Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/3 uku. 3
  • “Wakristo” Wote Ni Wakristo wa Kweli?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Wakristo” Wote Ni Wakristo wa Kweli?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kutambua Wakristo wa Kweli
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Namna Gani Unaweza Kuipata Ile Dini ya Kweli?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Ni Jambo la Maana Sana Kulinganisha Mambo Unaamini na Biblia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Ukuwe Hakika Kabisa Kama Uko na Kweli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/3 uku. 3

“Wakristo” Wote Ni Wakristo wa Kweli?

Mu dunia muko Wakristo ngapi? Kitabu Atlas of Global Christianity inaonyesha kama mu 2010, mu dunia yote mulikuwa Wakristo karibu miliare 2.3. Ileile kitabu inaonyesha kama wale Wakristo wanapatikana mu dini zaidi ya 41 000 na kila dini iko na mafundisho yake na kanuni zake. Juu kuko dini za mingi zenye kujiita kuwa za “Kikristo,” ile inafanya watu fulani wavurugike na kuvunjika moyo. Wote wenye kujiita Wakristo ni Wakristo wa kweli kabisa?

Tukamate mufano. Kama mutu iko nasafiri mu inchi ingine, wakati anafika ku mipaka anapaswa kusema anatoka mu inchi gani. Na juu ya kuhakikisha kama ni vile kabisa, anapaswa kuonyesha kitambulisho yake. Vilevile haitoshe kwa Mukristo kusema tu kama anamuamini Yesu. Anapaswa kufanya mambo fulani juu ya kuhakikisha kama anamuamini kabisa Yesu. Anapaswa kufanya nini?

Neno Mukristo ilitumiwa kwa mara ya kwanza wakati fulani kisha mwaka wa 44 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Mwandikaji wa Biblia mwenye kuitwa Luka aliandika hivi: “Ni kule Antiokia ndiko kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo.” (Mdo. 11:26) Tunaona kama Bilbila inaonyesha kuwa wanafunzi wa Yesu njo waliitwa Wakristo. Mutu anapaswa kufanya nini juu akuwe mwanafunzi wa Yesu Kristo? Kitabu The New International Dictionary of New Testament Theology inasema hivi: “Juu mutu akuwe mwanafunzi wa Yesu anapaswa kuwa tayari kufuata mufano wa Yesu maisha yake yote.” Kwa hiyo, Mukristo wa kweli ni mutu mwenye anafuata kwa moyo wote mafundisho na maagizo yote ya Yesu, mwenye alianzisha Ukristo.

Inawezekana kupata watu wa vile kati ya watu wengi wenye wanajiita Wakristo leo? Yesu alisema mambo gani yenye inaweza kutusaidia kutambua Wakristo wa kweli? Tunakutia moyo uone namna Biblia inajibia ile maulizo. Mu habari zenye kufuata, tutaona mambo tano yenye Yesu alisema yenye inaweza kutusaidia kutambua wanafunzi wake wa kweli. Tutaona namna Wakristo wa kwanza-kwanza walitimiza ile mambo. Na tutaona ni nani njo wanajikaza kutimiza ile mambo kati ya watu wengi wenye kujiita Wakristo leo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine