Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/2 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Habari Njema Yenye Iko mu Biblia Inatoka Kabisa kwa Mungu?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Biblia: Kitabu Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Biblia?
    Uko na mawazo gani juu ya Biblia?
  • Biblia Ni Kitabu Kilichotoka kwa Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/2 uku. 16
Kitabu cha kukunjwa cha zamani cha Biblia

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Kweli Biblia ni Neno la Mungu?

Ungetazamia Neno la Mungu liwe tofauti na vitabu vingine, na Biblia ni kitabu kilicho tofauti. Mamiliare ya Biblia zimechapishwa katika mamia ya luga. Hekima ya Biblia ina uwezo wa kubadilisha watu wawe na tabia nzuri.​—Soma 1 Wathesalonike 2:13; 2 Timotheo 3:16.

Tunajua kwamba Biblia ni Neno la Mungu kwa sababu inatabiri bila makosa mambo ya wakati unaokuja. Hakuna mutu anayeweza kufanya hivyo kwa uwezo wake mwenyewe. Kwa mufano, fikiria kitabu cha Isaya. Kopi moja ya kitabu hicho iliyoandikwa miaka zaidi ya mia moja mbele ya kuzaliwa kwa Yesu ilipatikana katika pango karibu na Bahari ya Chumvi. Kopi hiyo inasema kwamba muji wa Babiloni ungebaki bila kukaliwa. Jambo hilo lilitimia miaka mingi kisha utumishi wa Yesu duniani.​—Soma Isaya 13:19, 20; 2 Petro 1:20, 21.

Biblia iliandikwa namna gani?

Biblia iliandikwa katika kipindi cha miaka 1 600 hivi. Ni watu karibu 40 walioandika Biblia, na walizungumuzia kichwa kimoja cha habari bila kupingana. Hilo liliwezekana namna gani? Mungu aliongoza mambo waliyoandika.​—Soma 2 Samweli 23:2.

Wakati fulani Mungu alizungumuza na waandikaji hao kupitia malaika, maono, ao ndoto. Mara nyingi, Mungu alitia mawazo yake katika akili ya muandikaji na kumuruhusu achague maneno ya kutumia ili kueleza ujumbe wa Mungu.​—Soma Ufunuo 1:1; 21:3-5.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 2 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kuchukua kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine