HABARI YA KUJIFUNZA YA 19
WIMBO 6 Mbingu Zinatangaza Utukufu wa Mungu
Iga Mufano wa Malaika Waaminifu
“Mumusifu Yehova, ninyi malaika wake wote.”—ZB. 103:20.
WAZO KUBWA
Mambo yenye mufano wa malaika waaminifu unaweza kutufundisha.
1-2. (a) Tuko tofauti na malaika mu mambo gani? (b) Tunafanana na malaika mu mambo gani?
WAKATI Yehova alikuvuta katika kweli, alikualika mu familia yake ya waabudu mbalimbali wenye upendo, kati yao kuko mamilioni ya malaika waaminifu. (Da. 7:9, 10) Wakati tunafikiria namna malaika wanakuwaka, tunaona namna wako tofauti na siye. Kwa mufano, waliumbwa miaka mingi sana mbele wanadamu waumbwe. (Yob. 38:4, 7) Wako na nguvu sana kuliko siye. Ni watakatifu na wenye haki sana mu njia yenye wanadamu wenye hawakamilike hawawezi kufikia.—Lu. 9:26.
2 Lakini, hata kama tuko tofauti, tunafanana na malaika mu njia za mingi. Kwa mufano, kama malaika, tunaweza kuonyesha sifa za Yehova. Kama malaika, siye pia tuko na uhuru wa kuchagua. Kila malaika iko na jina yake na utu wake na kazi yake mu utumishi wa Yehova, na siye ni vile. Na kama malaika, siye pia tuko na uhitaji wa kumuabudu Muumbaji wetu.—1 Pe. 1:12.
3. Mufano wa malaika waaminifu unaweza kutufundisha nini?
3 Juu tunafanana na malaika mu mambo mingi, mufano wao unaweza kututia moyo. Kwa kweli, mufano wao unaweza kutufundisha mambo mingi ya lazima. Mu hii habari, tutajifunza namna tunaweza kuiga unyenyekevu wa malaika waaminifu, upendo wao kwa watu, uvumilivu wao, na namna wanajikaza kusaidia kutaniko iendelee kuwa safi.
MALAIKA NI WANYENYEKEVU
4. (a) Namna gani malaika wanaonyesha unyenyekevu? (b) Juu ya nini malaika ni wanyenyekevu? (Zaburi 89:7)
4 Malaika waaminifu ni wanyenyekevu. Hata kama wako na uzoefu, nguvu, na hekima, wanatii maagizo ya Yehova. (Zb. 103:20) Wakati wanatimiza migao yao, hawajivune juu ya mambo yenye wanafanya ao juu ya nguvu mingi yenye wako nayo. Wanafanya kwa furaha mapenzi ya Mungu hata kama majina yao haijulikane.a (Mwa. 32:24, 29; 2 Fa. 19:35) Wanakatala kupokea utukufu wenye Yehova tu njo anastahili. Juu ya nini malaika ni wanyenyekevu sana? Ni juu wanamupenda Yehova na wanamuheshimia sana.—Soma Zaburi 89:7.
5. Namna gani malaika fulani alionyesha unyenyekevu wakati alikuwa namurekebisha Yohana? (Ona pia picha.)
5 Fikiria hii mufano yenye kuonyesha kama malaika ni wanyenyekevu: Mu mwaka wa 96 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, malaika fulani mwenye hatujue jina yake, alimutolea mutume Yohana maono ya ajabu. (Ufu. 1:1) Yohana alifanya nini kisha kuona ile maono? Alijaribu kuabudu ule malaika. Lakini, palepale ule malaika mushikamanifu alimukataza; alimuambia hivi: “Fanya angalisho! Usifanye vile! Mimi ni mutumwa tu kama wewe na kama ndugu zako . . . Abudu Mungu!” (Ufu. 19:10) Ile ni unyenyekevu kabisa! Ule malaika hakukuwa najitafutia utukufu ao sifa. Palepale aliambia Yohana kama Yehova njo anastahili kuabudiwa. Zaidi ya ile, ule malaika hakumuzarau Yohana. Hata kama ule malaika alikuwa amemutumikia Yehova kwa muda murefu zaidi na alikuwa na nguvu sana kupita Yohana, kwa unyenyekevu alimuita Yohana kuwa mutumwa mwenzake. Na hata kama ule malaika alipaswa kumurekebisha Yohana, hakumufokea ao kumutendea kwa ukali. Lakini, alizungumuza naye kwa upole. Inawezekana ule malaika alielewa kama Yohana alitenda vile juu mambo yenye aliona ilimushangaza sana.
Malaika alionyesha unyenyekevu wakati alizungumuza na Yohana (Ona fungu ya 5)
6. Namna gani tunaweza kuiga unyenyekevu wa malaika?
6 Namna gani tunaweza kuiga unyenyekevu wa malaika? Siye pia tunapaswa kutimiza migao yetu bila kujivuna ao kujionyesha juu ya mambo yenye tuko nafanya. (1 Ko. 4:7) Zaidi ya ile, hatupaswe kujiona kuwa wa maana zaidi kupita wengine juu tumemutumikia Yehova kwa muda murefu zaidi ao juu tuko na mapendeleo ya mingi. Kwa kweli, mapendeleo ikiongezeka, unyenyekevu nao unapaswa kuongezeka. (Lu. 9:48) Kama malaika, tunapenda kutumikia wengine. Hatupendi kujionyesha.
7. Namna gani tunaweza kuonyesha unyenyekevu wakati inaomba turekebishe ao tushaurie mutu?
7 Ni muzuri pia kuonyesha unyenyekevu wakati inaomba turekebishe ao tushaurie mutu mwingine, kwa mufano Mukristo mwenzetu ao mutoto wetu. Wakati fulani inaomba kupatia mutu mashauri mazito. Lakini sawa vile malaika alimurekebisha Yohana kwa upole, tunaweza kupatia mutu mashauri mazito bila kufanya ajisikie mubaya. Kama hatujione kuwa wa maana kupita wengine, tutawatolea mashauri yenye kutegemea Biblia kwa heshima na kwa huruma.—Kol. 4:6.
MALAIKA WANAPENDA WATU
8. (a) Kulingana na Luka 15:10, namna gani malaika wanaonyesha kama wanapenda watu? (b) Malaika wanasaidia namna gani mu kazi ya kuhubiri? (Ona pia picha.)
8 Malaika, hawajitenge na wanadamu. Wanapenda watu. Wanafurahi wakati mutenda-zambi anatubu, ni kusema wakati kondoo wa Yehova mwenye alipotea anarudia ao wakati mutu anabadilisha maisha yake na anakubali kweli. (Soma Luka 15:10.) Pia malaika wanasaidia sana mu kazi ya kuhubiri habari njema. (Ufu. 14:6) Hata kama hawahubirie watu moja kwa moja, wanaweza kuongoza wahubiri kwa mutu mwenye anapenda kujifunza juu ya Yehova. Kusema kweli, hatuwezi kusema kwa uhakika kama malaika njo alituongoza kwa mutu fulani. Yehova anaweza kutumia njia ingine juu ya kutuongoza ao juu ya kusaidia watu wake. Kwa mufano, anaweza kutumia roho yake takatifu. (Mdo. 16:6, 7) Hata vile, anatumiaka sana malaika. Kwa hiyo, wakati tuko nahubiri habari njema, tunaweza kuwa hakika kama malaika wako pale ili kututegemeza.—Ona kisanduku “Sala Zao Zilijibiwa.”b
Bibi na bwana wanamaliza kufanya mahubiri ya mahali pa watu wengi. Wakati wako narudia ku nyumba, ule dada anaona mwanamuke mwenye anaonekana kuwa na huzuni. Ule dada anatambua kama malaika wanaweza kutuongoza kwa wale wenye pengine wako natafuta kumujua Yehova. Ile inamuchochea azungumuze na ule mwanamuke juu ya kumufariji (Ona fungu ya 8)
9. Namna gani tunaweza kuiga upendo wenye malaika wanaonyesha watu?
9 Namna gani tunaweza kuiga upendo wenye malaika wanaonyesha watu? Wakati tunasikia tangazo kama mutu fulani anarudishwa, tunaweza kufurahi sawa malaika. Tunaweza kufanya nguvu yetu yote ili kukaribisha ndugu yetu na kumuhakikishia kama tunamupenda. (Lu. 15:4-7; 2 Ko. 2:6-8) Tunaweza pia kuiga malaika kwa kufanya kazi ya kuhubiri kwa nguvu yetu yote. (Muh. 11:6) Na sawa vile malaika wanatutegemeza wakati tuko nahubiri, siye pia tutafute njia za kutegemeza ndugu na dada zetu mu mahubiri. Kwa mufano, tunaweza kufanya mipango ili kuhubiri na wahubiri wenye hawana uzoefu. Pia tunaweza kutegemeza ndugu na dada wenye kuzeeka ao walemavu juu nao pia wapate nafasi ya kuhubiri.
10. Mufano wa Sara unaweza kutufundisha nini?
10 Sasa tutafanya nini kama hali yetu haituruhusu kufanya mambo yote yenye tungependa kufanya mu kazi ya Yehova? Tunaweza kutafuta njia zingine za kutumika pamoya na malaika. Ona mufano wa Sara,c dada wa India. Kisha kufanya kazi ya upainia kwa miaka 20 hivi, Sara aligonjwa na hakuweza tena kutoka ku kitanda. Ile ilifanya ashuke moyo sana. Lakini kusoma Biblia kwa ukawaida, na musaada wa ndugu na dada vilimusaidia akuwe tena na mawazo ya muzuri. Sara alipaswa kutafuta njia zingine za kuhubiri zenye zilipatana na hali yake. Juu hangeweza kuikala na kuandika barua, alikuwa nahubiri tu kupitia telefone. Kwa hiyo aliita ku telefone watu wenye alipanga kurudilia na wale watu walimuambia kuhusu watu wengine wenye wanaweza kupenda kujifunza Biblia. Matokeo ilikuwa nini? Mu miezi kidogo tu, Sara alikuwa na mafunzo 70, na yeye mwenyewe hangeweza kuongoza ile mafunzo yote. Kwa hiyo, alipatia wengine mu kutaniko mafunzo fulani. Sasa wengi kati ya wale wanafunzi wa Biblia wameanza kuhuzuria mikutano. Bila shaka malaika wanafurahi sana kutumika pamoya na ndugu na dada sawa vile Sara, wenye wanafanya kazi ya kuhubiri kwa uwezo wao wote!
MALAIKA WANAONYESHA SIFA YA UVUMILIVU
11. Malaika waaminifu wanaonyesha namna gani uvumilivu wa ajabu?
11 Malaika waaminifu wanatuwekea mufano muzuri sana kuhusu kuonyesha uvumilivu. Wamevumilia ukosefu wa haki na matendo ya mubaya kwa maelfu ya miaka. Waliona namna Shetani na malaika wengine wenye walikuwa namutumikia Yehova pamoya nao, wanamuacha Yehova. (Mwa. 3:1; 6:1, 2; Yud. 6) Biblia inazungumuzia mufano wa malaika fulani muaminifu mwenye alipambana na upinzani wa roho muchafu mwenye nguvu. (Da. 10:13) Zaidi ya ile, mu historia yote ya wanadamu, malaika wameona kama ni watu kidogo tu njo wanaamua kumutumikia Yehova. Hata vile, malaika waaminifu wanaendelea kumutumikia Yehova kwa furaha na kwa bidii. Wanajua kama kwa wakati wenye kufaa, Mungu atamaliza ukosefu wote wa haki.
12. Nini njo inaweza kutusaidia tuvumilie?
12 Namna gani tunaweza kuiga uvumilivu wa malaika? Kama malaika, tunaweza kuona ukosefu wa haki ao tunaweza kupambana na upinzani. Lakini siye pia tuko hakika kama kwa wakati wenye kufaa, Mungu atatosha mambo ya mubaya. Kwa hiyo, kama malaika waaminifu, ‘hatuache kufanya mema.’ (Gal. 6:9) Na Mungu anatuahidi kama atatusaidia tuendelee kuvumilia. (1 Ko. 10:13) Tunaweza kumuomba Yehova roho yake takatifu, yenye inatusaidia kuonyesha sifa ya uvumilivu na furaha. (Gal. 5:22; Kol. 1:11) Utafanya nini kama unapambana na upinzani? Umutegemee Yehova kwa moyo wote, na usiogope. Sikuzote Yehova atakutegemeza na kukutia nguvu.—Ebr. 13:6.
MALAIKA WANASAIDIA KUTANIKO IENDELEE KUWA SAFI
13. Mu siku za mwisho, malaika wako na mugao gani wa pekee? (Matayo 13:47-49)
13 Mu siku za mwisho, Yehova amepatia malaika mugao wa pekee. (Soma Matayo 13:47-49.) Wakati tunahubiri habari njema, mamilioni ya watu wanapendezwa. Wamoja kati ya wale watu wanakamata hatua ya kuwa Wakristo wa kweli, lakini wengine hawafanye vile. Malaika wamepewa mugao wa “kutenganisha waovu kutoka kati ya wenye haki,” ni kusema wamepewa mugao wa kulinda usafi wa kutaniko. Ile haimaanishe kama kila mutu mwenye anaacha kumutumikia Yehova hatarudiaka tena; na haimaanishe kama mu kutaniko hamutakuwaka matatizo. Lakini, tunaweza kuwa hakika kama malaika wako natumika sana juu ya kusaidia kutaniko iendelee kuwa safi.
14-15. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunahangaikia usafi wa kutaniko sawa malaika? (Ona pia picha.)
14 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunahangaikia usafi wa kutaniko sawa vile malaika? Kwa kufanya nguvu yetu yote ili kutaniko iendelee kuwa na hali ya muzuri ya kiroho na iendelee kuwa safi. Juu tuweze kufanya vile tunapaswa kulinda moyo wetu kwa kuchagua marafiki wazuri na kwa kuepuka mambo yote yenye inaweza kutuchafua. (Zb. 101:3) Tunaweza pia kusaidia waabudu wenzetu waendelee kuwa waaminifu kwa Yehova. Kwa mufano, tunaweza kufanya nini ikiwa tunajua kama Mukristo mwenzetu alifanya zambi nzito? Juu tunamupenda, tunapaswa kumuomba azungumuze na wazee. Kama hafanye vile, tutaambia wazee juu ya ile jambo. Tunapenda Mukristo yeyote mwenye hali yake ya kiroho haiko muzuri, apate musaada bila kukawia!—Yak. 5:14, 15.
15 Jambo ya kuhuzunisha ni kama, Wakristo fulani wenye wamefanya zambi nzito wanapaswa kuondolewa mu kutaniko. Mu hali za vile, ‘tunaacha kushirikiana’ nao.d (1 Ko. 5:9-13) Mupango wa kuondoa watenda-zambi unasaidia kutaniko iendelee kuwa safi. Zaidi ya ile, wakati tunaepuka kushirikiana na wenye waliondolewa mu kutaniko, tunawaonyesha kama tunawapenda. Ile inaweza kuwachochea wapende kumurudilia Yehova. Kama wanafanya vile, tutafurahi pamoya na Yehova na malaika wake.—Lu. 15:7.
Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunajua kama Mukristo mwenzetu amefanya zambi nzito? (Ona fungu ya 14)e
16. Ni mu njia gani unaweza kujikaza kuiga malaika?
16 Ni pendeleo kubwa sana kuona namna Yehova anatupatia nafasi ya kujifunza juu ya malaika na kutumika pamoya nao! Tuige basi sifa zao za muzuri: unyenyekevu wao, upendo wao kwa watu, uvumilivu wao, na namna wanajikaza kulinda hali ya kiroho na usafi wa kutaniko. Kama tunaiga malaika waaminifu, na siye tunaweza kubakia mu familia ya waabudu wa Yehova milele.
WIMBO 123 Tutii Mupango wa Kiteokrasi
a Kuko mamia ya mamilioni ya malaika, lakini Biblia inataya majina ya wawili tu, Mikaeli na Gabrieli.—Da. 12:1; Lu. 1:19.
b Unaweza kupata mifano ingine mu kitabu Musaada wa Kutafuta Habari chini ya kichwa “Yehova Mungu” na kichwa kidogo “Malaika.”
c Majina fulani imebadilishwa.
d Sawa vile Ripoti ya 2 ya Baraza Yenye Kuongoza ya 2024 inaonyesha, kama mutu mwenye aliondolewa mu kutaniko anafika ku mikutano, muhubiri anaweza kutumia zamiri yake yenye kuongozwa na Biblia juu ya kuamua kama atamusalimia ao kumukaribisha.
e MAFASIRIO YA PICHA: Dada anaambia rafiki yake azungumuze na wazee. Kisha wakati fulani kupita, na rafiki yake hazungumuze na wazee, ule dada anaelezea yeye peke wazee ile jambo.