Lile Tukio la Maana Kubwa la Historia ya Kibinadamu
1 Yesu alikuja duniani, chini ya uongozi wa Baba yake, ili kutoa ushahidi kwa ile kweli inayoweza kutuongoza kwenye uhai wa milele. (Yn. 18:37) Kwa kubaki mwaminifu mpaka kufa, yeye alimheshimu Yehova, alilitakasa jina Lake na pia kutoa dhabihu ya ukombozi. (Yn. 17:4, 6) Yote hayo yanafanyiza kifo cha Yesu kuwa tukio la maana kubwa la historia ya kibinadamu.
2 Kati ya watu walioishi duniani tokea kuumbwa kwa Adamu, wawili tu ndio waliokuwa wakamilifu. Adamu angeweza kuwatolea wazao wake wa wakati ujao uwezekano wa kupata faida za ajabu. Badala yake, yeye aliasi kwa sababu za kichoyo, akiwaingiza katika maisha ya taabu yenye kupeleka kwenye kifo. Yesu alipokuja duniani, alijionyesha mwaminifu kabisa na pia mtiifu, akiwatolea hivyo wote ambao wangejizoeza imani uwezekano wa kuishi milele.— Yn. 3:16; Rum. 5:12.
3 Hakuna tukio lingine lolote linaloweza kulinganishwa na kifo cha dhabihu cha Yesu. Kilibadili historia. Kupitia kwacho, mabilioni ya watu wataweza kufufuliwa kutoka kwa wafu. Kimeweka msingi wa Ufalme wa milele ambao utamaliza ubaya na pia kugeuza dunia kuwa paradiso. Mwishowe kitaweka huru aina binadamu na uonevu na pia utumwa.—Zab. 37:11; Mdo. 24:15; Rum. 8:21, 22.
4 Hayo yote yanatusaidia kuelewa kwa nini Yesu aliamuru wanafunzi wake kukumbuka kifo chake kwa mwadhimisho wa Ukumbusho wa kila mwaka. (Luc 22:19) Tukiwa wenye kuelewa umaana wacho, tunangojea kwa hamu kukusanyika kama yatakavyofanya makutaniko ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote, Aprili 2, kisha kutua kwa jua. Kabla ya hilo, ingekuwa vizuri katika familia kusoma simulizi la kibiblia linaloelezea siku za mwisho za maisha ya Yesu duniani na kuchukua kwake msimamo wenye uhodari kwa ajili ya kweli. (Mitajo ya maandiko ya kusoma yanapatikana katika Kalenda 1996, kuanzia Machi 28 mpaka Aprili 2.) Yesu alituachia kielelezo kuhusu kumtukuza Muumbaji. (1 Pet. 2:21) Tufanye yote tuwezayo ili kualika kwenye mkutano huo wa maana watu tunaowajua na familia yetu, pia na wanafunzi wa Biblia na watu wengine waliotayari. Tuwafasirie mapema namna mambo yatakavyofanyika na pia umaana wa mifano (mkate na divai).—1 Kor. 11:23-26.
5 Wazee watapaswa kutengeneza mambo yao mapema ili kuwa hakika kwamba Jumba la Ufalme litakuwa safi na nzuri. Itafaa kujitayarisha mapema ili kuwa na mtu wa kutengeneza mifano. Kupitishwa kwa mifano kunapaswa kutengenezwe vizuri. Madokezo ya maana juu ya namna ya kuonyesha heshima kwa ajili ya Chakula cha Bwana yanapatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1985, ukurasa 17. Ingekuwa vizuri kwamba kutaniko lipangie mapema kuhubiri zaidi muda wa siku kadha kabla na kisha Ukumbusho.
6 Mwaka jana, jumla ya watu 13 147 201 walihudhuria kwenye mwadhimisho wa tukio hilo la maana kubwa. Kwa kuwa ndiyo siku iliyo ya maana kubwa mwakani, sisi sote tunapaswa kuwapo.