Tuwe Vielelezo Katika Usemi Na Katika Mwenendo
1 Mtume Paulo alimuhimiza Timotheo kuwa kielelezo katika usemi na katika mwenendo. (1 Tim. 4:12) Sisi pia, tunapaswa kuwa na usemi na mwenendo nzuri, hasa wakati tunapotimiza huduma yetu, kwani unaweza kuonyesha ikiwa tutagusa au hapana mioyo ya watu tunaokutana nao.
2 Adabu yetu nzuri inapaswa kuonekana katika hali zote, na hasa hali yetu ya urafiki, heshima yetu, wema wetu, staha yetu na busara yetu. Kwa kudhihirisha sifa hizo, tunaonyesha kwamba tunatambua matokeo ambayo matendo yetu yanaweza kuwa nayo juu ya hisia-moyo za wengine. Tungeweza kufananisha adabu nzuri katika huduma na viungo vinavyotumiwa kuongeza ladha (onjo) ya chakula. Kikikosa viungo, chakula kizuri kingeweza kuwa kisicho na ladha na kisicholeta huba. Ukosefu wa adabu katika uhusiano wetu mbalimbali pamoja na wengine ungeweza kuwa na matokeo yale yale.—Kol. 4:6.
3 Tuwe Vielelezo Katika Usemi: Cheko ya kirafiki na salamu yenye shauku ni mambo ya lazima kwa utoaji wetu wa habari njema. “Tunapokoleza” kwa shauku na unyofu utangulizi wetu, msikilizaji wetu anaelewa kwamba tunapendezwa hakika naye. Anaposema, tumsikilize kwa makini na tuheshimu kama ifaavyo wazo lake. Tunaposema, tufanye hivyo kwa busara na wema.—Ona Matendo 6:8.
4 Inafikia wakati mwingine kwamba tunakutana na mtu mkali, hata mwenye jeuri. Jinsi gani tungepaswa kuitikia? Petro alituagiza kusema ‘kwa upole na kwa heshima nyingi.’ (1 Pt. 3:15 ; Rom. 12:17, 18) Yesu alisema kwamba ikiwa mtu fulani angekataa kwa ukaidi ujumbe wa Ufalme, tungepaswa tu ‘kukunguta mavumbi kutoka kwenye miguu yenu.’ (Mt. 10:14) Kwa kulinda mwenendo usiolaumika katika hali za namna hizo, inawezekana turegeze mioyo ya watu wenye kutupinga.
5 Tuwe Vielelezo Katika Mwenendo: Kuhubiri habari njema katika barabara zenye kutembelewa na watu wengi na katika nafasi za watu wote kunaomba kwa upande wetu kuwa na adabu, kuwa siku zote wenye kiasi, kutoweza kamwe kuwa wenye kulazimisha na kusumbua wapita-njia. Tunapokuwa nyumbani mwa watu wanaonyesha kupendezwa, tunapaswa kufuata kanuni za adabu na kujiendesha kama waalikwa wenye adabu, wanaoonyesha shukrani yao kwa ukaribishaji wanaotuonyesha. Mtoto yeyote anayetushindikiza anapaswa kuheshimu wenye nyumba na mali zao, na angepaswa kusikiliza kwa adabu mazungumzo. Watoto wakaidi wanaacha sifa mbaya.—Mit. 29:15.
6 Hakuna awaye yote angepaswa kushakia, kwa hali yetu ya nje, kwamba sisi ni wahudumu wa Neno la Mungu. Mvalio wetu na kutembea kwetu hakungepaswa kuwa kwa ovyoovyo na kwa kujiachilia, wala kwenye kuvutia macho na kwa kiajabu-ajabu. Na hali yetu ya nje iwe siku zote yenye kustahili habari njema! (Ona Wafilipi 1:27.) Kwa kuonyesha uangalifu wa pekee kwa hali yetu ya nje na kwa vifaa vyetu, hatuwapi wengine nafasi yoyote ya kukwazika au kusema vibaya huduma yetu. (2 Kor. 6:3, 4) Usemi wetu na mwenendo wetu mzuri unafanya ujumbe wa Ufalme kuwa wenye kuvutia zaidi, na unamheshimisha Yehova.—1 Pt. 2:12.