Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp19 na. 3 uku. 14-15
  • Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Furaha Hata Leo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Furaha Hata Leo
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NAMNA YA KUWA MWENYE KUTOSHEKA
  • NAMNA YA KUVUMILIA WAKATI UKO MUGONJWA
  • NAMNA YA KUFANYA NDOA IKUWE YENYE NGUVU
  • Namna Mukristo Anaweza Kufanya Ndoa Yake Ikuwe ya Muzuri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Makuta Njo Chanzo ya Mambo Yote ya Mubaya?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Namna ya Kuwa Mwenye Kutosheka
    Amuka!—2021
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 1
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
wp19 na. 3 uku. 14-15
Mwanasayansi mumoja kati ya wenye tulizungumuzia iko anapiga chakula pamoja na bibi yake

Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Furaha Hata Leo

WAKATI wenye kuja, hakuna mutu mwenye atagonjwa, kuzeeka, ao kufa. Wewe pia unaweza kuwa na maisha ya vile! Lakini leo, maisha inajaa magumu na matatizo. Ni nini inaweza kukusaidia ukuwe na maisha yenye furaha leo? Biblia iko na mashauri yenye inaweza kukusaidia ukuwe mwenye furaha na ujisikie mwenye kutosheka hata leo. Tuzungumuzie matatizo fulani yenye kutokea mu maisha na tuone namna Biblia inaweza kutusaidia.

NAMNA YA KUWA MWENYE KUTOSHEKA

Shauri la Biblia: “Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza, wakati munatosheka na vitu vya sasa.”​—Waebrania 13:5.

Leo, kuko vitu mingi vyenye watu wanasema kama tunapaswa kuwa navyo. Lakini Biblia inasema kama tunaweza ‘kutosheka na vitu vya sasa.’ Namna gani?

Epuka “kupenda feza.” Juu tu ya “kupenda feza,” watu wanaweza kutia katika hatari afya yao, familia, urafiki, ao hata kupoteza mwenendo na heshima yao. (1 Timoteo 6:10) Lakini kufanya vile ni kujidanganya! Ku mwisho, mwenye kupenda mali “hatashiba.”​—Muhubiri 5:10.

Ona watu kuwa wa maana kuliko vitu. Ni kweli kwamba vitu vya kimwili vinaweza kutusaidia. Lakini haviwezi kutupenda ao kutushukuru; ni watu tu njo wanaweza kufanya vile. Kuwa na “rafiki wa kweli” kunaweza kutusaidia tukuwe wenye kutosheka katika maisha.​—Mezali 17:17.

TUNAWEZA KUFANYA MAISHA YETU IKUWE YENYE FURAHA HATA LEO KWA KUFUATA MASHAURI YA BIBLIA

NAMNA YA KUVUMILIA WAKATI UKO MUGONJWA

Shauri la Biblia: “Moyo wenye furaha ni dawa ya muzuri.”​—Mezali 17:22.

Kama vile “dawa ya muzuri,” kuwa mwenye furaha kunaweza kutusaidia kuvumilia magonjwa. Lakini, namna gani tunaweza kuwa wenye furaha hata kama tuko wagonjwa?

Ukuwe mwenye shukrani. Kama tunakaza akili juu ya magumu yetu, tutaona “siku zote” kuwa tu za mubaya. (Mezali 15:15) Lakini Biblia inasema, ‘ujionyeshe kuwa mwenye shukrani.’ (Wakolosai 3:15) Ujifunze kufurahia mambo ya muzuri mu maisha, hata kama ni ya kidogo. Mwangaza wenye kupendeza wakati jua linashuka, upepo wenye kutuliza, sura yenye furaha ya mutu mwenye unapenda; ile mambo inafanyaka maisha ikuwe yenye kufurahisha.

Fanya mambo kwa faida ya wengine. Hata kama afya yetu haiko muzuri, tunaweza kupata “furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Matendo 20:35) Wakati wengine wanatushukuru kwa sababu tunajikaza kufanya jambo fulani, ile inafanya tujisikie wenye kutosheka, na inafanya tusahau kwanza magumu yetu. Tunaweza kufanya maisha yetu ikuwe muzuri zaidi kwa kusaidia wengine wafanye maisha yao kuwa ya muzuri zaidi.

NAMNA YA KUFANYA NDOA IKUWE YENYE NGUVU

Shauri la Biblia: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”​—Wafilipi 1:10.

Bibi na bwana wenye wanapitisha pamoja wakati kidogo tu wanaweza kuharibisha uhusiano wao. Njo maana ni jambo lenye hekima bibi na bwana watie ndoa yao pa nafasi ya kwanza; ni kusema, waione kuwa kitu cha maana zaidi mu maisha yao.

Mufanye mambo pamoja. Kuliko kila mutu kufanya mambo yake mwenyewe, mupange kufanya mambo pamoja. Biblia inasema hivi: “Wawili ni muzuri zaidi kuliko mumoja.” (Muhubiri 4:9) Munaweza kupika chakula pamoja, kuenda ku shamba, kunywa kinywaji fulani, kufanya mazoezi ya mwili, ao kucheza muchezo fulani pamoja.

Onyesha kama unapenda mwenzako. Biblia inatia moyo bibi na bwana wapendane na kuheshimiana. (Waefeso 5:28, 33) Sura yenye furaha, kukumbatiana kwa upendo, ao zawadi ya kidogo vinaweza kusaidia sana ili ndoa ikuwe yenye nguvu. Lakini, ni bibi ao bwana yako tu njo mwenye unapaswa kuonyesha mapenzi.​—Waebrania 13:4.

“NILIFIKIA KUWA NA MAISHA YENYE KUSUDI!”

​—Ryoko Miyamoto, wa Inchi ya Japani Anaeleza Maisha Yake.

Maisha ilikuwa nguvu. Bwana yangu alikuwa mulevi na alipoteza kazi yake mara mingi. Aliacha kuhangaikia watoto wetu ine. Hata kama nilijikaza kutumika sana, ilionekana kama hali yetu haikuwa inabadilika. Nilijiuliza, ‘Njo vile Mungu alipanga maisha yangu ikuwe, ao iko ananipatia malipizi juu ya zambi zenye nilifanyaka zamani?’

Kisha, Shahidi mumoja wa Yehova aligonga ku mulango. Alinionyesha sura yenye furaha, na alikuwa mwenye kuchangamuka wakati alizungumuzia Ufalme wa Mungu na uzima wa milele. Aliniuliza kama nitapenda tujifunze Biblia. Bila kukawia, nilijifunza kama Mungu iko, kama ni mwenye hekima, haki, na mwenye upendo. Nilijifunza pia kuhusu hali ya wafu na kama haiko Mungu njo mwenye alipangaka mbele ya wakati mateso yenye kunipata.

Zaidi ya yote, nilifikia kutambua kama njia moja yenye inaweza kutusaidia tukuwe wenye kutosheka mu maisha, ni kumukaribia Mungu. Kujua kweli ya Biblia kumenitia moyo sana, na kumenisaidia kupata uhuru na kitulizo. Nilifikia kuwa na maisha yenye kusudi!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine