Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 78 uku. 184-uku. 185 fu. 1
  • Yesu Anahubiri Habari ya Ufalme

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anahubiri Habari ya Ufalme
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Yesu Anatuma Wanafunzi 70 ili Waende Kuhubiri
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Utumishi Wake Unapanuka Katika Galilaya
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 78 uku. 184-uku. 185 fu. 1
Yesu iko anahubiri pamoja na mwanafunzi wake

78

Yesu Anahubiri Habari ya Ufalme

Wakati kidogo kisha kubatizwa, Yesu alianza kuhubiri hivi: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’ Alitembea sana mu Galilaya na Yudea, na wanafunzi fulani walikuwa wanamusindikiza. Wakati Yesu alirudia Nazareti, kwenye alikomaliaka, alienda ku sinagogi. Kule, alifungua kitabu cha kukunjwa cha Isaya na kusoma kwa sauti: ‘Yehova amenipatia roho takatifu ili nihubiri habari njema.’ Watu walipenda afanye miujiza. Lakini sababu kubwa yenye ilifanya Mungu amupatie roho takatifu ilikuwa ili ahubiri habari njema. Kisha, aliambia wasikilizaji wake: ‘Leo, unabii huu umetimia.’

Kisha, Yesu akaenda ku Bahari ya Galilaya. Kule, aliona wavuvi ine wa samaki, wenye walikubali kuwa wanafunzi wake. Majina yao ni: Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana. Yesu aliwaambia: ‘Munifuate. Nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.’ Mara moja wakaacha kazi yao ya kuvua samaki na wakamufuata. Walisafiri mu Galilaya yote ili kuhubiri kuhusu Ufalme wa Yehova. Walihubiri mu masinagogi, mu soko, na mu barabara. Watu mingi waliwafuata kila fasi kwenye walienda. Habari kuhusu Yesu ilienea kila fasi, ilifika hata Siria.

Kisha, Yesu alipatia wamoja kati ya wanafunzi wake uwezo wa kuponyesha watu na kufukuza pepo wachafu. Wengine walikuwa wanamusindikiza wakati alikuwa anahubiri mu kila muji na mu kila kijiji. Wanamuke fulani waaminifu, sawa vile Maria Magdalene, Yoana, Susana, walikuwa wanatumia vitu vyao ili kuhangaikia mahitaji ya Yesu na ya wafuasi wake.

Kisha Yesu kuzoeza wanafunzi wake, aliwatuma waende kuhubiri. Wakati walikuwa wanahubiri mu Galilaya, watu wengine wengi wakakuwa wanafunzi wa Yesu na wakabatizwa. Kwa sababu watu mingi sana walitaka kuwa wanafunzi, Yesu alisema kama walikuwa sawa vile shamba lenye liko tayari kuvunwa. Alisema: ‘Muombe Yehova atume wafanyakazi mingi mu kazi ya kuvuna.’ Kisha alichagua wanafunzi 70 na kuwatuma waende kuhubiri wawili-wawili mu Yudea yote. Walifundisha watu wa namna zote habari ya Ufalme. Wakati walirudia, walielezea Yesu mambo yenye ilifanyika, na walikuwa na furaha sana. Hakuna kitu chenye Shetani angeweza kufanya ili kuzuia kazi ya kuhubiri.

Yesu alipenda wanafunzi wake waendelee kufanya ile kazi ya maana kisha yeye kurudia mbinguni. Kwa hiyo, aliwaambia: ‘Muhubiri habari njema mu dunia yote. Mufundishe watu Neno la Mungu na muwabatize.’

“Ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika miji ingine, kwa sababu nilitumwa ili kufanya vile.”​—Luka 4:43

Maulizo: Ni kazi gani yenye Yesu alipatia wanafunzi wake? Wanafunzi wake waliona ile kazi namna gani?

Matayo 4:17-25; 9:35-38; 28:19, 20; Marko 1:14-20; Luka 4:14-21; 8:1-3; 10:1-22

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine