Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/7 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/7 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Sababu gani watu wanafanya mambo mabaya?

Yesu anakataa falme zote za dunia zenye Ibilisi anamutolea

NI nani alijaribu kumuchochea yesu afanye mambo mabaya?—Mathayo 4:8-10

Kwa kawaida, watu wanapenda kuwa wenye amani, wenye kusema kweli na kutendeana kwa wema. Basi, sababu gani tunaona mara nyingi matendo ya kuumizana ao kuuana, ukosefu wa haki, na kutendeana bila huruma? Mara nyingi, vyombo vya habari vinatoa habari zenye kuogopesha. Kuna mutu fulani mwenye anajaribu kuchochea watu wafanye mambo mabaya?—Soma 1 Yohana 5:19.

Wakati Mungu aliumba wanadamu, walikuwa na mwelekeo wa kutenda mambo mabaya? Hapana, Yehova Mungu aliumba wanadamu kwa mufano wake; walikuwa na mwelekeo wa kuonyesha upendo kama Mungu. (Mwanzo 1:27; Ayubu 34:10) Lakini Mungu alipatia pia wanadamu uhuru wa kuchagua. Wakati wazazi wetu wa kwanza walichagua kufanya mambo mabaya, walikataa kufuata mufano wa Mungu na wakakuwa watu wasiokamilika. Tuliriti kutoka kwao mwelekeo wa kufanya zambi.—Soma Kumbukumbu la Torati 32:4, 5.

Watu wataendelea kufanya mambo mabaya milele?

Mungu anapenda tupiganishe mwelekeo wetu wa kufanya mambo mabaya. (Methali 27: 11) Kwa hiyo, anatufundisha namna ya kuepuka kufanya mambo mabaya na namna ya kupata furaha ya kweli. Lakini, leo hatuwezi kuonyesha kabisa-kabisa upendo kama Mungu.—Soma Zaburi 32:8.

Hata kama mambo mabaya yanaongezeka leo, Mungu anayaacha yaendelee kwa muda ili watu wote waone matokeo mabaya ya mambo hayo. (2 Petro 3:7-9) Lakini hivi karibuni, dunia itajaa watu wenye furaha na wenye kumutii Mungu.—Soma Zaburi 37:9-11.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 3 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza pia kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine