Tutembee Kwa Imani
1 Mamilioni ya watu wanajenga maisha yao juu ya vitu vya kimwili, wakitia kiupumbavu tumaini lao katika uwezo wenye kudanganya wa mali. (Mt. 13:22) Somo linakuwa chungu wakati mali zao zinapopotea, zinapoibiwa, au zinapoonekana kuwa zenye manufaa kidogo. Tunahimizwa sana kufuata njia ya hekima zaidi, kwa kutafuta kwa bidii hazina za kiroho. (Mt. 6:19, 20) Hilo humaanisha kwamba ‘tulitembea kwa imani.’—2 Kor. 5:7.
2 Neno “imani” hutafsiri usemi wa Kigiriki ulio na wazo la tumaini, uhakika imara. Kutembea kwa imani humaanisha kukabiliana na magumu kwa kuweka tumaini katika Mungu, kwa kutegemea uwezo wake wa kuongoza hatua zetu na kupenda kwake kutosheleza mahitaji yetu. Yesu anatoa kielelezo kikamilifu; alibaki mwenye kukaza akili juu ya kile kilichokuwa hakika cha lazima. (Ebr. 12:2) Vivyo hivyo, imetupasa kulinda moyo wetu ukiwa wenye kukazwa juu ya mambo ya kiroho, yale yasiyoonekana. (2 Kor. 4:18) Tukumbuke siku zote ufupi wa maisha ya sasa, na tutambue kabisa tegemeo letu kwa Mungu.
3 Tunapaswa pia kuwa hakika kwamba Yehova anatuongoza kupitia tengenezo lake lionekanalo, chini ya uongozi wa “mtumwa mwaminifu na mwenye akili.” (Mt. 24:45-47) Tunaonyesha imani yetu kwa ‘kutii wale wanaoongoza’ kutaniko. (Ebr. 13:17) Kutenda kwa unyenyekevu kulingana na mipango ya kitheokrasi kunashuhudia tumaini letu katika Yehova. (1 Pt. 5:6) Tungepaswa kujisikia wenye kuchochewa kutegemeza bila kipimo kazi ambayo tengenezo limekabiziwa. Kwa hiyo, tukiwa wenye kuunganishwa nguvu kabisa na upendo na umoja, tutawakaribia ndugu zetu.—1 Kor. 1:10.
4 Jinsi ya Kutia Nguvu Imani Yetu: Tusiache imani yetu iwe yenye kufa. Imetupasa kufanya vita nguvu ili kuikomaza. Ukawaida katika funzo, sala na hudhurio kwenye mikutano vitatusaidia kutia nguvu imani yetu, hivi kwamba kwa tegemezo la Yehova iweze kusimama imara mbele ya haidhuru jaribu gani. (Efe. 6:16) Je! tumejifanyia programu kwa ajili ya usomaji wa kila siku wa Biblia na kutayarisha mikutano? Je! tunatafakari kila mara juu ya yale tunayojifunza, na je! tunamkaribia Yehova katika sala? Je! ni zoezi letu kuhudhuria kwenye mikutano yote na kuishiriki wakati tunapokuwa na nafasi?—Ebr. 10:23-25.
5 Imani yenye nguvu inaonekana kwa matendo mema. (Yk. 2:26) Mojawapo ya njia nzuri ya kuonyesha imani yetu ni kuzungumzia tumaini letu kwa wengine. Je! tunachukua nafasi zinazojitokeza za kutangaza habari njema? Ni mabadiliko gani katika hali yetu ya kibinafsi yangetuwezesha kutumika zaidi katika mahubiri? Je! tunafuata madokezo tunayopokea ili kutengeneza ubora na matokeo mema ya huduma yetu? Je! tunajiwekea kibinafsi miradi ya kiroho na kujikaza kuifikia?
6 Yesu alituonya dhidi ya hatari ya sisi kujiacha kusumbuliwa na mambo ya maisha, na kuruhusu faida za kimwili au za kichoyo kuvuruga mwono wetu wa kiroho. (Lk. 21:34-36) Tunapaswa kujiangalia namna tunavyotembea, ili kuepuka kuzama kwa habari ya imani yetu. (Efe. 5:15; 1 Tim. 1:19) Kila mmoja wetu anatumaini kuweza kusema siku moja: “Nimepigana lile pigano zuri, mimekimbia ule mwendo hadi umalizo, nimeshika ile imani.”—2 Tim. 4:7, NW.