Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 2 uku. 16
  • Biblia Inasema Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia Inasema Nini?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tunaishi katika “siku za mwisho”?
  • Wakati wenye kuja wa wanadamu utakuwa namna gani?
  • Mwisho wa Dunia Uko Karibu?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Tunaishi Kweli Katika “Siku za Mwisho”?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Mwisho Utafika Wakati Gani? Mambo Yesu Alisema
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Mwisho wa Dunia​—Je, Ni Jambo Lenye Kuogopesha, Kuvutia, ao Kuvunja Moyo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 2 uku. 16
Watu wenye kukomaa na watoto wanafurahia maisha katika Paradiso

Watu wenye wataokoka siku za mwisho wataingia katika dunia paradiso

Biblia Inasema Nini?

Tunaishi katika “siku za mwisho”?

Unaweza kujibu nini?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Pengine

Mambo Biblia inasema

‘Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushugulika nazo.’ (2 Timotheo 3:1) Unabii wa Biblia, wenye kushuhudiwa na mambo yenye kutokea leo, unaonyesha kwamba tunaishi katika “siku za mwisho.”

Biblia inatufundisha tena nini?

  • Katika siku za mwisho kungekuwa vita, njaa, matetemeko ya inchi, na magonjwa hatari yenye kuenea.—Mathayo 24:3, 7; Luka 21:11.

  • Katika siku za mwisho, hali ya kiroho na mwenendo wa watu ungekuwa mubaya sana.—2 Timotheo 3:2-5.

Wakati wenye kuja wa wanadamu utakuwa namna gani?

Watu fulani wanaamini . . .kama siku za mwisho zitaisha kwa kuharibiwa kwa dunia na watu wote, lakini watu wengine wanatumaini kwamba hali zitabadilika na kuwa muzuri zaidi. Wewe unawaza nini?

Mambo Biblia inasema

“Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.” —Zaburi 37:29.

Biblia inatufundisha tena nini?

  • Siku za mwisho zitaisha kwa kuondolewa kwa ubaya wote.—1 Yohana 2:17.

  • Dunia itageuzwa kuwa paradiso. —Isaya 35:1, 6.

Ili kujua mengi zaidi juu ya “siku za mwisho,” ona sura ya 9 ya kitabu hiki, chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova

Kinapatikana pia kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine