Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • T-35 uku. 1-4
  • Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
  • Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
    Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
  • Kuko Siku Mateso Itaisha?
    Kuko Siku Mateso Itaisha?
  • Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
    Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Ufalme wa Mungu Ni Nini?
Ona Habari Zaidi
Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
T-35 uku. 1-4
Wazazi wanaangalia picha ya mutoto wao mwanamuke mwenye amekufa

Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?

Unaweza kusema . . .

  • ndiyo?

  • hapana?

  • ao pengine?

ONA JIBU LA BIBLIA

“Kutakuwa ufufuo.”​—Matendo 24:15, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?

Utapata faraja ao kitulizo wakati mutu mwenye unapenda anakufa.​—2 Wakorinto 1:3, 4.

Hautaogopa tena kifo.​—Waebrania 2:15.

Utakuwa na tumaini la kweli kama utakuwa tena pamoja na wapendwa wako wenye wamekufa.​—Yohana 5:28, 29.

Familia moja na mujane mumoja wanapata faraja kupitia tumaini la ufufuo

TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?

Ndiyo. Kuko sababu tatu hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:

  • Mungu njo aliumba uzima. Biblia inamuita Yehova Mungu “chemchemi ya uzima.” (Zaburi 36:9; Matendo 17:24, 25) Yeye njo alipatia viumbe vyote uzima. Kwa hiyo, iko na nguvu kabisa ya kurudishia tena uzima mutu mwenye amekufa.

  • Zamani, Mungu alifufua watu wenye walikuwa wamekufa. Biblia inazungumuzia watu munane wenye walifufuliwa na kuendelea kuishi hapa ku dunia. Kulikuwa vijana, wazee, wanaume na wanamuke. Wamoja kati yao walifufuliwa wakati kidogo tu kisha kufa, lakini mumoja alifufuliwa kisha kumaliza siku ine mu kaburi!​—Yohana 11:39-44.

  • Mungu anapenda sana kufufua tena watu wenye wamekufa. Yehova anachukia kifo; anaona kifo kuwa adui. (1 Wakorinto 15:26) Anapenda kabisa kutosha adui huyo, na atafanya vile kupitia ufufuo. Na anapenda sana kufufua watu wenye anachunga mu akili yake, na anapenda kuwaona wanaishi tena hapa ku dunia.​—Yobu 14:14, 15.

FIKIRIA ULIZO HILI

Mutoto mwanaume mwenye anakomaa na kuwa muzee

Juu ya nini watu wanazeekaka na kufa?

Biblia inajibu ulizo hilo mu MWANZO 3:17-19 na WAROMA 5:12.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine