Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 2 uku. 10-12
  • Kutoka Katika Utumwa—Wakati wa Zamani na Wakati Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kutoka Katika Utumwa—Wakati wa Zamani na Wakati Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • VITA INAFANYA UTUMWA UKUWE BIASHARA KUBWA
  • KUTOKA KATIKA UTUMWA
  • KUMALIZWA KABISA KWA UTUMWA
  • ‘Tumutumikie Yehova Kama Watumwa’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 2 uku. 10-12
Biashara ya watumwa kati ya Afrika na Amerika

Biashara ya watumwa kati ya Afrika na Amerika ilikuwa biashara yenye kuleta faida sana

Kutoka Katika Utumwa Wakati wa Zamani na Wakati Wetu

Wakati Blessinga alifika Ulaya alikuwa ameahidiwa kufanya kazi ya kutengeneza nywele. Lakini, kisha kupigwa mara kwa mara kwa siku kumi, na pia kuogopeshwa kwamba watu wa familia yake wenye walibaki nyumbani wangetendewa mubaya, alilazimika kutumika kama kahaba.

Muchoro wa watumwa wenye walikamatwa katika Misri ya zamani

Muchoro wa watumwa wenye walikamatwa katika Misri ya zamani

Blessing alitazamiwa kupata kila siku euro kati 200 na 300 ili kulipa deni lenye mwanamuke mwenye kusimamia nyumba yao ya ukahaba alikadiria kuwa zaidi ya euro 40000.b Blessing anasema hivi: “Mara nyingi niliwaza kutoroka, lakini niliogopa jambo lenye wangetendea familia yangu. Sikukuwa na jambo lingine la kufanya.” Habari ya Blessing inaonyesha hali ya watu milioni 4 wenye wamefanywa kuwa watumwa katika biashara ya ngono katika dunia.

Kumepita karibu miaka 4000 tangu kijana Yosefu aliuzishwa na ndugu zake. Alifikia kutumika katika nyumba ya mutu fulani mwenye kujulikana katika Misri. Tofauti na Blessing, mwanzoni hakutendewa mubaya na mukubwa wake. Lakini wakati alikataa kufanya uasherati na bibi ya mukubwa wake, alishitakiwa bila haki kuwa alijaribu kumulala kinguvu. Alitupwa katika gereza na akatiwa katika vyuma.​—Mwanzo 39:1-20; Zaburi 105:17, 18.

Yosefu alikuwa mutumwa wa wakati wa zamani; Blessing ni mutumwa wa wakati wetu. Lakini wote waliteseka kwa sababu ya biashara ya watu ya tangu zamani; wenye kufanya biashara hiyo wanaona watu kama vitu, wanahangaikia tu kupata feza.

VITA INAFANYA UTUMWA UKUWE BIASHARA KUBWA

Vita ilionekana kuwa njia ya mwepesi zaidi ya mataifa kupata watumwa. Inasemekana kuwa mufalme wa Misri Thutmose wa 3 alileta wafungwa 90000 kisha kupigana vita katika inchi ya Kanaani. Wamisri waliwafanya kuwa watumwa katika kazi ya kutafuta majiwe ya bei katika udongo, kujenga mahekalu, na kuchimba mifereji.

Katika Utawala wa Roma, vita ilisaidia pia kupata watumwa wengi, na wakati fulani kuwa na lazima ya watumwa kulifanya wapigane vita. Inakadiriwa kwamba katika mwaka wa 30 hivi, karibu nusu ya wakaaji wa muji wa Roma walikuwa watumwa. Watumwa wengi katika Misri na Roma walitumikishwa mubaya. Katika Roma, tumaini la kuishi la watumwa wenye walifanya kazi ya kutafuta majiwe ya bei katika udongo, lilikuwa la miaka karibu 30 tu.

Kadiri wakati uliendelea kupita, utumwa haukufikia kuwa muzuri. Kuanzia miaka ya 1500 mupaka miaka ya 1800, biashara ya watumwa kati ya Afrika na Amerika ilikuwa moja kati ya biashara yenye kuleta faida sana katika dunia. Ripoti moja ya shirika la UNESCO inaonyesha kwamba ‘inakadiriwa kuwa wanaume, wanawake, na watoto kati ya milioni 25 na milioni 30, walikamatwa kinguvu na kuuzishwa.’ Inasemekana kuwa mamia ya maelfu kati ya watu hao walikufa wakati walikuwa wanavuka bahari ya Atlantiki. Olaudah Equiano, mutumwa mwenye hakukufa katika safari hiyo, anasema hivi: “Vilio vya wanawake na sauti za watu wenye kukaribia kufa viliogopesha sana.”

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba utumwa haiko jambo la mubaya lenye lilitokea tu zamani. Kulingana na Shirika la Wafanyakazi Ulimwenguni, mupaka leo wanaume, wanawake, na watoto milioni 21 hivi, wanatumika kama watumwa, wanalazimishwa kufanya kazi lakini wanalipwa feza kidogo ao hawalipwe hata kidogo. Watumwa wa wakati wetu wanafanya kazi ya kutafuta majiwe ya bei katika udongo, wanatumika katika izine za kutengeneza nguo, za kutengeneza matofali, katika nyumba za makahaba, na katika nyumba za watu. Hata kama haikubaliwe na sheria, inaonekana kuwa aina hiyo ya utumwa inaendelea kuongezeka.

Watoto wanatumika kama watumwa katika uzine ya kutengeneza matofali

Mamilioni ya watu wangali wanatumika katika utumwa

KUTOKA KATIKA UTUMWA

Kwa sababu ya kutendewa mubaya, watumwa wengi wamepigana ili wapate uhuru. Katika mwaka wa 73 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, mupiganaji Spartacus na watumwa 100000 hivi walijaribu kupinga Roma, lakini hawakuweza. Karibu na mwaka wa 1800 watumwa katika kisiwa cha Karibea cha Hispaniola walipinga wakubwa wao. Mateso yenye watumwa hao walipata kwa sababu ya kutendewa mubaya katika mashamba ya miwa ilitokeza vita ya wenyewe kwa wenyewe yenye ilifanya miaka 13 na hilo liliongoza kuundwa kwa inchi huru ya Haiti katika mwaka wa 1804.

Kutoka kwa Waisraeli Misri ndiyo uhuru mukubwa wenye watumwa wamekwisha kupata katika historia. Inawezekana watu milioni 3, ni kusema, taifa lote, walikombolewa kutoka katika utumwa katika Misri. Kwa kweli, walistahili uhuru wenye walipata. Biblia inaonyesha kwamba maisha yao katika Misri ilikuwa katika “kila namna ya utumwa . . . chini ya uonevu.” (Kutoka 1:11-14) Farao mumoja alianzisha hata mupango wa kuua watoto wadogo ili kuzuia hesabu ya Waisraeli isiongezeke.​—Kutoka 1:8-22.

Namna Waisraeli walitoka katika utumwa katika Misri ilikuwa ya pekee kwa sababu Mungu mwenyewe ndiye alitenda. Mungu aliambia Musa hivi: “Nayajua vizuri maumivu waliyo nayo. Nami ninashuka ili kuwakomboa.” (Kutoka 3:7, 8) Mupaka leo, kila mahali Wayahudi wanasherehekea Pasaka kila mwaka ili kukumbuka tukio hilo.​—Kutoka 12:14.

KUMALIZWA KABISA KWA UTUMWA

Biblia inasema kwamba kwa Yehova Mungu wetu “hakuna ukosefu wowote wa uadilifu,” na inatuhakikishia kwamba hajabadilika. (2 Mambo ya Nyakati 19:7; Malaki 3:6) Mungu alituma Yesu ili “kuhubiri kuachiliwa huru kwa mateka [ao, watumwa] . . . , kuacha waliopondeka waende zao wakiwa wameachiliwa huru.” (Luka 4:18) Hilo lilimaanisha kukombolewa kwa wote wenye kuwa katika utumwa wa kimwili? Inawezekana hapana. Yesu alitumwa ili kukomboa watu kutoka katika utumwa wa zambi na kifo. Alifikia kusema hivi: “Kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Hata leo, kweli yenye Yesu alifundisha inakomboa watu katika njia nyingi.—Ona kisanduku “Kutoka Katika Aina Ingine ya Utumwa.”

Kwa kweli, Mungu alisaidia Yosefu na Blessing kutoka katika utumwa katika njia tofauti. Unaweza kupata habari nzuri ya Yosefu katika sura ya 39 mupaka 41 ya kitabu cha Mwanzo. Namna Blessing alitafuta uhuru ilikuwa ya ajabu pia.

Kisha kufukuzwa katika inchi moja ya Ulaya, Blessing alienda Hispania. Huko alikutana na Mashahidi wa Yehova na akaanza kujifunza Biblia pamoja nao. Kwa sababu alitaka kabisa kubadilisha maisha yake, alitafuta kazi yenye kutegemeka na akasadikisha mwanamuke mwenye alikuwa anamusimamia zamani apunguze deni lenye alipaswa kulipa kila mwezi. Siku moja, mwanamuke huyo aliita Blessing kwenye telefone. Alitaka kufuta deni lote la Blessing na kumuomba musamaha. Sababu gani alifanya hivyo? Yeye pia alikuwa ameanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova! Blessing anasema hivi: “Kweli inakuweka huru katika njia za ajabu.”

Yehova Mungu aliumia kwa sababu ya mambo mabaya yenye watumwa Waisraeli walikuwa wanatendewa katika Misri; bila shaka, leo anajisikia hivyo pia wakati anaona matendo kama hayo ya ukosefu wa haki. Kwa kweli, itaomba mabadiliko makubwa katika ulimwengu ili kumaliza aina yote ya utumwa. Lakini Mungu anaahidi kuleta mabadiliko hayo. ‘Kulingana na ahadi yake tunangojea mbingu mupya na dunia mupya, na humo uadilifu utakaa.’—2 Petro 3:13.

a Jina limebadilishwa.

b Wakati huo euro ilikuwa inalingana karibu na dola ya Amerika.

Kutoka Katika Aina Ingine ya Utumwa

Alonso na bibi yake

Alonso alikuwa katika aina ingine ya utumwa. Wakati alikuwa angali kijana alifikia kuwa mutumwa wa kutumia kokeini na heroini. Alonso anasema hivi: “Ili kupata feza za kuuza dawa za kulewesha, nilianza kuiba na nikaanza kufanya biashara ya dawa za kulewesha. Hata kama nilienda mara ine katika vituo vya kusaidia watu waache kutumia dawa za kulewesha, sikuweza kuacha tabia hiyo. Mwishowe polisi walinikamata na nikapitisha miaka ine katika gereza.”

Kisha kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha kwa miaka 30, Alonso alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Ujumbe wa Biblia uligusa moyo wake, na ukamufanya aazimie kuacha tabia hiyo. Anakumbuka hivi: “Kisha kuwa mutumwa kwa miaka mingi sana, ilikuwa vigumu kuacha. Lakini Yehova Mungu amenisaidia kushinda vita hiyo.”—Zaburi 55:22.

Alonso anasema hivi: “Bibi yangu anafurahi kuona namna nimebadilika sana. Ninamushukuru Yehova kwa kunisaidia kuacha tabia yenye ilikuwa inaharibu mwili wangu. Bila musaada wake, singeweza kutoka katika utumwa huo. Ao pengine, ningekuwa nimekufa.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine