaliwe. Kasoro yoyote haipaswe kuwa ndani yake. 22 Munyama yeyote wa toleo hapaswe kuwa kipofu, mwenye kuvunjika, mwenye mukato, mwenye kivimba, mwenye vigaga,* ao mwenye imba; hamupaswe kumutolea Yehova munyama yeyote katikati ya wanyama hao ao kumutolea Yehova toleo la namna hiyo kwenye mazabahu. 23 Munaweza kumutoa ngombe-dume ao kondoo mwenye kiungo kimoja kirefu sana ao kifupi sana kuwa toleo la kujipendea, lakini hatakubaliwa kuwa toleo la naziri. 24 Hamupaswe kumutolea Yehova munyama mwenye mapumbu yenye kuharibika ao kupondwa ao kungolewa ao kukatwa; na hamupaswe kutoa zabihu wanyama wa namna hiyo katika inchi yenu. 25 Na hamupaswe kupokea wanyama wa namna hiyo katika mukono wa mugeni na kuwatoa kuwa mukate wa Mungu wenu, kwa sababu ni wenye kuharibika na wenye kasoro. Hawatakubaliwa.’”

26 Yehova akasema tena na Musa, na kumuambia: 27 “Wakati ngombe-dume ao mwana-kondoo dume ao mbuzi anazaliwa, ataendelea kuwa na mama yake kwa siku saba (7),+ lakini kuanzia siku ya munane (8) na kuendelea atakubaliwa kuwa toleo, toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto. 28 Kuhusu ngombe-dume ao kondoo, hamupaswe kumuchinja yeye na kitoto chake siku ileile.+

29 “Kama munamutolea Yehova zabihu ya shukrani,+ munapaswa kutoa zabihu hiyo ili mukubaliwe. 30 Inapaswa kukuliwa siku ileile. Hamupaswe kuacha sehemu yoyote ya zabihu hiyo mupaka asubui.+ Mimi ni Yehova.

31 “Munapaswa kushika amri zangu na kuzifuata.+ Mimi ni Yehova. 32 Hamupaswe kuchafua jina langu takatifu,+ na ninapaswa kutakaswa katikati ya Waisraeli.+ Mimi ni Yehova, mwenye kuwatakasa,+ 33 mwenye kuwatosha katika inchi ya Misri ili niwaonyeshe kwamba mimi ni Mungu wenu.+ Mimi ni Yehova.”

23 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Sikukuu za Yehova za vipindi+ zenye munapaswa kutangaza+ ni mikusanyiko mitakatifu. Hizi ni sikukuu zangu za vipindi vya hali ya hewa:

3 “‘Siku sita (6) kazi inaweza kufanywa, lakini siku ya saba (7) ni sabato ya pumuziko kamili,+ mukusanyiko mutakatifu. Hamutafanya kazi yoyote. Itakuwa sabato kwa ajili ya Yehova kila mahali kwenye mutaishi.+

4 “‘Hizi ni sikukuu za Yehova za vipindi, mikusanyiko mitakatifu yenye munapaswa kutangaza katika nyakati zenye ziliwekwa kwa ajili ya vipindi hivyo: 5 Katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na ine (14) ya mwezi huo,+ mangaribi wakati giza linaanza* ni Pasaka+ ya Yehova.

6 “‘Siku ya kumi na tano (15) ya mwezi huo ni Sikukuu ya Yehova ya Mikate Yenye Haina Chachu.+ Kwa siku saba (7) munapaswa kula mikate yenye haina chachu.+ 7 Siku ya kwanza, mutafanya mukusanyiko mutakatifu.+ Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu. 8 Lakini kwa siku saba (7) mutamutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto. Kutakuwa mukusanyiko mutakatifu siku ya saba. Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.’”

9 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 10 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Wakati mutaingia mwishowe katika inchi yenye ninawapatia na kuvuna mavuno yake, munapaswa kumuletea kuhani+ fungu la matunda ya kwanza+ ya mavuno yenu. 11 Na kuhani atatikisa fungu hilo mbele na nyuma mbele ya Yehova ili mukubaliwe. Kuhani atalitikisa siku yenye inafuata siku ya Sabato. 12 Siku yenye fungu hilo linatikiswa, munapaswa kutoa mwana-kondoo dume katika mwaka wake wa kwanza mwenye hana kasoro, ili akuwe toleo la kuteketezwa kwa Yehova. 13 Toleo lake la nafaka litakuwa sehemu mbili za kumi (2/10) za efa* ya unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta, ili kuwa toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, harufu ya muzuri.* Toleo lake la kinywaji litakuwa sehemu moja ya ine (1/4) ya hini* ya divai. 14 Hamupaswe kula mukate wowote, nafaka yoyote yenye kukaangwa, ao nafaka mupya mupaka siku hiyo, mupaka wakati mutaleta toleo la Mungu wenu. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kila mahali kwenye mutaishi.

15 “‘Munapaswa kuhesabu sabato saba (7) kuanzia siku yenye inafuata siku ya Sabato, kuanzia siku yenye munaleta fungu la mbegu la toleo la kutikiswa.+ Yanapaswa kuwa majuma ya kuenea. 16 Mutahesabu siku makumi tano (50)+ mupaka siku yenye inafuata Sabato ya saba (7), na kisha mutamutolea Yehova toleo mupya la nafaka.+ 17 Munapaswa kuleta mikate mbili kutoka mahali kwenye munaishi ili ikuwe toleo la kutikiswa. Mikate hiyo inapaswa kutengenezwa na sehemu mbili za kumi (2/10) za efa* ya unga muzuri. Inapaswa kupikwa na chachu,+ ni matunda ya kwanza yenye kukomaa yenye yanatolewa kwa Yehova.+ 18 Na munapaswa kutoa mikate hiyo pamoja na wana-kondoo dume saba (7) wenye hawana kasoro, kila mumoja anapaswa kuwa na mwaka mumoja, na ngombe-dume mumoja mudogo na kondoo-dume wawili.+ Watakuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya Yehova pamoja na toleo lao la nafaka na matoleo yao ya vinywaji, ili kuwa toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumupendeza* Yehova. 19 Na munapaswa kutoa mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi+ na wana-kondoo dume wawili, kila mumoja anapaswa kuwa na mwaka mumoja, ili wakuwe zabihu ya ushirika.+ 20 Kuhani atawatikisa mbele na nyuma pamoja na ile mikate ya matunda ya kwanza yenye kukomaa, ili kuwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova, pamoja na wale wana-kondoo dume wawili. Ni vitu vitakatifu vyenye vinatolewa kwa Yehova kwa ajili ya kuhani.+ 21 Siku hiyo mutafanya tangazo+ kwa ajili ya mukusanyiko mutakatifu kwa ajili yenu. Hamutafanya kazi yoyote ya nguvu. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kila mahali kwenye mutaishi.

22 “‘Wakati munavuna mavuno ya inchi yenu, haupaswe kuvuna mavuno yote ya mipaka ya shamba lako na haupaswe kuokota masalio ya mavuno yako.+ Unapaswa kuyaachia maskini*+ na mukaaji mugeni.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

23 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 24 “Waambie Waisraeli, ‘Katika mwezi wa saba (7), siku ya kwanza ya mwezi huo, mutakuwa na pumuziko kamili, ukumbusho wenye utatangazwa kwa kupiga tarumbeta,+ mukusanyiko mutakatifu. 25 Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu, na mutamutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto.’”

26 Yehova akasema tena na Musa, na kumuambia: 27 “Lakini, siku ya kumi (10) ya mwezi huo wa saba (7) ni Siku ya Kufunika Zambi.+ Mutafanya mukusanyiko mutakatifu, na munapaswa kujitesa*+ na kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto. 28 Hamupaswe kufanya kazi yoyote siku hiyo ya pekee kwa sababu ni siku ya kufunika zambi ili kufunika zambi+ kwa ajili yenu mbele ya Yehova Mungu wenu. 29 Mutu yeyote mwenye hatajitesa* siku hiyo ataondolewa* katikati ya watu wake.+ 30 Na kila mutu* mwenye atafanya kazi yoyote siku hiyo, nitamuharibu kutoka kati ya watu wake. 31 Hamupaswe kufanya kazi yoyote. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kila mahali kwenye mutaishi. 32 Ni sabato ya pumuziko kamili kwa ajili yenu, na mutajitesa*+ siku ya kenda (9) ya mwezi huo wakati wa mangaribi. Mutafanya sabato kuanzia mangaribi hiyo mupaka mangaribi yenye inafuata.”

33 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 34 “Waambie Waisraeli, ‘Siku ya kumi na tano (15) ya mwezi huo wa saba (7) ni Sikukuu ya Vibanda* ya siku saba kwa ajili ya Yehova.+ 35 Kutakuwa mukusanyiko mutakatifu siku ya kwanza, na hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu. 36 Kwa siku saba (7) munapaswa kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto. Siku ya munane (8), mutafanya mukusanyiko mutakatifu,+ na munapaswa kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto. Ni mukusanyiko mukubwa. Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.

37 “‘Hizi ni sikukuu za Yehova za vipindi+ zenye mutatangaza kuwa mikusanyiko mitakatifu+ ya kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto: toleo la kuteketezwa+ na toleo la nafaka+ la zabihu na matoleo ya vinywaji+ kulingana na programu ya kila siku. 38 Matoleo hayo yanaongezwa juu ya matoleo yenye yanatolewa wakati wa sabato za Yehova,+ na zawadi zenu,+ matoleo yenu ya naziri,+ na matoleo yenu ya kujipendea,+ yenye munapaswa kumutolea Yehova. 39 Lakini, siku ya kumi na tano (15) ya mwezi wa saba (7), wakati mutakuwa mumekusanya mazao ya inchi, mutafanya sikukuu ya Yehova kwa siku saba.+ Siku ya kwanza ni pumuziko kamili na siku ya munane (8) ni pumuziko kamili.+ 40 Siku ya kwanza, mutakamata matunda ya miti yenu mikubwa na yenye kupendeza, matawi ya miti ya mitende,+ matawi ya miti yenye majani mengi na miti ya mierebi ya bonde,* na mutashangilia+ mbele ya Yehova Mungu wenu kwa siku saba (7).+ 41 Mutamufanyia Yehova sikukuu hiyo kwa siku saba (7) katika mwaka.+ Kwa kuwa ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote, munapaswa kuifanya katika mwezi wa saba. 42 Mutakaa katika vibanda kwa siku saba (7).+ Wote wenye walizaliwa katika Israeli watakaa katika vibanda, 43 ili vizazi vyenu vya wakati wenye kuja vijue+ kwamba nilifanya Waisraeli wakae katika vibanda wakati nilikuwa ninawatosha katika inchi ya Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

44 Kwa hiyo Musa akaambia Waisraeli juu ya sikukuu za Yehova za vipindi.

24 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Uamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni zenye kupondwa, ili taa ziendelee kuwaka kila wakati.+ 3 Katika hema ya mukutano, inje ya pazia la Ushuhuda, Haruni atafanya mipango ili taa hizo ziendelee kuwaka kila wakati kuanzia mangaribi mupaka asubui mbele ya Yehova. Hiyo ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote. 4 Anapaswa kupanga taa hizo kwa utaratibu kwenye kinara cha taa+ cha zahabu safi mbele ya Yehova kila wakati.

5 “Utakamata unga muzuri na kupika mikate kumi na mbili (12) ya muviringo. Kila mukate utatengenezwa na sehemu mbili za kumi (2/10) za efa.* 6 Utapanga mikate hiyo moja juu ya ingine katika mistari mbili, kila mustari utakuwa na mikate sita (6),+ juu ya meza ya zahabu safi mbele ya Yehova.+ 7 Unapaswa kutia ubani safi juu ya kila mustari, na mikate hiyo itakuwa toleo la kumbukumbu+ lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto. 8 Kila siku ya Sabato, anapaswa kupanga mikate hiyo mbele ya Yehova kwa ukawaida.+ Ni agano la kudumu katikati yangu na Waisraeli. 9 Mikate hiyo itakuwa ya Haruni na wana wake,+ na wataikula katika mahali patakatifu,+ kwa sababu ni kitu kitakatifu sana kwa ajili yake kutoka katika matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto; itakuwa sharti la kudumu.”

10 Sasa kati ya Waisraeli kulikuwa mwana mumoja wa mwanamuke Mwisraeli na mwanaume Mumisri,+ na mapigano yalitokea kati yake na mwanaume Mwisraeli katika kambi. 11 Mwana huyo wa mwanamuke Mwisraeli akaanza kutukana lile Jina* na kulilaani.*+ Kwa hiyo wakamuleta mbele ya Musa.+ Kumbe mama yake alikuwa Shelomiti, binti ya Dibri wa kabila la Dani. 12 Wakamutia katika kifungo mupaka wakati walijulishwa uamuzi wa Yehova.+

13 Kisha Yehova akamuambia Musa: 14 “Umupeleke inje ya kambi ule mwenye alilaani, na wale wote wenye walimusikia wanapaswa kuweka mikono yao juu ya kichwa chake, na kisha mukusanyiko wote unapaswa kumupiga majiwe.+ 15 Na utawaambia Waisraeli, ‘Kama mutu yeyote anamulaani Mungu wake, atajibu kwa sababu ya zambi yake. 16 Kwa hiyo ule mwenye anatukana jina la Yehova anapaswa kabisa kuuawa.+ Mukusanyiko wote unapaswa kabisa kumupiga majiwe. Mukaaji mugeni anapaswa kuuawa sawasawa na mwenyeji kwa sababu ya kutukana lile Jina.

17 “‘Kama mutu anaondoa uzima wa mutu mwingine,* anapaswa kabisa kuuawa.+ 18 Kila mutu mwenye anamupiga munyama wa kufugwa* na kumuua anapaswa kulipa, uzima kwa uzima.* 19 Kama mutu anamuumiza mwanadamu mwenzake, basi anapaswa kufanyiwa jambo lenye alifanya.+ 20 Mufupa wenye ulivunjika kwa mufupa wenye ulivunjika, jicho kwa jicho, jino kwa jino, tendo lilelile la kuumiza lenye alitendea mwenzake ndilo atatendewa.+ 21 Mutu mwenye anamupiga munyama na kumuua anapaswa kulipa,+ lakini mutu mwenye anamupiga mutu mwingine na kumuua anapaswa kuuawa.+

22 “‘Uamuzi moja wa hukumu utatumika kwa ajili yenu, ikuwe mukaaji mugeni ao mwenyeji,+ kwa sababu mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

23 Basi Musa akasema na Waisraeli, na wakamupeleka inje ya kambi ule mwenye alisema maneno ya kulaani, na wakamupiga majiwe.+ Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.

25 Yehova akasema tena na Musa kwenye Mulima Sinai, na kumuambia 2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Wakati mutaingia mwishowe katika inchi yenye ninawapatia,+ basi inchi hiyo itashika sabato ya Yehova.+ 3 Kwa miaka sita (6) utapanda mbegu katika shamba lako, na kwa miaka sita utapunguza matawi ya mizabibu yako, na utavuna mazao ya inchi.+ 4 Lakini katika mwaka wa saba (7) kutakuwa sabato ya pumuziko kamili kwa ajili ya inchi, sabato kwa ajili ya Yehova. Haupaswe kupanda mbegu katika shamba lako wala kupunguza matawi ya mizabibu yako. 5 Haupaswe kuvuna kitu chenye kinajiotea kutokana na mbegu zenye ziliachwa kisha mavuno, na haupaswe kuchuma zabibu kwenye miti ya mizabibu yenye matawi yake hayajakatwa. Inchi inapaswa kupumuzika kabisa kwa mwaka mumoja. 6 Lakini, unaweza kula chakula chenye kinaota katika inchi katika mwaka huo wa sabato; wewe, watumwa wako wanaume na wanamuke, mufanyakazi wako wa kulipwa, na wakaaji wageni wenye wanaishi pamoja na wewe munaweza kula chakula hicho, 7 na pia wanyama wa kufugwa na wanyama wa pori wenye kuwa katika inchi yako. Kila kitu chenye inchi inatoa kinaweza kukuliwa.

8 “‘Utahesabia miaka saba (7) ya sabato, miaka saba mara saba, na siku za miaka saba ya sabato zitakuwa miaka makumi ine na kenda (49). 9 Kisha utapiga baragumu kwa sauti kubwa katika mwezi wa saba (7), siku ya kumi (10) ya mwezi huo; katika Siku ya Kufunika Zambi,+ mutapiga baragumu ili isikiwe katika inchi yenu yote. 10 Munapaswa kutakasa mwaka wa makumi tano (50) na kutangaza uhuru katika inchi kwa ajili ya wakaaji wake wote.+ Itakuwa Yubile kwenu, na kila mumoja wenu atarudia kwenye uriti wake na kila mumoja wenu atarudia katika familia yake.+ 11 Mwaka wa makumi tano (50) utakuwa Yubile kwenu. Hamutapanda mbegu wala kuvuna kitu chenye kilijiotea kutokana na mbegu zenye ziliachwa wala kuchuma zabibu kwenye miti ya mizabibu yenye matawi yake hayajakatwa.+ 12 Kwa maana ni Yubile. Itakuwa takatifu kwenu. Munaweza kula kitu chenye inchi inatoa yenyewe.+

13 “‘Katika mwaka huo wa Yubile, kila mumoja wenu anapaswa kurudia kwenye uriti wake.+ 14 Kama unauzisha kitu chochote kwa mwenzako ao kama unanunua kitu chochote kwake, mutu asimupunje mwenzake.+ 15 Utanunua kwa mwenzako, kulingana na hesabu ya miaka yenye imepita kisha Yubile, na atauzisha kitu hicho kwako kulingana na miaka yenye inabakia ya mazao.+ 16 Kama kungali miaka mingi, anaweza kuongeza bei, na kama kunabakia miaka kidogo, anapaswa kupunguza bei, kwa sababu anauzisha kwako hesabu ya mazao yenye yatavunwa. 17 Hakuna mutu kati yenu mwenye anapaswa kumupunja mwenzake,+ na munapaswa kumuogopa Mungu wenu,+ kwa sababu mimi ni Yehova Mungu wenu.+ 18 Kama munashika sheria zangu na kufuata maamuzi yangu ya hukumu, mutaishi kwa usalama katika inchi.+ 19 Inchi itatoa mazao yake,+ na mutakula na kushiba na kuishi kwa usalama ndani yake.+

20 “‘Lakini kama munasema: “Tutakula nini katika mwaka wa saba (7) kama hatupande mbegu ao kuvuna mavuno yetu?”+ 21 Nitaamuru baraka zangu kwa ajili yenu katika mwaka wa sita (6), na inchi itatoa mazao ya kutosha kwa ajili ya miaka tatu (3).+ 22 Kisha mutapanda mbegu mwaka wa munane (8) na kula mavuno ya miaka yenye ilitangulia mupaka mwaka wa kenda (9). Mutakula mavuno yenye yalitangulia mupaka wakati mavuno ya mwaka wa kenda yatafika.

23 “‘Inchi haipaswe kuuzishwa kwa muda wa kudumu,+ kwa sababu inchi ni yangu.+ Kwa maana ninyi ni wakaaji wageni na wahamiaji mbele ya macho yangu.+ 24 Katika inchi yote yenye munariti, mutatoa haki ya kununua tena inchi.

25 “‘Kama ndugu yako anakuwa maskini na analazimika kuuzisha sehemu fulani ya uriti wake, mukombozi mwenye kuwa mutu wa karibu wa jamaa yake atakuja na kununua tena sehemu yenye ndugu yake aliuzisha.+ 26 Kama mutu hana mukombozi lakini anakuwa tajiri na anapata uwezo wa kuikomboa, 27 anapaswa kuhesabia samani ya sehemu hiyo kulingana na miaka yenye ilipita tangu wakati aliiuzisha na kumurudishia ule mwenye aliiuza kiasi chenye kinabakia. Kisha atarudia kwenye uriti wake.+

28 “‘Lakini kama hana uwezo wa kukomboa sehemu yenye aliuzisha, itabakia katika mikono ya mwenye aliiuza mupaka mwaka wa Yubile;+ na atarudishiwa sehemu hiyo katika mwaka wa Yubile, na atarudia kwenye uriti wake.+

29 “‘Sasa kama mutu anauzisha nyumba yenye kuwa katika muji wenye kuzungukwa na ukuta, haki yake ya kuikomboa itaendelea pia mupaka mwisho wa mwaka mumoja tangu wakati alimaliza kuiuzisha; kwa mwaka muzima atakuwa na haki ya kuikomboa.+ 30 Lakini kama hainunuliwe tena kwenye mwisho wa mwaka muzima, nyumba hiyo yenye kuwa katika muji wenye kuzungukwa na ukuta itakuwa mali ya kudumu ya ule mwenye aliinunua katika vizazi vyake vyote. Haipaswe kurudishwa katika Yubile. 31 Lakini, nyumba zenye kuwa katika makao yenye haizungukwe na ukuta zinapaswa kuonwa kuwa sehemu ya mashamba ya eneo la mashamba. Haki ya kuzikomboa inapaswa kuendelea, na zinapaswa kurudishwa katika Yubile.

32 “‘Kuhusu nyumba za Walawi zenye ziko katika miji yao,+ Walawi watakuwa na haki ya kudumu ya kuzikomboa. 33 Wakati mali ya Walawi hainunuliwe tena, nyumba yenye iliuzishwa katika muji wa Walawi itarudishwa pia katika Yubile,+ kwa sababu nyumba zenye ziko katika miji ya Walawi ni uriti wao kati ya Waisraeli.+ 34 Tena, shamba la eneo la malisho+ lenye kuzunguka miji yao halipaswe kuuzishwa, kwa sababu ni uriti wao wa kudumu.

35 “‘Kama ndugu yako mwenye kuwa karibu anakuwa maskini na hawezi kujitegemeza, unapaswa kumutegemeza,+ kama vile ungemutegemeza mukaaji mugeni na muhamiaji,+ ili aendelee kuwa muzima pamoja na wewe. 36 Usikamate faida ao usitafute faida ya juu sana kwake.+ Unapaswa kumuogopa Mungu wako,+ na ndugu yako ataendelea kuwa muzima pamoja na wewe. 37 Usimukopeshe feza ili akurudishie faida+ ao kumupatia chakula ili upate faida. 38 Mimi ni Yehova Mungu wenu, mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri+ ili kuwapatia inchi ya Kanaani, ili niwaonyeshe kwamba mimi ni Mungu wenu.+

39 “‘Kama ndugu yako mwenye anaishi karibu na wewe anakuwa maskini na analazimika kujiuzisha kwako,+ haupaswe kumulazimisha akutumikie kama mutumwa.+ 40 Unapaswa kumutendea kama mufanyakazi wa kulipwa,+ kama muhamiaji. Atakutumikia mupaka mwaka wa Yubile. 41 Kisha atakuacha, yeye na watoto* wake, na kurudia kwa watu wa jamaa yake. Anapaswa kurudia kwenye uriti wa mababu zake.+ 42 Kwa maana wao ni watumwa wangu wenye nilitosha katika inchi ya Misri.+ Hawapaswe kujiuzisha kama vile mutumwa anauzishwa. 43 Haupaswe kumutendea kwa ukali,+ na unapaswa kumuogopa Mungu wako.+ 44 Watumwa wako wanaume ao wanamuke wanapaswa kutoka katika mataifa yenye kukuzunguka, unaweza kununua mutumwa mwanaume ao mwanamuke katika mataifa hayo. 45 Pia katikati ya wana wa wahamiaji wageni wenye wanaishi pamoja na ninyi,+ katikati yao na katikati ya watu wa familia zao wenye walizaliwa katika inchi yenu munaweza kununua watumwa, na watakuwa mali yenu. 46 Unaweza kuwafanya kuwa uriti wa wana wako kisha wewe ili wawariti kuwa mali yao ya kudumu. Munaweza kuwatumia kama wafanyakazi, lakini haupaswe kutendea ndugu zako Waisraeli kwa ukali.+

47 “‘Lakini kama mukaaji mugeni ao muhamiaji kati yenu anakuwa tajiri na ndugu yako amekuwa maskini karibu naye na analazimika kujiuzisha kwa mukaaji mugeni ao muhamiaji mwenye anaishi kati yenu, ao kwa mutu wa jamaa ya ule mukaaji mugeni, 48 ataendelea kuwa na haki ya kukombolewa kisha yeye kujiuzisha. Mumoja kati ya ndugu zake anaweza kumununua tena,+ 49 ao ndugu ya baba yake ao mwana wa ndugu ya baba yake anaweza kumununua tena, ao mutu yeyote wa jamaa ya karibu,* mutu wa familia yake, anaweza kumununua tena.

“‘Ao kama yeye mwenyewe amekuwa tajiri, anaweza kujinunua tena.+ 50 Atahesabia wakati pamoja na mwenye alimununua tangu mwaka wenye alijiuzisha mupaka mwaka wa Yubile,+ na feza zenye zilimununua zitalingana na hesabu ya miaka hiyo.+ Siku zenye alifanya kazi katika miaka hiyo zitapimwa kama siku za mufanyakazi wa kulipwa.+ 51 Kama kungali miaka mingi, anapaswa kulipa bei yake ya ukombozi kulingana na miaka yenye inabakia. 52 Lakini kama kunabakia miaka kidogo tu mbele ya mwaka wa Yubile, basi anapaswa kuhesabu mwenyewe na kulipa bei yake ya ukombozi kulingana na miaka yenye inabakia. 53 Ataendelea kumutumikia mwaka kwa mwaka kama mufanyakazi wa kulipwa; na munapaswa kuhakikisha kwamba ule mwenye alimununua hamutendee kwa ukali.+ 54 Lakini, kama hawezi kujinunua tena yeye mwenyewe kulingana na maagizo hayo, basi ataachiliwa huru katika mwaka wa Yubile,+ yeye na watoto* wake.

55 “‘Kwa maana Waisraeli ni watumwa wangu mwenyewe. Ni watumwa wangu wenye nilitosha katika inchi ya Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.

26 “‘Hamupaswe kujitengenezea miungu yenye haina mafaa yoyote,+ na hamupaswe kujisimamishia sanamu ya kuchongwa+ ao nguzo takatifu, na hamupaswe kutia jiwe lenye kuchongwa+ katika inchi yenu ili kuliinamia;+ kwa maana mimi ni Yehova Mungu wenu. 2 Munapaswa kushika sabato zangu na kuheshimia* patakatifu pangu. Mimi ni Yehova.

3 “‘Kama munaendelea kufuata sheria zangu na kushika amri zangu na kuzitenda,+ 4 nitawapatia matone ya mvua kwa wakati wake wenye kufaa,+ na inchi itatoa mazao yake,+ na miti ya mashamba itatoa matunda yake. 5 Kipindi chenu cha kupiga-piga nafaka kitaendelea mupaka wakati wa kuvuna zabibu, na kipindi cha kuvuna zabibu kitaendelea mupaka wakati wa kupanda; na mutakula mukate na kushiba na kuishi kwa usalama katika inchi yenu.+ 6 Nitatia amani katika inchi,+ na mutalala pasipo mutu wa kuwaogopesha;+ na nitaondoa katika inchi wanyama wote wakali wa pori, na upanga wa vita hautapita katika inchi yenu. 7 Hakika mutafuatilia maadui wenu, nao watakufa kwa upanga mbele yenu. 8 Watu tano (5) kati yenu watafuatilia mia moja (100), na mia moja watafuatilia elfu kumi (10 000), na maadui wenu watakufa kwa upanga mbele yenu.+

9 “‘Nitawaonyesha wema wangu* na kuwafanya muzae na kuongezeka,+ na nitatimiza agano lenye nilifanya pamoja na ninyi.+ 10 Wakati mutakuwa mungali munakula mazao ya zamani ya mwaka wenye ulitangulia, mutakuwa na lazima ya kuondoa mazao hayo ya zamani ili kupata nafasi ya kutia mazao ya mupya. 11 Na nitatia tabenakulo yangu katikati yenu,+ na sitawakataa.* 12 Nitatembea kati yenu na nitakuwa Mungu wenu,+ na ninyi kwa ngambo yenu mutakuwa watu wangu.+ 13 Mimi ni Yehova Mungu wenu, mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri ili musiendelee kuwa watumwa wao, na nilivunja nira yenu na kuwafanya mutembee vichwa vyenu vikiwa wima.*

14 “‘Lakini, kama hamunisikilize wala kushika amri hizo zote,+ 15 na kama munakataa sheria zangu,+ na kama munachukia maamuzi yangu ya hukumu ili musishike amri zangu zote, na kuvunja agano langu,+ 16 basi, mimi, nitawatendea mambo haya: nitawapatia azabu kupitia taabu, kupitia ugonjwa wa kifua kikubwa na homa kali, ili kufanya macho yenu yafifie na uzima wenu ukuwe* zaifu. Mutapanda mbegu yenu bure, kwa maana maadui wenu wataikula.+ 17 Nitakunja uso wangu juu yenu, na maadui wenu watawashinda;+ na wale wenye kuwachukia watawakanyanga-kanyanga,+ na mutakimbia wakati hakuna mwenye anawafuatilia.+

18 “‘Hata kama mambo hayo hayawafanye munisikilize, nitawapatia azabu mara saba (7) zaidi kwa sababu ya zambi zenu. 19 Nitavunja kiburi chenu kigumu na nitafanya mbingu zenu zikuwe kama chuma+ na inchi yenu kama shaba. 20 Mutapoteza nguvu zenu bure, kwa maana inchi yenu haitatoa mazao,+ na miti ya inchi haitazaa matunda.

21 “‘Lakini kama munaendelea kunipinga na kukataa kunisikiliza, basi nitawapiga mara saba (7) zaidi kulingana na zambi zenu. 22 Nitatuma wanyama wa pori kati yenu,+ na watafanya mukose watoto+ na wataua wanyama wenu wa kufugwa na kupunguza hesabu yenu, na barabara zenu hazitakuwa na watu.+

23 “‘Kama hamukubali rekebisho langu+ kisha mambo hayo na munaendelea kunipinga, 24 basi mimi pia nitawapinga, na nitawapiga mara saba (7) kwa sababu ya zambi zenu. 25 Nitaleta upanga wenye kulipiza kisasi juu yenu kwa sababu ya kuvunja agano langu.+ Kama munakusanyika katika miji yenu, nitatuma ugonjwa katikati yenu,+ na mutatiwa katika mukono wa adui.+ 26 Wakati nitaharibu akiba* yenu ya mikate,*+ wanamuke kumi (10) watapiga mikate yenu katika jiko moja tu na kupima mikate kwenye mizani;*+ na mutakula lakini hamutashiba.+

27 “‘Kama hamunisikilize ijapokuwa mambo hayo na munaendelea kunipinga, 28 nitawapinga vikali,+ na nitawapatia azabu mara saba (7) kwa sababu ya zambi zenu. 29 Kwa hiyo mutalazimika kula nyama ya watoto wenu wanaume, na mutakula nyama ya watoto wenu wanamuke.+ 30 Nitaharibu mahali penu patakatifu pa juu+ na kuangusha chini vinara vyenu vya uvumba na nitarundika mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu zenye kuchukiza,*+ na nitawachukia* na kuwaacha.+ 31 Nitaacha miji yenu iharibiwe kwa upanga+ na nitafanya mahali penu patakatifu pakuwe ukiwa, na sitafurahia harufu ya muzuri* ya zabihu zenu. 32 Mimi mwenyewe nitaifanya inchi ikuwe ukiwa,+ na maadui wenu wenye wataishi ndani yake wataiangalia kwa mushangao.+ 33 Na nitawasambaza kati ya mataifa,+ na nitachomoa upanga na ninyi mutakimbizwa;+ na inchi yenu itakuwa ukiwa,+ na miji yenu itaharibiwa.

34 “‘Wakati huo inchi italipa sabato zake siku zote zenye itakuwa ukiwa, wakati mutakuwa katika inchi ya maadui wenu. Wakati huo inchi itapumuzika,* kwa maana inapaswa kulipa sabato zake.+ 35 Siku zote zenye itakuwa ukiwa itapumuzika, kwa sababu haikupumuzika wakati wa sabato zenu wakati mulikuwa munakaa ndani yake.

36 “‘Kuhusu wale wenye watabakia,+ nitajaza ndani ya mioyo yao hisia ya kupoteza tumaini katika inchi za maadui wao; na sauti ya jani lenye kupeperushwa na upepo itawafanya wakimbie, na watakimbia kama mutu mwenye anakimbia upanga na kuanguka bila mutu mwenye anawafuatilia.+ 37 Watajikwaa mumoja juu ya mwingine kama wale wenye wanakimbia upanga, hata kama hakuna mwenye anawafuatilia. Hamutaweza kusimama mbele ya maadui wenu.+ 38 Mutakufa kati ya mataifa,+ na inchi ya maadui wenu itawakula. 39 Wamoja kati yenu wenye watabakia wataachwa ili waoze katika inchi za maadui wenu+ kwa sababu ya kosa lenu. Ndiyo, wataoza kwa sababu ya makosa ya baba zao.+ 40 Kisha wataungama kosa lao+ na kosa la baba zao na ukosefu wao wa uaminifu na watatambua kwamba walijiendesha kwa kukosa uaminifu kwa kutembea kwa kunipinga.+ 41 Kisha niliwapinga pia+ kwa kuwapeleka katika inchi ya maadui wao.+

“‘Pengine wakati huo mioyo yao yenye haitahiriwe* ingenyenyekezwa,+ na kisha walipie kosa lao. 42 Na nitakumbuka agano lenye nilifanya na Yakobo,+ na agano lenye nilifanya na Isaka,+ na pia agano lenye nilifanya na Abrahamu,+ na nitakumbuka inchi yao. 43 Wakati walikuwa wameacha inchi yao, ilikuwa inalipa sabato zake+ na ilikuwa imeachwa bila wao, na walikuwa wanalipia kosa lao, kwa sababu walikataa maamuzi yangu ya hukumu na walichukia* sheria zangu.+ 44 Lakini ijapokuwa mambo hayo yote, wakati watakuwa katika inchi ya maadui wao, sitawakataa kabisa+ wala sitawatupa mupaka kufikia kuwaharibu kabisa, kufanya vile kungevunja agano+ lenye nilifanya nao; kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao. 45 Kwa ajili yao nitakumbuka agano lenye nilifanya na mababu zao+ wenye nilitosha katika inchi ya Misri mbele ya macho ya mataifa,+ ili nijionyeshe kuwa Mungu wao. Mimi ni Yehova.’”

46 Hayo ni masharti, maamuzi ya hukumu, na sheria zenye Yehova alitia kati yake na Waisraeli kwenye Mulima Sinai kupitia Musa.+

27 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Kama mutu anafanya naziri ya pekee+ ya kumutolea Yehova feza zenye zinalingana na samani yenye kukadiriwa ya mutu,* 3 samani yenye kukadiriwa ya mwanaume mwenye miaka kuanzia makumi mbili (20) mupaka makumi sita (60) itakuwa shekeli* makumi tano (50) za feza kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.* 4 Lakini kama ni mwanamuke, samani yenye kukadiriwa itakuwa shekeli makumi tatu (30). 5 Kama mutu iko* na miaka kuanzia tano (5) mupaka makumi mbili (20), samani yenye kukadiriwa ya mwanaume itakuwa shekeli makumi mbili na ya mwanamuke shekeli kumi (10). 6 Kama mutu iko* na mwezi mumoja mupaka miaka tano (5), samani yenye kukadiriwa ya mwanaume itakuwa shekeli tano za feza na ya mwanamuke shekeli tatu (3) za feza.

7 “‘Kama mutu iko* na miaka makumi sita (60) na zaidi, samani yenye kukadiriwa ya mwanaume itakuwa shekeli kumi na tano (15) na ya mwanamuke shekeli kumi (10). 8 Lakini kama iko* maskini sana na hawezi kulipa samani yenye kukadiriwa,+ mutu huyo atasimama mbele ya kuhani, na kuhani atakadiria samani yake. Kuhani atakadiria samani kulingana na feza zenye mutu mwenye alifanya naziri anaweza kupata.+

9 “‘Kama naziri hiyo inahusu munyama mwenye anastahili kutolewa kwa Yehova, kila kitu chenye kinaweza kutolewa kwa Yehova kitakuwa kitakatifu. 10 Hawezi kutia munyama mwingine pa nafasi yake ao kubadilisha munyama muzuri pa nafasi ya mubaya ao mubaya pa nafasi ya muzuri. Lakini kama anabadilisha munyama huyo na mwingine, munyama wa kwanza na mwenye alibadilishwa naye wote wawili watakuwa watakatifu. 11 Kama ni munyama mwenye haiko safi+ mwenye hawezi kutolewa kwa Yehova, basi atasimamisha munyama huyo mbele ya kuhani. 12 Kisha kuhani atakadiria samani yake, kama ni munyama muzuri ao mubaya. Samani yenye kukadiriwa na kuhani itakuwa vile. 13 Lakini kama siku moja anataka kununua tena munyama huyo, basi anapaswa kulipa samani yenye kukadiriwa ya munyama huyo kwa kuongeza ile sehemu moja ya tano (1/5) juu ya samani hiyo.+

14 “‘Sasa kama mutu anatakasa nyumba yake ili ikuwe kitu kitakatifu kwa Yehova, basi kuhani atakadiria samani ya nyumba hiyo, kama ni ya muzuri ao ni ya mubaya. Samani yenye itakadiriwa na kuhani ndiyo itakuwa bei yake.+ 15 Lakini kama mutu mwenye anatakasa nyumba yake anataka kuinunua tena, basi anapaswa kulipa feza zenye zilikadiriwa kuwa samani ya nyumba hiyo na kuongeza sehemu moja ya tano (1/5) juu ya feza hizo, kisha itakuwa yake.

16 “‘Kama mutu anatakasa sehemu fulani ya shamba lake ili ikuwe ya Yehova, samani yake itakadiriwa kulingana na mbegu zenye zinahitajika kupandwa katika sehemu hiyo: homeri* ya mbegu za shayiri itakuwa shekeli makumi tano (50) za feza. 17 Kama anatakasa shamba lake kuanzia mwaka wa Yubile,+ samani yake itabakia kama vile ilikadiriwa. 18 Kama anatakasa shamba lake kisha Yubile, kuhani atakadiria bei kwa ajili yake kulingana na miaka yenye inabakia mbele ya mwaka wa Yubile wenye kufuata, na samani yenye ilikadiriwa itapunguzwa.+ 19 Lakini kama siku moja ule mwenye alitakasa shamba hilo anataka kulinunua tena, basi anapaswa kulipa feza za samani yenye ilikadiriwa kuwa bei ya shamba hilo na kuongeza sehemu moja ya tano (1/5) juu ya feza hizo, kisha litaendelea kuwa lake. 20 Sasa kama hanunue tena shamba hilo na linauzishwa kwa mutu mwingine, haliwezi kununuliwa tena. 21 Wakati shamba hilo litarudishwa katika Yubile, litakuwa kitu kitakatifu kwa ajili ya Yehova, shamba lenye limetolewa kwake. Litakuwa mali ya makuhani.+

22 “‘Kama mutu anatakasa shamba lenye alinunua lenye haliko sehemu ya uriti wake ili likuwe mali ya Yehova,+ 23 kuhani atamufanyia hesabu ya kadirio la bei mupaka mwaka wa Yubile, na mutu huyo atalipa siku hiyo samani yenye itakadiriwa.+ Ni kitu kitakatifu kwa ajili ya Yehova. 24 Katika mwaka wa Yubile, shamba hilo litarudia kwa ule mwenye alilinunua kutoka kwake, kwa mutu mwenye shamba hilo ni mali yake.+

25 “‘Kila samani itakadiriwa kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu. Shekeli moja itakuwa sawa na gera* makumi mbili (20).

26 “‘Lakini, mutu yeyote asimutakase muzaliwa wa kwanza wa wanyama, kwa sababu anazaliwa akiwa muzaliwa wa kwanza kwa ajili ya Yehova.+ Ikuwe ngombe-dume ao kondoo, tayari ni wa Yehova.+ 27 Kama munyama huyo iko* kati ya wanyama wenye hawako safi na anamukomboa kulingana na samani yenye ilikadiriwa, anapaswa kulipa samani yenye ilikadiriwa na kuongeza sehemu moja ya tano (1/5) juu ya samani hiyo.+ Lakini kama munyama huyo hanunuliwe tena, atauzishwa kulingana na samani yenye ilikadiriwa.

28 “‘Lakini kila kitu chenye mutu anamutolea Yehova bila kuweka masharti* chenye kinatoka katika vitu vyake hakipaswe kuuzishwa ao kununuliwa tena, ikuwe kinatoka katikati ya watu ao wanyama ao shamba lake. Kila kitu chenye kimetolewa kwa Mungu ni kitu kitakatifu sana kwa ajili ya Yehova.+ 29 Tena, kila mutu mwenye amehukumiwa na kuwekwa pembeni ili aharibiwe hawezi kukombolewa.+ Anapaswa kabisa kuuawa.+

30 “‘Kila sehemu moja ya kumi (1/10)*+ ya inchi, ikuwe inatoka katika mazao ya shamba ao matunda ya miti, ni mali ya Yehova. Sehemu hiyo ni kitu kitakatifu kwa ajili ya Yehova. 31 Kama siku moja mutu anataka kununua tena sehemu yake yoyote ya kumi, anapaswa kuongeza sehemu moja ya tano (1/5) juu ya sehemu hiyo. 32 Kuhusu kila sehemu moja ya kumi (1/10) ya mifugo na kundi, kila kitu chenye kinapita chini ya fimbo ya muchungaji, munyama wa kumi* atakuwa kitu kitakatifu kwa ajili ya Yehova. 33 Hapaswe kuchunguza kama munyama huyo ni muzuri ao ni mubaya, wala hapaswe kumubadilisha na mwingine. Lakini kama siku moja anajaribu kumubadilisha na mwingine, munyama wa kwanza na ule mwenye alibadilishwa naye wote wawili watakuwa kitu kitakatifu.+ Hakiwezi kununuliwa tena.’”

34 Hizo ni amri zenye Yehova alimupatia Musa kwenye Mulima Sinai kwa ajili ya Waisraeli.+

Tnn., “wana wa Israeli.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “mafuta yenye kuzunguka figo.”

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “mafuta yake yenye kuzunguka figo.”

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Ao “majivu yenye mafuta,” ni kusema, majivu yenye kujaa mafuta ya zabihu.

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

Ao “masuke ya mubichi.”

Ao “zabihu ya matoleo ya amani.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Tnn., “mukate,” ni kusema, fungu la Mungu la zabihu ya ushirika.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Tnn., “mukate,” ni kusema, fungu la Mungu la zabihu ya ushirika.

Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “majivu yenye mafuta,” ni kusema, majivu yenye kujaa mafuta ya zabihu.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Ao “nafsi.”

Tnn., “amesikia laana (kiapo).” Pengine amesikia tangazo kuhusu kosa lenye lilifanywa na laana yenye itamupata mukosaji ao shahidi yeyote mwenye anakataa kutoa ushahidi.

Ao “nafsi.”

Inaonekana mutu huyo hatimize kiapo chake.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Sehemu moja ya kumi ya efa ilikuwa sawa na litre 2.2 (vibaba 2). Angalia Nyongeza B14.

Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

Ao “shekeli takatifu.”

Ao “nafsi inatenda.”

Ao “eko.”

Ao “nafsi inatenda.”

Ao “eko.”

Ao “nguo ya ndani.”

Ao “majivu yenye mafuta,” ni kusema, majivu yenye kujaa mafuta ya zabihu.

Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

Sehemu moja ya kumi ya efa ilikuwa sawa na litre 2.2 (vibaba 2). Angalia Nyongeza B14.

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “nafsi yenye itakula sehemu fulani ya zabihu hiyo itajibu.”

Ao “nafsi hiyo inapaswa.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Ao “nafsi inagusa.”

Ao “nafsi hiyo inapaswa.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Ao “Nafsi yoyote yenye inakula damu yoyote inapaswa.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Ao “mushipi.”

Ao “taji takatifu.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “mafuta yenye kuzunguka figo.”

Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Tnn., “kujaza mikono yenu.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Ao “eko.”

Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Pezi ni kiungo cha samaki chenye kinamusaidia kuogelea.

Pezi ni kiungo cha samaki chenye kinamusaidia kuogelea.

Pezi ni kiungo cha samaki chenye kinamusaidia kuogelea.

Ao “Kila kidudu.”

Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Ao “kigeu-geu.”

Ao “Musifanye nafsi zenu.”

Ao “kuchafua nafsi zenu.”

Ao “nafsi yenye uzima yenye.”

Ao “nafsi yenye.”

Ao “hezi.”

Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.

Ao “hezi.”

Ao “eko.”

Kigaga ni ngozi ngumu juu ya kidonda chenye kinakaribia kupona.

Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “ukoma” liko na maana pana na linaweza kutia ndani magonjwa mbalimbali yenye kuambukizwa ya ngozi. Linaweza pia kutia ndani magonjwa fulani yenye kuambukizwa ambayo yanapatikana kwenye nguo na ndani ya nyumba.

Kigaga ni ngozi ngumu juu ya kidonda chenye kinakaribia kupona.

Ao “ugonjwa huo umeenea.”

Ao “mara ya pili.”

Kigaga ni ngozi ngumu juu ya kidonda chenye kinakaribia kupona.

Ao “eko.”

Ao “hawezi kuwaambukiza wengine.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Tnn., “ndani ya ngozi ya mwili wake.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Masharubu ni nywele zenye kuota kwenye mudomo wa juu.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio wa.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mushindio.” Angalia Maana ya Maneno.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Sehemu tatu za kumi za efa zilikuwa sawa na litre 6.6 (vibaba 6). Angalia Nyongeza B14.

Logi moja ilikuwa sawa na litre 0.31 (painti 0.66). Angalia Nyongeza B14.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Sehemu moja ya kumi ya efa ilikuwa sawa na litre 2.2 (vibaba 2). Angalia Nyongeza B14.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Hapa lipu ni muchanganyiko wa chokaa, muchanga na maji wenye unapakwa juu ya ukuta ili kuufanya ukuwe sawasawa na laini.

Ao “mortier.”

Ao “mortier.”

Hapa lipu ni muchanganyiko wa chokaa, muchanga na maji wenye unapakwa juu ya ukuta ili kuufanya ukuwe sawasawa na laini.

Hapa lipu ni muchanganyiko wa chokaa, muchanga na maji wenye unapakwa juu ya ukuta ili kuufanya ukuwe sawasawa na laini.

Hapa lipu ni muchanganyiko wa chokaa, muchanga na maji wenye unapakwa juu ya ukuta ili kuufanya ukuwe sawasawa na laini.

Ao “mortier.”

Hapa lipu ni muchanganyiko wa chokaa, muchanga na maji wenye unapakwa juu ya ukuta ili kuufanya ukuwe sawasawa na laini.

Tnn., “zambi.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Tnn., “zambi.”

Kigaga ni ngozi ngumu juu ya kidonda chenye kinakaribia kupona.

Ao “eko.”

Tnn., “mwili wake.”

Ao “eko.”

Ao “Tandiko lolote la.”

Ao “shahawa.”

Ao “shahawa iko.”

Ao “shahawa.”

Ao “eko.”

Ao “hezi.”

Ao “hezi.”

Ao “hezi.”

Ao “hezi.”

Ao “hezi.”

Ao “shahawa.”

Ao “nguo za ndani.”

Ao “mwili wake wenye haufunikwe.”

Pengine neno hilo linamaanisha “Mbuzi Mwenye Anapotea.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “mutu mwenye kuwa tayari.”

Ao “kutesa nafsi zenu.” Kwa ujumla inaeleweka kuwa “kujitesa” kunamaanisha njia mbalimbali za kujinyima, kutia ndani kufunga.

Ao “kutesa nafsi zenu.”

Tnn., “mwenye mukono wake utajazwa.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Tnn., “mbuzi.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Ao “nafsi hiyo yenye inakula.”

Ao “nitamuua kutoka.”

Ao “nafsi ya iko.”

Ao “kwa ajili ya nafsi zenu.”

Ao “nafsi yenye.”

Ao “nafsi.”

Ao “nafsi ya.”

Ao “nafsi iko.”

Ao “nafsi ya.”

Ao “atauawa.”

Tnn., “kufunua uchi,” katika mustari huu na katika mistari yenye kufuata.

Tnn., “Ni uchi wa baba yako.”

Ao “Eko.”

Ao “eko.”

Tnn., “Usifunue uchi wa ndugu ya baba yako.”

Katika desturi ya Waebrania shangazi ni dada ya mama ao dada ya baba, ao bibi ya ndugu ya baba.

Tnn., “ni uchi wa ndugu yako.”

Ao “mwenendo wa haya; mwenendo muchafu sana. ”

Ao “jirani yako, rafiki yako.”

Ao “nafsi zote zenye kufanya mambo hayo zinapaswa.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Tnn., “kumuogopa.”

Ao “nafsi hiyo inapaswa.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Ao “wenye kuteseka.”

Ao “kuita ubaya juu ya.”

Tnn., “damu ya.”

Ao pengine, “Haupaswe kusimama bila kufanya kitu wakati uzima wa mwenzako uko katika hatari.”

Tnn., “yenye hayatahiriwe.”

Ao “Musipunguze; Musikate.”

Ao “kwa ajili ya nafsi yenye imekufa.” Katika mustari huu, neno la Kiebrania neʹphesh linamaanisha mutu mwenye amekufa.

Tnn., “kuogopa.”

Ujazo ni ukubwa ao wingi wa kitu chenye kujaza nafasi ao kitu fulani.

Ao “kilo.”

Tnn., “kipimo sahihi cha efa.” Angalia Nyongeza B14.

Tnn., “kipimo sahihi cha hini.” Angalia Nyongeza B14.

Ao “nitamuua kutoka.”

Ao “Nitamuua kutoka.”

Ao “nafsi yenye inaendea.”

Ao “nafsi hiyo.”

Ao “kumuua kutoka.”

Ao “anaita ubaya juu ya.”

Tnn., “amefunua uchi wa baba yake.”

Ao “mwenendo wa haya; mwenendo muchafu sana.”

Ao “kuuawa.”

Tnn., “Amefunua uchi wa dada yake.

Ao “eko.”

Ao “hezi.”

Ao “kuuawa kutoka.”

Ao “eko.”

Tnn., “amefunua uchi wa ndugu ya baba yake.”

Tnn., “Amefunua uchi wa ndugu yake.”

Ao “kufanya nafsi zenu kuwa zenye.”

Ao “mwenye iko na roho ya kutabiri matukio.”

Ao “nafsi yenye ilikufa.”

Ao “eko.”

Ao “chakula cha,” ni kusema, zabihu.

Tnn., “mwenye mukono wake ulijazwa.”

Ao “kukaribia nafsi yoyote yenye imekufa.” Katika mustari huu neno la Kiebrania neʹphesh linahusiana na neno la Kiebrania lenye kumaanisha “mwenye amekufa.”

Tnn., “mbegu yake.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “ao mwenye pua yenye kukatika.”

Ao pengine, “mwenye kukonda sana na zaifu.”

Ni ugonjwa fulani wa ngozi.

Tnn., “mbegu ya.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Tnn., “wanapaswa kujitenga na.”

Ao “nafsi hiyo itaondolewa.”

Ao “nafsi yenye imekufa.”

Ao “shahawa.”

Tnn., “mugeni yeyote,” ni kusema, mutu mwenye haiko wa familia ya Haruni.

Ao “ananunua nafsi.”

Ao “anaolewa na mugeni.”

Tnn., “mugeni,” ni kusema, mutu mwenye haiko wa familia ya Haruni.

Kigaga ni ngozi ngumu juu ya kidonda chenye kinakaribia kupona.

Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”

Sehemu mbili za kumi za efa zilikuwa sawa na litre 4.4 (vibaba 4). Angalia Nyongeza B14.

Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

Hini ilikuwa sawa na litre 3.67 (painti 7.75). Angalia Nyongeza B14.

Sehemu mbili za kumi za efa zilikuwa sawa na litre 4.4 (vibaba 4). Angalia Nyongeza B14.

Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Ao “wenye kuteseka.”

Ao “kutesa nafsi zenu.” Kwa ujumla inaeleweka kuwa “kujitesa” kunamaanisha njia mbalimbali za kujinyima, kutia ndani kufunga.

Ao “Nafsi yoyote yenye haitajitesa.” Ao pengine, “Mutu yeyote mwenye hatafunga.”

Ao “atauawa kutoka.”

Ao “nafsi.”

Ao “mutatesa nafsi zenu.”

Ao “Makao ya Muda.”

Ao “bonde la muto.”

Sehemu mbili za kumi za efa zilikuwa sawa na litre 4.4 (vibaba 4). Angalia Nyongeza B14.

Ni kusema, jina Yehova, kulingana na mustari wa 15 na 16.

Ao “kuita ubaya juu ya jina hilo.”

Ao “Kama mutu anapiga nafsi yoyote ya mwanadamu mupaka inakufa.”

Ao “mwenye anapiga na kuua nafsi ya munyama.”

Ao “nafsi kwa nafsi.”

Tnn., “wana.”

Ao “mutu yeyote mwenye iko na uhusiano wa damu pamoja naye.”

Tnn., “wana.”

Tnn., “kuogopa.”

Tnn., “Nitageuka kuwaelekea.”

Ao “nafsi yangu haitawakataa.”

Tnn., “mutembee mukiwa wima.”

Ao “nafsi yenu ikuwe.”

Tnn., “fimbo.” Inawezekana ni fimbo zenye zilikuwa zinatumiwa ili kuwekea mikate.

Ao “chakula.”

Ao “kilo.”

Pengine neno la Kiebrania lenye linatumiwa hapa linahusiana na maneno “mavi ya wanyama” na linatumiwa ili kuonyesha zarau.

Ao “nafsi yangu itawachukia.”

Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

Ao “itashika sabato.”

Ao “mioyo yao migumu.”

Ao “nafsi zao zilichukia.”

Ao “nafsi.”

Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.

Ao “shekeli takatifu.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Homeri moja ilikuwa sawa na litre 220 (vibaba 200). Angalia Nyongeza B14.

Gera moja ilikuwa sawa na grame 0.57 (aunsi troi 0.01835). Angalia Nyongeza B14.

Ao “eko.”

Ao “ili kiharibiwe.”

Ao “Kila zaka.”

Ao “kichwa cha kumi.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine