Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp16 na. 4 uku. 14-15
  • Ni Jambo la Maana Sana Kulinganisha Mambo Unaamini na Biblia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Jambo la Maana Sana Kulinganisha Mambo Unaamini na Biblia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NAMNA YA KULINGANISHA MAMBO YENYE TUNAAMINI NA BIBLIA
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
wp16 na. 4 uku. 14-15

Ni Jambo La Maana Sana Kulinganisha Mambo Unaamini Na Biblia

WEWE ni Mukristo? Kama jibu ni ndiyo, uko kati ya watu zaidi ya miliare mbili katika dunia, ni kusema, mutu 1 juu ya kila watu 3 mwenye kujiita Mukristo. Leo, kuna maelfu ya vikundi vya dini vyenye kujiita kuwa za Kikristo, lakini mafundisho na mawazo ya vikundi hivyo hayapatane. Kwa hiyo, mambo unaamini yanaweza kuwa tofauti na mambo yenye watu wengine wenye kusema kuwa ni Wakristo wanaamini. Ni jambo la maana kabisa kujua mambo yenye tunaamini? Jibu ni ndiyo kama unataka kufuata Ukristo wenye kufundishwa katika Biblia.

Wanafunzi wa kwanza wa Yesu Kristo walifikia kuitwa “Wakristo.” (Matendo 11:26) Haikuwa lazima wakuwe na majina mengine ya kuwatambulisha, kwa sababu kulikuwa imani moja tu ya Kikristo. Wakristo walifuata kwa umoja mafundisho na mambo yenye Yesu Kristo, mwenye alianzisha Ukristo, aliwaomba wafanye. Kanisa lako linafanya hivyo? Uko hakika kwamba kanisa lako linafundisha mambo Kristo alifundisha na mambo wanafunzi wa kwanza waliamini? Ni jambo gani linaweza kukusaidia ukuwe hakika? Kuna jambo moja tu la kufanya: kutumia Biblia ili kulinganisha mambo yenye unaamini na mambo Biblia inasema.

Fikiria jambo hili: Yesu Kristo aliheshimia sana Maandiko; aliyaona kuwa Neno la Mungu. Yesu hakukubali wale wenye walizarau mafundisho ya Biblia kwa kutia pa nafasi ya kwanza desturi za watu. (Marko 7:9-13) Tunaweza kusema na uhakika wote kwamba mafundisho ya wanafunzi wa kweli wa Yesu yanapaswa kutegemea Biblia. Kwa hiyo, ni muzuri kila Mukristo ajiulize, ‘Mafundisho ya kanisa langu yanapatana na mambo Biblia inasema?’ Ili kujibu ulizo hilo, sababu gani usilinganishe mambo kanisa lako linafundisha na mambo Biblia inasema kabisa?

Yesu alisema kwamba ibada yetu kwa Mungu inapaswa kupatana na kweli, na kweli hiyo inapatikana katika Biblia. (Yohana 4:24; 17:17) Na mutume Paulo alisema kwamba kupata “ujuzi sahihi wa kweli” ni jambo la maana sana ili tupate wokovu. (1 Timotheo 2:4) Kwa hiyo, mambo yenye tunaamini yanapaswa kutegemea kweli sahihi ya Biblia. Ni lazima kufanya hivyo, kwa sababu wokovu wetu uko katika hatari.

NAMNA YA KULINGANISHA MAMBO YENYE TUNAAMINI NA BIBLIA

Tunakualika kusoma maulizo sita yenye kuwa katika habari hii na uone majibu ya Biblia kwa maulizo hayo. Soma maandiko ya Biblia yenye kutajwa, na uwaze sana juu ya majibu ya maulizo hayo. Kisha, ujiulize, ‘Mafundisho ya kanisa langu yanapatana na mambo Biblia inasema?’

Sehemu hii fupi ya maulizo inaweza kukusaidia kufanya jambo la maana sana, ni kusema, kulinganisha mambo unaamini na Biblia. Uko tayari kulinganisha mafundisho mengine ya kanisa lako na mambo Biblia inasema? Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia kuchunguza kweli yenye kuwa wazi ya Biblia. Sababu gani usiombe Shahidi mumoja ajifunze na wewe Biblia bila kulipa? Ao unaweza kufungua adresi yetu ya Internete, jw.org.

1 ULIZO: Mungu ni nani?

JIBU: Yehova, Baba ya Yesu, ni Mungu wa milele na Muumbaji Mweza-Yote wa vitu vyote.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

• ‘Sikuzote sisi tunamushukuru Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, tunaposali kwa ajili yenu.’—Wakolosai 1:3.

• “Unastahili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.”—Ufunuo 4:11.

• Ona pia Waroma 10:13; 1 Timotheo 1:17.

2 ULIZO: Yesu Kristo ni nani?

JIBU: Yesu ni Mwana muzaliwa wa kwanza wa Mungu. Yesu aliumbwa, na kwa hiyo, iko na mwanzo. Yesu anajitiisha kwa Mungu na anatii mapenzi Yake.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

• ‘Baba ni mukubwa kuliko mimi.’—Yohana 14:28.

• ‘[Yesu] ndiye mufano wa Mungu asiyeonekana, muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.’—Wakolosai 1:15.

• Ona pia Mathayo 26:39; 1 Wakorintho 15:28.

3 ULIZO: Roho takatifu ni nini?

JIBU: Roho takatifu ni nguvu yenye Mungu anatumia ili kutimiza mapenzi yake. Haiko mutu. Watu wanaweza kujazwa roho takatifu na kutiwa nguvu na roho takatifu.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

• ‘Elisabeti aliposikia salamu za Maria, yule mutoto muchanga katika tumbo lake la uzazi akaruka; na Elisabeti akajazwa roho takatifu.’—Luka 1:41.

• ‘Mutapokea nguvu wakati roho takatifu itakapofika juu yenu.’—Matendo 1:8.

• Ona pia Mwanzo 1:2; Matendo 2:1-4; 10:38.

4 ULIZO: Ufalme wa Mungu ni nini?

JIBU: Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni. Yesu ndiye Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Karibuni, Ufalme huo utafanya mapenzi ya Mungu yatendeke juu ya dunia yote.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

• ‘Malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake. Na sauti kubwa zikatokea mbinguni, zikisema: Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala akiwa mufalme milele na milele.’—Ufunuo 11:15.

• Ona pia Danieli 2:44; Mathayo 6:9, 10

5 ULIZO: Watu wote wazuri wanaenda mbinguni?

JIBU: Hapana. Watu kidogo waaminifu, wenye kuitwa ‘kundi ndogo,’ wanachaguliwa na Mungu ili kuenda mbinguni. Watakuwa wafalme na watatawala pamoja na Yesu juu ya wanadamu.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

• ‘Musiogope, kundi ndogo, kwa sababu Baba yenu amekubali kuwapa ninyi ufalme.’—Luka 12:32.

• “Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye.”—Ufunuo 20:6.

• Ona pia Ufunuo 14:1, 3.

6 ULIZO: Mapenzi ya Mungu juu ya dunia na wanadamu ni nini?

JIBU: Chini ya Ufalme wa Mungu, dunia itakuwa paradiso na wanadamu waaminifu watakuwa na afya kamilifu, amani na uzima wa milele.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

• “Wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”—Zaburi 37:10, 11.

• “Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:3, 4.

• Ona pia Zaburi 37:29; 2 Petro 3:13

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine