Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • T-30 uku. 1-4
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Biblia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Biblia?
  • Uko na mawazo gani juu ya Biblia?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
    Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
  • Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
    Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Kuko Siku Mateso Itaisha?
    Kuko Siku Mateso Itaisha?
Ona Habari Zaidi
Uko na mawazo gani juu ya Biblia?
T-30 uku. 1-4

Uko na Mawazo Gani Juu ya Biblia

Unawaza ni . . .

  • kitabu chenye kuwa na hekima ya watu?

  • kitabu cha hadisi za kuwazia-wazia tu?

  • ao Neno la Mungu?

ONA JIBU LA BIBLIA

“Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu.”​—2 Timoteo 3:16, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?

Utapata majibu ya muzuri juu ya maulizo ya maana mu maisha.​—Mezali 2:1-5.

Utapata mashauri ya muzuri yenye itakuongoza mu maisha yako ya kila siku.​—Zaburi 119:105.

Utakuwa na tumaini la muzuri juu ya wakati wenye kuja.​—Waroma 15:4.

Mwanaume na mwanamuke wanasoma Biblia; familia yenye furaha inapitisha wakati pamoja kwa furaha

TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?

Ndiyo. Kuko sababu tatu hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:

  • Inapatana kwa njia yenye kushangaza. Biblia iliandikwa na watu 40 hivi, katika kipindi cha miaka zaidi ya 1600. Wengi kati ya wale wenye waliandika Biblia hawakuonana hata siku moja. Lakini, Biblia yote inapatana, na inazungumuzia wazo moja kubwa!

  • Inazungumuzia mambo bila kuficha. Mara mingi, waandikaji wa ulimwengu hawaandike juu ya kushindwa kwa inchi zao. Lakini, waandikaji wa Biblia hawakuficha kitu; waliandika juu ya makosa yao na hata kushindwa kwa inchi yao.​—2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16; Zaburi 51:1-4.

  • Unabii wa Biblia unatimiaka sikuzote. Biblia ilisema juu ya kuharibiwa kwa muji wa zamani wa Babiloni miaka 200 hivi mbele ule muji uharibiwe. (Isaya 13:17-22) Biblia ilionyesha namna Babiloni ingeanguka, na hata jina la mutu mwenye angekamata ule muji!​—Isaya 45:1-3.

    Unabii mwingine mbalimbali wa Biblia ulitimia hata mu mambo ya kidogo-kidogo. Hilo haliwezi kutushangaza juu Biblia ni Neno la Mungu.​—2 Petro 1:21.

FIKIRIA ULIZO HILI

Baba, mama, mutoto mwanaume na mutoto mwanamuke

Namna gani Neno la Mungu linaweza kukusaidia ukuwe na maisha ya muzuri?

Biblia inajibu ulizo hilo mu ISAYA 48:17, 18 na 2 TIMOTEO 3:16, 17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine