Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 15/5 uku. 13
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Musalaba
    Amuka!—2017
  • Ulijua?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Je, Ulijua?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mutu Mwenye Hana Kosa Anateseka Kwenye Muti
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 15/5 uku. 13

MAULIZO YA WASOMAJI WETU

Je, Waisraeli waliwatundika wahalifu kwenye miti?

Waroma waliwafunga kwa kamba ao kuwapigilia misumari kwenye muti. Wahalifu hao waliendelea kuishi kwenye muti kwa muda wa siku fulani, kisha walikufia hapo kwa sababu ya maumivu, kiu, njaa, mvua, jua, na hali zingine. Kwa Waroma, malipizi hayo yalikuwa ya haya na yalipewa watu waliokuwa wahalifu sana.

Mambo yalitendeka namna gani katika taifa la Israeli? Je, Waisraeli walitundika wahalifu kwenye miti? Sheria ya Musa ilisema hivi: ‘Ikiwa mutu atakuwa na zambi inayostahili hukumu ya kifo, naye ameuawa, nawe umemutundika juu ya muti, maiti yake isibaki usiku kucha juu ya muti; bali kwa vyovyote utamuzika siku hiyo.’ (Kum. 21:22, 23) Kwa hiyo, inaonekana wazi kwamba wakati Maandiko ya Kiebrania yalikuwa yakiandikwa, mutu aliyestahili kifo aliuawa kwanza kisha mwili wake ulitundikwa kwenye muti.

Andiko la Walawi 20:2 linasema hivi: ‘Mutu yeyote wa wana wa Israeli, na mukaaji mugeni yeyote anayekaa akiwa mugeni katika Israeli, anayemupa Moleki yeyote kati ya uzao wake, lazima auawe. Watu wa inchi watamupiga kwa mawe mupaka afe.’ Wale waliokuwa na ‘roho ya kuwasiliana na pepo’ walipaswa kuuawa pia. Namna gani? ‘Walipigwa kwa mawe.’​—Law. 20:27.

Katika Kumbukumbu la Torati 22:23, 24, tunasoma hivi: ‘Ikiwa kulikuwa na musichana bikira aliyechumbiwa na mwanamume, na mwanamume fulani akamukuta jijini na kulala naye, mutawatoa wote wawili mupaka kwenye lango la jiji na kuwapiga kwa mawe, nao lazima wafe, yule musichana kwa sababu hakupiga mayowe jijini, na yule mwanamume kwa sababu alimufezehesha muke wa mwenzake. Kwa hiyo lazima utaondolea mbali lililo ovu kutoka katikati yako.’ Kwa hiyo, kwa Waisraeli, kupiga mutu mawe ilikuwa njia kubwa ya kuua wahalifu.a

Inaonekana wazi kwamba wakati Maandiko ya Kiebrania yalikuwa yakiandikwa, mutu aliyestahili kifo aliuawa kwanza kisha mwili wake ulitundikwa kwenye muti

Kumbukumbu la Torati 21:23 inasema kama “mutu aliyetundikwa ni kitu kilicholaaniwa na Mungu.” Kwa hiyo, kuacha maiti ya muhalifu kwenye muti kuliwatolea wengine onyo.

a Watu wengi walio na elimu ya Biblia wanakubali kwamba chini ya Sheria, muhalifu aliuawa mbele atundikwe kwenye muti. Hata hivyo, inaonekana kwamba wakati wa mitume, Wayahudi waliwatundika wahalifu fulani kwenye muti wakiwa wangali wazima nao walifia hapo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine