Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 5 uku. 5
  • Uko na Malaika Mulinzi?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uko na Malaika Mulinzi?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna Gani Malaika Wanaweza Kukusaidia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Iga Mufano wa Malaika Waaminifu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 5 uku. 5

HABARI KUBWA | MALAIKA​—WAKO KABISA? SABABU GANI TUFIKIRIE JAMBO HILO?

Uko na Malaika Mulinzi?

Biblia haifundishe kama kila mutu iko na malaika mulinzi. Ni kweli kwamba siku moja Yesu alisema hivi: ‘Angalieni musimuzarau mumoja wa hawa wadogo [wanafunzi wa Kristo], kwa maana ninawaambia ninyi kwamba malaika zao mbinguni sikuzote huuona uso wa Baba yangu aliye mbinguni.’ (Mathayo 18:10) Hata hivyo, kuliko kusema kwamba kila mutu iko na malaika mulinzi, Yesu alikuwa akisema tu kwamba malaika wanapendezwa sana na kila mumoja wa wanafunzi wake. Kwa hiyo, waabudu wa kweli hawajiingize katika hatari kwa kufikiri kwamba malaika wa Mungu watawalinda.

Hilo linamaanisha kama malaika hawasaidie wanadamu? Hapana. (Zaburi 91:11) Watu fulani wanaamini kabisa kwamba Mungu amewatumia malaika ili kuwalinda na kuwaongoza. Kenneth, mwenye kutajwa katika habari ya kwanza, anajisikia hivyo pia. Hata kama hatuwezi kuhakikisha kabisa jambo hilo, pengine inaweza kuwa kweli. Mara nyingi, Mashahidi wa Yehova wanajionea ushuhuda wa musaada wa malaika wakati wanafanya kazi yao ya kuhubiri. Lakini, kwa sababu hatuwezi kuona malaika, hatuwezi kusema ni kwa kadiri gani Mungu anawatumia ili kusaidia watu katika njia mbalimbali. Hata hivyo, hakuna ubaya wowote kumushukuru Mweza-Yote kwa musaada wowote wenye anaweza kutupatia.​—Wakolosai 3:15; Yakobo 1:17, 18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine