Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/12 uku. 3
  • Shuguli za Watu Wakati wa Noeli

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Shuguli za Watu Wakati wa Noeli
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/12 uku. 3

Shuguli za Watu Wakati wa Noeli

TAREHE 23 MWEZI WA 12, 2008, BRAD HENRY, LIWALI WA ZAMANI WA JIMBO LA OKLAHOMA [États-Unis], alisema hivi: “Ni vyepesi sana mutu kujiingiza katika shuguli za wakati wa Noeli. Watu wanafanya desturi za Noeli kwa sababu tu ya kulazimishwa, na kwa sababu ya shuguli nyingi, hawana wakati mwingi wa kuwa pamoja na watu wa familia na marafiki wao. Furaha ambayo tungepaswa kuwa nayo, inakosekana wakati fulani kwa sababu ya kuwa na mahangaiko mengi.”

WAKATI wa Noeli unapokaribia, nyimbo, filme, na programu za televizyo, yote hayo yanafanya kipindi cha Noeli kiwe chenye kufurahisha na chenye kusisimua. Unawaza ni nini kinachosukuma watu kuwa na shuguli nyingi wakati huo wa Noeli? Unawaza ni

● Kumukumbuka Yesu Kristo?

● Kuwa na furaha ya kutoa?

● Kusaidia wenye uhitaji?

● Kuwa pamoja na watu wa jamaa?

● Kuwa na amani na watu wengine?

Kama Liwali Henry, aliyetajwa mwanzoni mwa habari hii alivyosema, watu wengi wanaofanya sikukuu ya Noeli wanaona kuwa ni vigumu kutimiza mambo hayo yote wakati wa Noeli. Mara nyingi wakati wa Noeli unakuwa wakati wenye shuguli nyingi, wenye mahangaiko, na zaidi ya yote, unakuwa wakati wa biashara. Je, inawezekana kuwa na furaha na kuonyesha upendo ambao watu wanatazamia wakati huo?

Biblia inatutia moyo sisi wote kumukumbuka Yesu Kristo, kuwa wakarimu, kusaidia wenye uhitaji, na kupitisha wakati pamoja na watu wa jamaa zetu. Pia inatufundisha namna ya kuwa watu wenye amani. Kwa hiyo, habari hii na zingine zinazofuata hazitazungumuzia sababu gani watu wengine hawafanye sikukuu ya Noeli,a lakini zitazungumuzia maulizo yanayofuata:

● Watu wengine wanasema ni nini inapaswa kuwa sababu ya kufanya sikukuu ya Noeli?

● Sababu gani ni vigumu kutimiza mambo wanayotazamia wakati wa Noeli?

● Ni kanuni gani za Biblia ambazo zimewasaidia watu wengi kupata jambo nzuri zaidi kuliko Noeli?

[Maelezo ya chini]

a Ili kujua sababu za kimaandiko zinazowafanya watu wengine wasifanye sikukuu ya Noeli, soma habari yenye kichwa “Wasomaji Wetu Wanauliza​—Sababu Gani Watu Wengine Hawafanye Sikukuu ya Noeli?” kwenye ukurasa wa 10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine