Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/12 uku. 4
  • Kumukumbuka Yesu Kristo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kumukumbuka Yesu Kristo
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Shuguli za Watu Wakati wa Noeli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Noeli ni ya Wakristo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Sababu gani watu wengine hawafanye sikukuu ya Noeli?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/12 uku. 4

Kumukumbuka Yesu Kristo

“Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”​—LUKA 22:19.

Sababu inayowafanya watu wengine wafanye sikukuu ya Noeli.

Juu ya sikukuu ya Noeli, watu wengine wanasema kama wanafanya sikukuu hiyo “kwa ajili ya Yesu.” Wanafanya sikukuu ya Noeli ili kukumbuka kuzaliwa kwake.

Je, hiyo ni sababu yenye kufaa?

Miziki inayotumiwa na watu wengi na desturi zinazofanywa na watu wengi wakati huo wa Noeli, yote hayo hayana uhusiano wowote na Yesu Kristo. Watu wengi sana wanaofanya sikukuu ya Noeli hawamuamini Yesu; wengine kati yao hawaamini hata kuwa Yesu aliishi. Kuliko kumukumbuka Yesu, wafanyabiashara wengi wanatumia wakati wa Noeli ili kufanya matangazo ya biashara yao.

Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kutusaidia?

“Mwana wa binadamu alikuja . . . kutoa nafsi yake iwe fidia badala ya wengi.” (Marko 10:45) Ni wazi kwamba Yesu alisema maneno yanayotajwa mwanzoni mwa habari hii usiku uliotangulia kufa kwake, wala si siku ya kuzaliwa kwake. Mangaribi hiyo, alianzisha tukio la kukumbuka kifo chake ambalo halikuwa na mambo mengi. Lakini, sababu gani Yesu alitaka wafuasi wake wakumbuke kifo chake kuliko kukumbuka kuzaliwa kwake? Kwa sababu zabihu ya Yesu ya ukombozi inatolea wanadamu watiifu nafasi ya kupata uzima wa milele. Biblia inasema hivi: ‘Mushahara ambao zambi inalipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu anatoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.’ (Waroma 6:23) Kwa hiyo, kila mwaka, siku ya kukumbuka kifo cha Yesu Kristo, wafuasi wake wanamukumbuka kama ‘muokozi wa ulimwengu,’ wala si kama mutoto muchanga.​—Yohana 4:42.

‘Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi kielelezo ili mufuate hatua zake kwa ukaribu.’ (1 Petro 2:21) Ili kumuheshimu na kumukumbuka Yesu, unapaswa kujifunza mufano alioweka akiwa mutu mukamilifu na mwenye akili. Pia, ufikiri sana juu ya namna Yesu alivyoonyesha huruma, uvumilivu, na uhodari ili kufanya yaliyo mema, na utafute nafasi za kumuiga katika maisha yako.

‘Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala akiwa mufalme milele na milele.’ (Ufunuo 11:15) Unapomukumbuka Yesu Kristo, fikiria kazi anayofanya sasa. Leo, Yesu ni Mufalme anayetawala huko mbinguni. Je, unawaza hawahangaikie wanadamu kwa sababu iko mbali sana nao? Hapana. Neno la Mungu lilitabiri juu ya Yesu hivi: “Atawahukumu kwa uadilifu watu wa hali ya chini, atakaripia kwa unyoofu kwa ajili ya watu wapole wa dunia.” (Isaya 11:4) Sifa hizo zenye kuvutia si za mutoto muchanga, lakini ni za Mutawala mwenye nguvu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine