Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/2 uku. 3
  • Musa Alikuwa Nani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Musa Alikuwa Nani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Muti Mudogo Unawaka Moto
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Musa​—Mwanaume Aliyeonyesha Upendo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Tuige Imani ya Musa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Unamuona “Yeye Asiyeonekana”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/2 uku. 3

KICHWA: MUFANO WA MUSA UNATUFUNDISHA NINI?

Musa Alikuwa Nani?

[Picha katika ukurasa wa 3]

Unafikiria nini unaposikia jina Musa? Je, unafikiria . . .

  • mutoto ambaye mama yake alificha ndani ya kikapu kwenye Muto Nile?

  • mutoto mwanaume aliyelelewa na binti ya Farao katika maisha ya raha ya huko Misri, lakini ambaye hakusahau hata kidogo kwamba alikuwa Muisraeli?

  • mwanaume aliyeishi akiwa muchungaji katika Midiani kwa miaka 40?

  • mwanaume aliyezungumuza na Yehovaa mbele ya kichaka kilichokuwa kinawaka moto?

  • mwanaume aliyesimama mbele ya mufalme wa Misri, na kumuomba bila woga awaachilie huru Waisraeli kutoka katika utumwa?

  • mwanaume ambaye, kwa muongozo wa Mungu, alitangaza Mapigo Kumi juu ya Misri wakati mufalme wa Misri alikataa kumutii Mungu wa kweli?

  • mwanaume aliyeongoza Waisraeli katika safari ndefu kutoka Misri?

  • mwanaume aliyetumiwa ili kugawanya mara mbili Bahari Nyekundu?

  • mwanaume aliyewapatia Waisraeli Amri Kumi kutoka kwa Mungu?

MUSA alifanya mambo yote hayo na alifanya hata zaidi ya hayo. Haishangaze kuona kwamba mwanaume huyo mwaminifu anaheshimiwa sana na Wakristo, Wayahudi na pia Waislamu.

Ni wazi kwamba Musa alikuwa nabii ambaye alionyesha ‘hofu kubwa.’ (Kumbukumbu la Torati 34:10-12) Aliruhusu Mungu amutumie kwa njia yenye nguvu sana. Lakini, Musa alikuwa mwanadamu wa kawaida. Kama vile tu nabii Eliya, ambaye alionekana pembeni ya Musa katika maono wakati wa utumishi wa Yesu duniani, Musa alikuwa mutu “mwenye hisia kama zetu.” (Yakobo 5:17; Mathayo 17:1-9) Musa alipambana na matatizo mengi kama yale tunayopambana nayo, na aliweza kuyashinda.

Je, ungependa kujua ni nini kilimusaidia kushinda matatizo hayo? Chunguza sifa tatu nzuri kati ya sifa ambazo Musa alionyesha na yale tunaweza kujifunza kutokana na mufano wake.

a Yehova ni jina la Mungu kama inavyofunuliwa katika Biblia

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine