Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • T-33 uku. 1-4
  • Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
  • Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
    Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
    Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
  • Kuko Siku Mateso Itaisha?
    Kuko Siku Mateso Itaisha?
Ona Habari Zaidi
Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
T-33 uku. 1-4

Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?

Unawaza ni . . .

  • Mungu?

  • wanadamu?

  • ao mutu mwingine?

ONA JIBU LA BIBLIA

“Ulimwengu wote unatawaliwa na yule muovu.”​—1 Yohana 5:19.

“Mwana wa Mungu alikuja . . . kuiharibu kazi ya Ibilisi [ao, Shetani].”​—1 Yohana 3:8, Biblia Habari Njema.

UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?

Utajua muzuri juu ya nini kuko magumu mu dunia.​—Ufunuo 12:12.

Utakuwa na sababu ya kuamini kama dunia hii itakuwa muzuri.​—1 Yohana 2:17.

Shetani anatawala mambo ya politike, ya jeshi, na ya dini ya ulimwengu huu na watu

TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?

Ndiyo. Kuko sababu tatu hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:

  • Utawala wa Shetani utaharibiwa. Yehova ameamua kabisa kumaliza utawala wa Shetani juu ya wanadamu. Ametoa ahadi (malako) kama ‘atamuharibu . . . Ibilisi,’ na kumaliza mambo yote ya mubaya yenye ameleta.​—Waebrania 2:14, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

  • Mungu amemuchagua Yesu Kristo ili akuwe mutawala wa dunia. Yesu haiko hata kidogo kama mutawala wa dunia hii mwenye kuwa mukali na mwenye kutafuta faida zake mwenyewe. Juu ya utawala wa Yesu, Mungu ametoa ahadi hii: “Atamusikilia huruma mutu wa hali ya chini na maskini . . . Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”​—Zaburi 72:13, 14.

  • Mungu hawezi kusema uongo. Biblia inasema waziwazi kama “haiwezekane Mungu aseme uongo.” (Waebrania 6:18) Kama Yehova anaahidi kufanya jambo fulani, ni kama vile jambo hilo limefanyika! (Isaya 55:10, 11) “Mutawala wa ulimwengu huu atatupwa inje.”​—Yohana 12:31.

FIKIRIA ULIZO HILI

Watu wa familia yenye furaha wanapitisha wakati pamoja

Dunia itakuwa namna gani kisha mutawala wake kutoshwa?

Biblia inajibu ulizo hilo mu ZABURI 37:10, 11 na UFUNUO 21:3, 4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine