Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • T-34 uku. 1-4
  • Kuko Siku Mateso Itaisha?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuko Siku Mateso Itaisha?
  • Kuko Siku Mateso Itaisha?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
    Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
  • Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
    Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
    Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
Ona Habari Zaidi
Kuko Siku Mateso Itaisha?
T-34 uku. 1-4

Kuko Siku Mateso Itaisha?

Unawaza . . .

  • ndiyo?

  • hapana?

  • ao pengine?

ONA JIBU LA BIBLIA

“Mungu . . . atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.” ​—Ufunuo 21:3, 4, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?

Utaamini kabisa kama haiko Mungu njo mwenye anatuleteaka mateso.​—Yakobo 1:13.

Utapata kitulizo wakati unajua kama Mungu anajisikia mubaya wakati tunateseka.​—Zekaria 2:8.

Utakuwa na tumaini kama mateso yote itaisha.​—Zaburi 37:9-11.

Mwanaume mwenye iko anasoma Biblia anaona mu akili mwisho wa mateso na mambo ya mubaya katika dunia

TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?

Ndiyo. Kuko sababu mbili hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:

  • Mungu anachukia wakati watu wanateseka na kutendewa mubaya. Waza namna Yehova Mungu alijisikia wakati watu wake walitendewa mubaya sana zamani. Biblia inasema kama alihuzunika juu “walikuwa wanawatendea mubaya.”​—Waamuzi 2:18, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

    Mungu anachukia sana wale wenye wanatesa wengine. Kwa mufano, Biblia inasema kama anachukia “mikono yenye kumwanga damu yenye haina kosa.”​—Mezali 6:16, 17.

  • Mungu anahangaikia kila mutu. Kila mutu anajua “pigo lake [ao, mateso yake] mwenyewe na maumivu yake mwenyewe,” lakini Yehova naye anaijua!​—2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

    Hivi karibuni, Yehova atatumia Ufalme wake ili kumaliza mateso ya kila mutu. (Matayo 6:9, 10) Mbele wakati huo ufike, anafariji kwa upendo watu wenye wanamutafuta kwa moyo wote.​—Matendo 17:27; 2 Wakorinto 1:3, 4.

FIKIRIA ULIZO HILI

Wanamuke wawili wanajifunza Biblia

Juu ya nini Mungu anaacha watu wateseke?

Biblia inajibu ulizo hilo mu WAROMA 5:12 na 2 PETRO 3:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine