Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w24 Mwezi wa 9 uku. 19
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Anatuma Wanafunzi 70 ili Waende Kuhubiri
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • “Siku Hii Itakuwa Ukumbusho Kwenu”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Chakula cha Mangaribi cha Bwana Chenye Hakina Mambo Mingi, Kinatufundisha Nini Juu ya Mufalme wa Mbinguni?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Chakula cha Mangaribi cha Mwisho cha Yesu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
w24 Mwezi wa 9 uku. 19
Yesu alianzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana pamoya na mitume wake waaminifu.

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wakati Yesu alianzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana, wale wanafunzi 70 wenye alitumaka kuhubiri walikuwa wapi? Walikuwa wamemuacha?

Hatupaswe kuwaza kama wale wanafunzi 70 walikuwa wamemuacha Yesu ao walikuwa wamekataliwa juu tu hawakukuwa pale wakati Yesu alianzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Yesu alipenda tu akuwe na mitume wake ku ile tukio.

Ikuwe wale 12 ao wale 70, wote walikuwa wanafunzi wa Yesu. Yesu alichagula kwanza kati ya wanafunzi wake wanaume 12 wenye aliita mitume. (Lu. 6:12-16) Alikuwa Galilaya wakati ‘aliita wale Kumi na Mbili’ na “akawatuma kuhubiri Ufalme wa Mungu.” (Lu. 9:1-6) Kisha, wakati alirudia Yudea “akachagua wengine makumi saba (70) na akawatuma wawili-wawili.” (Lu. 9:51; 10:1) Kwa hiyo, Yesu alikuwa na wanafunzi fasi mbalimbali kwenye ujumbe wake ulihubiriwa.

Wayahudi wenye walifikia kuwa wanafunzi wa Yesu, walikuwa wangali wanaendelea kusherehekea Pasaka ya kila mwaka, inawezekana walifanya vile pamoya na watu wa familia zao. (Kut. 12:6-11, 17-20) Wakati kifo yake ilikaribia, Yesu na mitume walienda Yerusalemu. Lakini Yesu hakuita wanafunzi wake wote juu washerehekee Pasaka pamoya naye, ni kusema wanafunzi wake kutoka Yudea, Galilaya, na Perea. Ni wazi kama, Yesu alipenda kuwa tu na mitume wake mu ile tukio. Aliwaambia hivi: “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja na ninyi mbele niteseke.”—Lu. 22:15.

Yesu alikuwa na sababu ya muzuri yenye ilimuchochea afanye vile. Karibuni Yesu alipaswa kufa kama “Mwana-Kondoo wa Mungu mwenye anatosha zambi ya ulimwengu.” (Yoh. 1:29) Ile ilipaswa kufanyika mu Yerusalemu, kwenye watu walikuwa wanamutolea Mungu zabihu tangu zamani. Kondoo wa Pasaka alikumbusha Waisraeli kama Yehova aliwakomboa kutoka Misri, lakini zabihu ya Yesu ingeleta baraka mingi zaidi. Ingekomboa wanadamu wote kutokana na zambi na kifo. (1 Ko. 5:7, 8) Zabihu ya Yesu ilifanya wale 12 wakuwe sehemu ya musingi wa kutaniko ya Kikristo. (Efe. 2:20-22) Yerusalemu, muji mutakatifu, uko na “majiwe ya musingi kumi na mbili (12)” kwenye kunaandikwa “majina kumi na mbili ya mitume kumi na mbili wa Mwana-Kondoo.” (Ufu. 21:10-14) Kwa kweli, mitume waaminifu wa Yesu walipaswa kuwa na daraka kubwa mu utimizo wa kusudi ya Mungu. Tunaelewa juu ya nini Yesu alipenda kuwa kabisa na mitume wake ku Pasaka ya mwisho na ku tukio yenye ilifuata ni kusema, wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana.

Wale 70 na wanafunzi wengine wa Yesu hawakukuwa ku ile Chakula cha Mangaribi cha Bwana pamoya na Yesu. Lakini wanafunzi wote waaminifu wa Yesu walifaidika na Chakula cha Mangaribi cha Bwana, na Wakristo wote wenye walitiwa mafuta waliingia mu agano kwa ajili ya ufalme yenye Yesu alizungumuzia pamoya na mitume wake ile usiku.—Lu. 22:29, 30.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine