Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w24 Mwezi wa 12 uku. 30
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Iga Mufano wa Malaika Waaminifu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Namna Gani Malaika Wanaweza Kukusaidia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Ukweli Kuhusu Malaika
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
w24 Mwezi wa 12 uku. 30

Maulizo ya Wasomaji Wetu

“Malaika wenye walichaguliwa” wenye kuzungumuziwa mu 1 Timoteo 5:21 ni nani?

Mutume Paulo aliandikia hivi Timoteo muzee mwenzake: “Ninakuagiza kwa uzito mbele ya Mungu na Kristo Yesu na malaika wenye walichaguliwa, kwamba ushike maagizo haya bila upendeleo wala ubaguzi wowote.”—1 Ti. 5:21.

Kwanza, tuzungumuzie wale wenye haiwezekane wakuwe wale malaika wenye walichaguliwa. Ni wazi kama, hawako kati ya wale 144000. Wakati Paulo alimuandikia Timoteo, Wakristo watiwa-mafuta walikuwa hawayaanza kufufuliwa juu waende mbinguni. Mitume na Wakristo wengine watiwa-mafuta walikuwa hawayakuwa viumbe wa roho, kwa hiyo haiwezekane wakuwe “malaika wenye walichaguliwa.”—1 Ko. 15:50-54; 1 Te. 4:13-17; 1 Yo. 3:2.

Pia, “malaika wenye walichaguliwa” hawawezi kuwa malaika wenye hawakumutii Mungu wakati wa Garika. Wale malaika walijiunga na Shetani na wakakuwa pepo wachafu, na walikuwa maadui wa Yesu. (Mwa. 6:2; Lu. 8:30, 31; 2 Pe. 2:4) Wakati wenye kuya, watafungwa katika abiso kwa miaka 1000 na kisha wataharibiwa milele pamoya na Shetani.—Yud. 6; Ufu. 20:1-3, 10.

“Malaika wenye walichaguliwa” wenye Paulo alizungumuzia wanapaswa kuwa malaika waaminifu wenye kuwa mbinguni wenye wanategemeza “Mungu na Kristo Yesu.”

Kuko maelfu ya maelfu ya malaika waaminifu. (Ebr. 12:22, 23) Hatupaswe kuwaza kama wote wanakuwaka na mugao uleule wakati moya. (Ufu. 14:17, 18) Kumbuka kama wakati fulani malaika moya alipewa mugao wa kuharibu maaskari wa Ashuru 185000. (2 Fa. 19:35) Inawezekana malaika wengi wamepewa mugao wa ‘kukusanya kutoka katika Ufalme [wa Yesu] vitu vyote vyenye vinafanya watu wakwazike na pia watu wenye matendo ya kuvunja sheria.’ (Mt. 13:39-41) Inawezekana wengine wako na mugao wa ‘kukusanya watu wake wenye kuchaguliwa’ juu waende mbinguni. (Mt. 24:31) Na wengine wanapewa mugao wa ‘kutulinda katika njia zetu zote.’—Zb. 91:11; Mt. 18:10; linganisha na Matayo 4:11; Lu. 22:43.

Malaika iko naongoza bibi na bwana ku nyumba fulani mu mahubiri. Mwanaume mwenye kuwa mu ile nyumba iko nasali.

Inawezekana “malaika wenye walichaguliwa” wenye kuzungumuziwa mu 1 Timoteo 5:21 walipewa mugao wa pekee wa kuhangaikia mambo yenye kuhusu kutaniko. Kama tunasoma ile habari yote, tunaona kama Paulo alitoa mashauri ya hekima kuhusu wazee, wenye kutaniko inapaswa kuonyesha heshima. Wazee pia, wanapaswa kutimiza migao yao “bila upendeleo wala ubaguzi wowote” na hawapaswe kukamata maamuzi ao kuhukumu bila kufikiri sana. Jambo ya maana sana yenye inapaswa kuwachochea wafuate mashauri ya Paulo yeye iliongozwa na roho ya Mungu, ni juu wanatumika “mbele ya Mungu na Kristo Yesu.” Ni wazi kama malaika fulani wamepewa mugao wa kushugulikia mambo yenye kuhusu kutaniko, sawa vile kulinda kutaniko, kusimamia kazi ya kuhubiri, na kutoa ripoti kwa Yehova.—Mt. 18:10; Ufu. 14:6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine