Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • T-36 uku. 1-4
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
    Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
  • Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
    Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
  • Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
    Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
  • Kuko Siku Mateso Itaisha?
    Kuko Siku Mateso Itaisha?
Ona Habari Zaidi
Ufalme wa Mungu Ni Nini?
T-36 uku. 1-4
Watu wa mahali mbalimbali wako wanasali Ufalme wa Mungu ukuje

Ufalme wa Mungu ni nini?

Unawaza ni . . .

  • jambo fulani lenye kuwa mu moyo wako?

  • maneno ya mufano?

  • ao serikali (guvernema) yenye iko mbinguni?

ONA JIBU LA BIBLIA

“Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme wenye hautaharibiwa hata siku moja.”​—Danieli 2:44, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

“Tumepewa mwana na serikali itakaa juu ya bega lake.”​—Isaya 9:6; maelezo ya chini.

UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?

  • Kutakuwa serikali ya haki yenye inaweza kukuletea faida.​—Isaya 48:17, 18.

  • Utakuwa na maisha ya furaha na afya kamilifu mu dunia mupya.​—Ufunuo 21:3, 4.

Watu wanatengeneza mabustani na wanafurahia maisha mu paradiso ku dunia katika utawala wa Ufalme wa Mungu

TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?

Ndiyo. Kuko sababu mbili hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:

  • Yesu alionyesha mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanya. Yesu alifundisha wanafunzi wake waombe Ufalme wa Mungu ukuje na mapenzi ya Mungu ifanyike hapa ku dunia. (Matayo 6:9, 10) Yesu alionyesha namna sala hiyo itajibiwa.

    Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, alikulisha watu wenye njaa, aliponyesha wagonjwa, na alifufua watu wenye walikuwa wamekufa! (Matayo 15:29-38; Yohana 11:38-44) Juu Yesu njo angekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu, alionyesha mbele ya wakati mambo ya muzuri yenye Ufalme huo utafanyia watu wenye utatawala.​—Ufunuo 11:15.

  • Leo, mambo yenye kufanyika mu dunia inaonyesha kama Ufalme wa Mungu uko karibu kuja. Yesu alisema kama mbele Ufalme ulete amani ku dunia, ku dunia kungekuwa vita, njaa, na matetemeko ya inchi.​—Matayo 24:3, 7.

    Leo, tuko tunaona ile mambo yote. Kwa hiyo, tunaweza kuamini kabisa kama, hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utamaliza ile magumu yote.

FIKIRIA ULIZO HILI

Dunia ya muzuri sana yenye kutawaliwa na Ufalme wa Mungu

Maisha itakuwa namna gani wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia?

Biblia inajibu ulizo hilo mu ZABURI 37:29 na ISAYA 65:21-23.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine