Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova
Kwako Wewe Unayemupenda Yehova:
Yesu alisema: ‘Mutaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.’ (Yohana 8:32) Maneno hayo yanatia moyo kabisa! Ndiyo, inawezekana kujua kweli, hata katika hizi “siku za mwisho” zilizo hatari, wakati ambapo uongo umeenea mahali pote. (2 Timotheo 3:1) Unakumbuka ni wakati gani kwa mara ya kwanza ulitambua kama umeipata kweli iliyo katika Neno la Mungu? Wakati huo ulifurahi sana, sivyo?
Kujua kweli na kuwahubiria wengine kwa ukawaida kweli hiyo ni jambo la lazima. Lakini, tunapaswa pia kuishi kupatana na kweli hiyo. Ili tuweze kufanya hivyo, ni lazima tubaki katika upendo wa Mungu. Hilo linamaanisha nini? Jibu linapatikana katika maneno ambayo Yesu aliwaambia mitume wake waaminifu usiku mbele ya kufa kwake. Aliwaambia hivi: ‘Mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba na kukaa katika upendo wake.’—Yohana 15:10.
Andiko hilo linaonyesha kama Yesu alibaki katika upendo wa Mungu kwa kushika amri za Baba yake. Sisi pia tunapaswa kufanya hivyo. Ili kubaki katika upendo wa Mungu, lazima tuishi kulingana na kweli. Usiku huohuo, Yesu alisema tena hivi: ‘Ikiwa munajua mambo haya, wenye furaha ni ninyi ikiwa munayatenda.’—Yohana 13:17.
Tunatumaini kabisa kama kitabu hiki kitakusaidia uendelee kuishi kupatana na kweli na ukifanya hivyo utabaki katika “upendo wa Mungu . . . kwa kutazamia uzima wa milele.”—Yuda 21.
Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova